Showing posts with label SOPHIA SIMBA. Show all posts
Showing posts with label SOPHIA SIMBA. Show all posts

27 Nov 2009


Uwajibikaji uliotukuka au kupitiliza majukumu?Who cares as long as we are kept safe.Katika magazeti mbalimbali ya hapa Uingereza kuna habari kwamba Waziri wa Usalama,Lord West,amehenyeshwa na askari baada ya kusimamishwa na kusachiwa (stop and search) kwa mujibu wa sheria za kuzuia ugaidi.Uzuri wa hawa wenzetu ni ile tabia ya "hapendwi mtu",yaani kutekeleza majukumu kwa maadili badala ya kuangalia urembo au haiba.

Sidhani kama kuna haja ya kuwakumbusha madudu ya Waziri wetu mwenye jukumu la utawala bora (which includes mapambano dhidi ya ufisadi) alivyojitokeza kuwa mama mlezi wa mafisadi.Ni katika tawala ambazo mtu anaweza kuropoka chochote na akaendelea kuitwa mheshimiwa ndipo hadi muda huu Sophia Simba anaendelea na wadhifa unaohitaji uadilifu wa hali ya juu,including umakini katika kauli.

Sasa kama askari wanaweza kudili na bosi wao kama raia mwingine iweje basi waziri wetu mwenye dhamana ya kuhakikisha mafisadi "wananyea ndoo" gerezani awe mtetezi wao mkubwa?Jibu jepesi ni kwamba Waziri Simba anapata jeuri hiyo kutoka mahala flani.Na si yeye tu bali viongozi wetu wengi wametokea kuwa na jeuri ya ajabu kwa vile wanafahamu fika hakuna wa kuwaadhibu.Kama aliyekuteua haonekani kuerwa na madudu yako why would you care kurekebisha madudu hayo?

Unfortunately,lawama nyingi zimekuwa zikielekezwa kwa watendaji wabovu badala ya kumkalia kooni aliyewapa fursa ya kuweka hadharani udhaifu wao.Ni kama katika futiboli;kocha akipanga kikosi kibovu basi lawama zaidi zitaelekezwa kwake kwa vile kikosi alichopanga hakijichagua chenyewe.Na ndio maana hivi majuzi kocha wa timu ya taifa ya Scotland alijikuta akifungashiwa virago vyake baada ya timu hiyo kufanya vibaya kwenye kampeni yake ya kushiriki Kombe la Dunia hapo mwakani.

Na ukidhani mie ni malalamishi nisiye na hoja basi SOMA HAPA uelewe chanzo cha tatizo kiko wapi.

11 May 2009


HIVI KARIBUNI,WAZIRI WA NCHI OFISI YA RAIS (MENEJIMENTI NA UTUMISHI WA UMMA),USTAADHA HAWA GHASIA,ALITOA ONYO KALI DHIDI YA WATU WANAOJIHUSISHA NA KILE ALICHOKIITA "WIZI WA NYARAKA ZA SERIKALI".NISINGEPENDA KUREJEA REACTIONS MBALIMBALI ZILIZOTOKANA NA KAULI HIYO LAKINI MMOJA YA SAUTI ZILIZOPINGA VIKALI TAMK HILO LA GHASIA NI MBUNGE WA KARATU NA KATIBU MKUU WA CHADEMA,DR WILBROAD SLAA.MWANASIASA HUYO NGULI WA MAPAMBANO DHIDI YA UFISADI ALIELEZA WAZIWAZI KWAMBA NYARAKA ZINAZOFICHA UFISADI HAZIPASWI KUWEKWA KWENYE KUNDI LA NYARAKA ZA SIRI ZA SERIKALI.DR SLAA ALIELEZA BAYANA KWAMBA PINDI AKILETEWA NYARAKA ZA AINA HIYO ATAZIMIA PASI UOGA KWA VILE NI KWA NJIA HIYO NDIO TUMEFANIKIWA KUBAINI SKANDALI KAMA ZA EPA,RICHMOND NA NYINGINEZO.


NI DHAHIRI TAMKO LA WAZIRI GHASIA LILENGA KUWATISHA WATU KAMA DR SLAA.LAKINI PIA WAZIRI HUYO ALIFANYA HIVYO KWA VILE NI MIONGONI MWA VIONGOZI WA SERIKALI WENYE DHAMANA NA MASUALA YANAYOHUSU IDARA MBALIMBALI ZA SERIKALI.


BILA KUUMAUMA MANENO,HEBU TUJIULIZE: HIVI ROSTAM AZIZ ALIPOITISHA PRESS CONFERENCE YAKE NA KUTOA "USHAHIDI" MBALIMBALI KUPIGILIA MSUMARI HOJA YAKE KUWA REGINALD MENGI (MWENYEKITI MTENDAJI WA MAKAMPUNI YA IPP) NI FISADI NYANGUMI,ALIZIPATAJE NYARAKA MBALIMBALI ZINAZOPASWA KUWA KATIKA HIFADHI YA TAASISI HUSIKA ZA SERIKALI?

ROSTAM SI MTUMISHI WA MAMLAKA YA MAPATO AU MWAJIRIWA KATIKA WIZARA YA FEDHA KIASI CHA KUWA NA "DATA" ALIZOTOA KUHUSU MENGI.NA KWA VILE MAMLAKA HUSIKA ZIMEKUWA KIMYA KUHUSU WAPI MBUNGE HUYO WA IGUNGA ALIPATA NYARAKA HIZO NI WAZI KWAMBA ALIPATIWA KWA RIDHAA YA WAHUSIKA.

WATETEZI WA ROSTAM,KUANZIA WAZIRI SOPHIA SIMBA NA KAPTENI GEORGE MKUCHIKA WAMEKUWA KIMYA KABISA KUKEMEA "HUKUMU" ALIYOTOA ROSTAM DHIDI YA MENGI TOFAUTI NA WALIVYOKURUPUKA MARA BAADA YA KIPENZI CHAO KUTAJWA KUWA NA MENGI KUWA NI FISADI PAPA.BY THE WAY,MENGI SI MTU WA KWANZA KUMTUHUMU ROSTAM KUWA NI FISADI.HIYO NI OPEN SECRET,NA KINACHOKWAZA WATU HAWA KUCHUKULIWA HATUA NI NJAA TU ZA HAO WENYE WAJIBU WA KUFANYA HIVYO ZINAZOKIDHIWA NA JEURI YA FEDHA ZA MAFISADI HAO.

SASA,SIJUI WAZIRI GHASIA ANAWEZA KUTUELEZA NINI KUHUSU WIZI WA NYARAKA ZA SERIKALI ULIOFANYWA NA ROSTAM.NAUITA WIZI KWA VILE ROSTAM SIO TRA,DPP,MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI AU TAASISI YOYOTE YA SERIKALI YENYE DHAMANA YA KUWA NA NYARAKA ZILIZOTUMIWA NA MFANYABIASHARA HUYO KWENYE "KUJENGA KESI" YAKE DHIDI YA MENGI.

SASA NAELEWA KWANINI ROSTAM ANAWEZA KU-WISH ASINGEJIBU HOJA ZA MENGI KWANI WATAPOFIKA MAHAKAMANI ANAPASWA KUULIZWA YEYE ALIKUWA NA NYARAKA HIZO KAMA NANI?ALIZIPATAJE?NA JE KUWA NAZO SIO KOSA (KWA KUREJEA "MKWARA" WA WAZIRI GHASIA?

NA HIYO NI NJE YA TAARIFA ZA KUAMINIKA KUWA NYINGI YA DATA ALIZOTUMIA ROSTAM NI "MAKANJANJA" (FAKE DATA) AMBAPO WAJANJA WA MJINI WALIPOSIKIA KUNA TENDA YA FEDHA NYINGI YA KUWEZESHA KUPATIKANA KWA INCRIMINATING EVIDENCE DHIDI YA MENGI WAKACHANGAMKIA TENDA HIYO LAKINI KATIKA HALI YA UFISADI.WHY NOT,KUMFISADI FISADI NI SAWA KABISA NA KULIPA KWA NOTI BANDIA MANUNUZI YA CHENI ILIYOTENGENEZWA KWA DHAHABU FEKI.


MWISHO,NAPENDA KUSISITIZA KWAMBA SINA CHUKI NA ROSTAM AU MTANZANIA YEYOTE MWENYE ASILI YA NJE YA NCHI.ILA SIFICHI UKWELI KWAMBA NINA ZAIDI YA CHUKI,HASIRA,DUA BAYA (NA MENGINE NISIYOWEZA KUTAJA HAPA) DHIDI MAFISADI.UTETEZI WA KIPUUZI WA MAFISADI UMEKUWA KWENYE VITU KAMA RANGI,DINI,KABILA,NK.MTAKUMBUKA MKURUGENZI WA IPC,EMMANUEL OLE NAIKO ALIZONGWA KUHUSU KWANINI ALITOA KIBALI CHA UWEKEZAJI KWA KAMPUNI YA KITAPELI YA RCHMOND,KIMBILIO LAKE KUU LILIKUWA UKABILA.ETI "NAANDAMWA KWA VILE NATOKA ENEO MOJA NA LOWASSA"!

LEO HII AKINA ROSTAM,MANJI,SOMAIYA,JEETU NA SUBASH WANATAKA KUTUAMINISHA KUWA TUHUMA DHIDI YAO ZINACHANGIWA NA "UTANZANIA" WAO WENYE ASILI YA NJE YA NCHI.HUU NI UTETEZI MUFILIS NA NI WA KIFISADI KAMA WANAVYOTUHUMIWA.HIVI WANATAKA KUTUAMBIA KUWA TULIPOPAMBANA NA MKOLONI,MJERUMANI NA MWINGEREZA TULIKUWA WABAGUZI WA RANGI?

4 May 2009


MWANASIASA MAKINI ANAPASWA KUCHUNGA ULIMI WAKE.ANAPASWA PIA KUELEWA KWAMBA LOLOTE LITOKALO MDOMONI MWAKE LAWEZA KUTAFSIRIWA KUWA NI KAULI YA SERIKALI.

KWA MAANA HIYO,KAULI ZA SOPHIA SIMBA NA GEORGE MKUCHIKA KUMTETEA ROSTAM AZIZ WAZIWAZI ZIMEWAFANYA WANANCHI WENGI KUWAONA MAWAZIRI HAO KAMA VIBARAKA WA ROSTAM,MFANYABIASHARA NA MWANASIASA ANAYEHUSISHWA NA TUHUMA LUKUKI ZA UFISADI.

SOPHIA SIMBA NA MWENZIE MKUCHIKA WALILIPUKA KUMTETEA ROSTAM PASIPO KUELEWA KWAMBA MHINDI HUYO NAE ALIKUWA ANA MPANGO WA KUJIBU SHUTUMA ZA MENGI.NA KATIKA KUJIBU SHUTUMA HIZO,ROSTAM AMEJIGAMBA KUWA MENGI AMEKEMEWA NA WAZIRI SIMBA NA MKUCHIKA.

HIVI WATU WAZIMA HAWA NA AKILI ZAO HAWAONI KUWA WAMEDHALILISHWA?YAANI INA-SOUND AS IF WALITUMWA NA ROSTAM IN THE FIRST PLACE KABLA YA MTUHUMIWA HUYO WA UFISADI KUITISHA PRESS CONFERENCE.MAWAZIRI WAZIMA WANA-ACT AS IF NI SPOKESPERSONS WA,SIO SERIKALI,BALI MHINDI FLANI MWENYE FEDHA?

BAADA YA PRESS CONFERENCE YA ROSTAM HAPO JANA,BAADHI YA WATU WANAULIZA "YUKO WAPI SOPHIA SIMBA?YUKO WAPI MKUCHIKA?" WAKITARAJIA MAWAZIRI HAO WATAMTENDEA HAKI MENGI KWA KUMKEMEA ROSTAM.HAWANA JEURI WALA UBAVU HUO.SIMPLY BECAUSE KAMA KUITWA FISADI PAPA KWA MHINDI HUYU KULIWAKURUPUA KUROPOKA WALIYOSEMA,NI DHAHIRI KUWA ROSTAM AKIKOHOA TU NA WAO WANALIPUKA.UJASIRI HUO WA KUMKEMEA WATOE WAPI.NA KATIKA SIASA HIZI ZA KIMAFIA ZILIZOLETWA NA WANAMTANDAO,MWANASIASA YEYOTE ATAKAYETHUBUTU KUMGUSA THE DON,MR UNTOUCHABLE,BASI NAYE ATACHAFULIWA.

YOTE HIYO NI TAMAA YA MADARAKA.WAKO RADHI KUUZA UTU WAO KWA AJILI YA KUMPIGIA MAGOTI FISADI FLANI AWASDAIDIE KUFIKIA MALENGO YAO.NA SI SOPHIA SIMBA NA MKUCHIKA PEKEE,KUNA WENGI TU WANAOWAOGOPA MAFISADI KWA VILE NDIO WALIOFADHILI HARAKATI ZAO ZA KISIASA.

HALAFU HAWA NDIO WA KUWATEGEMEA KUTULETEA MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA?LABDA MAISHA BORA KWA MAFISADI NA VIBARAKA WAO!

SHAME ON THEM!


27 Apr 2009


KUNA MAMBO YANAYOTOKEA HUKO NYUMBANI YANAKERA KUPITA MFANO.HIVI HAWA WATANZANIA WENZETU WALIOKABIDHIWA DHAMANA YA KUTUONGOZA (TUKIAMINI KABISA KUWA WANA UPEO MZURI TU WA KUTAFAKARI MAMBO) WANAWEZAJE KUONGEA MAMBO YA AJABU NAMNA HII?ANYWAY,HEBU SOMA KWANZA HABARI HUSIKA KISHA TUENDELEE KUJADILI



* Waziri Sophia Simba asema Mengi kachemsha
*Mkuchika naye asema wanamchunguza

Ramadhan Semtawa na Leon Bahati

MAWAZIRI wawili, Sophia Simba na George Mkuchika jana walimshambulia mfanyabiashara maarufu nchini, Reginald Mengi ambaye wiki iliyopita alitangaza majina ya wafanyabiashara watano wenye asili ya Kiasia, akisema ni mafisadi waliokubuhu.

Simba, ambaye ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Utawala Bora) na Mkuchika, Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo walisema mfanyabiashara huyo wa jijini Dar es salaam "amechemsha".

Mengi alitangaza majina ya wafanyabiashara hao Alhamisi iliyopita akisema ni kati ya watu wasiozidi 10 ambao alidai wanaifilisi nchi na kutaka wadhibitiwe mapema kabla hawajaitingisha na kuiyumbisha nchi. Hata hivyo, Mengi, ambaye alidai katika taarifa yake kuwa juhudi za Rais Jakaya Kikwete zinakwamishwa na watu hao, hakueleza jinsi watano hao wanavyoitafuna nchi zaidi ya kusema kuwa wanatorosha fedha wanazozipata 'kifisadi'.

Jana, kwa nyakati tofauti jijini Dar es Salaam mawaziri hao wawili walitoa kauli za kumshambulia mwenyekiti huyo mtendaji wa makampuni ya IPP, kauli ambazo zinadokeza mtazamo wa serikali katika mjadala unaoendelea wa vita dhidi ya ufisadi na vinara wake.

Waziri Simba, ambaye wizara yake pia inawajibika katika vita dhidi ya ufisadi, alisema: "Kakosea... watoto wa mjini wanasema kachemsha." Simba alitoa msimamo huo jijini Dar es Salaam jana muda mfupi baada ya kufungua semina ya wadau wa vyama vya siasa kuhusu namna ya kuiboresha Sheria ya Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma ya mwaka 1995.

Simba alisema Mengi hana mamlaka hayo ya kutaja watu wanaotuhumiwa kwa ufisadi.

Kabla ya kujibu swali kuhusu kitendo cha Mengi, ambaye anamiliki televisheni ya ITV na kituo cha redio cha Radio One Stereo, kutaja majina ya watu hao aliowaita
mafisadi papa, Simba alihoji: " Hapa kuna mtu wa ITV?." Baadaye alisema: "Sikilizeni, kwanza kitendo alichokifanya Mengi si sahihi, kakosea hawezi kuhukumu watu, mamlaka hayo anatoa wapi?"

Simba, huku akionekana kama mtu ambaye alikuwa akitafuta jukwaa kuzungumzia suala hilo, alisema Mengi amekosea kwa kuwa baadhi ya watu aliowataja wana kesi mahakamani."Anahukumu watu," alisema. "Kuna mtu kama Jeetu (Patel) ana kesi mahakamani (EPA), sasa unapokuja kusema ni fisadi wakati mahakama haijathibitisha, unakuwa na maana gani.

"Kwanza kwanini awatuhumu wafanyabiashara wenzake tu, ina maana si ana nia mbaya nao."

Alisema Mengi amechukua uamuzi huo kama vile serikali, wakati serikali ipo siku zote na imekuwa ikifanya kazi zake kwa umakini kwa kufuata misingi ya sheria.

"Serikali ipo na inafanya kazi kwa misingi ya sheria, sasa yeye kukaa na kutangaza watu nasema si sahihi kabisa. Mahakama pekee ndiyo inaweza kumtia mtu hatiani, lakini huwezi kuhukumu watu kama hakuna mamlaka."

Waziri Simba, ambaye pia ni mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake wa CCM (UWT), alisema Mengi hapaswi kutumia vyombo vyake vibaya. "Asitumie vyombo vyake kufanya atakavyo yeye. Huwezi kukaa katika chombo chako na kuanza kuhukumu watu. Kila mtu akifanya hivyo itakuaje," alihoji.

Akiongea na Mwananchi baada ya kupata taarifa za kauli ya Simba, Mengi alisema: "Namuombea kwa Mwenyezi Mungu na kwa maskini wa Tanzania ili wamsamehe kwa sababu hajui anenalo." Mengi hakutaka kuzungumza zaidi kuhusu hatua hiyo ya Mama Simba.

Naye Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, George Mkuchika aliwaambia waandishi wa habari kuwa serikali itamchukulia hatua za kisheria Mengi iwapo itabainika alikiuka taratibu na kanuni za nchi kwa kutangaza majina ya watu anaowatuhumu kwa ufisadi
.

Mkuchika alisema jijini Dar es Salaam jana kwa sasa serikali inafanya uchunguzi juu ya suala hilo na itatumia mikanda ya video pamoja na maelezo ya kimaandishi aliyoyatoa Mengi siku alipokutana na waandishi wa habari.

"Tumekusudia kupata ule mkanda wa video, pia tusome maelezo yake ya kimaandishi... tukigundua kuna mahala ambapo sheria haikuzingatiwa, (Mengi) atachukuliwa hatua," alisema Mkuchika.

Mkuchika alisema serikali imepokea malalamiko mengi kutoka kwa watu wengi, wakishutumu hatua iliyochukuliwa na Mengi, ambaye pia anamiliki viwanda vya vinywaji.

Bila kutaka kuwataja majina, Mkuchika alisema miongoni mwa walalamikaji, wapo walioeleza kuwa vyombo vya habari vya mfanyabiashara huyo havikuwatendea haki watuhumiwa waliotajwa kuwa ni mafisadi wakuu.

Alisema ni kutokana na vyombo hivyo kuwataja majina watuhumiwa bila ya kuwapa fursa ya kujibu madai dhidi yao. Waziri Mkuchika alipotakiwa kueleza siku ambayo uchunguzi huo utakamilika, alijibu wananchi wanapaswa kuwa watulivu kwa sababu serikali ikimaliza kuchunguza, itawatangazia yale waliyobaini.

Hii ni mara ya pili katika kipindi cha miezi takribani mitatu kwa Mengi kuingia katika mvutano na serikali baada ya kuvutana mapema mwaka huu na Waziri wa Mambo ya Ndani, Lawrence Masha kutokana na kutangaza kuwa kuna mipango ya kumfilisi na kumuua.

Mengi pia amewahi kujikuta katika malumbano na watendaji wa serikali hasa na waziri wa zamani wa nchi, ofisi ya rais (utawala bora), Wilson Masilingi alipotoa tuhuma kuwa suala la utoaji zabuni ya ununuzi wa hoteli ya Kilimanjaro, hivi sasa inajulikana kama Kilimanjaro Kempiski, kulikuwa na kitu alichokiita "mchezo mchafu". Suala hilo liliamsha malumbano makali, lakini liliishia hewani.

Katika tuhuma za wiki iliyopita, Mengi aliwahusisha wafanyabiashara hao watano na kashfa za wizi wa fedha kwenye Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA), utoaji zabuni ya ufuaji umeme wa dharura kwa kampuni ya Richmond Development (LLC) na uuzwaji wa jengo la Mfuko wa Hifadhi ya Taifa ya Jamii (NSSF).

Mengi, ambaye kituo chake cha televisheni cha ITV kiliwahi kuendesha mchezo mkubwa wa bahati nasibu ya Jackpot Bingo, pia aliitaja Bahati Nasibu kuwa katika tuhuma hizo, pamoja na mradi wa makaa ya mawe wa Mchuchuma.


CHANZO: Mwananchi


HALAFU TUKISEMA UFISADI NI MIONGONI MWA SERA ZA CCM TUTAITWA WACHOCHEZI?CHADEMA WALIPOTOA LIST OF SHAME CCM,KAMA KAWAIDA YAKE,IKAJA JUU KUDAI HIZO NI POROJO ZA KISIASA.WENGINE WAKAENDA MBALI ZAIDI NA KUTISHIA KUWAPELEKA AKINA SLAA MAHAKAMANI KWA MADAI YA "KASHFA".HADI LEO HAKUNA HATA MMOJA WAO ALIYEKWENDA MAHAKAMANI,NA SANASANA BAADHI YA WATUHUMIWA HAO KWA SASA WAKO MAHAKAMANI WAKITUHUMIWA KUHUSU YALEYALE YALOTAJWA KWENYE LIST OF SHAME.


TATIZO LA MAWAZIRI WOTE WAWILI SIO MANJI AU THE PATELS.NI MR UNTOUCHABLE.HUYU AKIGUSWA BASI NDIO KAMA UMEPIGA LUMUMBA,HQ YA CCM.HAIHITAJI UPEO WA JUU KUBAINI KUWA WANACHOONGEA MAWAZIRI HAO WAWILI NI SAWA NA SELF-DENIAL.YAANI TUKIMJUA MWIZI TUSIMUITE MWIZI MPAKA AFIKISHWE MAHAKAMANI?TUTAMFIKISHAJE HUKO PASIPO KUMTUHUMU IN THE FIRST PLACE?


NA KWANINI ALALAMIKE WAZIRI SIMBA NA MKUCHIKA NA SIO HAO WALIOTAJWA NA MENGI?WAMETUMWA AU WANATUMIWA?WASITUFANYE WATOTO KUHUSU HABARI ZA HAO MAPAPA WA UFISADI KUFIKISHWA MAHAKAMANI KWA VILE HILO HALIWEZEKANI.KWANI KUNA SABABU NYINGINE INAYOSABABISHA KUSUASUA KUWATAJA WAMILIKI WA KAGODA ZAIDI YA UKWELI KUWA AMONG THE WAMILIKI NI MR UNTOUCHABLE?


AH,SIJUI MAMBO HAYA YATAENDELEA HADI LINI!

26 Dec 2008

CHAGUZI NDANI YA CCM HAZIISHIWI VIOJA.RUSHWA IMETAPAKAA MNO NDANI YA CHAMA HICHO KANA KWAMBA NI SEHEMU YA KATIBA YAKE.SIO MATUSI KUAMINI KWAMBA PENGINE INGEKUWA RAHISI ZAIDI KWA CCM KUAHIDI KUENDELEZA LIBENEKE LA RUSHWA KWENYE MANIFESTO YAKE YA 2005 KULIKO AHADI ZA MAISHA BORA,MAHAKAMA YA KADHI,NK MAMBO AMBAYO HADI SASA YAMEENDELEA KUWA AHADI ZISIZOTEKELEZEKA.NI WAZI,RUSHWA HUZAA VIONGOZI WABOVU,MAFISADI NA WABABAISHAJI.HABARI MBAYA NI KWAMBA HAKUNA DALILI ZA KUISHA KWA GONJWA HILO HATARI NDANI YA CHAMA TAWALA.TAASISI ZA UMMA ZA KUKABILIANA NA RUSHWA ZINAISHIA KUALIKWA TU KWENYE CHAGUZI "KUZUIA RUSHWA" NA VIONGOZI WAANDAMIZI WA CHAMA HICHO WAMEISHIA KUPIGA KELELE TU (SINA HAKIKA KAMA NI ZA DHATI) KUHUSU RUSHWA KWENYE CHAGUZI,LAKINI SOTE TUNAJUA KWAMBA KELELE ZA CHURA HAZIMZUII NG'OMBE KUNYWA MAJI.ENEWEI,HEBU CHEKI MKASA HUU HAPA CHINI KISHA SOMA HITIMISHO LANGU BAADA YA HABARI HII:
Zikiwa zimesalia siku 14 kufika siku ya uchaguzi wa viongozi wa ngazi ya taifa wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), mambo si shwari katika mchakato wa kumpata mwenyekiti wake. 

Uchaguzi huo unatarajiwa kufanyika mjini Dodoma Januari 7, mwakani ambapo nafasi ya uenyekiti itagombewa na Janet Kahama, Sophia Simba na Joyce Masunga. 

Hali hiyo, ambayo inazidi kuipaka matope CCM, imedhihirika baada ya mgombea wa nafasi ya Janeth Kahama kuwasilisha rasmi malalamiko kwa Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete, akimtuhumu mpinzani wake, Sophia Simba kwamba amewahonga wajumbe wote wa Mkutano Mkuu rushwa ya Sh. 100,000 ili wampe kura. 

Mbali na tuhuma za rushwa, Simba, ambaye ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Utawala Bora), anatuhumiwa pia na Kahama kuwa yeye na wapambe wake wamekuwa wakiitumia Ikulu kuwaomba kura wajumbe wa Mkutano Mkuu. 

Kahama, ambaye ni Mbunge wa Viti Maalum (CCM), amewasilisha malalamiko hayo kupitia barua yake yenye kumbukumbu Na. JBK/01/08 ya Desemba 20, mwaka huu, iliyopelekwa kwa Rais Kikwete, Ikulu, jijini Dar es Salaam. 

Nakala ya barua hiyo, ambayo Nipashe inayo, imepelekwa kwa Katibu Mkuu wa UWT Taifa na Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba. 

Makamba alipoulizwa na Nipashe juzi jioni kama amepokea nakala ya barua hiyo, alithibitisha kuipokea. 
Simba anadaiwa kutoa hongo hiyo kupitia kadi alizochapisha kwa lengo la kuwatakia heri ya Mwaka Mpya wajumbe wa Mkutano Mkuu wa UWT Taifa. 

Kadi hizo, ambazo zinadaiwa kusambazwa na Diwani wa Kata ya Ilala, Moshi Kondo, zina picha, jina na saini ya Waziri Simba, kalenda ya Mwaka Mpya wa 2009 na nembo ya CCM. 

Barua hiyo yenye kichwa cha habari kisemacho: `Yah: Malalamiko dhidi ya Mhe. Sophia Simba kugawa vipeperushi mikoani`, Kahama anamueleza Mwenyekiti Kikwete kama ifuatavyo: 

``Kwa heshima ya pekee, nakuomba uhusike na mada ya barua hii kama inavyosomeka hapo juu. Mheshimiwa Mwenyekiti, kama unavyofahamu, Jumuiya yetu ya UWT hivi sasa ipo katika mchakato wa uchaguzi wa viongozi wa ngazi ya taifa unaotarajiwa kufanyika mapema mwakani.`` 

``Mimi nikiwa mmoja wa wagombea wa nafasi hiyo ya Mwenyekiti wa Taifa wa UWT, natambua kuwa wagombea wote tulizuiwa na vikao vya UWT Taifa kutoa vipeperushi vya aina yoyote kwa minajili ya kujinadi kwa wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Taifa wa UWT.`` 

``Lakini, ajabu ni kwamba, mgombea mwenzangu, Bi Sophia Simba amechapisha kalenda na kadi za `Heri ya Mwaka Mpya` zenye picha yake na nembo ya CCM na kuzisambaza kwa wajumbe wote wa Mkutano Mkuu wa UWT Taifa nchi nzima, ndani zikiwa na kitita cha Sh. 100,000 (kwa kila kadi).`` 

``Mheshimiwa Mwenyekiti, nalazimika kukuandikia waraka huu ili kukupa angalizo juu ya suala hilo hasa ikizingatiwa kuwa Mheshimiwa Sophia Simba ni Waziri katika ofisi yako mwenye dhamana ya Utawala Bora.`` 

``Hivyo hatua yake na nembo ya CCM, inakwenda kinyume na kanuni za uchaguzi za CCM, kipengele cha Miiko ya Kuzingatiwa wakati wa Shughuli za Uteuzi na Uchaguzi`, ibara ya 33 kifungu kidogo cha 14 kinachosema: `Ni mwiko kutumia makaratasi ya kampeni nje ya utaratibu wa chama au kutumia vishawishi vya aina yoyote ile kwa minajili ya kupata kura.`` 

``Je, hatua hii ya Mheshimiwa Simba kuchapisha nyaraka hizo zenye picha yake na nembo ya CCM na kuzitawanya nchi nzima, si uvunjaji wa makusudi wa kanuni hizo za uchaguzi za CCM tena kipindi hiki cha kuelekea kwenye Uchaguzi Mkuu wa UWT?`` 

``Je hatuoni kwamba hatua yake hiyo ambayo haijakemewa mpaka sasa ni kielelezo kingine cha ubabe na matumizi mabaya ya madaraka yake kama Waziri tena mwenye dhamana ya Utawala Bora? 

Nasisitiza hili kwa sababu Mheshimiwa Simba na wapambe wake wamekuwa wakipita mikoani na kupotosha wapigakura kuwa yeye ndiye chaguo la Ikulu.`` 

``Mheshimiwa Mwenyekiti, nawasilisha kwako waraka huu wenye malalamiko haya ili uweze kujua nini kinaendelea na kuchukua hatua kwani kama kitaachwa, kinaweza kujenga matabaka ndani ya UWT na mpasuko usio wa lazima ndani ya chama chetu, hasa pale hisia za mgombea mmoja kuandaliwa mazingira ya ushindi dhidi ya wenzake zinapoanza kujengwa.`` 

``Naambatanisha moja ya vipeperushi hivyo vya Mheshimiwa Simba vilivyosambazwa mikoani kinyume na utaratibu nilioueleza hapo juu.`` 

Makamba alipoulizwa na Nipashe juzi, licha ya kukiri kupokea nakala ya barua hiyo ya Kahama, alimtaka mwandishi kama ana swali lolote kuhusiana na suala hilo, akamuulize Rais Kikwete kwa vile ndiye aliyeandikiwa barua hiyo. 

``Mtafute Mwenyekiti wa CCM, yeye ndiye aliyeandikiwa barua, aliyeandikiwa ndiye anayejibu. Mimi nimepewa nakala, anayepewa nakala, anaarifiwa tu,`` alisema Makamba. 

Nipashe ilipowasiliana na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Ikulu, Salvatory Rweyemamu, alisema kwa vile malalamiko ya Kahama yanahusiana na Chama, anayepaswa kujibu suala hilo ni Katibu Mkuu. 

Baada ya Makamba kuulizwa tena, alisema: ``Mimi sina cha kusema, sijaisoma (hiyo barua), sijajua maudhui. 

Nitakapoisoma na kujua maudhui, nitatoa maoni yangu.`` 

Kahama alipoulizwa na Nipashe jana kama barua hiyo ndiye aliyeiandika, hakukiri wala kukanusha, badala yake alisema kwa sasa hawezi kuzungumza lolote kwa vile kipindi hiki ni cha sikukuu ya Krismasi, ambayo yeye kama Mkristo anapaswa kuitukuza. 

``Sina comments (maoni) kabisa kabisa, mpaka nionane na Katibu Mkuu. Pia mimi ni Mkristo na kipindi hiki ni cha Krismasi,`` alisema. 

Naye Diwani wa Kata ya Ilala, Moshi Kondo, alipoulizwa juzi, alikataa kuzungumzia suala hilo, badala yake alimtaka mwandishi akamuulize Simba. 

``Kwani Sophia Simba mimi ni nani kwake?`` alihoji Kondo, ambaye alipojibiwa na mwandishi kuwa ``Simba anadaiwa kuwa ni mtu wake wa karibu``, alisema: ``Nenda kamuulize Simba.`` 

Tangu juzi hadi jana jioni Nipashe ilimtafuta Simba bila kumpata na baadaye kuelezwa na mmoja wa wanafamilia yake kuwa yuko safarini Malaysia. 

CHANZO:Nipashe

WAKATI MAMA KAHAMA AMETUMIA HAKI YAKE YA MSINGI KAMA MGOMBEA NA MWANANCHAMA WA UWT/CCM KUWASILISHA MALALAMIKO YAKE KWA MWENYEKITI WA CCM TAIFA (JK),NADHANI ANGEWEZA PIA KUWASILISHA TUHUMA HIZO POLISI AU TAKUKURU.HIVI KUTOA RUSHWA SI NI KOSA LA JINAI?JE MAMA KAHAMA YUKO MORE CONCERNED NA RUSHWA HIYO KUATHIRI NAFASI YAKE YA KUCHAGULIWA KULIKO UKWELI KWAMBA MTUHUMIWA (SOPHIA SIMBA) SIO WAZIRI TU BALI NI WAZIRI MWENYE DHAMANA YA UTAWALA BORA (ISOMEKE MAPAMBANO DHIDI YA RUSHWA)?


Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.