Showing posts with label SIM CARD TAX. Show all posts
Showing posts with label SIM CARD TAX. Show all posts

24 Jul 2013



Naam, Tanzania yetu imewahi kuwa na viongozi mbalimbali wabovu, lakini linapokuja suala la mawaziri wakuu, basi Mizengo Kayanda Pinda, anaweza kabisa kuingia kwenye kumbukumbu kama WAZIRI MKUU MBOVU KULIKO WOTE KATIKA HISTORIA YA NCHI YETU.

Ndio, Kuna Edward Lowassa, aliyeng'oka kwa kashfa ya Richmond, lakini angalau yeye hakuwa m-babaishaji katika kauli zake. N apengine kilichmosaidia Lowassa ni kutambua busara kuwa mdomo sharti ushirikiane na ubongo kabla ya kutoa kauli yoyote ile.

Pinda, anayeitwa Mtoto wa Mkulima, amekuwa maarufu zaidi kwa kauli zake za kipuuzi kuliko utendaji kazi.Mbabaishaji huyo aliwahi kuzua sokomoko huko nyuma alipohalalisha MAUAJI: kwa uzembe tu wa kufikiri, Pinda alidai kuwa anaguswa sana na mauaji ya maalbino,kwahiyo ni ruksa kwa wananchi kuwauwa WATUHUMIWA wa mauaji hayo. Japo kitaaluma  mwanasheria, lakini Pinda hakuona tatizo katika kauli yake hiyo ambayo kimsingi ilikuwa inahamisha nguvu za polisi na mahakama na kuzikabidhi kwa umma.Kwa lugha nyingine, mzembe huyo alikuwa anahalalisha mob justice.

Badala ya ku-behave kama mtu mzima, Pinda akenda bungeni na kujitetea kwa KULIA KAMA MTOTO.Lakini kwa bahati nzuri, wengi wa wabunge wetu wapo bize zaidi na posho zao kuliko kuwatendea haki wananchi wanaowawakilisha, na machozi hayo ya kinafiki ya Pinda yakamnusuru.


Katika kuonyesha kuwa Tanzania kwa sasa ni kama haina Waziri Mkuu kwani Pinda anayeshikilia nafasi hiyo ni so useless kiasi kwamba uwepo au kutokuwepo kwake hakuna tofauti, majuzi akakurupuka tena na kauli nyingine ya kibabaishaji.Akatangaza kuwa ni ruksa kwa polisi kupiga raia ZAIDI...Yaani kana kwamba unyanyasaji unaofanywa na polisi hautoshi, na sasa wanahamasishwa kutoa vipigo zaidi.

Watu tumesema weee kuhusu kauli hiyo ya kihuni lakini kwa vile aliyemteua Pinda kushika nafasi hiyo hana tofauti sana na Pinda, Waziri Mkuu huyo bado yupo madarakani hadi dakika hii.

Na uwepo wake huo umepelekea ujinga mwingine. Majuzi kumezuka sokomoko la kodi mpya ya SIM kadi.Badala ya kusikia kilio cha mamilioni ya Watanzania wanaopinga kodi hiyo, mropokaji Pinda akadai eti "wanaopinga kodi hiyo hawaitakii mema nchi yetu..." COMPLETELY USELESS!

Bahati nzuri, safari hii Rais Kikwete kaamua kutumia busara, na kwa namna flani, amemudu KUMUUMBUA PINDA. Rais amezitaka mamlaka husika kukaa pamoja kutafuta ufumbuzi wa haraka kuhusu kodi hiyo inayolalamikiwa na wananchi wengi. Rais aliyasema hayo alipokutana na viongozi wa Wizara ya Fedha, na wale wa Wizara ya Sayansi na Teknolojia, na Mamlaka ya Mawasiliano TCRA.

SIJUI MTOTO WA MKULIMA ANAJISIKIAJE MUDA HUU....ONE THING FOR SURE, PINDA AMETHIBITISHA KWA MARA NYINGINE KUWA YEYE NI MTU MZIMA OVYO ASIYEFAA HATA KUONGOZA DARASA KAMA KIRANJA, ACHILIA MBALI HUO UWAZIRI MKUU.NI WABABSIAHJI KAMA PINDA WANAOIFANYA SIASA KUWA MCHEZO MCHAFU ZAIDI YA UCHAFU WA SIASA.

CAN'T WAIT TO SEE HIM GONE COME 2015, OR EVEN EARLIER...GOOD RIDDANCE.

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.