Showing posts with label SOCIOLOGY OF RELIGION. Show all posts
Showing posts with label SOCIOLOGY OF RELIGION. Show all posts

19 Jun 2008

Makala yangu katika toleo la wiki hii la gazeti la Raia Mwema inaanza kwa kuwashutumu watangazaji wa radio na runinga za Bongo ambao wanafanya mzaha kwenye shughuli muhimu.Makala inawalenga watangaza taarifa za habari ambao aidha hawajiandai vya kutosha kabla ya news bulletins kiasi cha kuchapia maneno,especially majina ya watu na sehemu,au wanaokuwa too obsessed na sauti za akina Jacob Tesha,Ahmed Kipozi,Ahmed Jongo,Abubakari Liongo,Charles Hillary,nk to an extent wanaishia kusoma madudu badala ya habari.Kuiga sauti sio uhaini lakini kwa kufanya hivyo isiwe sababu ya kusoma vitu vya ajabu.


Pia makala yangu inazungumzia suala zima la ushirikina hapa nyumbani ambapo nimejaribu kulitazama kwa upande mmoja kama mwanafunzi wa zamani wa sosholojia ya dini (sociology of religion) na kwa upande mwingine kama mwanajamii ninayeelewa nini kinanizunguka,hata kama tunaona aibu kukiongelea.Sio siri kwamba mambo ya ushirikina yameshika hatamu sana katika jamii mbalimbali za Kiafrika,lakini hii ya Fisadi Mzee wa Vijisenti kumwaga ndumba ndani ya Bunge inaonyesha jinsi gani mambo yanakwenda mrama sana katika nchi hii tuliyoahidiwa kuwa maisha bora kwa kila aliyezaliwa hapa yanawezekana.Nisikunyime uhodno,bingirika na makala hiyo pamoja na nyingine zilizokwenda shule ya kutosha KWA KUBONYEZA HAPA

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.