Showing posts with label THE GAME. Show all posts
Showing posts with label THE GAME. Show all posts

11 Sept 2008

Sidhani kama kuna ubishi kwamba Kanye West ana kipaji cha hali ya juu katika muziki,both as a rapper and a producer.Sasa sijui ni yale ya mgema akisifiwa tembo hulitia maji au ni matokeo ya ile ajali ambayo almanusura ichukue uhai wake,lakini something is wrong with Kanye.Hebu angalia HAPA kasheshe aliyoizua leo huko Los Angeles Airport.

Hapa chini kuna kazi mbili za msanii huyo.Ya kwanza ni wimbo wake mwenyewe wa Through The Wire na ya pili ya ni production yake kwa The Game katika wimbo Dreams.




12 Jan 2008

Afrika imetoa mastaa kadhaa waliotamba na wanaotikisa nchini Marekani na duniani kwa ujumla."Zaire" ilitupatia Dikembe Mutombo na Senegal imetuzawadia Akon.Tanzania nayo inaelekea kupata kitu zaidi ya umaarufu wa Mlima Kilimanjaro au mbuga ya Selous.Hapa namzungumzia TK...TEDDY KALONGA,Mtanzania anayeleta matumaini ya kuliweka jina la nchi yetu kwenye ramani huko Hollywood.Mwenyewe anasema "kuna vipaji na taaluma,uzoefu na nia",nukuu ambayo imenivutia sana hadi nimeinakili kwenye msahafu wangu wa nukuu.Mwanadada huyu ambaye ndiye "covergirl" katika toleo la mwezi Desemba 2007 la jarida la MIMI,anaelezea kwamba kwake tafsiri ya neno "mafanikio" (success)ni kuwa na furaha,afya njema na jina linalojulikana duniani...na utajiri" (nani asiyependa kuwa tajiri?).Pia anadhamiria kuwa mfano wa kuigwa (role model) kwa wanawake wa Kiafrika.Inapendeza kuona tunazungumzia Mtanzania mwenzetu ambaye Hollywood,sehemu ngumu kabisa "kuitawala " sio tu mahala anapoishi bali pia ni eneo lake la kazi.Trust me,ni rahisi zaidi kuukamata udaktari wa falsafa kuliko kuikamata Hollywood,na kwa hilo dada yetu TK (ambaye blogu yake inapatikana hapa) anastahili kila anaina ya sapoti kutoka kwetu tunaopenda kuona Tanzania haiishii kutajwa kwenye media kwa habari za ufisadi kama ule wa BOT bali pia kwa mambo mazuri kama namna akina Mutombo na Akon walivyoweza kufanya kwa nchi zao na bara letu kwa ujumla.Big up,TK!!!!

For TK & all go-getter sistaz&brothers out there,here is an inspirational message from NAS....I Know I can





And who wouldn't fancy CRUISIN' when both ends meet?

And this is for all you having DREAMS (at least not in a gansta way)

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.