Showing posts with label TALIBAN. Show all posts
Showing posts with label TALIBAN. Show all posts

30 Aug 2014

Kikundi cha kigaidi cha Taliban huko Aghanistan kilikuwa kipo tayari kumwachia huru Sajenti wa Jeshi la Marekani Bowe Bergdahl ili kumpata mwanamama huyu. Magaidi wa ISIS nao walikuwa wapo tayari kumwachia mwandishi wa habari wa Marekani waliyemuua kwa kumkata kichwa, James Foley iwapo mwanamama huyo angeachiwa huru. Je kwanini takriban kila kikundi kikubwa cha kigaidi kinamhitaji Aafia Siddiqui?

Miaka miwili iliyopita, maafisa waandamizi wa masuala ya usalama wa taifa nchini Marekani walipokea 'ofa' ya kushangaza kutoka Pakistani. Iwapo Marekani wangekubali kumwachia mwanamke mmoja anayetumikia kifungo kirefu huko Texas kwa kosa la jaribio la kuua, basi Sajenti Bowe Bergdahl aliyetekwa na Taliban tangu mwaka 2009 angeachiwa huru.

Kwa mujibu wa taarifa za kiusalama, Rais Barack Obama na maafisa wake walikataa 'ofa' hiyo. Kumwachia mwanamke huyo, Bowe Bergdahl kunekinzana na msimamo wa Marekani wa kutofiki amakubaliano na magaidi. Kadhalika, kumwachia huru mwanamke huyo kungemrejesha uraiani mtu hatari kwa usalama.

Siddique, mwenye umri wa miaka 42, na anayefahamika kwenye anga za kupmbana na ugaidi kama 'Lady al-Qaeda' ameshahusishwa na mmoja wa magaidi wahusika wa  mashambulizi ya kigaidi ya Septemba 11 Khalidi Sheikh Mohammed, na wakati flani alikuwa katika orodha ya magaidi wanaosakwa zaidi (most wanted terrorist list).

Gaidi huyo wa kike alipata elimu yake katika chuo kikuu kinachoheshimika sana duniani cha M.I.T na ana shahada ya uzamifu (PhD). Mwaka 2008, alikamatwa akiwa na kemikali ya Sodium Cyanide, pamoja na nyaraka za jinsi ya kutengeneza silaha za kemikali, mabomu ya kusababisha madhara makubwa (smart bombs) na jinsi ya kuitumia Ebola kama silaha. Maofisa wa Shirika la Upelelezi la FBI walipojaribu kumhoji, mwanamke huyo alichukua silaha na kufyatua risasi.

Japo Marekani haikulipa uzito wazo la kubadilishana mwanamke huyo na 'mateka waliokuwa mikononi mwa magaidi,' Siddique amekuwa turufu muhimu kwa magaidi kila linapokuja suala la 'kubadilishana mateka' mbalimbali wa Marekani na Ulaya walio mikononi mwa magaidi.

Jumanne iliyopita, kikundi cha kigaidi cha ISIS kilidai gaidi huyo wa kike aachiwe huru ili nao wamwachie huru mwanamke mmoja wa Kimarekani aliyetekwa huko Syria alipokuwa akifanya kazi katika shirika la misaada ya kibinadamu. Maafisa wanaamini kuwa ISIS inawashikilia mateka angalau Wamarekani wengine wanne, ikiwa ni pamoja na mwandishi wa habari Steven Sotloff. Magaidi hao wanataka kulipwa Dola za Marekani milioni 6.6 ili wamwachie huru mwanamke huyo mtumishi wa shirika la misaada ya kibinadamu ambaye ndugu zake wameomba jina lake lihifadhiwe.

Wakati Ikulu ya Marekani imekuwa ikikataa katakata wazo la kumwachia huru mwanamke huyo gaidi ili kuwezesha kuachiwa huru kwa mateka wa nchi hiyo waliopo katika mikono ya magaidi, "Twafahamu kuna wanaotengeneza mazingira katika 'Wizara ya Ulinzi' ya kuangalia uwezekano wa kubadilishana mateka kwa kumtumia Siddique."

Mjadala mkubwa uliibuka baada ya kuchinjwa kwa Foley kuhusu aidha kulipa fedha kwa magaidi au kuwaachia wafungwa kama wanavyodai magaidi hao. Marekani, tofauti na nchi nyingi za Ulaya, huwa hailipi fedha kwa ajili ya kuachiwa huru raia wake waliotekwa. Na inaelezwa kuwa hiyo ni miongoni mwa sababu zinazowavunja moyo magaidi kuwateka nyara Wamarekani kwa minajili ya kudai fidia ili mateka hao waachiwe huru, kwa mujibu wa mtaalam mmoja wa ugaidi.

Siddique ni kama 'celebrity' flani nchini Pakistan, ambapo kifungo chake mwaka 2010 kilipelekea maandamano nchini humo (Pakistan). Matokeo ya kifungo cha Siddique yalikuwa hahabari zilizoongoza katika magazeti yote makubwa.

Hukohuko Pakistan, kikundi kijiitacho 'Brigedia ya Aafia Siddique'kimeshafanya mashambulizi kidhaa dhidi ya serikali ya nchi hiyo kama upinzani na malalamiko yao dhidi ya wanachokiona kama kifungo kisicho cha haki kwa mwanamke huyo hatari.

CHANZO: Jarida la Foreign Policy



8 May 2009

Pakistan's army declared a "full-scale" offensive against Taliban insurgents holed up in the Swat valley today as warplanes pounded militant bunkers and caused thousands more residents to flee.The fighting was concentrated in the main town, Mingora, where an estimated 4,000 Taliban fighters are heavily dug in. Artillery and helicopter gunships battered militant-held buildings, while the Taliban planted mines across the city in expectation of a major ground offensive... continue

6 Jan 2008


Nimesoma makala moja ndefu katika toleo la leo la Sunday Times (la hapa Uingereza) kuhusu hali ilivyo kwa majirani zetu wa Kenya.Kwa kweli inatisha na kusikitisha.Mauaji na ubakaji ni miongoni mwa unyama unaozidi kushamiri nchini humo.Lakini inasikitisha zaidi kuona hata watoto wadogo wa miaka 12 wanakumbwa na ukatili huo.

Lakini kilichonikurupusha kuandika makala hii ni habari kwamba vurugu hizo zinahusisha pia makundi mawili hatari:Mungiki (la Wakikuyu) na Taliban (la Waluo).Kwa namna inavyoonekana,makundi haya ni sawa na magenge ya wahalifu ambayo kwao vurugu za aina yoyote ni sawa na msimu wa mavuno.Inaelezwa kwamba Mungiki wamekuwa wakiwatahiri kwa nguvu "mateka" wao wa Kiluo (kwa mila zao,wanaume wa Kiluo huwa hawatahiri) huku Taliban wakijibu mashambulizi kwa kuwafyeka mapanga Wakikuyu.

Inatisha na kusikitisha kusikia kwamba watu kadhaa waliuawa kinyama kwa kuchomwa moto wakiwa ndani ya kanisa walilojihifadhi.Kwa nchi ambayo asilimia kubwa ya wakazi wake ni Wakristo,hiyo ni ishara kwamba chuki kati ya makundi yanayopingana zimevuka nguvu za mshikamano wa jamii kama dini na utaifa,na inaelekea kinachoangaliwa sasa ni ukabila tu.

Haihitaji ujuzi wowote wa mambo ya uchaguzi kubaini kwamba Kibaki amejirejesha kwa nguvu madarakani.Hivi anajisikiaje wakati yeye yupo Ikulu,mamia ya Wakenya wenzake,ikiwa ni pamoja na Wakikuyu wenzie,wanapoteza maisha yao kila siku huku wengine wanaishi kwa hofu na mashaka ya kuuawa,kubakwa,kutahiriwa kwa nguvu na udhalilishaji mwingine usiopaswa kufanyika katika jamii yoyote ile iliyostaarabika.Damu inayomwagika kila kukicha (sambamba na mateso yanayowakuta wananchi wasio na hatia) iko mikononi mwa Kibaki.

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.