Showing posts with label TANESCO. Show all posts
Showing posts with label TANESCO. Show all posts

28 Jun 2011

Pichani ni jengo la "Tanesco ya Senegal",Senelec,lililoshambuliwa na waandamanaji wenye hasira kuhusu kukatika umeme mara kwa mara jijini Dakar.Akina sie tunashambulia kwa matusi,lawama,na manung'uniko huko Twitter na Facebook!!!

Sio siri kwamba upole wa Watanzania ni miongoni mwa sababu kuu za mabaya mengi yanayotokea huko nyumbani.Na kama kuna suala linalosikitisha kuhusu mwamko wa Watanzania kudai haki zao ni tatizo la mgao wa umeme sambamba na ubabaishaji wa hali ya juu wa serikali na Tanesco katika kushughulikia tatizo hilo.

Sasa hivi,mitandao ya jamii ya Twitter na Facebook imetawaliwa na malalamiko ya Watanzania wengi kuhusu mgao.Wengine wanaishiwa na uvumilivu na kuishia kuitukana Tanesco,kana kwamba matusi hayo yatarejesha umeme.Wengine wamekuwa wakipeana taarifa kuhusu maeneo ambayo "Tanesco wameshachukua umeme wao".Kwa kifupi,kinachosikika zaidi ni manung'uniko,lawama,vilio na hata matusi.Cha kusikitisha ni kwamba hakuna dalili yoyote kutafsiri malalamiko hayo into vitendo.

Sio kama nawasimanga ndugu zangu.I really feel you lakini ukweli mchungu ni kwamba kelele zenu haziwezi kumaliza tatizo hilo.Kinachohitajika ni kudai haki kwa nguvu.By "nguvu" simaanishi vurugu bali kuchukua hatua za makusudi kuhakikisha serikali na Tanesco wanawajibika.Mgao utaendelea milele iwapo Watanzania wataishia kulalamika tu.Hakuna miujiza katika kuleta mabadiliko.Either watu wajitoe muhanga kudai haki yao kama walipakodi au waendelee kuteswa na mgao.

Bahati nzuri,wenzetu nchini Senegal wanatuonyesha namna gani matatizo yanayoathiri nchi yanavyoshughulikiwa na umma.Nisieleze kwa maneno yangu bali naomba usome habari ifuatayo:

Associated Press

DAKAR,Senegal: Maelfu ya waandamanaji wameingia mitaani katika mji mkuu wa Senegal kupinga kukatika umeme mara kwa mara.Maandamano hayo ni tukio la tatu la vurugu nchini humo ndani ya wiki.

Wananchi wenye hasira walivamia ofisi za shirika la umeme la Senelec,jijini Dakar baada ya maandamano ya kupinga kukatika kwa umeme kwa muda mrefu.

Watu kadhaa walishambulia majengo ya serikali hapo jana.Wanadaia kuwa baadhi ya maeneo yamekuwa yakikosa umeme kwa masaa 24 au zaidi.

Kama ilivyo kawaida kwa vyombo vya dola barani Afrika,askari wa kikosi cha kutuliza ghasia walipambana na waandamanaji kwa kutumia maji na mabomu ya machozi.Msemaji wa polisi hakuweza kuthibitisha idadi ya waliojeruhiwa katika ghasia hizo.

Alhamisi iliyopita,vurugu kubwa ziliibuka kupinga mpango wa mabadiliko ya katiba ya nchi hiyo

Uchaguzi ni wenu Watanzania wenzangu.Mwendelee kulalama huku Serikali na Tanesco wakiendelea kuwasanifu (mgao wa umeme hauwagusi kwa vile aidha wana jenereta zinazojazwa mafuta na hela yako mlipakodi au maeneo wanayoishi hayakatwi umeme kutokana na unyeti wake) AU muige mfano wa wenzetu wa Senegal.Hakuna njia ya mkato katika kutatua matatizo sugu yanayosababishwa na watendaji wasiotimiza wajibu wao.It's now or never!

23 Jun 2011


Mgao wa Tanesco ukiwa kazini
Sio siri kwamba kinachowapa jeuri mafisadi kuwapalekesha Watanzania ni upole kupita kiasi walionao wanachi.Watu wanalipa kodi-kwenye mishahara kwa walioajiriwa,katika VAT kwenye manunuzi ya bidhaa mbalimbali,na utitiri mwingine wa kodi-lakini faida ya kodi hiyo inaonekana zaidi kwenye ukubwa wa vitambi vya viongozi wetu,thamani ya magari na mahekalu yao,na kuongezeka kwa idadi ya vimada na nyumba ndogo zao.

Sasa Tanesco wamekuja na kali kubwa kwa kutangaza mgao wa umeme usio na kikomo,masaa kumi kwa kila siku ya wiki.Ukienda huko Twitter utasikia "aah Tanesco wamechukua umeme wao".Wengine wanaishia kuitukana Tanesco kwa matusi ya "sehemu za siri za mama yake Tanesco".Hizi zote ni dalili za watu walioishiwa na mbinu zakudai haki zao.Hivi "kumtukana mama yake Tanesco" kutafupisha mgao wa umeme?

Imefika wakati Watanzania watambue kuwa mara nyingi HAKI HAITOLEWI KAMA ZAWADI BALI HUDAIWA...KWA NGUVU IKIBIDI.Hakuna uwezekano wa tatizo la mgao wa umeme kuisha kwa njia za kistaarabu.Utatuzi hauwezi kupatikana kwa vile sekta ya nishati,kama ilivyo ya madini ni kitega uchumi kikubwa kwa mafisadi wetu.Kukatika umeme kunawaingizia baadhi ya majambazi hao mamilioni ya shilingi kila siku.

Nina tatizo kubwa zaidi na Wtanzania wa tabaka la kati.Hawa ndio tunaokutana nao huko Twitter na Facebook...Kiingereza kiiingi huku nchi inateketea.Hawa ndio tunaowaona wakijirusha kwenye kumbi mbalimbali za "starehe".Kuna starehe gani kuwepo kwenye ukumbi unaobadilisha taa kutoka rangi moja kwenda nyingine (kwa kutumia jenereta) kisha kurudi nyumbani na kukumbana na kiza na joto kwa vile "Tanesco wamechukua umeme wao" na feni haiendeshwi kwa mafuta ya taa!

Kwanini nailamu middle class yetu?Ni kwa vile hiki ni kiungo muhimu kati ya tabaka tawala na tabaka la walalahoi.Hawa ndio wenzetu wenye shahada au stashahada katika fani moja au nyingine.Hawa ni watu wenye upeo na wanaweza kuihamasisha jamii kutambua na kudai haki zao.Wengi katika tabaka hili ni walalahoi wanaojaribu kuiga maisha ya wale wa tabaka la juu.

Uchaguzi ni wenu.Kujifanya mmezowea maumivu na mafisadi waendelee "kupeta" au kuweka kando "ubishoo na usistaduu" na kuungana na tabaka la walalahoi kuhamasisha mabadiliko katika nchi yetu.Akina sie tunatekeleza wajibu kwa namna kama inavyofanya makala hii.Sasa ni wajibu wa kila mmoja wetu kutimiza wajibu wake ili kuinusu nchi yetu.

Enewei,hebu soma stori husika hapa chini
Tanesco yatangaza mgawo wa saa 10 kwa siku nchi nzima
Wednesday, 22 June 2011 21:06

Waandishi Wetu
SHIRIKA la Umeme (Tanesco), limetangaza mgawo mkubwa wa umeme usio na kikomo, utakaokuwa kwa saa 10, siku saba kwa wiki nchi nzima.

Maafisa wa shirika hilo na Wizara ya Nishati na Madini wamesema mgawo huo umetokana na upungufu wa maji katika bwawa la Mtera na transfoma zake kuzalisha umeme mdogo kuliko mahitaji.Kwa mujibu wa tangazo la ratiba ya mgao huo lililotolewa na Tanesco jana, mgao huo utakuwa wa kati ya saa sita hadi 10 kwa siku ambapo maeneo yatabadilishana muda wa mgawo.

Hata hivyo, tangazo hilo la Tanesco limekuja wakati maeneo mengi nchini yakiwa na mgawo wa muda mrefu na ambao unachukua muda wa saa zaidi ya zilizotangazwa jana na shirika hilo hali iliyosababisha malalamiko kwa wananchi.

Kwa mujibu wa ratiba hiyo mgawo huo utakuwa wa kila siku kuanzia Jumatatu hadi Jumapili ambapo baadhi ya maeneo yatakosa umeme mchana na mengine yatakosa usiku.Tanesco ilisema katika baadhi ya maeneo umeme utakatika kuanzia saa 2.00 asubuhi hadi saa 12.00 jioni, wakati maeneo mengine yatakosa umeme kuanzia saa 12.00 jioni hadi saa 5.00 usiku.

Akizungumza katika maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma jana, Mhandisi Mkuu wa Tanesco, Juliana Pallangyo alisema mgawo huo unatokana na kupungua kwa kina cha maji katika bwawa la Mtera.

Alisema mahitaji ya umeme ni megawati 850 wakati uzalishaji ni megawati 600 hali inayochangia upungufu wa umeme.

“Mahitaji yaliyopo ni makubwa wakati umeme unaozalishwa ni mdogo, tunashindwa kumudu mahitaji ya watu wote kwa wakati mmoja na ndiyo maana tunakuwa na mgawo,” alisema Pallangyo.Aliongeza kuwa licha ya matatizo hayo shirika hilo lina malengo ya kusambaza umeme vijijini ambako bado hakujafikiwa na umeme.

Katibu adai mgawo utakuwa historia

Akizungumzia kuhusu mgawo huo, Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini, David Jairo alisema mgawo huo unaweza kuwa historia katika miaka miwili ijayo na kwamba hali ya sasa inatokana na upungufu wa maji katika bwawa la Mtera ambalo linaweza kufungwa kwa sababu hiyo.

Katika hatua nyingine, Jairo alisema Serikali ya China itatoa mkopo wa dola za Marekani 778 milioni sawa na Sh1,167,000 bilioni, kwa Serikali ya Tanzania kwa ajili ya kufunga bomba kubwa la kusafirisha gesi kutoka mkoani Mtwara hadi Dar es Salaam, itakayosaidia kuongeza uzalishaji wa umeme nchini.

Alisema hatua hiyo itafanyika endapo Serikali ya Tanzania itafikia makubaliano na Serikali ya China katika mazungumzo baina yao yanayotarajia kuyafanya wiki ijayo.Iwapo mpango huo utafanikiwa kampuni ya China Petrolium Company ndiyo itakayozalisha umeme.

Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Jairo alisema, kiasi hicho cha fedha ni kulingana na upembuzi yakinifu uliofanywa na kwamba gesi itakayozalishwa itasaidia kupunguza tatizo la umeme na uharibifu wa mazingira nchini.

Alisema bomba linalozalisha gesi kwa sasa kutoka Mtwara hadi Dar es Salaam ni dogo likiwa na ukubwa inchi 30 hivyo uzalishaji wake pia ni mdogo.“Sisi kama wizara tunajitahidi kuweka mipango ya muda mfupi ya kukabiliana na tatizo la umeme lililopo nchini kwa hiyo Serikali ya China itatupa fedha hizo kama mkopo kwa ajili ya kuzalisha gesi hiyo,”alisema Jairo

CHANZO: Mwananchi

26 Apr 2011


Wakati habari kuhusu chama tawala CCM "kujivua magamba" zinaendelea kukamata nafasi ya juu,ni vema tukakumbushana magamba halisi yanayopaswa sio kuvuliwa tu bali kutekeketezwa kwa moto wa gesi.CCM wanaweza kutuchezea shere kwa usanii wao lakini ukweli unabaki kuwa ni migongano ya kimaslahi miongoni mwao ndio inayopelekea hizi ngonjera za kujivua magamba.Ufisadi katika taasisi za umma na serikalini kwa ujumla ndio magamba halisi yanayopaswa kuchunwa kwa nguvu badala ya kuwaruhusu wenye magamba hayo wajivue kwa hiari.By the way,tangu lini uchafu ukajiondoa wenyewe pasipo kutumika nguvu ya sabuni na mkono aumashine ya kufulia?

Soma habari hii ujionee mwenyewe namna Tanzania yetu inavyozidi kuwa shmba la bibi

Kashfa mpya ya Ufisadi Tanesco
Tuesday, 26 April 2011 10:14

CAG ADAI IMEILIPA DOWANS BILIONI MOJA ISIVYO HALALI
Mwandishi Wetu
SHIRIKA la Umeme Tanzania (Tanesco), limeingia katika kashfa nyingine ya ufisadi baada ya kubainika kuwa limeilipa Kampuni ya kufua umeme ya Dowans dola za Marekani 1.2 milioni ikiwa ni gharama ya kusafirisha mitambo ya kampuni hiyo kuja nchini kwa ndege badala ya dola 120,000.

Matumizi hayo ya ziada yanayokadiriwa kufikia Sh1.4 bilioni za Tanzania yanaelezwa kwamba yaliingizwa katika akaunti ya Dowans kimakosa.

Hata hivyo, mpaka sasa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), amesema Tanesco imeshindwa kumpelekea ripoti ya matumizi ya fedha hizo alizoziita kuwa ni ufisadi.

Mbali na hivyo CAG amelitaka shirika hilo limpelekee mchanganuo wa matumizi ya dola za Marekani 4,865,000 sawa na Sh6.8 bilioni.

Jana, alipotakiwa kufafanua kuhusu ripoti hiyo, CAG Ludovic Utoh alisema: “Nashukuru kwa kunipigia, lakini nyie si mnazo ripoti hizo, mnaweza mkasoma na kuendelea kuripoti.”

Kwa mujibu wa gazeti la The East African, toleo la Aprili 25, mwaka huu, ripoti ya CAG iliyoishia Juni 30, 2010 inaonyesha kuwa Tanesco ilifanya malipo hayo kupitia akaunti ya gharama za mikutano.

Taarifa hiyo imeonyesha kuwa Tanesco ilishindwa kutoa maelezo kuhusu malipo hayo kwa ajili ya kukodisha ndege maalumu ya kusafirishia mitambo hiyo. Pia inaonyesha kuwa kiasi cha Sh13,000,000 ziliripotiwa kimakosa kama Sh1,300,000,000 kwenye kifungu cha matumizi ya vikao na pia kiasi cha Sh11.0 bilioni kinachohusu malipo kupitia barua ya mkopo (letter of credit) na kuingizwa katika akaunti ya makusanyo ya shirika kupitia benki ya NBC.
CAG pia alibaini kuingizwa mara mbili kwa Sh101 milioni katika akaunti ya mitambo ya Tanesco kinyume na taratibu.

CAG alisema kuwa ndani ya Tanesco hakufanyiki usuluhishi wa mapato yatokanayo na mauzo katika matawi yake kukiwemo pia jumla ya Sh103,000,000 za masurufu ambazo hazijarejeshwa. Pia umeme unaozalishwa na ule unaouzwa unaonyesha kwamba shirika hilo linapata hasara kutokana na sababu za kiufundi.

Ripoti hiyo inasema, Tanesco ilionyesha hasara za uniti 1,188 KwH’m kutoka katika uniti 4,831 KwH’m inazozalisha ikionyesha kwamba kuna hasara katika mapato. Hasara hizo zinachangiwa na kuwepo kwa wateja wasio waaminifu, bili za uongo na uunganishaji haramu wa umeme.

Imeeleza kwamba hata wateja waliokatiwa umeme, wanaendelea kutumia huduma hiyo kama kawaida licha ya kudaiwa wastani wa dola za Marekani 65,000.CAG, Utouh alikaririwa akisema manunuzi katika shirika la Tanesco yalirekodiwa kimakosa na kwa udanganyifu.

Utouh alisema wakati wa ukaguzi, iligundulika kwamba Tanesco, hawakuwa wakifanya ‘reconciliation’ (upatanisho) ya mwezi kati ya mauzo na mapato.Kwa mujibu wa CAG, kuna hasara katika idara za uzalishaji na usambazaji wa umeme kwenda wateja.

“ Kuna mapendekezo niliyoyatoa yanayotakiwa kuchukuliwa hatua na Serikali, Bunge, Kamati ya Hesabu za Serikali, Bodi ya Wakurugenzi na maofisa watendaji wakuu kupitia ripoti ya fedha iliyoishia Juni 30,2009,” ilisema ripoti hiyo.

Katika ripoti hiyo, CAG alisema katika ripoti ya mwaka uliopita ya ukaguzi katika mamlaka za umma na bodi nyingine kuna mapendekezo 15 yaliyotolewa kwa utekelezaji: “Lakini hadi sasa mapendekezo hayo hayajatekelezwa kikamilifu.”

Alisema mapendekezo hayo ambayo hayajatekezwa yanahitaji ufumbuzi wa Serikali ili kuyawezesha mashirika mengine ya umma kufanya vizuri.

Badra Masoud, Meneja mahusiano wa Tanesco hakuweza kupatikana jana kuzungumzia suala hiyo baada ya simu yake kuita muda wote bila kupokelewa huku simu ya Mkurugenzi wa Tanesco William Mhando ikiwa haipatikani.

CHANZO: Mwananchi

24 Dec 2010


Majuzi,msomaji mmoja wa blogu hii alinitumia maoni ambapo pamoja na mambo mengine aliashiria kuwa nina chuki dhidi ya Rais Jakaya Kikwete.Msomaji huyo aliyejitambulisha kuwa mkazi wa hapa Glasgow alidai (namnukuu) "...I know you hate JK because whatever happens to him you have a negative view, even a tyre puncture...",yaani kwa Kiswahili,"najua unamchukia JK kwa vile chochote kinachotokea kwake wewe una mtizamo hasi,hata pancha ya tairi".Hii ndio mitizamo ya Watanzania wenzetu ambao licha ya kubahatika kuwa nje ya nchi,hususan nchi zilizoendelea kama hapa Uingereza,bado wana mitizamo mgando ambayo kwa kiasi kikubwa imechangia kutufanya hata miaka 49 baada ya uhuru kutamani mkoloni arejee.

Yah,huwezi kuwalaumu wanaotama mkoloni arejee japo mie si mmoja wao.Hivi tunawezaje kuelezea namna Watanzania wanavypelekeshwa kama watoto wadogo tena yatima siku chache tu baada ya Kikwete na CCM yake kupita huku na kule kuahidi neema,only for madudu and more madudu kuibuka kila kukicha?Unajua,angalau mkoloni alipotupelekesha alikuwa na excuse (japo isiyokubalika) kwamba yeye hakuwa Mtanganyika,na hakuwa na uchungu na nchi yetu.Na kwa wanaokumbuka vizuri somo la historia wanafahamu bayana kuwa ujio wa mkoloni ulikuwa kwa minajili ya kuendeleza nchi zao za asili,yaani kukwapua raslimali zetu kwa ajili ya viwanda vyao,kupata masoko ya bidhaa zao na eneo la makazi kwa nguvukazi ya ziada katika nchi hizo za wakoloni.Sasa ondoa neno mkoloni kisha weka neno FISADI,na yayumkinika kuhitimisha kuwa angalau mkoloni alikuwa na ajenda ya maendeleo huko kwao japo at our expense.Mafisadi nao wana ajenda za maendeleo pia,ila ni katika kutunisha akaunti zao kwenye mabenki ya hukohuko kwa wakoloni,kuongeza idadi ya nyumba ndogo zao (isomeke ufuska au uzinzi),kuongeza idadi ya mahekalu yao na magari ya kifahari,na sasa ajenda mpya ya kuimarisha himaya zao kwa kutumbukiza kila mwanafamilia na ndugu wa karibu kwenye siasa ili pindi baba akiondoka madarakani basi mwana amrithi kuzuia uwezekano wa baba mtu kukaliwa kooni kwa madudu aliyofanya akiwa madarakani.

Nimelazimika kuandika makala hii sio kwa minajili ya kumjibu huyo msomaji wangu wa hapa Glasgow bali ni baada ya kusoma toleo la mtandaoni la gazeti la Mwananchi ambapo kuna habari kuwa Tanesco wametangaza tena mgao wa umeme nchi nzima.Hivi sio majuzi tu shirika hilo lilitangaza mwisho wa mgao wa umeme?Tuwe wakweli,hivi uhuni huu wa Tanesco,ambao mie natafsiri kuwa ni uhuni wa serikali iliyopo madarakani,utaendelea hadi lini?So far,hakuna taarifa za wazi kuhusu athari za mgao wa umeme lakini haihitaji sayansi ya roketi au dissertation ya quantum physics kumaizi kwamba mgao huo una madhara makubwa mno kwa uchumi wa taifa na kwa maisha ya walalahoi kwa ujumla (vigogo licha ya kunufaika na ufisadi unaowawezesha kuuza jenereta kila mgao unapotangazwa lakini pia hawaathiriki kwa vile majumbani na maofisini kwao kuna jenereta zinazoendeshwa na fedha za kodi za walalahoi).

Hatuwezi kuilaumu Tanesco pekee kuhusiana na uhuni huu kwani ni siri ya wazi kuwa shirika hilo na sekta ya nishati kwa ujumla vimegeuzwa kitegauchumi kizuri kwa mafisadi.Majuzi tu tumesikia majambazi wa Richmond wakijiandaa kurejeshewa fedha walizotuibia ambapo watalipwa fidia ya mabilioni kwa mgongo wa binamu zao wa Dowans.Hatuwezi kumwepusha Kikwete na CCM yake na ufisadi huu kwa vile licha ya madudu hayo kushika hatamu wakati wa utawala wake,sasa tunafahamu kuwa amekuwa akiwakingia kifua mafisadi wasichukuliwe hatua za kisheria (thanks to nyaraka za siri za kidiplomasia zilizovujishwa na mtandao wa WikiLeaks).Kwa wale ambao hawajabahatika kusoma habari hizo,kuna nyaraka kutoka ubalozi wa Marekani hapo Dar zilizobeba maongezi kati ya bosi wa Takukuru Edward Hoseah na afisa ubalozi wa Marekani ambapo Hoseah alinukuliwa akieleza bayana kwamba Kikwete alishinikiza baadhi ya mafisadi wasichukuliwe hatua.Japo bosi huyo wa Takukuru amejaribu kuruka kimanga na kukana tuhuma hizo,kila mwenye akili timamu anafahamu kuwa ufisadi unashamiri Tanzania kwa vile Kikwete ameshindwa kuwachukulia hatua mafisadi papa licha ya madaraka lukuki aliyorundikiwa na Katiba.

Baadhi yetu tuliwaasa Watanzania wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu uliopita majuzi kwamba kuirejesha tena madarakani serikali ya Kikwete ni sawa na kumwaga chumvi kwenye kidonda kibichi,na matokeo yake ndio haya.Wakati tunaelekea mwezi wa pili tangu Kikwete atangazwe mshindi,hakuna lolote la maana lililokwishafanyika kuashiria kuwa kiongozi huyo ana ajenda mpya tofauti na zile zilizotawala miaka mitano iliyopita,kubwa ikiwa na kushamiri kwa ufisadi na uimarishaji himaya za mafisadi huko nyumbani.

Sawa,makosa yameshafanyika kwa kumrejesha Kikwete na CCM yake madarakani lakini hiyo isiwe sababu ya kuendelea kunung'unika kimoyomoyo huku nchi yetu ikizidi kuteketea.Umefika wakati Watanzania wasikubali kupelekeshwa namna hii.Kwanini Kikwete asibanwe kuhusu tatizo la umeme licha ya ahadi zake za mara kwa mara kuwa tatizo hilo lingekuwa historia?Au alimaanisha kuwa tatizo hilo litaendelea kuwa la kihistoria?

Nimesikia taarifa za mpango wa Chadema kuandaa maandamano ya nchi nzima kupinga kuongezwa bei ya umeme.Yaani licha ya mgao wa kila kukicha bado Tanesco wanataka kuongeza bei?Yayumkinika kuhisi kuwa wazo hilo la ongezeko la bei ya umeme ni la kifisadi lenye lengo la kupata fedha za kuwafidia mafisadi wa Richmond/Dowans.Ni muhimu kwa kila Mtanzania mzalendo kuunga mkono mpango huo wa maandamano ya amani ili kufikisha ujumbe kwa Kikwete na serikali yake kuwa Watanzania wamechoka kupelekeshwa.Hata hivyo,kama maandamano ya kuwapongeza wabunge wa upinzani yalizuiliwa na polisi,sidhani kama serikali itaridhia maandamano hayo ya kupinga ongezeko la bei ya umeme.

Mwisho,tuna choices mbili tu:kuchukua hatua sasa kabla hatujafika mahala ambapo hata tukichukua hatua itakuwa sawa na kutwanga maji kwenye gunia,au tusubiri kusoma rambirambi kuhusu nchi yetu hapo 2015.

27 Mar 2009


KWA MTU YEYOTE MWENYE AKILI TIMAMU,HATA AKIAMSHWA USINGIZINI AU AKIWA BWII KWA ULEVI,HAIINGII KICHWANI KUSIKIA HOJA ZA KIFISADI ZA KUNUNUA MITAMBO ILIYONGIZWA NCHI KITAPELI NA MAJAMBAZI WA RICHMOND NA HATIMAYE KURITHISHWA KISANII KWA WENZAO WA DOWANS.TUKIRUHUSU HILI LITOKEE,KUNA MAHALA ITAFIKA NCHI YETU NAYO ITAUZWA NA KISHA TUTATAKIWA KUINUNUA BACK....


Tausi Mbowe na Elias Msuya

KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo, Dk Wilbroad Slaa ameitaka serikali kuitaifisha mitambo ya Kampuni ya kuzalisha umeme ya Dowans badala ya kujadili manunuzi yake.

Dk Slaa aliyasema hayo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam baada yakutopa taarifa ya kamati kuu kilichokutana kwaajili ya kuandaa mkutano wa baraza kuu.

Alisema kuwa mitambo ya Dowans ilirithiwa kutoka kwenye kampuni ya Richmond ambayo ilibainika bungeni kuwa ni ya kifisadi kwahiyo hakuna haja ya kuinunua tena bali kuitaifisha.

“Msimamo wangu siku zote ni kutaifishwa kwa mitambo ile na siyo kuinunua. Naishangaa serikali, kutaka kuinunua mitambo ya Dowans wakati mitambo ile ilishabainishwa Bungeni kuwa ni ya kifisadi. Kama mtu umekamata kitu chako cha wizi utakinunua tena?" alihoji

Akizungumzia malumbano kati ya Mbunge wa Kyela Dk Harrison Mwakyembe na Mbunge wa Igunga Rostam Aziz, Dk Slaa alisema,

“Mradi wa kuzalisha umeme nimeushughulikia kwa miezi minane. Nilikwenda hadi kijiji cha Kisesida mkoni Singida ambako ndiko kampuni mbili za Power Pool East Africa ya Dk Mwakyembe na wenzake na Wind East Africa ya Rostam Aziz zimewekeza.

Kampuni ya Power Pool East Afrika ni ya wazalendo na imeshalipa fidia kwa wakazi wa kijiji cha Kisesida lakini ile ya Wind East Africa haijafanya hivyo, badala yake inabebwa na kiongozi wa ngazi za juu mkoani ambaye amekuwa akiwakejeli wanakijiji wa Kisesida. Ndiyo maana kuna kuwa na malumbano kati ya Rostam Aziz na Dk Mwakyembe,” alisema Dk Mwakyembe.

Akizungumzia tatizo la mgawo wa umeme ambalo litangazwa na Tanesco hivi karibuni, Dk Slaa alisema,"Baada ya kubainika kwa kashfa ya Richmond, Rais Kiwete alitangaza kuwa suala la mgawo wa umeme litakuwa historia katika nchi hii, sasa mgawo huu unatoka wapi tena? nendeni mkamwulize,” alisema Dk Slaa.

Aidha alimshangaa Rais Kikwete kwa kuendelea kumwacha madarakani Mkurugenzi wa Tanesco, Idriss Rashid wakati anatuhumiwa kwa ufisadi.

"Dk Rashid (PICHANI JUU) alihusishwa na ufisadi alipokuwa Gavana wa Benki kuu. Tumeshatoa vilelezo vyote kuthibitisha jinsi alivyoshiriki kwenye ununuzi wa rada na ndiyo maana sasa hivi anashirkiana na Dowans ili kununua mitambo yake kiufisadi. Tunashangaa kwanini Rais Kikwete hamchunguzi, wala kumwajibisha. Eti wanasema Serikali ya Uingereza inachunguza, wakati si kweli. Uingereza wanachunguza ushiriki wa BAE system siyo watu wetu,” alisema Dk Slaa.



CHANZO: Mwananchi
IT MAKES A LOT OF SENSE,DOESN'T IT?UNAMKAMATA KIBAKA NA MALI YAKO,BADALA YA KUMKWINDA AKUREJESHEE NA HATIMAYE KUMFIKISHA POLISI ETI UNAKUBALI AKUUZIE ALICHOKUIBIA!IT COULD ONLY HAPPEN IN TANZANIA,I SUPPOSE!

22 Mar 2009


As the public electricity power supply utility, Tanesco struggles with bail-out plans in order to avoid major power shedding expected to hit the nation by September this year, fresh details have emerged showing how the cash-strapped company missed a $300million power deal due to greed and battle for the control of big money running into billions of shillings.

According to details from the financier - Barrick Tanzania - the project was suspended early in January this year after Tanesco - Tanzania Electricity Supply Company - failed to adhere to the financing conditions issued in order to ensure that the billions are not swindled by some corrupt top officials within the state-owned company.

Barrick Tanzania had agreed to finance the $300million Mnazi bay power project, which could have produced 300megawatts, and forestalled the looming power crisis.

According to inside information, Barrick Tanzania, being one of the potential clients of the proposed deal, was approached by Tanesco and Artumas through a Power Purchasing Agreement (PPA).

Under this arrangement, Barrick, as a prospective client was to consider the possibility of investing in a generating company, TanGen, and recover its investment through sale of power under the Power Purchase Agreement.

It is through this arrangement that Barrick Tanzania was ready to give the needed billions to finance the stalled project.

Investigations conducted by The Guardian on Sunday have established that earlier, Barrick Tanzania, being alarmed by the financial mismanagement within Tanesco, gave the latter a condition that the two should open a joint venture account in order to manage the Sh390billion($300million).

But for unknown reasons, Tanesco flatly rejected the proposal, insisting that it should be given full mandate to control the $300million.

However, the move was strongly rejected by Barrick which among other things questioned the intention of Tanesco of declining to operate a joint venture account with the financier.

A senior official from Barrick Tanzania who declined to be named citing the sensitivity of the current power debate told The Guardian on Sunday this week: ``I am surprised, they (Tanesco) are crying to buy $50million Dowans plants while they have failed to utilise a $300million deal from us…This is a shame.

``We were surprised to hear that Tanesco management wasn`t ready to agree with a very simple condition they were being given by Barrick…And this led us to think that perhaps there were hidden motives about our money.``

After failure to agree on how to manage the billions which is close to the company`s annual revenue collections, Barrick Tanzania`s management decided to stop financing the project, casting a bleak future on the country`s energy sector.

Surprisingly on February 21, this year, while tabling the financial recovery plan of Tanseco before the parliamentary committee responsible for overseeing all publicly owned corporations, the Company`s Managing Director, Dr. Idris Rashidi, told the committee that he wasn’t aware why Barrick Tanzania pulled out of the project.

``This has come as a surprise to us because we banked our hopes on this project…we were shocked to learn that the financier had pulled out of the
project, `` the MD told the committee, indicating that he wasn’t aware why Barrick had pulled out at the final stages.

But contacted for comment, the Minister for Energy and Minerals, William Ngeleja said: ``I have already started a process to rescue the project…It is true that the negotiations hit a snag recently, but I am working on it.

``I have organised a meeting on March 25 at my office that will involve all concerned parties - Barrick, Tanesco and Artumas - to discuss how to rescue the plan.``

The Minister went on: ``You know that in any deal there`s always disagreement about contentious issues but that can be sorted out…I will ensure that the country gets the 300 megawatts electricity as planned.”

The revelations come after three weeks of a verbal wrangle between prominent leaders, focused on accusations and counter-accusations over an alleged hidden agenda on the proposed 60bn/- Dowans takeover, a situation that has opened the floodgates of mudslinging politics.

The two parliamentary committees - the one led by legislator Kabwe and the other chaired by fellow legislator William Shelukindo - have strongly differed on the Dowans deal, raising a heated debate during the past few weeks.

The company currently purchases about 59 percent of its power from private producers, which according to financial details eats up to 83 percent of the total revenue collected annually.

With dilapidated infrastructure built mainly during the 1970s, the company`s power supply capacity is estimated at 595 megawatts.

This year, the actual demand is 787 megawatts - creating a deficit of 192 megawatts.

According to available details, the company has only 670,000 customers.

Last year, the company planned to increase its customer base by about 100,000, but the target couldn’t be reached due to financial straints.

Still, based on the current economic growth, demand for electricity is estimated to increase by 15 percent annually, while the production capacity continues to dwindle due to various technical and non-technical factors.

Since there are no comprehensive power generating plans in 2010, the power deficit will surge to 300 megawatts, putting the country at risk of facing an even worse phase of power rationing.

Currently, the state-owned company needs about $200m for major repairs on its dilapidated infrastructure, but so far there’s nowhere to get the money from.

Just two years ago, the company borrowed $300m from a consortium of local banks at 10 percent interest per annum, but almost 80 percent of that money was spent on settling outstanding debts.

Currently according to the inside details, Tanesco is on the brink of collapse due to the heavy costs of operations, largely attributed to capacity charges.

In 2004, the company paid 43/- to private power producers for every 100/- it collected in revenue. By 2006, when dubious government deals were made with private companies, that figure had more than doubled, to 104/- for every 100/- collected, according to the parliamentary committee presentation.

In 2007/08, the company spent 83/- for every 100/- it collected to foot the bill of power generated by private producers, but this year, the figures will soar even higher - to 106/- for every 100/- collected, according to the financial recovery plan seen by The Guardian on Sunday.

In other words, 83 percent of the total revenue collected by the state-owned utility company will go to private power producers, leaving the company in dire financial straits.

Over the past two years, the company`s revenue collection has spiked by 122 percent, reaching 437bn/-, a year up from 196bn/- in 2006.

Today, the company`s electricity loss - meaning the amount of energy lost when transmitted from point A to point B - is 24 percent, a staggering amount when compared to countries like South Africa where that loss is below 4.5 percent.


5 Mar 2009

SAKATA la ununuzi wa mitambo ya ufuaji umeme wa dharura ya kampuni ya Dowans Tanzania Limited, jana lilimgusa spika wa bunge la Jamhuri ya Muungano, Samuel Sitta na kuamua kutoa tamko kali la kuitahadharisha serikali dhidi ya azma yake ya kutaka kuinunua mitambo hiyo yenye utata.

Spika Sitta pia ameonya kuwa mkasa wa kampuni tata ya Richmond Development (RDC) LLC uliotikisa kiasi cha kusababisha Edward Lowassa awajibike kwa kujizulu wadhifa wake wa waziri mkuu, lisifufuliwe upya kwa kutumia Dowans, ambayo ilirithishwa mkataba wa miaka miwili wa kufua umeme wa dharura.


Richmond ilishinda zabuni ya kufua umeme wa dharura kwa njia iliyojaa utata kabla ya matatizo ya usajili wake kuzua maswali mengi na kusababisha Dowans warithishwe mkataba huo mwaka 2006.

Katika mkutano wake na waandishi wa habari, Sitta alieleza nafasi ya Bunge katika kuisimamia na kuishauri serikali katika utekelezaji wa majukumu yake, huku akitaka ushauri wa Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini wa kuizuia serikali isinunue mitambo hiyo uheshimiwe.

Sitta pia alisema Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma haikustahili kufuatwa katika kutaka ushauri kuhusu suala hilo kwa kuwa suala hilo lipo kwenye Kamati ya Nishati na Madini na kwamba kama kuna sababu mbadala, wasi ililazimika kuliwasilisha upya kwa kamati hiyo.

"Naitahadharisha serikali juu ya athari zinazoweza kujitokeza iwapo itaamua kuendelea na mchakato wa ununuzi wa mitambo ya Dowans kwa kupuuza ushauri uliotolewa na Kamati ya Nishati na Madini," alisema Spika Sitta.

Alisema: "Isisahaulike kwamba Dowans ni kampuni iliyopatikana kwa kurithishwa mradi na kampuni ya Richmond katika mazingira yenye utata ambao hadi leo ni kitendawili."

Spika Sitta alifafanua kuwa uhalali wa utaratibu wa Richmond kumkabidhi mradi Dowans ulitiliwa mashaka na kamati teule ya Bunge, na kuongeza kuwa Dowans na Richmond ni kama kitu kimoja.

"Dowans na Richmond ni mtu na binamu yake na si vigumu kukubali kuwa bado wao ni wabia hadi sasa: Pamoja na yote mkasa wa Richmond haufai kufufuliwaaa upya kupitia Dowans," alisisitiza Sitta.

Aliongeza kuwa kama kweli Tanesco na serikali inazo Dola 69 milioni za Kimarekani (sawa na Sh90 bilioni za Kitanzania) ambazo ni bei ya mtambo wa Dowans, ingezitumia fedha hizo kama sehemu ya malipo ya kununua mitambo mipya. Alisema Tanesco ingetafuta ushauri kutoka Mamlaka ya Ununuzi Serikalini (PPRA) ili taratibu za dharula zitumike kununua mitambo mipya kukabiliana na "dharula inayotabiriwa".

Sitta alihoji mantiki itakayotumiwa na Tanesco kutaka kununua mitambo ambayo inamilikiwa na kampuni ambayo imeishtaki kwenye Baraza la Usuluhishi ambalo makao yake makuu yako Paris, Ufaransa.

"Gharama za mitambo na gharama za kuikodi haviwezi kuepukwa kuwa ni sehemu ya shauri lililo Paris," anasema Sitta. "NI kwa mantiki ipi kesi baina yao iendelee na hapo hapo mdaiwa (Tanesco) anunue mitambo kutoka kwa mdai (Dowans.

"Tanzania ilikuwa ikilipa Dowans shilingi za Kitanzania milioni 152 kwa siku (Dola 120,000) sawa na Dola 42 milioni kwa mwaka).

"Pamoja na yote, mkasa wa Richmond haufai kufufuliwa upya kupitia Dowans. Tanesco/serikali waelekeze nguvu zao katika njia mbadala za kulipatia taifa umeme wa dharura, badala ya njia hii ya Dowans iliyojaa utata."

Kuhusu mvutano kati ya Kamati ya Kudumu ya Hesabu za Mashirika ya Umma na ile ya Nishati na Madini, Spika Sitta amsema si sahihi kwa kamati yoyote ya Bunge isiyo ya sekta husika, kutoa maoni yake hadharani na kuishawishi jamii kwamba Bunge lina ushauri unaopingana kuhusu suala husika.

"Si sahihi kwa Kamati yoyote ya Bunge isiyo ya sekta kutoa maoni yake hadharani na kujenga taswira kwa umma kwamba, Bunge lina ushauri unaokinzana kuhusu suala lililo mbele yake. Kamati nyingine, haina budi kupitisha ushauri na maoni yake kwenye kamati ya kisekta," alisema Sitta.

Zitto Kabwe, ambaye ni mwenyekiti wa Kamati ya Hesabu za Mashirika ya Umma, alikaririwa na vyombo vya habari akieleza msimamo wa kamati yake kuunga mkono Shirika la Umeme (Tanesco), kuinunua mitambo ya Dowans kwa maelezo kuwa hatua itasaidia kulinusuru taifa katika janga kubwa la kukosa umeme na kwamba sheria ya manunuzi si msahafu, hivyo inaweza kubadilishwa.

Lakini Kamati ya Nishati na Madini, ambayo mwenyekiti wake ni William Shelukindo, inapinga hatua hiyo ikieleza kuw ainakiuka Sheria ya Manunuzi ya Umma, inayokataza serikali kununua vitu ambavyo tayari vimetumika.

Alisema ushauri kwa serikali kuhusu Tanesco kununua au kutonunua mitambo ya Dowans ulikwishatolewa kwa Wizara ya Nishati na Madini na Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini Desemba 14 mwaka uliopita.

"Huo ndiyo ushauri rasmi na sahihi wa Bunge ninaoutambua. Kwa msingi huo hoja ya kuzikutanisha Kamati hizi mbili (ya Nishati na Madini na ya Hesabu za Mashirika ya Umma) ili kurejea uamuzi au maoni yaliyokwishatolewa na Kamati inayohusika, haina msingi," alisema Sitta.

Alisema mkondo rasmi wa ushauri kwa serikali uliokusudiwa kwenye Ibara ya 63 (2) ya katiba ikisomwa na pamoja na kanuni za Bunge za mwaka 2007 ni kupiti Bunge zima au kamati zake za kisekta kila kamati na sekta yake.

Wakati Spika Sitta akibainisha msimamo wake na wa Bunge, mwenyekiti wa CUF, Prof. Ibrahim Lipumba ameunga mkono ununuzi wa mitambo hiyo huku akisema kauli ya Rais Jakaya Kikwete aliyoitoa jana inaweza kukwamisha mchakato wa ununuzi wa mitambo hiyo.

Lipumba alisema katika mfumo wa utawala bora wakati kamati za bunge zinazohusika na mambo hayo na bodi za mashirika zipo, rais hapaswi kujiingiza mapema katika mijadala.

“Katika mfumo wa utawala bora ambao una kamati za bunge zinazohusika na sekta ya umeme na manunuzi, kwa rais kujiingiza kunaweza kuwa ni kikwazo cha mchakato mzima wa ununuzi wa mitambo,” alisema Profesa Lipumba.

Alifafanua kuwa, sheria ya manunuzi ya Serikali ina upungufu kwa kuwa inalazimisha ununuzi wa mitambo mipya, jambo ambalo haliwezekani kwa nchi zinazoendelea kama Tanzania.

“Ununuzi wa mitambo ya kibiashara katika sekta ya biashara huwezi kulazimisha ununuzi wa mitambo mipya hususan katika nchi zinazoendelea kama ya kwetu. Jambo la msingi ni kuangalia uwezo wa mitambo katika kufanya kazi na si kwamba ni mipya au mikongwe,” alifafanua Lipumba na kuongeza:

“Sheria yetu ya manunuzi ni nzuri na inafaa sana kwa kununua vitu vya huduma za serikali, kama magari na vifaa vingine.”

Aliitaka Tanesco kuwa wazi kwa kuwa ni wao waliosema mitambo hiyo hawaitaki hivyo kuamuwa kuvunja mkataba na Dowans iweje leo wanageuka na kusema mitambo hiyo ni mizuri na kuitaka serikali iinunuwe.

“Tanesco walituambia kuwa mitambo hiyo hawaitaki na walivunja mkataba na Dowans, sasa inakuaje leo wanageuka na kusema kwamba mitambo hiyo ni mizuri na inunuliwe kwa ajili ya kuzalishia umeme? Tunahitaji uwazi zaidi kutoka Tanesco,” alihoji Profesa Lipumba.

Naye Stephen Menad ambaye ni mshauri wa masuala ya nishati na mazingira, alisema hakuna kitu kipya kwenye mitambo hiyo ya Dowans hivyo isinunuliwe na badala yake itafutwe mipya ili kuondoa mvutano baina ya wananchi na serikali.

Mussa Hassan, mkazi wa jijini Dar es Salaam ambaye ni mfanyabiashara, alisema ni aibu kwa serikali kula matapishi na kwamba viongozi wasisahau yaliyotokea wakati mitambo ya Richmond ilipokuja na mwisho wake kuwaweka pabaya viongozi waliokuwa serikalini.

Anthony Chambi, ambaye ni mfanyabiashara katikati ya jiji la Dar es Salaam, alisema hataki kusikia kuhusu mitambo hiyo kwa kuwa tayari ilishaiabisha serikali. Alisema anasikia kuna kesi Ufaransa kuhusu mitambo hiyo kitu kinachomshangaza kwa nini serikali inataka kununua mitambo ambayo ina kesi.
CHANZO: Mwananchi
BIG UP,MHESHIMIWA SPIKA.
BINAFSI HADI MUDA HUU SIELEWI HAO WANAOTAKA MITAMBO YA DOWANS INUNULIWE WANA AJENDA GANI!NACHANGANYWA ZAIDI NAPOSIKIA WATU KAMA ZITTO KABWA NA PROFESA LIPUMBA NAO WAKIPIGA DEBE MITAMBO YA DOWANS INUNULIWE.HUU NI UNAFIKI WA MCHANA KWEUPE.WHY?BECAUSE KUNUNUA MITAMBO HIYO NI KUHALALALISHA UJAMBAZI WA DOWANS NA KAKA YAKE RICHMOND.HIVI INAINGIA AKILINI KWELI PALE TAPELI ANAPOKUUZIA MALI FEKI KISHA UKAMKALIA KOONI MPAKA AKAKIRI KUWA KWELI ALICHOKUUZIA NI FEKI,HALAFU UKAISHIA KUONGEZA FEDHA KUNUNUA MALI HIYO FEKI!?
I WOULD ONLY SUPPORT MATUMIZI YA MITAMBO YA DOWANS LAITI INGEKUWA IMETAIFISHWA (NA SIJUI KWANINI HADI MUDA HUU HAIJATAIFISHWA...WE MISS YOU BABA WA TAIFA).ETI AKINA KABWE WANASEMA TUWEKE MBELE UTAIFA KWANZA!UTAIFA KWANZA KWA MANUFAA YA AKINA RICHMOND?HAWA WAMEINGIZWA MKENGE NA VITISHO VYA TANESCO KUWA ETI NCHI IKO HATARINI KUINGIA KIZANI!YALEYALE YA RICHMOND!
WIZI MTUPU!

4 Nov 2008

Nadhani unakumbuka wasiwasi nilioonyesha katika POST HII.Inaelekea suspicion yangu haiko mbali na ukweli.Zaidi,soma habari hii:
Serikali imesema itakuwa tayari kununua mitambo ya Kampuni ya Dowans Tanzania Ltd endapo Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), litaishauri kufanya hivyo. Dowans Tanzania Ltd jana ilitangaza rasmi zabuni ya kuuza mitambo yake ya kuzalisha umeme ikiwa ni miezi mitatu baada ya serikali kukatisha mkataba wake na Tanesco. 

Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja aliiambia HabariLeo jana kuwa kimsingi serikali haitakuwa na tatizo na mitambo hiyo endapo wataalamu wa Tanesco watashauri hivyo. “Tanesco ndiyo wataalamu wetu, tutawauliza wakisema tununue tutanunua, lakini kwa kufuata taratibu na sheria za manunuzi ya mitambo hiyo,” aliongeza Ngeleja. 

Endapo serikali au Tanesco watanunua mitambo hiyo, itasaidia kupunguza uwezekano wa kutokea mgawo wa umeme mara mitambo mingine ikipata hitilafu. Mwezi uliopita, Tanesco ililazimika kutangaza mgawo wa umeme baada ya mashine moja ya Kampuni ya Songas yenye uwezo wa kuzalisha megawati 40 kuharibika. 

Hata hivyo, Meneja Mawasiliano wa Tanesco, Badra Masoud alisema jana kuwa shirika hilo halijaamua kama watanunua au la. Alisema watatoa taarifa uamuzi ukifikiwa. Dowans Tanzania Limited ilirithi mkataba wa kuiuzia umeme wa megawati 120 Tanesco kutoka kwa Kampuni ya Richmond Development LLC ambayo baadaye iligundulika kuwa ni kampuni hewa. 

Serikali ilifikia uamuzi wa kusitisha mkataba huo Agosti mosi mwaka huu baada ya kuridhika kuwa mkataba huo haukuwa halali wala haukuwa na nguvu kisheria. Tangazo lililotolewa jana na kampuni hiyo lilimtaka mtu yeyote, taasisi, kampuni itakayotaka kununua mitambo hiyo ipange bei inayoona inaweza kutoa kuipata mitambo hiyo.


CHANZO: HabariLeo

8 Oct 2008

Hawa TANESCO vipi?Kwanza walitangaza mgao wa umeme wa takriban masaa matano kwa siku kabla ya kuongeza muda na kuwa takriban masaa kumi kwa siku.Siku chache baadaye wakatangaza kuisha kwa mgao huo,lakini kwa mujibu wa gazeti la Tanzania Daima,mgao umerejea tena.Ubabaishaji wa aina hii utaendelea hadi lini?

28 Sept 2008

Picha kwa hisani ya  Chesi Mpilipili
Shirika la Umeme Tanzania,TANESCO,limetangaza ratiba mpya ya mgao wa umeme ambao tofauti na yale masaa matano ya awali   sasa tatizo hilo litadumu kwa masaa kumi kwa siku.Ni muhimu kuwa tatizo hili linakuja wakati tatizo jingine la nishati ya mafuta likiwa halijatulia sawasawa.Angalau katika suala la kupanda kwa bei za mafuta liko nje ya uwezo wetu kwa vile linakuwa determined na soko la dunia.Lakini inakuwa vigumu kuingia akilini pale ambapo takriban kila mwaka lazima TANESCO watangaze mgao wa umeme.Na ninaposema kila mwaka najaribu ku-neglect power cuts za mara kwa mara zisizo na ratiba ambazo zimekuwa kama suala la kawaida huko nyumbani.

Kwa mtazamo wangu,tatizo kubwa zaidi linaloikabili TANESCO sio uhaba wa fedha bali namna linavyoendeshwa kisiasa.Pengine unaweza kudhani ufumbuzi wa tatizo hilo ni kulibinafsisha shirika hilo la umma.Lakini pengine kabla hujafikiri hivyo ni vema ukaangalia baadhi ya mashirika ya umma ambayo kubinafsishwa kwake hakujaweza kuyafanya yamudu uendeshwaji wa mafanikio.Mfano mzuri ni Sherika la Reli (TRC) ambapo huduma zake zimeendelea kuwa mbovu licha ya kupatiwa mwekezaji ambaye pengine mafanikio yake makubwa yamekuwa katika kuishawishi serikali impatie fedha za kumkwamua kila linapotokea tishio la mgomo wa wafanyakazi.Sikatai kwamba kuna some few success stories katika ubinafsishaji wa mashirika yetu ya umma,mfano mzuri ukiwa TBL,lakini mafanikio hayo yanaendelea kubaki kuwa mithili ya matone kwenye bahari.

Uendeshwaji wa TANESCO kisiasa ndio uliopelekea shirika hilo kusaini mkataba wa ajabu na kampuni ya IPTL.Mkataba huo umeendelea kuiumiza TANESCO kwa muda mrefu sana na hakuna dalili za kuisha kwa tatizo hilo.Ahadi za kupitia mikataba mibovu zimeendelea kubaki ahadi huko akina IPTL wakiendelea kuikalia kooni,hali inayopelekea maumivu zaidi kwa wananchi wa kawaida.

Kuna hujuma za kiwango kidogo dhidi ya TANESCo zinazofanywa na wezi wa mafuta ya transfoma,mita za luku na hata nyaya za umeme.Hujuma hizi zinazodaiwa kuwashirikisha baadhi ya watumishi wasio waaminifu wa shirika hilo haziwezi kulinganishwa hata kidogo na hujuma kubwa kama hiyo ya IPTL.Hivi inaingia akilini kweli kwa shirika kulilipa shirika jingine hata lisipotoa huduma inayokusudiwa kwenye mkataba?

Kuna Watanzania wenzetu wanaofanya kila liwezekanalo kuona TANESCO haiishi kulingana na matarajio yake na ya wateja wake.Hawa ni pamoja na wale waliotuingiza mkenge kwenye utapeli wa Richmond.Hawa wanaombea ukame ujitokeze tena ili waje na scams nyingine za kuongeza mabilioni ya shilingi kwenye akaunti zao.Ni katika mazingira ya namna hii ndipo tunapojikuta tukipatwa na hisia kwamba hata kuharibika kwa mitambo ya umeme ya Songas (ambapo imepelekea kuwepo kwa mgao huu wa sasa) kunaweza kuwa hujuma ya hao wenzetu ambao kuumia kwa wengi ndio mafanikio yao.

Kabla ya kuangalia chanzo kikubwa cha utendaji wa kiwango cha chini kabisa kwa TANESCO (mbali na uendeshwaji wa kisiasa) ni vema pia kuangalia sera nzima ya nishati nchini.Katika dunia hii ambayo nchi kama zetu za dunia ya tatu (na hivi karibuni hata kwa nchi zilizoendelea) hazina uwezo madhubuti wa kukabiliana na matukio yasiyotarajiwa (eg kupanda kwa bei ya mafuta katika soko la dunia na the current world economy crisis) ni muhimu kujitengenezea mazingira ya kuzuia madhara ya huko mbeleni.Tukiendelea kutegemea mvua zijaze mabwawa ili mitambo ya TANESCO huko Kidatu na kwingineko ifanye kazi sawasawa,tutazidi kuumia.Pasipo kuwa na chombo madhubuti zaidi ya EWURA na TPDC,ni dhahiri wafanyabiashara wa mafuta wataendelea kuuza nishati hiyo kwa bei wapendazo wao.

Lakini ili yote yawezekane ni lazima kila Mtanzania aweke mbele maslahi ya taifa badala ya maslahi binafsi.Maamuzi mengi mabovu ni matokeo ya kukithiri kwa upungufu wa uzalendo na uchungu kwa taifa letu.Wataalam tunao lakini mara nyingi ushauri wao unapuuzwa kwa vile unaonekana kuathiri maslahi binafsi ya mafisadi.Kibaya zaidi,ushauri mzuri kwa maslahi ya taifa unaweza pia kutafsiriwa kuwa ni uchochezi.Siasa inaelekea kutawala kwenye kila nyanja na professionalism inanyang'anywa nafasi yake na hamasa za kisiasa.Nothing good ever comes out of putting emotions (in this case political sentiments) in front of common sense (hapa ni maslahi ya taifa)


25 Sept 2008

Kwa mujibu wa The Citizen,Tanzania itakumbwa na mgao wa umeme wa masaa matano kwa siku kutokana na kuharibika kwa mitambo ya Songas.Let's hope this won't lead to another Richmond-like scam.Lakini pengine huu ni wakati mwafaka wa kujiuliza ni lini matatizo ya umeme yatakwisha nchini.Katika kipindi nilichokuwa nyumbani hivi karibuni,katika baadhi ya maeneo kama Sinza ilikuwa as if tayari kuna mgao wa umeme.Yayumkinika kuhisi kwamba kuna mafisadi wanaoombea tatizo hilo liwe kubwa zaidi ili watuumize tena.Who know,they might even be the force behind the Songas turbine collapse.

11 Feb 2008

Uongozi wa kisiasa wa Tanzania,kama ilivyo sehemu mbalimbali duniani,umekuwa ukitegemea watu kutoka fani mbalimbali za maisha.Tuna viongozi wa dini (kama Mchungaji Lwakatware),Wasomi (kama Prof Mwandosya,Prof Msola,Prof Mwakyusa),wanajeshi (kama Kapteni John Komba,Kapteni Jaka Mwambi,Luteni Yusufu Makamba) na hata wasanii kama Khadija Kopa .Hivi karibuni,JK alielezea kutoridhishwa kwake na athari zinazoweza kutokana na kuwa na viongozi ambao pia ni wafanyabisahara.Ana hoja ya msingi hapo,lakini nadhani tatizo la msingi sio fani aliyotoka au anayoendela nayo kiongozi husika bali ni utashi alionao katika kuwahudumia Watanzania wenzake.Kadhalika,mkanganyiko uliopo kwenye kanuni za maadili ya uongozi ziko shaghala baghala,hasa baada ya kuuawa kwa Azimio la Arusha na kuzaliwa Azimio la Zanzibar.Endelea na makala yangu hii kwenye gazeti la Mtanzania.
MTANZANIA UGHAIBUNI-

Watanzania wengi wameipokea kwa furaha kauli ya Rais Jakaya Kikwete kuhusu umuhimu wa kutenganisha biashara na utumishi wa umma.Ni kauli mwafaka kwani hata katika Maandiko Mtakatifu tunafundishwa kwamba ni vigumu kutumikia mabwana wawili.

Naamini kwa mtazamo wa wengi,wafanyabiashara kama Watanzania wengine wana kila haki ya kushiriki katika shughuli za siasa ikiwa ni pamoja na kugombea ubunge au hata kuteuliwa mawaziri.Tatizo linakuja pale maslahi ya biashara zao yanapoingiliana na utekelezaji wa majukumu yao katika kuuhudumia umma.

Inaweza kuwa sio sahihi kuwalaumu wafanyabisahara wanaochanganya biashara na siasa pale ilhali hakuna miongozo maalumu (kama ya Marekani na Uingereza).Ndio maana wazo la kufanyika mchakato wa kuleta sheria na kanuni zitakazoweka bayana mazingira ambayo kwa upande mmoja hayatawanyima nafasi wafanyabiashara kushiriki kwenye siasa,na upande mwingine biashara zao kutoathiri majukumu waliyokabidhiwa na taifa,lina umuhimu mkubwa.

Pamoja na pongezi hizo ni muhimu kuangalia chanzo cha tatizo lililopo hivi sasa.Ni ukweli usiopingika kwamba wakati wanasiasa wengi wameendelea kuhubiri kwamba siasa ya Ujamaa na Kujitegemea bado ni mhimili wa taifa letu,hali halisi tuliyo nayo sasa inapingana kabisa na matamshi hayo.

Azimio la Arusha lilisaidia kuweka wazi mwelekeo wa taifa letu.Makala moja kama hii haiwezi kutosha kuelezea undani wa Azimio hilo lakini kilicho wazi ni kwamba Baba wa Taifa,ambaye kimsingi ndiye anayekubalika kama mwasisi wa itikadi hiyo,alikuwa na ndoto ya kuona jamii ya Watanzania inayoishi kwa usawa na haki.

Baadaye likaja Azimio la Zanzibar.Pengine mie ni mzembe wa kujua kilichomo katika Azimio hilo lakini naamini kwamba kuna Watanzania wengi ambao hadi leo hawajui kilichomo kwenye Azimio hilo.Labda ni kutokana na ufahamu mdogo uliopo miongoni mwa wananchi wengi kuhusu Azimio la Zanzibar ndio maana wengi wetu tunarahisisha majibu kwamba lilikuwa tamko rasmi la kifo cha Azimio la Arusha.Na katika hili,CCM inastahili kubeba lawama zote kwani haijafanya jitihada zozote za makusudi kuuelewesha umma kuhusu madhumuni na kulichomo kwenye Azimio hilo (la Zanzibar).

Kuna mapungufu makubwa katika suala zima la uwazi pindi yanapojiri masuala nyeti kwa taifa letu.Mfano mzuri ni kwamba wengi wetu tulikuwa hatufahamu kwamba hadi uteuzi wake unatenguliwa na Rais,aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu aliyeondolewa madarakani,Dkt Daudi Ballali,hakuwa mtumishi wa serikali.Pengine taratibu zinasema hivyo lakini kwa vile mtu anayekalia nafasi hiyo ndiye mwenye kushika dhamana ya fedha za Watanzania wote,nadhani kulikuwa na kila sababu ya wenye fedha zao (Watanzania) kufahamishwa kuhusu hilo badala ya kusubiri mpaka litokee tatizo la ufisadi kwenye taasisi hiyo muhimu kwa taifa.

Hadi muda huu,ukiwauliza viongozi wa CCM kwamba je Azimio la Arusha bado ni mwongozo muhimu kwa maendeleo na mwelekeo wa taifa,sanasana utachoambulia ni hadithi ndefu zisizotosha kutoa jibu moja la kueleweka.Ni dhahiri muuliza swali atakumbana na ugumu wa aina hiyohiyo pindi akiuliza iwapo nchi yetu bado inafuata siasa ya Ujamaa na Kujitegemea.Na haiishii hapo kwani majibu yataendelea kuwa tete pindi mtu akiuliza iwapo CCM bado ni chama cha wakulima na wafanyakazi.

Na ni katika hilo la wakulima na wafanyakazi ndipo napoona kuna tatizo la msingi.Inasemekana Azimio la Zanzibar lilihalalisha watumishi wa umma (wafanyakazi) kumiliki mali kinyume na katazo lililowekwa na Azimio la Arusha.Laiti wakati wanasiasa wetu walipokutana Zanzibar kuua Azimio la Arusha wangeangalia mbali,ni dhahiri wangebaini uwezekano wa kutokea mgongano kati ya biashara na utumishi wa umma.Haraka ya kupitishwa Azimio hilo inaweza kuwa sababu muhimu ya wanasiasa hao kutoangalia mbali.Lakini pia haraka hiyo inaweza kuwa ilichochewa na ukweli kwamba wakati wanasiasa wengi walikuwa wakituimbia ngonjera za Ujamaa na Kujitegemea majukwaani,majumbani mwao walikuwa wakicheza ngoma za ubepari.

Dhana hapo ni kwamba Azimio la Zanzibar lilipitishwa chapchap ili wajamaa wa hadharani waliokuwa mabepari wa kificho waweze kuendesha maisha yao bila hofu na bughudha ya kuonekana wanatenda kinyume na imani ya taifa letu kwa wakati huo.Hawa ni pamoja na wale ambao walikuwa wakituaminisha kwamba ni watu wa karibu na Baba wa Taifa kumbe moyoni walikuwa wakiomba dua Mwalimu aondoke madarakani ili watumie vile walivyokuwa wakikusanya kwa kificho katika zama hizo za Ujamaa na Kujitegemea.Na wengine japo Mwalimu aliwasaidia kuwaingiza madarakani akidhani ni waumini wa siasa zake,wamestaafu wakiacha skandali lukuki.

Kama kuna madhara mabaya zaidi ya mfumo wa chama kimoja basi ni kule kutoruhusu mawazo tofauti na ya watawala,hata kama mawazo hayo ni ya kuchochea maendeleo ya taifa.Kinadharia kila Mtanzania ana uhuru wa kutoa mawazo yake alimradi asivunje sheria halali za nchi,lakini kiuhalisia bado kuna chembechembe zilizorithiwa kutoka katika mfumo wa chama kimoja ambapo mawazo tofauti ni sawa na uhaini.

Katika zama za chama kimoja,hoja kama ile ya “chama kushika hatamu” zilisaidia baadhi ya mafisadi wa wakati huo kupata kinga dhidi ya wale maovu yao.Sote tulikuwa ni Watanzania tusio na tofauti,tunaoamini kwamba ili nchi yetu iendelee tunahitaji ardhi,watu,siasa safi na uongozi bora.Mwalimu aliamini kuwa hiyo ni njia sahihi ya maendeleo kwani alishuhudia namna ilivyofanikiwa sehemu kama China na Cuba.Kosa lake ni kuamini kwamba walio karibu yake walikuwa na imani ya dhati kama yeye.Angalau leo tunawajuwa wanafiki hawa,lakini kwa sababu za “kulinda umoja wa kitaifa” na kutaka “wapumzike kwa amani” tunaendelea kuwaheshimu kwa kutowaumbua hadharani.

Kumkosoa mzazi ni kosa,na kwa mwananchi wa kawaida au hata kiongozi kumkosoa Rais inaweza kutafsiriwa kuwa ni utovu wa nidhamu.Hata hivyo,kutoa ushauri kwa heshima na taadhima ni jambo linalokubalika.Ni kwa kuzingatia hilo ndio maana naamini kwamba wakati Watanzania wengi wanakubaliana na mtizamo wa Rais Kikwete kuhusu kutenganisha siasa na biashara,ni vema katika utekelezaji wa dhamira yake hiyo akaweka maanani namna Baba wa Taifa alivyosalitiwa na baadhi ya watu wake wa karibu.

Nasema hivyo kwa sababu naamini hata zikiwekwa sheria nzuri namna gani za maadili ya uongozi,pasipo kutengeneza mazingira yatakayozuia wasimamizi wa sheria hizo kuzihujumu,itakuwa ni kazi bure.Mwanasiasa anaweza kabisa kutangaza kwamba biashara zake za awali zimekabidhiwa kwa wadhamini flani,lakini pasipo usimamizi mzuri mfanyabiashara huyo anaweza kuendelea kuendesha biashara zake huku akiwa mwanasiasa japo machoni mwa umma anaonekana ametekeleza sheria hiyo tarajiwa ya kutenganisha biashara na siasa.

Mfano mzuri wa ninachosema ni hili sakata linaloendelea la fedha za EPA huko Benki Kuu.Yayumkinika kubashiri kwamba kama itafikia hatua ya watu flani kupelekwa mbele ya vyombo vya sheria,kuna uwezekano watu hao wakawa ni wamiliki “hewa” ambao majina yao yalitumika tu kuficha wamiliki halali.Katika mazingira ambapo taasisi kama TAKUKURU ilikuwa ya kwanza kudai mradi wa Richmond haukuwa na harufu ya rushwa ilhali sasa tunaona suala hilo likiwaka moto huko bungeni,tutarajie nini pindi wakipewa jukumu la kuhakikisha mfanyabishara anayetaka kuingia kwenye siasa kweli amekabidhi biashara yake kwa wadhamini kama sheria itakavyokuwa inataka?

Mwisho,kikao kinachoendelea cha bunge kimeonyesha dalili kwamba baadhi ya wawakilishi wetu wamechoka kupiga mihuri kupitishwa miswada inayoonekana mizuri machoni lakini inaishia kwa mashirika kama ATC kununua ndege mbovu,TANESCO kujikuta hohehahe kwa kulipa madeni yaliyosababishwa na walafi flani wasio na uchungu na taifa au kuletewa umeme hewa ulioahidiwa na makampuni ya kisanii.Hoja hapa sio kuitupilia mbali miswada ya manufaa kwa taifa au kuchochea upinzani dhidi ya serikali bali kuwabana mafisadi wote wananaotumia nyadhifa zao kulikamua taifa letu.
BAADA YA POLITIKI ZA BONGO,HEBU ANGALIA HIZI ZA NAS KUHUSU THE N-WORD


13 Dec 2007

Makala ya wiki hii ndani ya gazeti la Mtanzania inaangalia namna mafisadi wa kigeni wanavyonufaika kutokana na uzembe wa baadhi ya Watanzania wenzetu tuliowakabidhi dhamana za uongozi.Lakini hata kama wawekezaji hao wangekuwa waadilifu hivi kweli ndoto ya "maisha bora kwa kila Mtanzania" itatimia wakati Waziri mwenye dhamana ya maendeleo ya sekta ya Maji (Waziri wa Maji) nae ni miongoni mwa wadaiwa sugu wa maji waliokatiwa huduma hiyo na DAWASCO?Makala nzima hii hapa chini

Waziri wa Maji anasubiri nini ofisini?

na evarist chahali, uskoch


Hadi muda huu haijaniingia akilini niliposoma habari kwamba aliyekuwa mwekezaji kwenye hoteli ya Millenium Tower “ameingia mitini” na kuacha deni kubwa la kodi ya jengo na bili nyingine.Kwa mujibu wa uongozi wa LAPF ambao ndio wamiliki wa jengo hilo,mwekezaji huyu alianza kuonyesha dalili za ubabaishaji muda mrefu kidogo kabla hajaamua kutoroka,lakini nachoshindwa kuelewa ni kwanini uongozi huo haukuchua hatua za tahadhari kuhakikisha kwamba wanalipwa kilicho chao kabla huyu jamaa hajaondoka kimyakimya.

Pengine ni vema nikitoa mfano halisi wa taratibu za upangaji zilivyo hapa Uingereza.Ukitembelea miji mikubwa kama London,Manchester,Birmingham na mingineyo,au hata kwenye mji mdogo kama Aberdeen (hapa ninapoishi) utakuta kuna jamaa wanaopata hifadhi ya makazi kwenye viambaza vya maduka na majengo mengine huko mjini kati.Hawa ni watu wasio na makazi,na japo wengine wameishia katika hali hiyo kutokana na uzembe wao,wapo wale ambao si rahisi kwao kupata makazi kutokana na ugumu katika utaratibu mzima wa kuingia mikataba ya makazi.Wamiliki wa majengo ya kupangisha wako makini mno kuhakikisha kwamba hawapangishi wababaishaji.

Na kwa wageni inakuwa suala zito zaidi kwani nyaraka kadhaa zinahitajika kabla mwenye jengo hajakukabidhi funguo la pango la kuishi.Mara nyingi taratibu za kupanga jengo huhusisha wanasheria ili pindi upande mmoja utakapokwenda kinyume na mkataba wa pango basi iwe rahisi kuhakikisha haki inapatikana.Hapa nawazungumzia wamiliki binafsi na sio makampuni yenye majengo ya kupangisha.

Pengine wamiliki wa nyumba za kupanga wanakuwa makini kwa vile wana uchungu na mali zao,lakini pengine ni kutokana na utaratibu mzuri wenye kumnufaisha mwenye nyumba na mpangaji.Lakini hata huko nyumbani kuna taratibu kama hizo japo zinatofautiana kwa kiwango flani.Inawezekana mwenye nyumba unayotaka kuhamia asijali sana kudadisi ulikotokea,lakini mara nyingi utaratibu unaofahamika ni kutanguliza malipo ya awali ambayo huweza kuwa sawa na kodi ya nusu mwaka au mwaka mzima.Na wengine hufikia hatua ya kuomba “kilemba” kana kwamba anayetaka kupanga anachumbia kwa mwenye nyumba,yote hiyo ni kwa mwenye mali yake kuhakikisha kuwa hatoishia kujilaumu baada ya kumruhusu mpangaji kuingia kwenye jengo lake.

Naamini kabisa kwamba laiti jengo la hoteli ya Millenium Tower lingekuwa mali ya mtu binafsi basi huyo mwekezaji tapeli asingeweza kutoroka kirahisi namna hiyo.Na kwanini watueleze sasa kuwa mpangaji wao kaingia mitini ilhali walishakuwa na matatizo naye kwa muda mrefu?Jibu jepesi kwangu ni kwamba hawana uchungu na fedha za waliowezesha jengo hilo kufikia hapo lilipo.Na hili ni tatizo kubwa sana katika hii inayoitwa mifuko ya jamii.Maamuzi ya mali zinazomilikiwa na mifuko hiyo yamebaki mikononi mwa watu wachache ambao pindi hasara ikitokea wanaishia kutoa sababu moja au nyingine na wala sio kuelezea namna gani hasara hiyo itakavyofidiwa

Natambua kwamba ni vigumu kuiwezesha demokrasia ichukue mkondo wake katika mfuko wa jamii wenye wanachama elfu kadhaa kama sio laki na kitu.Demokrasia nayozungumzia hapa ni ile ya maamuzi yanayofikiwa kwa makubalino ya wanachama wote.Hata hivyo,hiyo haitoi nafasi kwa wachache waliokabidhiwa dhamana ya kufanya maamuzi kwa niaba ya wanaowawakilisha wakafanya mambo kiholela kwa vile tu fedha zinazoteketea hazitoki mifukoni mwao.

Tumeshuhudia sehemu kadhaa zikibadilishwa majina kila mwaka baada ya wawekezaji wa awali kuondoka na kurusha mpira kwa wawekezaji wapya.Kubadili jina la biashara sio kosa kisheria kwani hata jina la mtu binafsi linawezwa kubadilishwa mahakamani.Tatizo hapa ni kwamba wawekezaji matapeli hutumia misamaha ya kodi na masharti mepesi wanayopatiwa wakati wanaingia mikataba na wakishachuma faida ya kutosha wanaondoka kistaarabu (kwa kutangaza kwamba wamekuwa wanapata hasara) au kibaradhuli (kwa kuingia mitini kama huyo mwekezaji wa zamani wa hoteli ya Millenium Tower).

Mwaka juzi nilialikwa kumtembelea rafiki yangu mmoja aliyeko Marekani.Nilipofika ubalozi wa nchi hiyo jijini London kuomba viza,nilijionea mwenyewe namna gani wenzetu wanavyojithamini wao kwanza kabla ya wageni.Utaratibu wa kuingia hapo hauna tofauti na ule wa zamani katika ubalozi wa Uingereza hapo Dar ambapo waomba viza walikuwa wanalazimika kukesha usiku kucha kuwahi foleni ya kuonana na maofisa wa ubalozi huo.Japo sina hakika lakini nadhani utaratibu wa sasa wa kufanya maombi mtandaoni unaweza kuwa umepunguza tatizo hilo.Katika ubalozi huo wa Marekani hapo London,raia wa Marekani hawapatwi na usumbufu wa kukaa kwenye foleni ndefu au kupigwa na mvua au kibaridi (kulingana na majira ya mwaka) bali hupewa upendeleo maalumu.

Na hata kwenye maeneo ya kuangalia nyaraka za uraia na makazi kwenye viwanja vya ndege,wenzetu hujitahidi kuhakikisha kuwa raia wao hawapati usumbufu mkubwa kama ule tunaoupata wageni na wapita njia kama akina sie.Angalau pale uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Nyerere kuna kutenganishwa kati ya Watanzania,raia wa Afrika Mashariki na wengineo,lakini wengi mtakubaliana nami kuwa tuna kasumba ya kuwanyenyekea wageni kulko tunavyowanyenyekea Watanzania wenzetu.Wawekezaji feki wamekuwa wakiitumia vizuri fursa hiyo sambamba na ubabaishaji wa taratibu za mikataba kuhakikisha kwamba wanachuma vya kutosha na pale wanapovimbiwa wanaamua kuondoka bila matatizo.

Wageni hapa Uingereza wana uwezo wa kuomba viza ya makazi kwa kigezo cha biashara ndogondogo kwa wale wenye uwezo mdogo au biashara kubwa kwa wale wenye uwezo wa kutosha.Nizungumzie hilo kundi la kwanza ambalo kimsingi linatoa mwanya kwa wageni wengi zaidi kutokana na ukweli kwamba mtaji unaohitajika sio mkubwa sana.Kinachowakwamishwa wengi ni umakini katika utaratibu mzima ambao hautoi fursa hata chembe kwa wababaishaji.Mwingereza hawezi kukubali uje uwekeze nchini mwake kwenye sekta ya usafiri wa reli ilhali unategemea mabehewa na injini chakavu kutoka huko ulikotoka.

Tatizo la kunyenyekea haliishii kwenye uwekezaji pekee bali hata kwa taasisi nyingine zinazopaswa kujiendesha kibiashara badala ya kutegemea ruzuku ya serikali.Niliposikia Dawasco ikitangaza kwamba itakata huduma ya maji “kwa vigogo” nilibaki najiuliza kama mamlaka hiyo ingeweza kutoa tishio la namna hiyo iwapo wadeni wake wangekuwa ni wale wa “uswahilini” (kama maji yangekuwa yanapatikana huko).Kama ilivyo kwa Tanesco (na pengine hata TTCL),malalamiko makubwa ya makampuni hayo ni kwamba huwa wanaingiliwa na vigogo kila wanapowabana wadaiwa sugu.Nisichoelewa ni hofu ya vigogo wa makampuni hayo kuchukua hatua madhubuti dhidi ya vigogo wanaowatisha hasa ikizingatiwa kuwa Mkurgenzi wa Dawasco au Tanesco anateuliwa na Rais,kwahiyo wakitishiwa na vigogo wengine wanaweza kabisa kukimbilia kwa Rais kumjulisha wanavyosumbuliwa na vigogo wadaiwa sugu.Japo najua itakuwa ni usumbufu usio na lazima kwa Mkuu wa nchi,lakini naamini kwamba iwapo makampuni yanayokwamishwa na vigogo ambao ni wadeni sugu yakiwajulisha vigogo hao kwamba yanawakatia huduma na “wakileta zao za kuleta” watawaripoti kwa Rais ni lazima watalipa madeni hayo.

Lakini pengine taarifa za hivi karibuni kuwa miongoni mwa wadaiwa wa DAWASCO ni pamoja na Waziri wa Maji zinaweza kutufanya tuionee huruma Mamlaka hiyo.Katika utetezi wake,Waziri huyo anadai kuwa hajawahi kupata huduma ya maji kwa miaka kadhaa,na amekuwa akinunua maji kutoka kwa wafanyabiashara.Swali linakuja,je iwapo yeye kama waziri wa maji anatumiwa bili ilhali hapatiwi huduma ya maji alifanya jitihada gani kuhakikisha sio yeye tu bali Watanzania wengine hawakumbani na adha hiyo?Mbona alikuwa kimya siku zote hizi?Hivi karibuni,Mkuu wa polisi wa usalama barabarani huko Wales alilazimika kujiuzulu baada ya kunaswa na kamera zinazodhibiti mwendo kasi barabarani akiwa anaendesha gari yake zaidi ya kiwango kinachoruhisiwa kisheria.Kwa kuvunja sheria aliyopaswa kuisimamia,kamanda huyo alilazimika kujiuzulu.

Sitarajii waziri wa maji kujiuzulu kutokana na deni hilo,na wala sitarajii hilo kwa mawaziri na vigogo wengine wanaodaiwa kwa vile msamiati “KUJIUZULU” ulishafutika kwenye kamusi ya medani ya uongozi huko nyumbani.Ni udhaifu wa namna hii unaowapa jeuri wawekezaji feki kwani kabla ya kuingia mikataba huwa wanasema udhaifu wa hao waliopewa mamlaka ya kusaini mikataba ya uwekezaji.Kwa mtaji huu,ndoto ya maisha bora kwa kila Mtanzania ina safari ndefu sana kutimia.


Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.