Showing posts with label TID. Show all posts
Showing posts with label TID. Show all posts

14 May 2010

Picha kwa Hisani ya SARAH wa Angalia Bongo.

Bila shaka ushaskia msemo wa Kiswahili 'Kufa Kufaana'.Nadhani kwa kimombo ndio tunachoita 'blessing in disguise'.Na ndivyo inavyoelekea kutokea katika sakata la 'ugomvi' kati ya msanii T.I.D na supastaa wa mpira wa kikapu,Mtanzania Hasheem Thabit,anayechezea timu ya Memphis Grizzliers kwenye ligi maarufu ya NBA huko Marekani.Katika pitapita yangu mtandaoni nimekuta habari hiyo imeshadakwa na vyombo vya habari vya kimataifa.Why not wakati Hasheem ni jina kubwa huko Marekani?

Sasa yayumkinika kusema kuwa sakata hilo limemnufaisha T.I.D 'kiaina' kwa vile katika kuripoti habari hiyo jina lake pia limekuwa likitajwa kama inavyoonekana katika habari ifuatayo kwenye mtandao wa kituo cha runinga cha FOX MEMPHIS cha huko Marekani:

MEMPHIS, Tenn. - The agent for Memphis Grizzlies center Hasheem Thabeet has told the team that an alleged incident involving Thabeet and R&B singer T.I.D never took place.


FOX13 Sports Director Matt Stark spoke with Ugo Udezue, Thabeet's agent, by phone Tuesday night, and Mr. Udezue said the allegations that Hasheem had knocked out the singer were completely false.


Udezue acknowledged that Thabeet was in a nightclub last weekend when an altercation broke out, but that the Grizzlies center was in a private section of the club and being protected by three bodyguards at the time, which is the norm for Thabeet when staying in Tanzania. Udezue says his client was immediately removed from the club, and was stunned later to hear the allegations that he had been involved.


Udezue said he believes the singer made the story up as a publicity stunt, and to get his music played on the radio.


Habari hiyo imekamata kasi kwenye mtandao kama inavyoonyesha HAPA.Japo natambua kuwa msanii T.I.D  'ana jina' kiasi chake katika anga za kimataifa,lakini ni dhahiri tukio hili linaweza kuwa limemtangaza zaidi kuliko ilivyokuwa hapo awali.

I just hope ugomvi huo haukuwa publicity stunt na publicity iliyojitokeza kwa T.I.D ni coincidental tu.Otherwise,mastaa wa kimataifa wataendelea kukutana na zahma kama hizo kwani zinaelekea kuwa na manufaa kwa upande mmoja wa wahusika wa tukio.

Ama kweli kufa kufaana!

11 Nov 2008


Msanii wa muziki wa kizazi kipya, Khalid Mohamed maarufu kama TID, amekata rufaa katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam kupinga adhabu ya kifungo cha mwaka mmoja jela alichohukumiwa mwaka huu. 

Rufani hiyo ya msanii huyo ambaye tangu ahukumiwe kifungo hicho amekwishatumikia adhabu hiyo kwa miezi minne, itaanza kusikilizwa leo na Jaji Robert Makaramba; kwa mujibu wa habari zilizotolewa na ofisa mmoja wa mahakama hiyo. 

TID alihukumiwa kwenda jela mwaka mmoja kutokana na kutiwa hatiani kwa kosa la kushambulia na kumjeruhi kichwani na mkononi kijana aliyefahamika kwa jina la Ben Mashibe. Msanii huyo alimjeruhi Mashibe kichwani na mkononi kwa kutumia chombo cha kuwekea majivu ya sigara ‘ash tray’ na alisomewa mashtaka hayo mara ya kwanza Julai 10, mwaka huu mbele ya Hakimu Hamisa Kalombola wa Mahakama ya Wilaya ya Kinondoni. 

Mwendesha Mashtaka wa kesi hiyo, Inspekta Nyagabona alidai TID alitenda kosa hilo Julai 2, mwaka jana saa sita na nusu usiku katika Hoteli ya Slipway iliyopo Msasani Dar es Salaam. TID mwenye umri wa miaka 26, alitiwa hatiani na Hakimu Kalombola baada ya hakimu huyo kuridhika na ushahidi uliotolewa na mashahidi wanne walioletwa mahakamani na upande wa mashitaka

22 Jan 2008

Usiku huu (kwa saa za hapa Uingereza) msanii wa Bongofleva,T.I.D,alifanya mahojiano mafupi na kituo cha runinga cha BEN cha jijini London,kuhusu ziara ya msanii huyo nchini hapa.Inapendeza kuona msanii kutoka nyumbani akihojiwa,lakini nahisi kulikuwa na tatizo kidogo katika mfumo wa mahojiano hayo ambapo kwa mtizamo wangu,nadhani mtangazaji alitaka interview iwe ya Kiswahili lakini T.I.D alijibu maswali mengi kwa "Lugha ya Mama" (kimombo),japo sina budi kumsifu kwamba aliimudu kwa kiasi chake.Pia sidhani kama mtangazaji huyo atajiskia vibaya iwapo atatokea mtu wa kuhoji kama alijiandaa vya kutosha kufanya mahojiano hayo au ilikuwa ni ghafla.Anyway,kuna clips mbili hapa nilizozirekodi kwa kutumia simu ya zamani kidogo,Sony Ericsson W810i lakini nadhani itakuwa imejitahidi kwenye ubora wa video.Enjoy


Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.