Showing posts with label SOKA. Show all posts
Showing posts with label SOKA. Show all posts

13 Feb 2012

24 Oct 2011

Lighting the fuse: Mario Balotelli strikes the ball towards the bottom corner of United's goal
Mario Balotelli akifungua ukurasa wa mabao
No stopping that: United goalkeeper David De Gea attempts to get across but can't prevent the shot going in
Mpende au mchukie lakini Mtaliano huyu mweusi ni moto wa kuotea mbali
Read all about it: Balotelli (left) celebrates by revealing a t-shirt that read 'why always me?'
Kama kawaida yake,Balotelli haishiwi vituko.Hapa akionyesha maandishi "Kwanini Mimi?" 
Super Mario: Balotelli (right) pops up at the far post to score City's second goal
Balotelli akitundika bao la pili

Three is the magic number: Sergio Aguero (left) followed Balotelli onto the scoresheet for the third goal
Aguero akiandika bao la tatu

Kneesy does it: Edin Dzeko (left) bundles in his side's fourth goal from close range
Dzeko akifunga bao la nne
Still scoring: Spanish midfielder Silva slots his finish under De Gea (not seen) in injury time
Silva akitundika bao la tano
That does it: Dzeko rounds off the scoring with a cool finish for City's sixth goal
Dzeko akifunga bao la sita
Let's all do the Poznan: City fans celebrate their stunning win at the home of their rivals
Mashabiki wa Manchester City wakishangilia kipigo ha haja kwa majirani zao wa Manchester United
Plenty to ponder: Sir Alex Ferguson was left to reflect on a devastating defeat
Kocha wa Manchester United Sir Alex Ferguson akiwa hoi
Game for a laugh: City manager Roberto Mancini enjoys his side's thrilling performance
Kocha wa Manchester City Roberto Mancini akifurahia kazi ya vijana wake

CHANZO: DailyMail

29 Dec 2007


Kapteni wa timu ya soka ya Motherwell ya Scotland,Phil O'Donnell,amefariki dunia muda mfupi baada ya kuanguka uwanjani katika mchezo wa Ligi Kuu ya hapa dhidi ya Dundee United.Mchezaji huyo aliyeanguka wakati anabadilishana nafasi na mchezaji mwenzie (substitution),alitibiwa kwa muda mfupi uwanjani hapo kabla ya kupelekwa hospitalini,na hatimaye kupatikana habari kuwa amefariki.Katika mechi hiyo iliyofanyika kwenye uwanja wa Fir Park,mjini Motherwell,timu ya marehemu huyo ilishinda kwa mabao 5-3,na kufanikiwa kushika nafasi ya tatu nyuma ya Celtic na Glasgow Rangers. 

22 Aug 2007

Asalam aleykum,

Nianze na habari “nyepesi nyepesi.” Kwa mujibu wa utafiti ambao matokeo yake yalinukuliwa na gazeti la Daily Mail la hapa Uingereza,kioo kinaweza kuwa na majibu kuhusu hali ya afya ya binadamu.Inaelezwa kwamba “kujishangaa” kwenye kioo kwa muda flani kunaweza kukupatia tetesi kuhusu dalili za matatizo ya kiafya katika mwili wako.Pengine hii itakuwa habari njema zaidi kwa baadhi ya akinamama ambao,kama wengi wetu tujuavyo,huweza kutumia hata nusu saa wakijiangalia kwenye vioo,hususan kabla ya kufanya “mtoko” (kwenda kwenye harusi,kitchen party,ubarikio,nk).Mie ni miongoni mwa “wazembe” ambao naweza kupitisha hata siku tatu bila kujiangalia kwenye kioo (na pengine siko peke yangu).Lakini kwa mujibu wa utafiti huo,kujiangalia kwenye kioo japo kwa muda michache kunaweza kubainisha matatizo ya kiafya kama vile maambukizo ya bacteria,kupanda kwa “cholesterol”, “anaemia”, “arthritis”,upungufu wa Magnesium mwilini,mshtuko wa moyo na hata kubaini ujauzito.Kwa mfano,ukijitazama kwenye kioo na kubaini kuwa macho yamekuwa meupe kuliko kawaida,basi hiyo inaweza kuwa dalili ya kuzidi kwa “cholesterol” mwilini;macho yakiwa yamevimba pasipo sababu inaweza kuwa dalili ya maambukizo ya bacteria au pengine “arthritis”;kope (“eyelids”) zinazoonekana kama zinataka kunyonyoka zinaweza kuashiria dalili za “anaemia”;jicho linalozunguka bila kuzungushwa (“myokymia”) linaweza kuashiria upungufu wa Magnesium;kupauka kwa rangi ya mwili kunaweza kumaanisha dalili za homa ya manjano au matatizo ya maini;fizi zinazotoka damu zinaweza kuashiria “leukaemia” au ujauzito;na mipasuko kwenye “lips” kunaweza kuashiria kisukari.Hata hivyo,kama yalivyo matokeo ya tafiti nyingi,matokeo ya utafiti huu kuhusu “faida za kioo katika kubaini hali ya mwili” hayamaanishi kuwa kila dalili utakayoiona kwenye kioo (kati ya hizo zilizotajwa) basi lazima inaashiria ugonjwa flani.Ni dhahiri kwamba mtu “akilamba” mzinga mzima wa “Mzaramo” (Konyagi) basi siku inayofuatia anaweza kuwa na macho yaliyovimba,na wala si dalili za “arthritis” au maambukizo ya bacteria (sidhani kama bacteria wana jeuri ya kumudu makala ya Konyagi.,,natania tu!).Lakini nadhani licha ya kujiangalia kwenye kioo kwa madhumuni ya kujua kama “reception” (sura) iko maridhawa,kujitazama mwenyewe kwenye kioo kunaweza kukusaidia kujisuta kama umefanya jambo baya,kujipongeza kama umefanya jambo zuri na hata kujishauri pale unapokuwa njia panda kutokana na matatizo au ugumu wa kutoa maamuzi.

Na utafiti mwingine kwa mujibu wa jarida la Saikolojia ya Uchumi (the Journal of Economic Psychology) watu wenye sura nzuri wana uhakika wa kipato kizuri zaidi kushinda wale wenye “sura mbaya.” Wachumi James Andreoni na Ragan Petrie wanaeleza kwamba katika kuangalia mafanikio ya kipato kati ya watu wenye sura nzuri na wale wasio na sura nzuri wamebaini kuwa hata pale watu wa makundi hayo mawili wanapofanya jitihada zinazolingana,wengi wa wenye sura nzuri “wanaibuka kidedea”.Watafiti hao wanaamini kwamba kinachowasaidia wenye sura nzuri kuwa na mafanikio ni ukweli kwamba watu wa aina hiyo huwa na matarajio makubwa ambayo wangependa yawe na matokeo mazuri yatakayoshabihiana na sura zao nzuri.Pia walibaini katika utafiti huo kwamba watu wenye sura nzuri wakizembea “kulinda uzuri wao” (kwa mfano kutojiweka “sopu-sopu” au kuongezeka “nyama za uzembe”) basi wale wanaonekana “wabaya” kwa sura wanapata nafasi ya “kuwapiga bao” (kuchukua nafasi za) hao wenye sura nzuri.Swali nililobaki nalo baada ya kusoma taarifa hizo ni kwamba nani ana mamlaka ya kusema flani mzuri au flani mbaya,pengine kwa kuzingatia msemo wa Kiswahili kwamba “apendae,chongo huona kengeza” au hata pengo kuitwa mwanya.

Pia,siku chache zilizopita wanafunzi kutoka nje ya Uingereza tulipata habari iliyowaacha baadhi ya “wenyeji” wetu wakiwa wamenuna.Kwa mujibu wa Dokta Bernard Lamb,msomi (reader) wa “genetics” kutoka Imperial College London,wengi wa wanafunzi wa kigeni wanaonekana kukimudu vema Kiingereza kuliko wanafunzi wazawa (Waingereza),ambapo wageni hao huwa na makosa machache wanapoandika au kuongea lugha hiyo ulinganisha na hao wenye lugha yao.Dr Lamb alieleza kwamba wanafunzi kutoka nchi za Singapore na Brunnei ndio wanaoongoza kwa ubora wa Kiingereza japokuwa lugha hiyo sio yao ya asili (ni second language).Amesema kwamba sio jambo gani kwa wanafunzi wazawa kuandika kwenye insha zao maneno kama “there” pale inapopaswa kuwa “their” au “bean” pale inapopaswa kuwa “been,” au kutamka “effect” badala ya “affect” na “sun” badala ya “son,” au badala ya wingi (plural) ya “tomato” kuwa “tomatoes” wao wanachapia “tomatos” na badala ya “theories” kama wingi wa “theory” wao wanaibuka na “theorys.” Msomi huyo anadai kuwa udhaifu mkubwa uko kwenye sarufi (grammar) na vituo (punctuation),na sasa anaandaa kitabu cha kuziumbua mamlaka za elimu kwa kuzembea kuweka mkazo kwenye kuboresha somo la Kiingereza mashuleni.

Kadhalika,moja ya mambo yaliyotawala anga za siasa za ndani za Marekani ni tangazo la mpanga-mikakati mkuu (“chief political strategist”) wa rais Bush,Karl Rove,kuwa anajiuzulu mwishoni mwa mwezi huu.Huyu jamaa ana akili sana,tena sana.Tayari wapo wanaodai kuwa hakuna mtu mwenye uwezo wa kuziba pengo lake hapo White House baada ya kuondoka kwake.Inategemea unazungumza na mtu aliye upande gani wa mjadala,kwani kuna watu wanaomtuhumu Rove kwa “kumpotosha” Bush katika maamuzi mbalimbali,na wanadai kuwa kupungua kwa umaarufu wa urais wa Bush (huko Marekani kila baada ya muda flani huwa zinatolewa “ratings” za utendaji kazi wa rais, “congress”,nk na kwa sasa wanaorodhishwa na utendaji kazi wa Bush ni asilimia 32.9 tu huku asilimia 62.4,yaani zaidi ya nusu ya Wamarekani,hawaridhishwi na utendaji kazi wake) kumechangiwa kwa kiasi kikubwa na swahiba huyo wa Bush.Lakini,mpende au mchukie,mwanamikakati huyu ni mtu mwenye kipaji cha hali ya juu katika kuhakikisha ushindi unapatikana kwa kila aina ya mbinu.Na ndio maana haishangzi kuona baadhi ya watu wakijiuliza kama kutatokea mtu mwenye kipaji kama cha Karl Rove.Yayumkinika kusema kuwa kujiuzulu kwake kumekuja wakati mbaya kwani ripoti inayosubiriwa kwa hamu kutoka kwa kamanda wa majeshi ya Marekani huko Irak,Jeneral David Petraeus,kuhusu mwenendo mzima wa vita ya Irak inatarajiwa kuwasilishwa katikati ya mwezi ujao,na wapo wanaodhani kwamba kukosekana kwa Rove katika kipindi hicho muhimu kunaweza kuwa ni tatizo kwa Bush iwapo ripoti hiyo itakuwa siyo nzuri.Rove ambaye anaelezwa kama mtu atakayengia kwenye vitabu vya historia kama kiumbe asiye na huruma (ruthless) linapokuja suala la kufanikisha matakwa ya kisiasa ya bosi wake,na ambaye alipachikwa jina la utani la “the Architect” (msanifu) kutokana na ufanisi wake kwenye sanaa ya kupanga mikakati,alimsaidia Bush kupata ugavana wa jimbo la Texas mwaka 1994,kabla ya lutoa mchango wa hali ya juu katika ushindi wa Bush kwenye chaguzi za urais za mwaka 2000 na 2004.Japo naweza kuwa miongoni mwa wale wanaoamini kuwa kuna maeneo ambayo “alimpotosha” Bush,na ukweli kwamba tofauti na nguli huyo,mrengo wangu kisiasa ni wa kati ya kushoto (Centre-Left),nimetokea kumhusudu sana Karl Rove (na nadiriki kumwita “role model” katika malengo yangu ya mbeleni).Ukipata nafasi ya kusoma kitabu kiitwacho “Boy Genius: Karl Rove, the Brains Behind the Remarkable Political Triumphs of George W Bush” au “Bush's Brain: How Karl Rove Made George W. Bush Presidential” unaweza kuungana nami “kumkubali” huyu jamaa.

Mwisho,napenda kuwapongeza watani wetu wa jadi Yanga kwa kunyakua kombe la Tusker.Nimesikia “rambirambi” zao kwamba fedha inayotolewa na waandaaji wa mashindano hayo haikidhi gharama halisi walizoingia hadi kufikia hatua ya fainali,lakini nadhani walipaswa kutafakari suala hilo kabla ya kuanza mashindano hayo.Licha ya “kuukosa ubingwa” (haituumi kwa vile hatukufungwa bali tulijitoa) wana Msimbazi tunafarijika na hilo “contract” la nguvu la kuitangaza “chata” ya kimataifa ya “ADDIDAS.” Simba ina bahati na wadhamini,pengine kutokana na rekodi yake nzuri kwenye mechi za kimataifa,lakini ni muhimu kwa Kaduguda na wenzie kuhakikisha kuwa udhamini huo unasaidia katika kutimiza ndoto ya Watanzania kuona vikombe vya michuano mikubwa ya vilabu barani Afrika vinatua nchini.

Alamsiki

22 Aug 2006

KULIKONI UGHAIBUNI:

Kombe la Dunia mwaka 2006.Wenyewe wanaiita shughuli hii “the biggest show on earth.” (yaani mashindano makubwa kabisa duniani).Inaweza kuwa kweli.Kombe la dunia linawaunganisha mamilioni kwa mamilioni ya watu katika takriban kila pembe ya sayari hii.Wapo wale wanaofuatilia timu zao za taifa zikitafuta nafasi katika vitabu vya historia ya soka,wengine tukiwamo Watanzania tunafuatilia michuano hiyo kwa vile wengi wetu tunapenda soka japokuwa kwa sababu zinazoweza kuchukua mwaka mzima kuzitaja hatujui lini nasi tutakuwa washiriki.

Kuna mjadala mdogo japo muhimu unaoendelea huku Ughaibuni na pengine hata kwingineko kuhusu kama ni kweli michuano hii na michezo kwa ujumla inaleta umoja na sio mpasuko miongoni mwa timu au nchi shiriki na mashabiki ulimwenguni kote.Pengine hakuna sehemu nzuri zaidi ya kuanzia mjadala huu kama hapa Uingereza.Pengine ni vema kuielezea Uingereza kwa kutumia majina wanayotumia wenyewe.United Kingdom ni muungano wa “nchi” nne:England,Scotland,Wales na Northern Ireland. Great Britain ni hizo tatu za mwanzo ukitoa Northern Ireland (ambayo kijiografia haiko katika ardhi moja na hizo tatu).Kwa hiyo kuna wakati utasikia nchi hii ikiitwa The United Kingdom of Great Britain and Northern Ireland.Kwa kawaida,katika mashindano mbalimbali Uingereza huwakilishwa na timu za taifa au klabu kutoka “nchi” hizo nne kama vile ilivyo kwa timu za Taifa za Bara na Zanzibar zinavyoiwakilisha Tanzania.

Katika mchakato wa kutafuta nafasi ya kushiriki katika Kombe la Dunia ni England pekee iliyofanikiwa na kuziacha Wales, Scotland na Northern Ireland kubaki watazamaji tu.Hapo ndipo shughuli inapoanza.Kwanza Waziri Mkuu (First Minister) wa Scotland Jack McConnell aliweka msimamo wake wazi kwamba hatashabikia England,ambayo kwa hapa Scotland inajulikana kwa jina la kiutani kama Auld Enemy (Adui wa zamani) na badala yake angeshabikia Trinidad and Tobago-au kwa kifupi T&T.Na si yeye pekee mwenye mtizamo huo.Asilimia kubwa ya Waskotishi walishabikia T&T ilipopambana na England.Wapo waliotoa kisingizio kwamba ushabiki wao ulitokana na ukweli kwamba kuna mchezaji wa T&T mwenye ubini Scotland (anaitwa Jason Scotland,anayechezea timu ya daraja la kwanza ya St Johnstone) lakini wengine hawakuwa hata na haja ya kutoa visngizio bali kusema ukweli kwamba ushindi kwa England ni karaha kwao.Kama kuna sehemu zaidi ya nchini T&T ambako jezi za timu yake ya taifa ziliuzika sana basi si kwingine bali Scotland.
Kuna hii kitu inayoitwa “bendera ya Mtakatifu Joji” (St George flag).Nadhani kwa wale wanaofuatilia mechi za England watakuwa wameona bendera hiyo nyeupe yenye msalaba mwekundu.Bendera hiyo ina historia ndefu ambayo pengine hapa si mahala pake,lakini lililo wazi ni kwamba inahusishwa kwa kiwango flani na hisia za ubaguzi wa rangi (racism).Hata baadhi ya taasisi zimekuwa na wasiwasi pale watumishi wake wanapopeperusha bendera hizo.Kwa mfano,hivi karibuni supamaketi kubwa iitwayo Tesco ilipiga marufuku madereva waliokuwa wanaleta mizigo kwenye supamaketi hiyo huku wakipeperusha bendera ya Mtakatifu Joji,japo baadaye uamuzi huo ulibatilishwa.Pia mamlaka ya viwanja vya ndege (BAA) ilipiga marufuku kupeperusha bendera hiyo kwenye majengo yanayofanyiwa ukarabati Terminal 5 Heathrow Airport.Mkanganyo zaidi kuhusu bendera hii umeongezwa na ukweli kwamba BNP,chama cha siasa chenye mtizamo wa kibaguzi,kimekuwa kikiitumia bendera hiyo katika harakati zake dhidi ya wahamiaji na wageni.Watetezi wa bendera hiyo wanasema inawaonyesha uzalendo na sio alama ya ubaguzi.

Tofauti na huko nyumbani ambako hadi hivi karibuni kitendo kutundika bendera ya Taifa dirishani kingeweza kukupeleka Segerea (jela) huku kwa wenzetu bendera ni miongoni mwa alama za kujivunia utaifa/uzalendo wao.Hata hivyo,wapo wanaotumia utaifa kama kifuniko (cover) cha dhamira zao za kibaguzi.Mara nyingi vikundi vinavyoendekeza siasa za kibaguzi vimekuwa vikitumia sana bendera za mataifa yao kujitambulisha (kama ilivyo kwa BNP).Utaifa uliopindukia ni mithili ya ulafi:kula sio kitendo kinachoudhi lakini kula kupita kiasi (ulafi) unaudhi kwa vile unaweza kuwaathiri watu wengine,kwa mfano kuwalaza na njaa.Wachambuzi wa soka la Hispania walikuwa na wasiwasi iwapo timu yao ingefanya vizuri kwenye Kombe la Dunia kutokana na ukweli kwamba Waspanishi wengi wanajali zaidi timu zinazotoka katika miji yao (kwa mfano Real Madrid,Barcelona au Valencia) kuliko timu ya taifa.Hapo tatizo ni zaidi ya utaifa bali asili ya mtu anakotoka katika taifa.

Na pengine ni kwa vile waandaaji wa Kombe la Dunia wanafanya kila jitihada kupambana na wakora wa soka ndio maana inapunguza na vitendo visivyopendeza machoni wa watu kwa mfano kutoa sauti kama za nyani kuwakashifu watu weusi.Matukio ya ubaguzi katika soka yamekuwa ni tatizo linalowagusa watu wengi.Hali ni mbaya sana huko Ulaya Mashariki ambapo kwa mfano baadhi ya timu za hapa zenye wachezaji weusi huwa zinatahadharishwa mapema kabla ya kwenda huko kuwa zitegemee wachezaji hao weusi kunyanyaswa na mashabiki wabaguzi.Soka la Hispania katika siku za karibuni limegubikwa mno na kelele za kibaguzi dhidi ya wachezaji weusi.Italia pia inasifika kwa hilo kama ilivyo kwa Ujerumani yenyewe.Hata hapa Uingereza kuna hisia kwamba miongoni mwa sababu zinazoifanya timu kama Chelsea “kuchukiwa” ni kwa vile mmiliki Roman Abramovich si Mwingereza, kocha Jose Maurinho ni Mreno na wachezaji wengi ni kutoka nje ya Uingereza.

Kwa kumalizia,ngoja niwachekeshe kidogo.Hapa kuna kundi la akina mama wanaojiita “Wajane wa Kombe la Dunia.”Hawa ni wale wanaoyaona mashindano haya kama adhabu kwa vile waume zao wakereketwa wa soka huwasahau kwa muda wake zao na akili yote kuelekezwa kwenye michuano hiyo.Huenda hata huko nyumbani kuna “wajane” pia.Si unajua tena wapo wanaotumia kisingizio cha kwenda “kucheki boli” kupata wasaa wa kuzungukia nyumba ndogo…huo ni utani tu.

Alamsiki

18 Jun 2006

KULIKONI UGHAIBUNI:

Asalam aleykum,

Leo tuzungumize michezo,hususan soka.Kwa takriban wiki nzima sasa habari ya soka iliyotawala katika vyombo vya habari vya hapa Uingereza ni kuhusu suala la mchezaji mahiri wa klabu ya Manchester United na timu ya Taifa,Wayne Rooney.Ishu yenyewe ni kwamba ilidaiwa kuwa Rooney alikuwa na madeni yanayofikia pauni 700,000 (takribani shilingi milioni 140 za huko nyumbani) aliyokuwa akidaiwa na makampuni ya kamari (betting).Inasemekana tayari amemalizana na wadai wake.Wapo waliomlaumu mchezaji huyo kwa kutumia vibaya fedha zake,lakini wengine wamemtetea kwamba haikuwa ubaya kutumia kipato chake kinachotokana na ajira yake.

Ndio,soka huku Ughaibuni na hata katika baadhi ya nchi za huko Afrika ni ajira.Ni ajira ambayo inamwezesha mtu kama Rooney kutumbukiza zaidi ya shilingi milioni 100 kwenye kamari.Pointi yangu sio uhusiano wa soka na kamari bali soka kama ajira.Tukirudi huko nyumbani,siku chache zilizopita klabu kongwe za Simba na Yanga zilichimba mkwara kuwa zingesusia ligi kuu ya Bara iwapo mgao wa mapato ungeendelea kuwanufaisha zaidi wengine badala ya wao wanaovuja jasho dakika 90.Binafsi niliguswa sana na hoja za klabu hizo japokuwa kwa bahati mbaya nasikia wakongwe hao wamenywea katika kutimiza azma yao ya kutaka “kieleweke.”Sijui kuufyata huko ni kwa vile viongozi wa klabu hizo walitoa hoja hiyo kama kutingisha kiberiti,au sijui ni ubabe wa vyama vyetu vya michezo huko nyumbani!Lakini naamini klabu hizo zilikuwa na hoja ya msingi kabisa.

Pambano lao la mwisho liliingiza milioni 98 kama sijakosea.Lakini kila klabu ikaambulia shilingi milioni 23.6 tu.Kwa kweli huo ni sawa na uonevu.Mapato hayo yalitokana na umaarufu wa klabu hizo,hivyo zenyewe ndio zilipaswa kunufaika zaidi na mapato hayo.Nadhani klabu hizo zilistahili kupata kiwango kikubwa zaidi ya hicho hasa ikizingatiwa kuwa timu hizo kwa sasa ni kama za kulipwa kutokana na kuwa na wachezaji kadhaa wa kigeni ambao mishahara yao ni ya juu.Jitihada za kuzigeuza klabu hizo kuwa kampuni zimekuwa zikikwama mara kwa mara.Kwa hiyo tofauti na klabu kubwa za huku Ughaibuni ambazo zinaendeshwa kwa mfumo wa kampuni hivyo kutotegemea sana mapato ya uwanjani,chanzo kikuu cha mapato kwa vilabu vyetu vya nyumbani ni mapato yanayotokana na watu wanaoingia uwanjani kushuhudia mechi zao.

Imenisikitisha sana kuona hoja ya klabu hizo imekufa kienyeji.Lakini sikushangaa sana kwa vile sio siri kwamba vilabu vyetu huko nyumbani vinaendeshwa kwa ubabaishaji sana.Kwanza kwa Simba na Yanga hawapaswi kutegemea mapato ya uwanjani kama chanzo pekee cha mapato.Japo hoja ya klabu hizo kugeuzwa kuwa kampuni bado ni ya muhimu sana ingawaje wenyewe wanapuuzia,vipo vyanzo vingine kadhaa vya mapato ambavyo vimetelekezwa.Kwa mfano,kwa kutengeneza kalenda 100,000 zenye picha za wachezaji ambazo zingekuwa katika ubora unaostahili na kuziuza angalau kwa shilingi 500 kila moja,klabu ingejiingizia shilingi milioni 50.Hilo linawezekana kabisa hasa kwa vile gharama za utengenezaji wa kalenda sio kubwa sana na kuna uwezekano wa kupatikana wadhamini wa kugharamia mradi wa aina hiyo.
Kwa mtizamo wangu,watu wanaopaswa kubeba lawama zaidi katika suala zima la ubabaishaji kwenye vilabu vyetu ni hao wanaoitwa wanachama.Hao ndio wanaochagua viongozi wabovu,na ni haohao ambao hawakawii kwenda mahakamani kupinga uongozi ambao wao wenyewe waliuweka madarakani.Wanang’ang’ania kujiita wanachama wakati mchango wao mkubwa katika kuendesha klabu hizo ni kwenda kwenye vyombo vya habari kutaka uongozi wa klabu ujiuzulu,au kocha hafai au wakati mwingine kusema lolote tu ili wasikike hewani.Kama kweli wanachama wa Simba na Yanga wangekuwa wenye mwamko unaostahili basi naamini wangetumia nguvu za wingi wao kuhakikisha hoja zilizotolewa na viongozi wao kuetetea maslahi ya klabu hizo zinashinda.Badala ya hoja hizo kuonekana ni ajenda binafsi za Wambura au Kifukwe zingekuwa ni hoja za klabu na wanachama wa Simba na Yanga.

Kulalamika bila kutoa ufumbuzi wa tatizo ni sawa na kulikuza tatizo.Kwa hiyo,nawajibika kutoa mchango wangu katika kupata ufumbuzi.Nadhani Tenga na wenzie wa TFF wanapaswa kuliangalia upya suala la mgao wa mapato kwa klabu,na sio kwa Simba na Yanga pekee bali vilabu vyote.Vilabu vina haki ya kudai ziada ya wanachokipata kutokana na jitihada zo uwanjani.Kuhusu uendeshaji wa vilabu,Serikali inapaswa kuingilia kati kwa kutengeneza sera ambayo haitotota fursa ya uababishaji,iwe wa viongozi au wanachama.

Alamsiki.

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.