Showing posts with label TRL. Show all posts
Showing posts with label TRL. Show all posts

8 Jun 2009


WHY SHOULD WE ALWAYS LESS,IF NOT NOTHING AT ALL?HIVI TUNGEKUWA NA WAWEKEZAJI NCHINI INDIA (WANAKOTOKA WABABAISHAJI WA TRL) HALAFU WASHINDWE KUKIDHI MATARAJIO YA WAHINDI,UNADHANI WASINGETIMULIWA?POROJO KWAMBA PASIPO TRL HUDUMA ZA RELI YA KATI NDIO KWISHNE HAZIINGII AKILINI HATA KIDOGO.KAMA TUNAWEZA KUWALIPA WABUNGE WETU MAMILIONI YA SHILINGI KILA MWEZI PASIPO KUHITAJI MSAADA WA WAWEKEZAJI,SIONI KWANINI TUSHINDWE KUMUDU UENDESHAJI WA HUDUMA YA TRENI RELI YA KATI.




Abiria 552 waliotakiwa kusafiri na treni ya kati juzi, wamekwama jijini Dar es Salaam baada ya wafanyakazi wa Kampuni ya ReliTanzania (TRL), kugoma kwa lengo la kushinikiza uongozi wa shirika hilo, kusaini mkataba wa Maisha Bora unaojulikana kwa jina la Mkataba wa Hiyari.

Wakizungumza na 'HabariLeo Jumapili' katika nyakati tofauti, baadhi ya abiria waliokuwa wakitarajia kwenda Tabora, Mwanza na Kigoma, walisema walipaswa kusafiri juzi lakini ilipofika saa mbili usiku, walitangaziwa kuwa safari hiyo haipo na kutakiwa kusubiri hadi kesho yake (jana) kujua hatma ya safari hiyo.

“Kweli tulisubiri na ilipofika leo (jana) saa tano, tulitangaziwa kuwa safari haitakuwapo hivyo tujipange kwenye mstari ili turudishiwe nauli zetu. “Sisi tumefedheheshwa sana na kitendo hiki hivyo tunaiomba serikali ichukue hatua madhubuti ili abiria wanaotegemea usafiri wa treni wasiendelee kuumia,” alisema abiria aliyejitambulisha kwa jina la Masanja Said.

HabariLeo Jumapili imeshuhudia abiria wakiwa katika mistari mirefu wakisubiri kurejeshewa fedha za nauli wakati watoto na wazee walikuwa wamelala sakafuni kwenye jengo la kampuni hiyo. Meneja Uhusiano wa TRL, Midladjy Maez, alisema mgomo huo hautambuliki kisheria kwa kuwa viongozi wa Chama cha Wafanyakazi wa Reli (Trawu) wanasema hawajatangaza mgomo.

“Baada ya wafanyakazi kugoma, uongozi uliwasiliana na viongozi wa Trawu lakini viongozi hao walisema hawajatangaza mgomo kwani kisheria tangazo la mgomo linatolewa saa 48 kabla ya kuanzamgomo. Hata hivyo hakuna tangazo lolote wala kiongozi wa mgomo hajulikani,” alisema Meaz.

Inadaiwa kuwa wafanyakazi hao waligoma baada ya viongozi wa Trawu kuwapatia ripoti kwamba uongozi wa kampuni umegoma kusaini mkataba wahiyari na kwamba uongozi umeondoa kipengele kinachomtaka mwajiri kuwalipa wafanyakazi wanaopunguzwa kazi mishahara ya miezi 20 hadi 40 kama mkono wa heri.

Meaz alisema, uongozi wa TRL uliamua kurejeshea abiria fedha zao baada ya juhudi za kuwataka wafanyakazi hao kusitisha mgomo kutozaa matunda. Alisema uongozi umejaribu kuwasiliana na TRAWU Taifa na kujibiwa kuwa hakuna mgomo ila ni shinikizo.

“Tatizo haijulikani nani kiongozi wa mgomo, kila anayeulizwa anasema hajui lolote. Kisheria hakuna mgomo lakini katika hali halisi wafanyakazi wamegoma na ndio maana abiria wamerudishiwa fedha zao za nauli,” alisema Meaz. Juhudi za kuwapata viongozi wa Trawu haikuzaa matundakwa kuwa ofisi zao zilikuwa zimefungwa pia simu za mkononi zilikuwa zimefungwa.

CHANZO: Habari Leo


11 Apr 2009

MAELEZO YA PICHA KUTOKA KATIKA GAZETI LA HABARI LEO YANASOMEKA:

Behewa la mafuta la TRL liliacha njia eneo la Kurasini, Dar es Salaam na kuanguka.Wafanyakazi wa kampuni hiyo walikutwa wakikinga mafuta hayo ili kuyahifadhi katika mapipa chini ya ulinzi mkali wa polisi. (Picha na Yusuf Badi).
NADHANI MWENZANGU PIA UKIANGALIA PICHA HIYO KWA MAKINI UTABAKI UNAJIULIZA KWAMBA HAO WAHINDI WA TRL NI WAWEKEZAJI KWELI AU VIINIMACHO?TALKING OF VIINIMACHO,YAYUMKINIKA KUJIULIZA IWAPO HAWA JAMAA HAWAJAWAROGA HAO WANAONG'ANG'ANIA KUENDELEZA MKATABA WA KIMAZINGAOMBWE NA TRL.KAMA ILIVYO DESTURI YETU YA ZIMAMOTO,TUNASUBIRI WALIKOROGE KWANZA,KISHA WAINGIE MITINI HALAFU KUNYWA TULINYWE SIE!NA HAPA NENO "KULIKOROGA" LINAMAANISHA KU-MESS UP NA MAISHA YA ABIRIA WANAOTEGEMEA USAFIRI WA RELI YA KATI.

22 Dec 2008

Photo courtesy of MJENGWA

KURA YANGU INAWAANGUKIA WABABAISHAJI WA TRL.CHEKI "MBELEKO" NYINGINE HII KUTOKA KWA SUMATRA:

HATIMAYE Kampuni ya MAMLAKA ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra), imeiruhusu Kampuni ya Reli (TRL) kuanza kutumia mabehewa yake 23 ya mitumba yaliyokodishwa kutoka Kampuni ya Reli ya India. Awali Sumatra waliizuia TRL kutumia mahehewa hayo kwa madai kwamba hayakuwa na obora unaotakiwa.

Hata hivyo, meneja uhusiano wa TRL, Midrahji Meiz alisema jana kuwa Sumatra sasa imewaruhusu kuendelea kutumia mabehewa hayo baada ya vigezo vilivyokuwa vinahitajika kukamilika.

“Tumesharuhusiwa na Sumatra kuanza kutumia mahehewa hayo na hivi sasa utaratibu unafanyika ili yanze kusafirisha abiria... baada ya utaratibu huo kukamilika tutatoa taarifa rasmi,” alisema Meiz na kuongeza: “Suala la usafiri wa treni ni suala la msingi kabisa na ndiyo maana tunajitahidi kuboresha usafiri huo kila wakati ili abiria wasafiri katika mazingira mazuri.”

Mkurugenzi na mdhibiti wa reli wa Sumatra, Alfred Nalitolela alikiri kuwepo kwa suala hilo na kusema kuwa wameamua kuiruhusu TRL indelee kutumia mabehewa hayo kwa kuwa wamekamilisha marekebisho yaliyokuwa yanahitajika.

“Tulibaini kwamba mabehewa hayo hayana ubora unaostahili kwa matumizi ya reli yetu, na moja ya vitu hivyo ni kiungio kati ya behewa moja na jingine, usambazi wa umeme ndani ya mabehewa, belling, spring, breki ya mkononi na magurudumu,” alisema Nalitolela na kuongeza:

“Tulipokwenda India kukagua mabehewa hayo, tuliwaeleza wafanye vitu hivyo lakini wakaleta mabehewa kabla ya kukamilika kwake ndipo ikabidi tuwakataze kuyatumia mpaka wamalize kuyafanyia marekebisho hayo.”

Alifafanua kwamba baada ya hapo walichukuwa moja ya kiungio cha mabehewa na kuyapeleka katika maabara ya ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na kuyafanyia utafiti kama ni vifaa vipya na kuomba maelezo ya kina.

“Unafahamu katika suala hili lile jumba la behewa ndilo linalotakiwa kuwa mtumba, lakini vifaa vyote vinavyofanya mabehewa hayo yafanye kazi vinatakiwa kuwa vipya, ikiwemo usambaji wa nyaya za umeme ndani ya behewa. Na hicho ndicho tunachokikagua na kukiangalia na kuhakikisha kwamba viko salama kila wakati,” alifafanua Nalitolela.
CHANZO:Mwananchi
JE MWENZANGU KURA YAKO INAANGUKIA WAPI?


KAMPUNI iliyopewa jukumu la kusimamia na kutunza mali za lililokuwa Shirika la Reli Tanzania (RAHCO), imeanza kukatakata injini 27 na mabehewa 19 ili yauzwe kama chuma chakavu.

Mabehewa hayo na injini zake yanadaiwa yalikuwa na hali nzuri, lakini mwekezaji akayakataa wakati anachukua shirika kwa maelezo kuwa hayamfai.

Habari zilizopatikana zinaeleza kuwa hatua hiyo imefikiwa baada ya mwekezaji Kampuni ya Reli Tanzania (TRL) kudai kuwa, mabehewa hayo yalikuwa yamechakaa zaidi na hayawezi kutumiwa tena, huku Rahco ikidai kuwa yalikuwa yanafaa kuendelea kutumika.

Tayari zabuni ya kupata makampuni ya kununua vyuma hivyo chakavu imeshafanyika na washindi kupatikana.

Makampuni ambayo yameshinda zabuni yameshaanza kukata mabehewa hayo na injini katika mikoa ya Dar es Salaam, Morogoro, Tabora na Kigoma.

Mwananchi Jumapili wiki hii ilishuhudia baadhi ya mafundi wa kampuni iliyoshinda zabuni wakikata mabehewa yaliyopo katika Stesheni ya Dar es Salaam.

Meneja Uhusiano wa RAHCO, Musita John aliiambia Mwananchi Jumapili kuwa, wameamua kuchukua hatua hiyo baada ya kushindwa kuzifanyia kazi injini hizo na mabehewa.

Alisema kuwa endapo injini hizo na mabehewa zingefanyiwa ukarabati mdogo zingeendelea kuisaidia kampuni hiyo kupunguza matatizo ya usafiri lakini mwekezaji hakuzikubali.

John alisema wakati mwekezaji anachukua shirika hilo alikuta jumla ya injini 116 na 92 kati yake zilikuwa zinafanya kazi, lakini yeye aliamua kuchukuwa 79 tu na zingine akazikataa kwa madai kwamba hazimfai.

Alisema mbali na injini hizo, pia alikuta jumla ya mabehewa ya abiria 164, yaliyokuwa yanafanya kazi ni 125, lakini yeye aliamua kuchukuwa mabehewa 106 tu na 19 yaliyobaki aliyakataa.

John alifafanua kwamba baada ya mwekezaji huyo kumaliza tathimini ya mali za TRC alizokuta kabla hajaanza kazi waliamua kuziweka katika madaraja mbalimbali, ambapo daraja (A) lilikuwa ni mabehewa na injini yaliyokuwa yanafanya kazi.

Alisema Daraja (B) lilikuwa ni la mabehewa na injini zilizokuwa zinahitaji matengenezo madogo, ingawa yalikuwa bado yanaendelea na kazi ya kusafirisha abiria na mizigo wakati daraja (C) ni yale ambayo alikuta yameondolewa kazini, baada ya kuharibika na kupelekwa kwenye karakana ili yafanyiwe ukarabati, lakini pia aliyakataa kwa madai kwamba hayamfai.

Aliongeza kuwa kulikuwa na daraja (D) ambalo lilihusisha injini na mabehewa yaliyoharibika, yasiyofaa kutumika na daraja E ni yale ambayo yalishakaguliwa na kubainika kwamba, yalishafikia katika kiwango cha vyuma chakavu.

Hata hivyo, habari kutoka ndani ya TRL, zinaeleza kwamba mbali na injini na mabehewa hayo, mali zingine ambazo mwekezaji huyo alizikataa ni vifaa vya ofisini ambavyo hivi sasa pia viko katika orodha ya vitu vinavyouzwa na RAHCO kama vyuma chakavu.

Wakati RAHCO ikiendelea kukatakata injini hizo na mabehewa TRL hivi sasa inadaiwa kuwa katika hali mbaya kutokana na baadhi ya injini zake aina ya ‘73 class’ zilizokodishwa kutoka India kuwa na uwezo mdogo wa kuvuta mzigo, kiasi kwamba wanalazimika kuziunganisha mbili ndipo ziweze kuvuta mzigo ambao ungevutwa na injini moja aina ‘88 class’ za Tanzania alizozikataa.

Meneja Uhusiano wa TRL, Midlajy Maez alipotakiwa kutoa ufafanuzi wake kuhusiana na suala hilo alisema wanaotakiwa kulizunguzia ni RAHCO.

CHANZO:Mwananchi

HIVI KWANINI TUNAENDELEA KUWANG'ANG'ANIA HAWA WABABAISHAJI WA KIDOSI?JIBU JEPESI NI KWAMBA WALIOWAKARIBISHA NI WABABISHAJI WENZAO,SO SIO RAHISI KWAO KUONA UBABAISHAJI ULIOPO.TUNA WAZIRI,NAIBU WAZIRI,KATIBU MKUU,NAIBU KATIKA MKUU,MKURUGENZI,NK,NK,NK WOTE KATIKA WIZARA HUSIKA.HAWA WANALIPWA MSHAHARA NA MARUPURUPU MENGINE KUTOKA KWA WALIPA KODI WA TANZANIA LAKINI SIJUI WANASHINDWA NINI KUCHUKUA HATUA STAHILI DHIDI YA USANII HUU ULIOPEWA JINA LA UWEKEZAJI.MWEKEZAJI GANI AMBAYE ILI ALIPE MSHAHARA KWA WAAJIRIWA WAKE NI LAZIMA APEWE TAFU NA SERIKALI?

KAMA KAWAIDA,JAMAA WATAHARIBU RELI WEE MPAKA IWE TOO MUCH THEN WATAINGIA MITINI,AU MZEMBE FLANI ATAKURUPUKA USINGIZINI NA KUDAI IUNDWE TUME YA UCHUNGUZI (ISOMEKE TUME YA KULA FEDHA ZA VIKAO) LAKINI WAKATI HUO HUDUMA YA RELI YA KATI ITAKUWA IMEKUFA KABISA.CALL IT MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA AS WE ARE APPROACHING 2009!

8 Nov 2008


SERIKALI kwa mara nyingine imeingilia kati na kuamua kulipa mishahara ya wafanyakazi wa Kampuni ya Reli Tanzania (TRL), baada ya mwekezaji wake kushindwa kulipa mishahara ya mwezi uliopita.

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, alitangaza uamuzi huo bungeni jana, alipokuwa akijibu swali la papo kwa hapo la Mbunge wa Viti Maalumu, Halima Mamuya (CCM), aliyetaka kujua mpango wa serikali katika kuhakikisha mwekezaji huyo anaiendesha kampuni hiyo kwa ufanisi na kama alikuwa akijua kuwa hadi jana wafanyakazi wa kampuni hiyo walikuwa hawajalipwa mishahara yao ya mwezi uliopita.

“Serikali imelichukua tena tatizo hilo na tunalifanyia kazi. Ninaahidi kuanzia sasa wafanyakazi hawa hawatakosa tena mishahara, tutajaribu kuona kama hiyo nyongeza tutaweza kuilipa,” alisema Pinda.

Agosti, mwaka huu, tatizo la wafanyakazi kukosa mishahara lilipotokea kwa mara ya kwanza, Waziri Mkuu ndiye aliyekuwa mtu wa kwanza kuokoa jahazi na hadi jana na juzi alikuwa akihaha kuhakikisha wafanyakazi hao wanalipwa mishahara yao ya Oktoba.

“Hadi juzi nilikuwa nahangaikia suala hili, ahadi ya serikali ilimalizika Agosti na tulitarajia uongozi wa TRL ungeendelea kulipa viwango vipya vya mishahara kuanzia Oktoba kama tulivyokubaliana, lakini kwa bahati mbaya wameshindwa na tunalazimika tena kulipia mishahara ya wafanyakazi hao hadi Novemba,” alisema Pinda.

Hii ni mara ya tatu kwa serikali kulazimika kuiokoa kampuni hiyo, baada ya uongozi wake kushindwa kulipa mishahara ya wafanyakazi.

Miezi mitano tangu mwekezaji alipolichukua shirika hilo wakati huo likiitwa Shirika la Reli Tanzania (TRC), serikali iliingia mfukoni na kutoa fedha za walipa kodi zaidi ya sh bilioni tatu kuikopesha TRL kwa ajili ya kulipa mishahara ya wafanyakazi.

Septemba, mwaka huu, TRL ilikwama tena kulipia viwango vipya vya mishahara na serikali iliamua kulipa mishahara ya mwezi huo kwa ahadi kwamba kuanzia Oktoba mwekezaji angeweza kuendelea kulipa wafanyakazi wake bila matatizo.

Kampuni hiyo imeshindwa tena kulipa mishahara ya mwezi uliopita. Serikali kwa mara ya tatu sasa inajikuta ikilazimika kuingia tena mfukoni kuokoa jahazi.

Juzi wafanyakazi wa TRL walitangaza kuanza mgomo baridi, huku wakisubiri hatua zinazochukuliwa na mwekezaji kuikoa kampuni hiyo. Mbali na sula la TRL, Waziri Pinda pia alizungumzia suala la kuvuja kwa mitihani aliposema serikali inaliangalia kwa umakini Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA) kwani ndipo penye tatizo.

Serikali inajitahidi kuangalia namna bora ya kulisimamia kwani ni aibu kwa taifa kukaa na kuulizana maswali juu ya uvujaji wa mitihani. Amewataka wazazi na wanafunzi wanaotafuta mitihani kuacha kuendekeza tabia hiyo ya aibu.

“Natoa rai kwa wazazi kuwa tusikubali na tuwe wa kwanza kutoa taarifa tunapoona watoto wana mitihani ya kununua,” alisema Pinda.

Jibu hilo la Waziri Pinda lilitokana na swali la Mbunge wa Viti Maalum, Magdalena Sakaya (CUF), aliyetaka kujua mpango wa serikali katika kukabiliana na tatizo la kuvuja kwa mitihani na uchapishaji wa vyeti feki vinavyosambazwa mashuleni na kusababisha kushuka kwa kiwango cha elimu nchini.

Akizungumzia hali ya kiuendeshaji ya Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL), Pinda alikiri kwamba kwa sasa kampuni hiyo iko taabani, hali iliyosababisha serikali ilazimike kufanya mazungumzo na shirika moja nchini China, lengo likiwa ni kuinusuru ATCL katika hali hiyo mbaya.

Akijibu swali la Mbunge wa Vunjo, Aloyce Kimaro, aliyeitaka serikali ichukue jukumu la kununua vitabu vya kiada kwa shule za msingi na sekondari na kuvisambaza badala ya jukumu la sasa la kutumia wakandarasi, Waziri Pinda alisema utaratibu wa sasa ni kwamba serikali inatoa fedha kwa halmashauri, nazo zinatumia wakandarasi ambao wengine si waaminifu.

“Wakandarasi mara nyingine hununua vitabu vya mitaani vinavyokuwa katika kiwango cha chini, hivyo tumekubaliana na wizara tutafute utaratibu mzuri wa upatikanaji wa vitabu,” alisema.


CHANZO: Tanzania Daima

KUMWOKOA MWEKEZAJI KILA ANAPOKWAMA SIO UFUMBUZI,BALI UAHIRISHAJI WA UFUMBUZI,WA TATIZO.NI MUHIMU KUJIULIZA HUYU MWEKEZAJI ATAENDELEA KUOKOLEWA HADI LINI,AND WHAT'D HAPPEN IF HATOOKOLEWA!

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.