Showing posts with label UBABAISHAJI. Show all posts
Showing posts with label UBABAISHAJI. Show all posts

24 Jul 2013



Naam, Tanzania yetu imewahi kuwa na viongozi mbalimbali wabovu, lakini linapokuja suala la mawaziri wakuu, basi Mizengo Kayanda Pinda, anaweza kabisa kuingia kwenye kumbukumbu kama WAZIRI MKUU MBOVU KULIKO WOTE KATIKA HISTORIA YA NCHI YETU.

Ndio, Kuna Edward Lowassa, aliyeng'oka kwa kashfa ya Richmond, lakini angalau yeye hakuwa m-babaishaji katika kauli zake. N apengine kilichmosaidia Lowassa ni kutambua busara kuwa mdomo sharti ushirikiane na ubongo kabla ya kutoa kauli yoyote ile.

Pinda, anayeitwa Mtoto wa Mkulima, amekuwa maarufu zaidi kwa kauli zake za kipuuzi kuliko utendaji kazi.Mbabaishaji huyo aliwahi kuzua sokomoko huko nyuma alipohalalisha MAUAJI: kwa uzembe tu wa kufikiri, Pinda alidai kuwa anaguswa sana na mauaji ya maalbino,kwahiyo ni ruksa kwa wananchi kuwauwa WATUHUMIWA wa mauaji hayo. Japo kitaaluma  mwanasheria, lakini Pinda hakuona tatizo katika kauli yake hiyo ambayo kimsingi ilikuwa inahamisha nguvu za polisi na mahakama na kuzikabidhi kwa umma.Kwa lugha nyingine, mzembe huyo alikuwa anahalalisha mob justice.

Badala ya ku-behave kama mtu mzima, Pinda akenda bungeni na kujitetea kwa KULIA KAMA MTOTO.Lakini kwa bahati nzuri, wengi wa wabunge wetu wapo bize zaidi na posho zao kuliko kuwatendea haki wananchi wanaowawakilisha, na machozi hayo ya kinafiki ya Pinda yakamnusuru.


Katika kuonyesha kuwa Tanzania kwa sasa ni kama haina Waziri Mkuu kwani Pinda anayeshikilia nafasi hiyo ni so useless kiasi kwamba uwepo au kutokuwepo kwake hakuna tofauti, majuzi akakurupuka tena na kauli nyingine ya kibabaishaji.Akatangaza kuwa ni ruksa kwa polisi kupiga raia ZAIDI...Yaani kana kwamba unyanyasaji unaofanywa na polisi hautoshi, na sasa wanahamasishwa kutoa vipigo zaidi.

Watu tumesema weee kuhusu kauli hiyo ya kihuni lakini kwa vile aliyemteua Pinda kushika nafasi hiyo hana tofauti sana na Pinda, Waziri Mkuu huyo bado yupo madarakani hadi dakika hii.

Na uwepo wake huo umepelekea ujinga mwingine. Majuzi kumezuka sokomoko la kodi mpya ya SIM kadi.Badala ya kusikia kilio cha mamilioni ya Watanzania wanaopinga kodi hiyo, mropokaji Pinda akadai eti "wanaopinga kodi hiyo hawaitakii mema nchi yetu..." COMPLETELY USELESS!

Bahati nzuri, safari hii Rais Kikwete kaamua kutumia busara, na kwa namna flani, amemudu KUMUUMBUA PINDA. Rais amezitaka mamlaka husika kukaa pamoja kutafuta ufumbuzi wa haraka kuhusu kodi hiyo inayolalamikiwa na wananchi wengi. Rais aliyasema hayo alipokutana na viongozi wa Wizara ya Fedha, na wale wa Wizara ya Sayansi na Teknolojia, na Mamlaka ya Mawasiliano TCRA.

SIJUI MTOTO WA MKULIMA ANAJISIKIAJE MUDA HUU....ONE THING FOR SURE, PINDA AMETHIBITISHA KWA MARA NYINGINE KUWA YEYE NI MTU MZIMA OVYO ASIYEFAA HATA KUONGOZA DARASA KAMA KIRANJA, ACHILIA MBALI HUO UWAZIRI MKUU.NI WABABSIAHJI KAMA PINDA WANAOIFANYA SIASA KUWA MCHEZO MCHAFU ZAIDI YA UCHAFU WA SIASA.

CAN'T WAIT TO SEE HIM GONE COME 2015, OR EVEN EARLIER...GOOD RIDDANCE.

6 Jun 2013



Serikali yaumbuka sekta ya elimu
•  KITABU CHA HESABU CHAONESHA 2X7=15

na Edson Kamukara
SERIKALI imeingia katika kashfa nyingine kwenye sekta ya elimu baada ya kudaiwa kuruhusu vitabu vyenye maelekezo yasiyo sahihi.

Mbunge wa kuteuliwa na rais, James Mbatia (NCCR-Mageuzi) ndiye aliyeanika udhaifu uliomo kwenye vitabu vilivyoidhinishwa na serikali kutumika katika shule za msingi nchini ambapo aliviita ni sumu ya elimu.

Akichangia hotuba ya bajeti ya Wizara ya Elimu, Mbatia alionesha vitabu kadhaa bungeni huku akitaja makosa mengi yaliyomo na kuhoji viliidhinishwaje na Kamati ya Kuidhinisha Machapisho ya Kielimu (EMAC).

“Leo tunavuna tulichokipanda. Serikali imetumia fedha za chenji ya rada kusaini mikataba na kampuni zaidi ya 10 kwa ajili ya kusambaza vitabu kwenye shule zetu, lakini vitabu hivyo ni sumu kwa taifa,” alisema.

Alisema kuwa vitabu hivyo vimenunuliwa na fedha hizo sh bilioni 55.2 ambazo zilitengwa na serikali kwa ajili ya manunuzi ya vitabu na mihutasari.

Alisema kampuni hizo zilipewa mkataba wa zabuni ya kununua vitabu na mihutasari wa sh milioni 18 na ulisainiwa Machi 18 mwaka huu, huku wakitakiwa kumaliza ununuzi na usambazaji wake Septemba mwaka huu.

Mbatia alisema kuwa vitabu hivyo vikitumika vitalisababisha taifa kufa kielimu kwa vile watoto watajifunza mambo ambayo hayana ukweli.

Alitoa mfano wa kitabu cha Jiografia cha darasa la sita kilichoidhinishwa na EMAC ambacho kimekosewa kwa kuandikwa ‘Jografia’.

Vitabu vingine ni cha Hisabati cha darasa la nne katika ukarasa wa 49, ambapo imeandikwa sifuri gawanya kwa sifuri jibu lake ni sifuri wakati jibu sahihi ni haiwezekani.

Pia alisema kitabu cha Hisabati kingine kinaonesha 2x7=15 na kitabu cha Uraia pia kinaeleza kuwa ‘mtaa unaundwa na vitongoji mbalimbali na kuongozwa na wenyeviti wa vitongoji.

Mbatia alisema kitabu hicho kinasema kwamba wakazi wengi wa mtaa wameajiriwa na utumishi wa umma, viwanda na makampuni.

Alisema kampuni za Macmillan na Oxford zilizopewa jukumu la kuleta vitabu hivyo zimeshafukuzwa nchini Kenya baada ya kugundulika kuwa vitabu vyao havina ubora wa kitaaluma, lakini Tanzania imeendelea kuzikumbatia.

“Kama Rais Kikwete hivi karibuni akiwa Mbeya alikiri kuwa elimu yetu ina udhaifu, kwanini wabunge wa CCM hamtaki kukubali hili?” alihoji Mbatia na kupendekeza iundwe tume ya kudumu ya elimu itakayosimamia maslahi ya walimu, kasoro za elimu na mengineyo.

CCM wapindisha hoja

Katika hatua nyingine, wabunge wa CCM wamelazimika kupindisha mjadala wa hoja ya udhaifu wa elimu nchini ili kumwokoa Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk. Shukuru Kawambwa.

Hatua hiyo imetokea bungeni mjini hapa ambapo Waziri Kawambwa aliwasilisha hotuba yake ya bajeti kwa mwaka 2013/14 ambayo ilijadiliwa kwa siku mbili.

Kutokana na upinzani mkali ulioonekana tangu mapema kutoka kwa baadhi ya wabunge hasa wa upinzani, wakitaka Waziri na Naibu wake Philipo Mulugo wajiuzulu kutokana na matokeo mabaya ya kidato cha nne mwaka 2012, wabunge wa CCM walilazimika kukutana kwa dharura juzi.

Katika kikao hicho kilichoketi katika Ukumbi wa Pius Msekwa juzi saa 7:00 mchana, wabunge hao wa CCM walifundana na kuafikiana kumwokoa Waziri Kawambwa ili bajeti yake iweze kupitishwa.

Licha ya wabunge wawili wa chama hicho, Deogratius Ntukamazina (Ngara) na Said Mtanda (Mchinga) kuwa wachangiaji wa mapema kabla ya kikao hicho na hivyo kuishambulia wizara hiyo, waliofuata walikuja na visingizio vya kumwonesha waziri hana tatizo.

Katika michango yao, wabunge hao walijiegemeza kwenye hoja ya mgawanyo wa orodha ya shule za sekondari 1,200 zitakazofanyiwa ukarabati wakidai ifumuliwe kwa vile Mkoa wa Kilimanjaro umependelewa zaidi ya mikoa mingine.

Huku wakiunga mkono hoja ya waziri kwa asilimia mia moja na kisha kuanza kulalamikia kasoro zilizopo kwenye elimu, wabunge hao walimtetea Kawambwa kuwa hastahili kujiuzulu kwa vile wizara yake ina majukumu mengi yanayoingilina na Wizara ya Tamisemi.

“Jamani kusema Waziri Kawambwa ajiuzulu tunamwonea, hii wizara majukumu yake mengi yako pia Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, atawajibikaje mwenyewe kwa matokeo haya?” walisema.

Katika utetezi huo, waliongeza kuwa bajeti ya wizara hiyo ni ndogo na hivyo waziri amekwama kutekeleza majukumu yake huku wakilibebesha lawama Baraza la Taifa la Mitihani (Necta) kuwa ndilo limesababisha matokeo hayo kwa kupanga madaraja kimakosa.

Katika hatua iliyoibua msigano, wabunge hao walipendekeza serikali iunde tume nyingine ya wataalamu kuchunguza matatizo ya elimu nchini, jambo lililopingwa vikali na wapinzani wakihoji kwanini walikataa wazo hilo lilipoletwa na Mbatia.

Mbunge wa Iramba Magharibi, Mwigulu Nchemba, aliwaponda wapinzani akisema kuwa hawatambui kazi kubwa iliyofanywa na CCM na kumtaka Waziri Kawambwa achape kazi bila kuwasikiliza.

Aliitaka serikali kutowapeleka walimu wapya vituoni pasipo kuwapa fedha zao za kujikimu kwani inakuwa inatambua idadi yao, lakini akasisitiza kuwa waziri anakwamishwa na watendaji wake.

Peter Serukamba wa Kigoma Mjini, John Komba wa Mbinga Magharibi, Yahaya Kassim Issa wa Chwaka, Jason Rweikiza wa Bukoba Vijijini na Lutengano Kigola wa Mufindi Kaskazini, walilalamikia upendeleo kwenye mgawanyo wa shule, walimu kutopandishwa madaraja na Tamisemi kuondolewa majukumu ya elimu.

Hata hivyo, utetezi huo ulipingwa vikali na wabunge wa upinzani wakidai kuwa katika hilo serikali haiwezi kukwepa lawama kwa Waziri Kawambwa na naibu wake kuwajibika.

“Mimi nilikuwa mmoja wa wabunge waliopinga ugatuaji wa madaraka ya wizara hii kwenda Tamisemi, lakini wabunge wa CCM walitupinga vikali na kupitisha hoja hiyo, sasa leo mnatetea nini?

“Tamisemi iko chini ya Waziri Mkuu, kama leo tunamtetea Kawambwa na kuituhumu Tamisemi ina maana mnataka kusema Waziri Mkuu ndiye hafai,” alisema Mbunge wa Viti Maalumu Susan Lyimo (CHADEMA).

Mbunge wa Mhambwe, Felix Mkosamali (NCCR-Mageuzi) alisema kuwa hakuna tatizo jingine katika Wizara ya Elimu bali viongozi wake hawana uwezo wa kuongoza.

“Tunawaambieni kila siku kuwa hawa watu hawana uwezo wa kuongoza hii wizara…hawawezi, na msipobadilisha hawa watu tutaendelea kuimba nyimbo hizi kila siku,” alisema.
Alisema kuwa serikali inajenga shule mbovu na kuwataka wananchi wapeleke watoto wao huko wakati watoto wa viongozi hawasomi katika shule hizo.

Kuhusu Necta, alisema kuwa tangu kuingia kwa Katibu Mtendaji wa sasa, Dk. Joyce Ndalichako na wasaidizi wake, wameziba mianya yote ya wizi wa mitihani.

Mkosamali alisema kuwa wanaompiga vita wakitaka aondolewe ni wale wenye shule binafsi waliokuwa wakisababisha wizi huo ili shule zao zionekane bora.

Joseph Selelasini wa Rombo (CHADEMA) aliwashangaa baadhi ya wabunge kuibebesha lawama Necta kwa kasoro zilizojitokeza kwenye mfumo uliotumika kusahisha mitihani ya dini, ya Bible Knowledge na Islamic Knowledge akisema serikali inaendelea kukiuka katiba kwa kujihusisha na masuala ya dini wakati nchi haina dini.




14 Apr 2013



WAZIRI Mkuu, Mizengo Pinda anaweza kujikuta katika wakati mgumu, baada ya kuumbuliwa na ripoti ya tume ya uchunguzi wa matokeo mabaya ya mwaka 2010, inayodaiwa hakuifanyia kazi na badala yake akakimbilia kuunda tume nyingine.


Ripoti hiyo ambayo imesambazwa kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii, ikiwamo ule wa Jamii Forums, imekuja siku moja baada ya Mnadhimu Mkuu wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Tundu Lissu kuwashawishi wabunge wampigie kura Waziri Mkuu, Mizengo Pinda ya kutokuwa na imani naye, kutokana na kushindwa kumwajibisha Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk. Shukuru Kawambwa 



Katika ripoti hiyo ya mwaka 2011, iliyosambazwa kwenye mtandao wa Jamii Forum, na gazeti hili kuipata inabainisha upungufu wa wazi hasa kwa Serikali kwamba, uteuzi unaofanywa kwa viongozi mbalimbali wa kisiasa katika sekta ya elimu hauzingatii uzoefu, utaalamu, uwezo, uadilifu na uwajibikaji. 



Gazeti hili limebaini kuwa tume iliyokuja na ripoti hiyo iliongozwa na Profesa Sefue Mchome na utafiti wake ulifanywa kwa kuwashirikisha wadau mbalimbali wa sekta ya elimu.



Hata hivyo, Serikali imeshutumiwa kwa kushindwa kuiweka wazi na namna hatua ilizochukua baada ya kupokea ripoti hiyo.



Baadhi ya watu waliotoa maoni yao walionyesha kushangazwa na hatua ya Pinda kuunda Tume kuchunguza kushuka kwa ufaulu kwa matokeo ya mwaka jana, ili hali tayari kulikuwa na ripoti nyingine ambayo ilikuwa haijafanyiwa kazi.



Kitendo hicho kimetafsiriwa kuwa kilikuwa na lengo la kuwahadaa wananchi ili kuwaonyesha kuwa anauchungu na anataka kulifanyia kazi suala hilo kumbe sivyo.



Ripoti hiyo ambayo ilijikita katika kufanya utafiti wa kushuka kwa elimu nchini, ulifanywa kwa ushirikiano kati ya TAMISEMI na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi (WEMU), ikihusisha Taasisi ya Elimu Tanzania na Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA).



Moja kati ya mambo ambayo yamebainika katika utafiti huo ni pamoja na sababu za kushuka kwa kiwango cha ufaulu wa Mtihani wa Taifa wa Kidato cha 4 mwaka 2010, ambazo ni masuala ya kimfumo ikiwemo upungufu katika usimamizi na uendeshaji wa elimu nchini. 



Maeneo mengine ni katika kujenga uwezo wa wasimamizi na watekelezaji wa mitaala, kuhakikisha upatikanaji wa vifaa bora na vya kutosha vya kufundishia, kujifunzia na uboreshaji wa majengo na miundombinu ambayo yanahitaji nguvu ya pamoja kati ya Serikali na wabia wake.



Katika moja ya mapendekezo yake Utafiti huo uliitaka Serikali 



kuona umuhimu wa kushirikiana na washirika na wadau wa elimu nchini, ili kuweza kukabiliana na changamoto mbalimbali zinazojitokeza katika sekta ya elimu.



Itakumbukwa kuwa hivi karibuni, Waziri Mkuu Pinda aliunda Tume kuchunguza kushuka kwa ufaulu kwa matokeo ya kidato cha nne, kitendo ambacho kilipingwa na baadhi ya wadau waliosema kuwa hakukuwa na haja ya kufanya hivyo, kwa sababu kila kitu kipo wazi.

2 Feb 2012


Mkulo ‘amgomea’ Spika kujibu swali bungeni
 
Tuesday, 31 January 2012 22:07
Habel Chidawali, Dodoma
WAZIRI wa Fedha na Uchumi, Mustafa Mkulo jana ‘alimgomea’ Spika wa Bunge, Anne Makinda kujibu swali lililomtaka aeleze kama chenji iliyorejeshwa na Uingereza kutoka kwenye ununuzi ya rada, ingetumika kununua madawati kwa ajili ya wanafunzi shuleni.

Hata hivyo, baadaye Mkulo alisema hakufanya hivyo makusudi, bali alikuwa hajasikia akiitwa na Spika kujibu swali hilo na kuahidi kuwa makini zaidi katika siku zijazo.

Ilikuwa kichekesho bungeni baada ya Spika kumwita Waziri Mkulo kwa takriban mara nne, akimtaka ajibu swali hilo lililoulizwa na Mbunge wa Viti Maalumu (CCM), Martha Mlata lakini hakusimama kujibu.

Kitendo hicho kiliwafanya baadhi ya wabunge waduwae huku waziri huyo akiendelea kuwa kimya.
Tukio hilo lilitokea baada ya Mlata kuuliza swali hilo la nyongeza lililotokana na swali na msingi ambalo liliulizwa na Mbunge wa Musoma Mjini (Chadema), Vicent Nyerere.

Katika swali hilo, Mlata alitaka kujua namna Serikali ilivyojipanga katika matumizi ya fedha hizo za rada na kama kuna mpango wowote wa kuzitumika katika kupunguza tatizo la uhaba wa madawati shuleni.
Swali la msingi la Nyerere lilijibiwa na Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Elimu), Kassim Majaliwa.

“Swali hilo naomba Waziri wa fedha ujibu, waziri tafadhali jibu swali hilo. Waziri wa Fedha… namtaka waziri ajibu si yupo?” alisema Spika Makinda lakini, Mkulo hakusimama.

Makinda alisisitiza: “ Hilo swali anatakiwa kujibu waziri mwenyewe na asijibu naibu wake. Jamani Waziri wa Fedha hayupo? Vipi mbona kimya kuna nini? Haya endelea naibu waziri.’’

Wakati wote ambao Spika Makinda alikuwa akimtaka Mkulo kusimama na kutoa majibu, waziri huyo alikuwa akiteta jambo na Waziri wa Tamisemi, George Mkuchika ambaye alisimama pia kutaka kutoa majibu lakini, Makinda alimzuia awali kabla ya kumruhusu kutolea ufafanuzi jambo hilo. 

Baada ya kuona hali hiyo, Majaliwa alilazimika kusimama na kusogelea kipaza sauti na kulieleza Bunge kuwa zaidi ya Sh18 bilioni zitapelekwa huko kwa ajili ya kununulia madawati. 

Alipotafutwa baadaye na gazeti hili ili aeleze kwa nini hakutii amri ya Spika ya kusimama na kujibu swali hilo, Mkulo alisema: “Sikumsikia na kwa kuwa maswali yanaulizwa bungeni basi subiri kesho (leo) nitajibu ili irekodiwe.”
Makinda alishawahi kutangaza bungeni kuwa Mawaziri wanatakiwa kuwa makini kwa kila swali au jibu linalotolewa ndani ya ukumbi kwani wakati wowote anaweza kumtaka yeyote kujibu swali au kutoa ufafanuzi.

Serikali ya Uingereza ilikubali kuilipa Tanzania Pauni 29.5 milioni wastani wa Sh75bilioni, ambazo zilizidi katika biashara ya rada kati ya Serikali ya Tanzania na Kampuni ya BAE Systems.

BAE Systems ilikiri mahakamani kwamba pamoja na kupoteza kumbukumbu, lakini rada hiyo iliuzwa kwa bei kubwa ikilinganishwa na thamani halisi.

Fedha hizo ziliwahi kuibua mvutano kati ya Serikali ya Tanzania na Uingereza, baada ya kutaka fedha hizo zipelekwe kwa asasi za zisizo za kiserikali nchini.

Baadaye Uingereza ilikubali kuzikabidhi fedha hizo zifikie mikononi mwa Serikali ya Tanzania na kuelekezwa katika sekta ya elimu, ikiwa ni pamoja na kununulia vitabu na vifaa vingine ikiwemo madawati.

Sakata hilo la rada bado linaendelea kuitikisa nchi baada ya uchunguzi wa Taasisi ya Makosa Makubwa ya Jinai ya Uingereza (SFO), kuchunguza baadhi ya vigogo wa Serikali ya Awamu ya Tatu akiwemo aliyekuwa Mwanasheria Mkuu, Andrew Chenge ambaye anadaiwa kukutwa na kiasi cha Dola za Marekani 1.2 milioni katika Kisiwa cha Jersey.  

CHANZO: Mwananchi


31 Jan 2012

Blandina Nyoni

Lucy Nkya

Default Kituko Wizara ya Afya, Blandina Nyoni haivi na Lucy Nkya. Hawasalimiani hata wakikutana kwenye kordo

Ndugu zangu hii taarifa nimeipata kutoka kwa wandani wangu aliopo pale Wizara ya Afya. Kwamba Katibu Mkuu wa Wizara Bi Brandina Nyoni haivi na Naibu Waziri wake, Bi Lucy Nkya. Na inadaiwa kuwa hata wakikutana kwenye kordo huwa hawasalimiani. Kinachowazungumzisha ni Madokezo tu. 


Taarifa inasema kwamba ugomvi wao ulitokana na kitendo cha Katibu Mkuu kutaka kumlazimishia kumpa Dereva (Elias Mkumbo) ambae ni Informer wake. Mama Nkya alipotonywa na watumishi wa pale akamkataa huyo Dereva na ali command alitewe dereva aliyekuwa nae kutoka Wizara aliyokuwepo kabla kama sivyo abadilishiwe. Tangu wakati huo Wakuu hawa wa Wizara wamesusiana (Kama wanavyosema watu wa Pwani). 


Blandina Nyoni amekumbwa na matukio mengi ya kususiana na Wakubwa wenzako toka alipokuwa Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii ambapo alikuwa haivi na hasalimiani na Waziri wake Bi Shamsi Mwangunga. Alipohamishiwa Afya mwishoni mwa 2008 pia akagombana na Naibu Waziri wa wakati huo Bi Aisha Kigoda na hadi anaondoka Wizarani hapo bado walikuwa hawaivi. Sijui huyu Mama ni Mtu gani? Maana hata watumishi wake kuazia alipokuwa Hazina, Maliasili na Sasa Afya wamekuwa wamkimkataa kutokana na Uongozi wake Mbovu wa kutojali maslahi halali ya watumishi wake mfano malipo ya likizo, uhamisho, extra duty allowances, etc!
CHANZO: Jamii Forums 

2 Jan 2012

Magufuli achafua hali ya hewa Dar Send to a friend
Sunday, 01 January 2012 22:20

Waziri wa ujenzi Dk John Magufuli

BAADA YA KUWAAMBIA WAKAZI KIGAMBONI WAKISHINDWA KULIPA NAULI MPYA ZA VIVUKO WAPIGE MBIZI

Ramadhan Semtawa
WAZIRI wa Ujenzi, Dk John Magufuli amechafua hali ya hewa na kuingia kwenye mgogoro na wakazi wa Kigamboni, Dar es Salaam baada ya kuwaeleza kuwa ni lazima walipe nauli mpya za vivuko vya Mv Kigamboni na Alina na kama watashindwa, wapige mbizi baharini kuvuka.

Kauli hiyo ya Dk Magufuli imekuja siku mbili baada ya wizara hiyo kutangaza viwango vipya vya nauli mnamo Desemba 29, mwaka jana ambavyo vimepanda kwa asilimia 100 na vilianza kutumika jana Januari Mosi nchi nzima.

Baada ya kutangazwa kwa viwango hivyo vipya vya nauli, wakazi wengi wa Kigamboni walipinga kutokana na kile wanachosema hawakushirikishwa na ndipo jana asubuhi, Dk Magufuli alipoamua kufanya ziara ya ghafla katika vivuko hivyo na kusisitiza kwamba viwango hivyo lazima vilipwe.

Katika ziara hiyo, vyanzo vya kuaminika vilisema Dk  Magufuli alipofika eneo hilo la Kivukoni, alitoa msimamo huo na ndipo wananchi waliokuwa wakimsikiliza walipoanza kumzomea na kukatisha hotuba yake mara kwa mara.

Vyanzo hivyo viliongeza kwamba, kitendo hicho cha zomeazomea, kilimkera Dk Magufuli ambaye pamoja na mambo mengine, alisisitiza nauli hizo lazima zilipwe na mtu asiyetaka ni vyema akapiga mbizi kwa kuogelea kutoka Kigamboni hadi ng'ambo ya pili au apite Kongowe kuingia katika katikati ya jiji.

Msemaji: Waziri amechukizwa
Akizungumzia tukio hilo, Msemaji Mkuu wa wizara hiyo, Martin Ntemo alisema Waziri Magufuli hakufurahishwa na kitendo cha baadhi ya watu kumzomea wakati alipokuwa akizungumza... “Amechukizwa na baadhi ya watu kuzomea wakati alipokuwa akizungumza. Alichokuwa akisisitiza ni kwamba nauli mpya lazima ilipwe lakini wapo waliokuwa hawataki kuelewa wakawa wanapinga.”

Alisema kuna watu walikuwa wamepangwa kufanya mgomo kupinga nauli mpya kitendo ambacho pia kilimkera waziri alipokuwa kwenye ziara hiyo.


Magufuli na waandishi

Baada ya kuzomewa Kigamboni, Dk Magufuli alifanya mkutano na waandishi wa habari na kusisitiza kwamba, “Kuanzia Januari, Mosi, mwaka huu Wizara ya Ujenzi kupitia Wakala wa Ufundi na Umeme (Temesa), imeongeza viwango vya nauli katika vivuko vyote vya Serikali nchini.”

Alisema kwa muda wa miaka 14 iliyopita Kivuko cha Kigamboni kimekuwa kikitoza nauli ya Sh100 kwa mtu mmoja, wakati vivuko vingine vyote nchini, vimepandisha nauli zaidi ya mara mbili tangu mwaka 1997 kuendana na gharama za uendeshaji.

“'Kwa mfano, Kivuko cha Pangani ambako umbali wa uvushaji hauzidi ule wa Magogoni kilikuwa kinatoza Sh 200 na hali ya uchumi kwa wananchi ni ya chini kuliko Dar es Salaam. Kivuko cha Kilombero kilikuwa kikitoza Sh200 ikilinganishwa na Sh100 zilizokuwa zikitozwa hapa Magogoni.” 

Dk Magufuli alitaja sababu zilizochangia kupandisha nauli hizo kwamba ni pamoja na ongezeko la mishahara ya watumishi serikalini kwa zaidi ya asilimia 100, ongezeko alilosema la zaidi ya asilimia 400 la bei ya mafuta ya dizeli na mafuta ya kulainishia mitambo ambayo hutumika kuendeshea vivuko hivyo. 
Alitaja sababu nyingine kwamba ni pamoja na: “Ongezeko la bei za vipuri na kodi zake linalowiana na kushuka kwa thamani ya shilingi na ongezeko la bei kwa jumla.”

Alisema upandishaji wa nauli hizo ulifanywa kwa kuzingatia taratibu za kisheria na hatimaye kutangazwa kwenye Gazeti la Serikali toleo Na. 367 la Novemba 4, mwaka jana kwa mujibu wa sheria za uendeshaji wa vivuko vya Serikali.

“Sura 173 Kifungu cha 11(b), mwenye mamlaka ya kupanga nauli za vivuko vya Serikali ni Waziri mwenye dhamana na vivuko vya Serikali. Hata hivyo, kabla ya kufikia uamuzi huu, kumekuwa na jitihada za aina mbalimbali katika kuimarisha mapato ya vivuko. Machi, 2009, Wakala wa Ufundi na Umeme wakishirikiana na  
Jeshi la Polisi pamoja na Askari kutoka Kikosi cha Wanamaji waliendesha zoezi la kudhibiti mapato ya Kivuko.”

Alisema hilo liliwahi kufanywa na na Kampuni ya udalali ya Yono Auction Mart mnamo Aprili 17 hadi 20, mwaka jana kwa makubaliano na Temesa. “Zoezi hilo liliendeshwa tena Septemba 16 hadi 20, 2010 na 
Wizara kwa ushirikiano na Jeshi la Polisi.”

Alisema Julai, 2011, Temesa iliamua kubadili wakata tiketi na kuajiri wengine akisisitiza kuwa Serikali imechukua hatua mbalimbali kupambana na matukio ya watumishi wasio waaminifu. Hatua nyingine ni ile ya Temesa  kuondoa askari wa kuajiriwa na badala yake kuingia mikataba na kampuni za ulinzi.

“Kwa sasa katika Kivuko cha Magogoni, Kampuni ya ulinzi ya Suma JKT ndiyo inayotumika kufanya kazi hiyo,” alisema.

Alisema juhudi hizo zimesaidia kuongeza mapato kwa siku kutoka Sh5.5 milioni mwaka 2009 hadi Sh9 milioni kwa sasa katika Kivuko cha Magogoni na kusisitiza kwamba wizara itaendeleza hatua hizi kwa lengo la kubana uvujaji wa mapato na matumizi yasiyo ya lazima kwa vivuko vyote. 

Magufuli alisema kwa utaratibu, watumiaji wote wa huduma za vivuko wanatakiwa walipie huduma hiyo na kuongeza: “Tunaomba utaratibu huu uzingatiwe isipokuwa kwa wanafunzi waliovaa sare za shule. Tunasisitiza watumiaji wa vivuko waheshimu sheria na taratibu zote za vivuko kwa ajili ya usalama wao na ufanisi wa huduma.”



Mbunge achukizwa

Kwa upande wake Mbunge wa Kigamboni, Dk Faustine Ndugulile alikiri kusikia maneno ya Magufuli ambayo hayakuwafurahisha wapiga kura wake na kuahidi kuendelea kufuatilia kujua undani hasa wa kauli hizo. 

Dk Ndugulile alifafanua kwamba baada ya tangazo hilo la ongezeko la nauli, aliwasiliana na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Mecky Sadiki na taarifa alizonazo ni kwamba nauli hizo zimesitishwa.

Alifafanua kwamba baada ya kuwasiliana na waziri mkuu, jibu alilopata jana saa 1: 00 usiku ni kwamba mpango huo wa kupandisha nauli umesitishwa hadi hapo itakapoamuliwa vinginevyo.

Dk Ndugulile alisema sababu zilizomfanya yeye na wananchi kupinga nyongeza hiyo ya nauli ni Serikali kushindwa kueleza wazi vigezo vilivyotumika na kushindwa kuwashirikisha wananchi wa maeneo husika. Alitoa mfano wa Bajaji ambao alisema ni usafiri wa wanyonge uliokuwa ukitozwa Sh300 lakini kwa viwango hivyo vipya, itavushwa kwa Sh1,300 huku baiskeli ya miguu mitatu inayotumiwa na wanyonge pia kuchukulia bidhaa kutoka Kariakoo ikiongezewa nauli kutoka Sh200 hadi Sh1,800 na gari ndogo sasa zinatakiwa kulipa Sh1,500 badala ya Sh800.

“Sasa angalia hivyo vigezo, utaona mwananchi wa kawaida amezidi kuumizwa. Leo hii tayari bei za bidhaa zinazoletwa Kigamboni kutoka sokoni kama Kariakoo kwa kutumia maguta zimepanda. Mtu mwenye gari anapadishiwa bei chini ya mwenye guta, vigezo gani hivi? Baada ya kuona hivyo, niliwasiliana na Waziri Mkuu Ijumaa (Desemba 30, mwaka jana) na jana Mkuu wa Mkoa akanipa jibu kwamba Waziri Mkuu kasema nauli hizo zisipandishwe kwanza. Kwa hiyo mimi na wananchi wangu tunajua hivyo,” alisema na kuongeza:

“Hili ni jambo la ajabu sana. Yaani Waziri Mkuu anasema hivi halafu waziri wake anafanya vingine! Uko wapi sasa utendaji kazi wa pamoja wa Serikali?”


Baadhi ya wananchi wamelaani kauli hiyo za Dk Magufuli wakisema haikupaswa kutolewa na waziri ambaye ana dhamana ya kuhakikisha matatizo ya wananchi yanatatuliwa. Mmoja wa wakazi wa Kigamboni aliyejitambulisha kwa jina la Hamis Bwamkuu alisema: “Waziri anatoa kauli za kejeli namna hii! Ametusikitisha sana na kwa kweli tunamuomba Rais Jakaya Kikwete amchukulie hatua za kinidhamu.”

Pia wananchi hao wamemshutumu Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi, Dk Hurbet Mrango na Temesa kwa kushindwa kuwashirikisha na pia kumshauri vibaya waziri katika jambo hilo. 

"Katibu Mkuu ndiye mtendaji na Temesa wao ndiyo wakala lakini hawakumwambia kwamba wananchi hawakujua na hata mbunge wetu. Kwa hiyo hawa ni sehemu ya tatizo na hii si mara ya kwanza.”

28 Jul 2011


Bunge lachafuka
Wednesday, 27 July 2011 21:31

WENJE ATOLEWA KWA NGUVU, MBUNGE CCM ANUSRIKA KUPIGWA
Neville Meena na Habel Chidawali, Dodoma
MBUNGE wa Nyamagana (Chadema), Ezekia Wenje, jana alijikuta akitolewa bungeni na askari (wapambe) wa Bunge waliotii amri ya Mwenyeviti wa Bunge, Sylivester Mabumba, aliyeongoza kikao siku hiyo.Katika tukio ambalo ni la kwanza kutokea tangu kuanza kwa Bunge la Kumi linaloongozwa na Spika Anne Makinda, Mbunge wa Ludewa, Deo Filikunjombe (CCM), alinusurika kupigwa na wabunge wa kambi ya upinzani baada ya kuwakejeli Chadena akisema waache mambo ya kitoto.

Mabumba alitoa amri ya Wenje kutolewa nje baada kukaidi amri ya Mabumba kumtaka akae chini mbunge huyo wa Nyamagana alipokuwa akiomba mwongozo, katikati ya mabishano yaliyokuwa yakiwajumuisha wabunge wengine wakati huo.Wakati Wenje akisisitiza kuomba mwongozo kwa maelezo kwamba jambo analotaka kusema "lina maslahi ya nchi", Mabumba ghafla aliwaita askari (wapambe) wa Bunge na kuwaamuru wamtoe nje kwa kukiuka kanuni za Bunge.

Kabla ya kuwaita askari hao, Mabumba ambaye ni Mbunge wa Dole alikuwa amemwamuru mara tatu Wenje akae chini, lakini hakutii akisema: "Nina jambo la dharura ambalo ni kwa maslahi ya Taifa".

"Sargent Ant Arms, mtoe nje mheshimiwa Wenje," alisema Mabumba na hapo askari watatu waliingia na kumtoa nje Wenje, tukio ambalo liliacha kukiwa hakuna utulivu bungeni.

Pamoja na kusindikizwa na askari wa Bunge, baadhi ya wabunge wa Chadema na NCCR Mageuzi walitoka nje wakimsindikiza Wenje.Walipofika nje ya ukumbi wa Bunge walianza kumlalamika kwamba, Mabumba ameshindwa kuongoza Bunge na kudai kuwa anaonyesha upendeleo wa wazi katika uendeshaji wa vikao vya chombo hicho.

Nje ya Ukumbi wa Bunge
Nje ya Ukumbi wa Bunge ilizuka tafrani nyingine iliyosababisha Mbunge Filikunjombe (CCM), kunusurika kupokea kichapo kutoka kwa wabunge wa Chadema na NCCR Mageuzi baada ya kuingilia mazungumzo yao wakati wanajadili suala la Wenje kutimuliwa ukumbini.

“Tatizo lenu ninyi wabunge wa Chadema mnaishia kuwa wabishi kila wakati, jambo ambalo linawapotezea heshima kwa wananchi,’’ alisema Filikunjombe na kuongeza: “Acheni mambo ya kitoto rudini ndani kuendelea na Bunge. Sio kila siku ninyi Chadema tu, watu wamewachoka.’’

Kauli ya ilikuwa kama kumwaga petroli kwenye moto, kwani kundi la wabunge wa Chadema na NCCR Mageuzi ambao kwa wakati huo wakiongozwa na Moses Machali (Kasulu Mjini NCCR), walimvaa kama nyuki mbunge huyo na kuanza kurushiana maneno makali.

“We mjinga kweli, hapa sio wabunge wa Chadema hata sisi wa NCCR-Mageuzi tupo tunachojadili ni maslahi ya nchi sio ushabiki wa vyama, toka hapa mshamba wewe,’’ alisema Machali.

Mbunge wa Viti Maalum (Chadema), Susan Kiwanga, alimwambia Filikunjombe aache hadithi za kijinga kwani wananchi wa eneo lake wanaporwa chuma, lakini yeye (Filikunjombe) anashindwa kuwatetea badala yake anarukia mambo yasiyomuhusu.“Tuondolee ujinga wako hapa, wananchi wako katika maeneo ya Liganga wanaporwa mali usiku na mchana unashindwa kuwatetea leo unapotuambia tuna akili ya kitoto, hivi unataka Watanzania wafe ili ninyi mshangailie,’’alisema Kiwanga.

Wabunge wengine waliomwandama zaidi Mbunge huyo ni, Machali (NCCR-Mageuzi), Peter Msigwa (Iringa Mjini-Chadema), Mariam Msabaha na Susan Kiwanga wote wa Viti Maalum (Chadema) ambao walimzingira mbunge huyo na kuanza kumrushia maneno ya kejeli.

Hali ilizidi kuwa mbaya baada ya wabunge wengine wa Chadema, Godbles Lema (Arusha Mjini), Joseph Mbilinyi (Mbeya Mjini) na Vicent Nyerere (Musoma Mjini) walipoingilia ugomvi huo na kutaka Filikunjombe awaombe radhi, lakini alikataa.Kama si busara iliyotumiwa na Mbunge wa Kondoa Kusini, Juma Nkamia (CCM) hali ingekuwa mbaya kwani idadi ya wabunge wa Chadema ilipozidi yalisika maneno kuwa mbunge huyo apigwe, ndipo Nkamia alipofika na kuokoa jahazi akimtaka Filikunjombe aondoke katika eneo hilo.

Maelezo ya Wenje
Wenje aliwaambia waandishi wa habari nje ya ukumbi wa Bunge kuwa kitu alichokifanya hakikustahili adhabu kama aliyopewa kwa kuwa alikuwa sahihi. '' Pale mimi nilikuwa sahihi kabisa kwani sikutaka kuzungumzia suala la Lissu bali nilikuwa nazungumzia suala la masilahi ya Watanzania wote. Ikumbukwe kuwa kuna samaki walioingizwa bila polisi kujua na sasa wako sokoni wananchi wanakula hiyo ni hatari, sasa mwenyekiti anasema kuwa nitoke hajui kanuni yule,'' alisema Wenje.

Mbunge huyo alisema kitendo cha Mwenyekiti kuamuru atolewe nje kwa amri ni kukiuka kanuni na kwamba hajui kwani aliposema suala la dharula ni pale kunapotokea vita si kweli. '' Kanuni ya 47 (1-3) ndiyo niliyotumia na inaniruhusu kabisa kuomba mwongozo huo, kwani wananchi wanaumia halafu tunaambiwa hadi kuwe na vita, kama si umbumbumbu ni nini basi," alihoji Wenje akiwa ameshika kitabu cha Kanuni za Bunge.Kwa upande wake Mbunge wa Arusha Mjini, Godbles Lema (Chedema) alisema kinachomsumbua Mwenyekiti ni kutokujua kanuni.

Chanzo cha mtafaruku
Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu (Chadema) ndiye aliyeanzisha balaa ndani ya ukumbi wa Bunge baada ya kueleza kuwa Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Elimu), Kassim Majaliwa amesema uwongo bungeni.

Lissu alisema Majaliwa alipokuwa akijibu swali lake namba 313 kuhusu michango kwa wananchi, amedanganya kuwa wananchi hawalazimishwi kutoa michango hiyo na kusisitiza kuwa ana ushahidi unaothibitisha kwamba michango hiyo ni lazima.

“Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali haitumii nguvu katika kuwatoza wananchi michango hiyo, bali wanashirikishwa katika kuibua, kupanga na kuendesha miradi yao wenyewe,’’ alisema Naibu Waziri Majaliwa.Baada ya majibu hayo, Lissu alisimama na kulieleza Bunge kuwa Naibu Waziri alisema uongo huku akinukuu barua ya Mkuu wa Wilaya ya Singida iliyotolewa Mei 2,2005.

"Naomba kwanza niseme kwamba mimi namheshimu sana Mheshimiwa Naibu Waziri na kwa kweli huwa nakuwa mzito sana kusema Waziri amesema uongo. Lakini katika majibu haya naomba nitoe tamko kwamba, Mheshimiwa Naibu Waziri ameliambia Bunge hili uongo, na naomba nipewe nafasi ya kuthibitisha uongo huo leo leo, tena kwa ushahidi wa maandishi," alisema Lissu na kuongeza:

"Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sasa niulize swali dogo la nyongeza".Kabla ya kuuliza swali hilo, Mabumba alisema: "Mheshimiwa samahani naomba... Mheshimiwa umekiri katika maelezo yako kwamba Waziri ameshindwa kukuridhisha, maelezo yake hayalingani na swali lako. Kwa hiyo hutakuwa na nafasi ya swali la nyongeza nimtake Mheshimiwa Waziri, No! Nikutake wewe unipe ukweli kuhusu suala hili".

"Tafadhali naomba uliambie Bunge hili ukweli wa suala hili na bahati nzuri umesema hapo ulipo uko tayari kutoa maelezo haya. Tafadhali nafasi ni yako," alihitimisha Mabumba.

Baada ya kupewa fursa hiyo, Lissu alisema Naibu Waziri, Majaliwa si kwamba ameshindwa kumridhisha na kusisitiza kuwa Majaliwa amesema uongo.

"Ndiyo maneno niliyoyatumia, …Naibu Waziri amesema uongo na uthibitisho ni kwamba mimi mwenyewe hapa Bungeni, nina barua ya tarehe 2/5/2005 iliyoandikwa na aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Singida wakati huo, anaitwa Kepteni James Yamungu, ambayo kichwa chake cha habari kinasema; ‘Amri Na.1 ya Mkuu wa Wilaya ya Singida’ na inalazimisha wananchi kulipa michango".

Kabla hajamaliza kusoma barua aliyokuwa ameishika mkononi, Mbunge wa Mbozi Mashariki, Godfrey Zambi (CCM), aliomba mwongozo akisema kipindi hicho hakikuwa cha kutoa uthibitisho bali wabunge walipaswa kuendelea na mjadala wa maswali.Mwenyekiti alikubaliana na utaratibu huo, hivyo kumtaka Lissu awasilishe maelezo husika na kielelezo cha barua baada ya saamoja.

Hali ilibadilika
Hali hiyo ilimkera Mbunge wa Kasulu Mjini (NCCR-Mageuzi), Moses Machali, ambaye aliomba mwongozo wa Mwenyekiti na kutaka muda uongezwe kwa Lissu kabla ya kutoa uthibitisho wake.

“Mheshimiwa Mwenyekiti, muda uliompa Mheshimiwa Lissu kutoa uthibitisho ni mfupi na kwa kuwa Lissu ni mbunge saa tano anatakiwa kuwa ndani ya ukumbi kuendelea na shughuli za Bunge naomba mwongozo wako,’’ alisema Machali.Mwenyekiti wa Bunge hakukubaliana na ombi la Machali na kusema kuwa hawezi kuomba mwongozo juu ya mwongozo hivyo akasema alichokizungumza ndicho kinatakiwa kutekelezwa.

Yalizuka mabishano kwa muda mrefu kati ya Machali na Mabumba ambayo yalimfanya Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Uratibu na Bunge, William Lukuvi, kuingilia kati na kuwataka wabunge kutokuchukulia jambo hilo kwa jazba.

“Unajua hapa wabunge hampaswi kuliona jambo hili kuwa ni kubwa kiasi hicho, kwani hata Lissu anaweza kuomba kwa maandishi kuongezewa muda na akaleta kwa wakati wake,’’ alisema Lukuvi.Hata hivyo, kulikuwepo na majibizano na ukali wa maneno kutoka kwa Mwenyekiti ambaye alimwambia Machali: “Unaongea maneno kama tuko klabu cha pombe, unatakiwa kujiheshimu na kuzungumza kwa utaratibu mheshimiwa mbunge’’.

Wakati hayo yakiendelea, Wenje alisimama akiomba mwongozo lakini alimriwa kukaa chini na baada ya kukaidi, Mabumba aliamuru atolewe nje.

Mabumba ajitetea
Akiahirisha kikao cha bunge jana mchana, Mabumba alitumia takriban dakika kumi kujitetea kuhusu hatua yake ya kumtoa nje Wenje kwamba, alifanya hivyo kwa mujibu wa Kanuni za Bunge baada ya mbunge huyo kukaidi amri yake.

"Kwa mujibuwa Kanuni za majadiliano, mtakubaliana na mimi kwamba, Mheshimiwa Wenje alikiuka kanuni hizo maana alikuwa akibishana na kiti na mimi sikuwa nimempa ruhusa ya kuzungumza," alisema Mabumba huku akiwataka wabunge kuzingatia kanuni za Bunge.Alisema kwa mujibu wa kanuni hizo, Wenje alipaswa kutohudhuria kikao kizima cha jana kama adhabu, lakini kwa kuwa alitii amri ya kutoka nje, alimpunguzia adhabu hiyo hivyo anaruhisi kuhudhuria kikao cha jana jioni.

"Kwa mujibu wa Kanuni zetu, Wenje alipaswa kukosa kikao cha siku nzima ya leo (jana), lakini kwa kuwa ametii amri ya kutoka nje na mpunguzia adhabu hiyo anaweza kurejea ukumbini kuhudhuria kikao cha jioni kuanzia saa 11," alisema Mwenyekiti huyo wa Bunge.Hata hivyo, alisema katika mazingira aliyomkatalia Wenje kutoa hoja yake, alikuwa sahihi, kwani haikuwa rahisi kufahamu kwamba hoja ya mbunge huyo ni tofauti na kile kilichokuwa kikiendelea wakati huo.

"Wakati mwingine mazingira huwa ni magumu sana, ni kwa vipi mtu angeweza kufahamu kwamba alichokuwa akitaka kusema Wenje ni tofauti na hoja ya Mheshimiwa Lissu, ilikuwa vigumu sana," alijitetea Mabumba

CHANZO: Mwananchi

Wakati hayo yakiendelea,utoto mwingine umejitokeza Bungeni kama inavyoripotiwa katika habari ifuatayo

Saini ya Pinda yaghushiwa bungeni
Wednesday, 27 July 2011 21:32

Neville Meena na Habel Chidawali
VITUKO vya wabunge ndani ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania vimezidi kuongezekana; sasa baadhi ya wabunge wanadaiwa kugushi sahihi ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda kwa malengo ambayo bado hayajafahamika.

Kitendo cha kugushi sahihi ya Waziri Mkuu ndani ya ukumbi huo kunawaathiri zaidi wabunge wa upinzani, hasa wa Chadema ambao wamekuwa wakipelekewa ‘meseji’ za kuwadanganywa kuwa wanaitwa na Waziri Mkuu.

Juzi jioni kabla ya kikao cha Bunge kuahirishwa, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi, alialazimika kuomba mwongozo wa Mwenyekiti kukemea kitendo hicho alichokiita kuwa ni cha kihuni.

Lukuvi asimama mara tu baada ya Bunge kumaliza kupitisha makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika ambayo yalikuwa yalijadiliwa kwa siku mbili mfululizo.

“Naomba mwongozo wako kwamba, humu ndani imejitokeza tabia ambayo naona imezoeleka kidogo. “Kuna watu wanawaandikia wenzao meseji za kuwasumbua kwamba wanaitwa na mtu fulani halafu wanaweka sahihi na wakati mwingine haitokei,” alisema Lukuvi na kuongeza:

“ Nimeisikia hayo wiki iliyopita, lakini leo Mheshimiwa Joseph Selasini (Chadema) ameitwa kwa meseji inayodaiwa kuwa imesainiwa na Waziri Mkuu na hii nyingine ameitwa Mheshimiwa Leticia Nyerere (Chadema) kwamba anaitwa na Mheshimiwa Waziri Mkuu wakazungumze maneno ya maana, lakini Waziri Mkuu hana habari na wamegushi sahihi yake,’’ alisema Lukuvi.

Waziri huyo wa Sera, Uratibu na Bunge alitaka mwongozo wa Mwenyekiti kama jambo hilo linaweza kufanywa na Wabunge, ndani ya Bunge kwa wabunge kugushi taarifa ambazo alisema nyingine na zinatisha.

Mwenyekiti wa Bunge George Simbachawene alikiri kuwepo kwa tabia hiyo ndani ya ukumbi wa bunge ambayo imekuwa ikifanywa na baadhi yao na kamba inaonekana kuota mizizi.

“Nakushukuru sana Mheshimiwa Waziri, ni kweli kuna mtu amefanya hivyo na karatasi aliyoiandika ipo hapa, Kwa kweli siyo nzuri haionyeshi kama tupo serious (makini) na kazi,” alisema Simbachawene na kuisoma:

“Amemwandikia hivi, Mheshimiwa Joseph Selasini Mbunge, samahani nakuomba mara moja tuje tujadili suala moja muhimu ambalo ningependa kujua kutoka kwako. Ahsante. Mizengo Peter Pinda na sahihi”.

Simbachawene alisema Selasini alipokwenda kwa Waziri Mkuu alishindwa kusaidiwa kwa kuwa wakati huo Waziri Mkuu alikuwa makini kusikiliza hotuba ya Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika katika majumuisho yake.

Hata hivyo, mwenyekiti huyo alisema uongozi wa Bunge utafanya kila liwezekanalo kubaini ni nani mwenye tabia hiyo na kwamba ili kukomesha vitendo hivyo
CHANZO: Mwananchi

23 Jul 2011


Hili sio ombwe tena bali mkusanyiko wa wababaishaji walioteuliwa na mtu asiyejua kwanini aliwateua,na ndio maana wanaendesha mambo kama kwenye mchezo maarufu wa watoto ujulikanao kama kombolela.Watu wazima ovyoo!Lakini ni wazi wanapata jeuri ya kufanya ubabaishaji huo kwa vile wanafahamu fika kuwa aliyewateua hana jeuri ya japo kuwawajibisha,let alone kuwakemea.

Anyway,hebu soma madudu yao hapa chini:

DPP amkana Hoseah  
Friday, 22 July 2011 20:27

ASEMA HAJAPATA JALADA LA CHENGE, AAMBIWA AKAANGALIE MASJAJA
Nora Damian
SIKU moja baada ya Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Dk Edward Hoseah, kusema kwamba ofisi yake imekamilisha uchunguzi wa madai ya kumiliki Dola za Marekani 1.2 milioni katika Kisiwa cha Jersey, Uingereza yanayomkabili Mbunge wa Bariadi Magharibi (CCM), Andrew Chenge na kwamba imekabidhi faili lake kwa Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP) kwa ajili ya kumfungulia mashtaka, kiongozi wake, Eliezer Feleshi amejitokeza na kusema kwamba hawahi kuliona jalada hilo.

"Niko safarini subiri hadi wiki ijayo… kwanza ashtakiwe kwa kosa gani? Acheni siasa nyie,” alisema DPP alipotakiwa kuthibitisha kama jalada hilo limefika mezani kwake na lini Mwanasheria huyo Mkuu wa zamani wa Serikali atafikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazomkabili... “Aseme ni tarehe gani alileta jalada hilo kwangu?”

Kutokana na majibu hayo ya DPP, Mwananchi lilimtafuta Dk Hoseah kupata ukweli juu ya kauli yake hiyo aliyoitoa juzi huko Arusha na kusisitiza kuwa jalada hilo limepelekwa katika Ofisi ya DPP na kumtaka mkuu huyo wa Mashitaka nchini asiharakishe kusema hajaliona, kwani siyo lazima kila kitu akabidhiwe mikononi... “Kwani kila kitu kinachopelekwa kwake lazima akione? Ameangalia registry (masjala)?. Suala hili nimeshaliongea nanyi vya kutosha hivyo muulizeni zaidi DPP.”

Juzi, Dk Hoseah alisema taasisi yake imekamilisha uchunguzi dhidi ya tuhuma zinazomkabili Chenge na kwamba jalada lake limepelekwa kwa DPP kwa hatua zaidi. Alisema Chenge atashtakiwa chini ya Kifungu cha 27 cha Sheria ya Takukuru ya mwaka 2007. Kwa mujibu wa kifungu hicho, mtu akiwa na mali ambazo hazilingani na kipato chake alichokipata akiwa madarakani au baada ya kuondoka ni kosa kisheria.

Chenge anadaiwa kukutwa na kiasi hicho cha fedha mwaka 2008 baada ya uchunguzi wa kashfa ya ununuzi wa rada uliofanywa na Taasisi ya Makosa Makubwa ya Jinai ya Uingereza (SFO). Tuhuma hizo ndizo zilizomfanya alazimike kujiuzulu wadhifa wa Waziri wa Miundombinu mwaka huo.

Malumbano kati ya Dk Hoseah na Feleshi siyo ya kwanza. Mwaka jana waliwahi kulumbana baada ya mkuu huyo wa Takukuru kusema kuna majalada takriban 50 ya kesi za rushwa ambayo yamekaliwa na DPP.

Pia Dk Hoseah aliwahi kumshutumu DPP mbele ya wabunge wakati wa semina elekezi mapema mwaka huu akidai kwamba amekuwa kikwazo cha kesi kubwa za ufisadi kupelekwa mahakamani kwa kukwamisha majalada.

CHANZO: Mwananchi 

25 Jun 2011

Kabla ya kuwaletea habari na picha kuhusu ziara ya wabunge kadhaa waliokuja hapa Uingereza kufuatilia malipo ya fedha za rada,ninaomba kuweka bayana mtizamo wangu katika suala hili.Kwanza,naona kilichofanywa na wabunge hao ni mithili ya kuuza ng'ombe kwa ajili ya kesi ya kuku.Nilitamani walioongea na wabunge hao kuwauliza umuhimu wa wao kuwepo Uingereza muda huu ambapo kikao cha Bunge la Bajeti kinaendelea huko Dodoma.Kuna dharura gani kwa wao kuja hapa muda huu badala ya kusubiri kikao hicho cha Bunge kimalizike?Je wanawatendea haki wapiga kura wao?Na nani anawawakilisha wapiga kura wao wakati huu?

Nimesema hii ni sawa na kuuza ng'ombe kwa ajili ya kumudu kesi ya kuku kwa vile kila mbunge aliyekuja analipwa mamilioni ya fedha kama posho za kujikimu.Waheshimiwa hawa wanadai fedha za rada zitatumika kuendeleza elimu ya watoto huko nyumbani.Swali la kwanza,kwanini wasingeokoa fedha zinazotumika kama posho zao kwa muda wote watakapokuwa hapa Uingereza,kisha fedha hizo zikaelekezwa kwenye elimu ya watoto wetu huko nyumbani?Binafsi,nadhani suala hilo lingeweza kabisa kushughulikiwa na ubalozi wetu hapa Uingereza unless watuambie kuwa hawana imani na utendaji kazi na Balozi wetu Peter Kallaghe (ambaye ninamfahamu vizuri kuwa ni mchapa kazi mahiri tangu alipokuwa huko Foreign Affairs na Ikulu--nimefanya nae kazi pasipo kufahamiana,just in case you doubt my assessment of him).

Lakini la muhimu zaidi ni ukweli kwamba historia inatufundisha kwamba fedha za aina hii husihia mifukoni mwa wajanja wachache.Sana sana zitawezesha kumalizika kwa ujenzi wa mahekalu ya vigogo,kama sio kuongeza idadi ya nyumba ndogo zao na misururu ya magari yao ya kifahari.Hivi waheshimiwa hawa wanaweza kutuambia kwanini wanatolea macho hayo mamilioni ya rada ilhali wameshindwa kuhoji kuhusu marejesho ya fedha za EPA?Vipi kuhusu zile fedha za mfuko wa pembejeo?Vipi kuhusu "stimulus package" yetu ya kizushi?

Let's be honest,na nilitegemea sana wanahabari waliotuwakilisha kwenye press conference ya wabunge hao wangeibua hoja hizi,waheshimiwa hawa wamekuja Uingereza kutalii tu.Period!So far,katika habari husika hawatuelezi namna gani ujio wao utawezesha fedha hizo kupatikana,na kutuhakikishia kuwa kweli zitaelekezwa kwenye elimu ya watoto wetu.Remember,kamwe tatizo la viongozi wetu halijawahi kuwa kwenye upungufu wa maneno matamu bali utekelezaji wa ahaid wanazojiwekea wao wenyewe.

Anyway,naomba kuwasilisha habari husika kama nilivyotumiwa na Miss Jestina

Wabunge wanne waliokuja Uingereza kuzungumzia mgogoro wa pesa za kampuni inayouza vifaa vya ulinzi –BAE Systems wamefafanua namna zitakavyotumiwa. Wakiongea katika Ubalozi wetu Uingereza mjini London, Ijumaa mchana, viongozi hao walihimiza wanachofanya ni kufuatilia matokeo ya mahakama ya sheria inayochunguza rushwa (Serious Fraud Office-SFO) maana kadri muda unavyokwenda ndivyo riba inaongezeka.
Wabunge walikutana na House of Lords ambao ni maofisa na viongozi wa ngazi za juu sana wenye usemi mzito katika masuala ya kisisiasa Uingereza.

Mwezi Desemba mwaka jana SFO iliiamuru kampuni ya BAE kulipa faini paundi laki tano na kuipa serikali ya Tanzania paundi 29.5 milioni sawa na shilingi 75.3 bilioni za kitanzania kama pesa za kujisafisha uso. Toka tamko hilo litokee miezi sita iliyopita imezuka migogoro kadhaa.
Upande mmoja BAE system wanataka fedha zisipewe serikali ya Tanzania bali kwa mashirika ya fadhila toka nchi za nje upande mwingine uongozi wa Tanzania unasisitiza serikali inao mfumo imara utakaohakikisha fedha zitawafikia wahusika.

Mgogoro ulianza mwaka 1999 wakati Tanzania ilipotaka kununua vifaa vya kusaidia ulinzi wa viwanja vya ndege toka kampuni ya BAE. Ilidaiwa kuwa mfanya biashara Shailesh Vithlani wa kampuni ya Merlin aliyefanya dili kati ya BAE na Tanzania alipewa asilimia 30 ya pesa ya mauzo kama hongo. Pesa hizo ziliwekwa katika akaunti yake ya benki Uswisi. Wahusika wengine ni aliyekuwa Wakili wa Serikali, Andrew Chenge na Gavana wa benki kuu, Idriss Rashid. Wote hawajashtakiwa na Vithlani anadaiwa kujificha Uswisi, ilhali SFO imetoa tamko afikishwe mahakamani.

Akijibu swali kuhusu kutokuelewana huku, mwenyekiti wa msafara Mbunge Job Ndugai ambaye ni Naibu Spika wa Bunge la Taifa, alisema si vizuri BAE kutuingilia au kutueleza nini cha kufanya na pesa hizo ambazo ni maslahi yetu .
“Sisi tunafahamu mfumo gani utakaohakikisha pesa hizo zinatumika sawasawa, zikienda kwa mashirika ya ufadhili ni kama zimetolewa kwa watu wa nje.”

Mbunge mwingine, John Momose Cheyo ambaye ni mwenyekiti wa kamati ya Bunge inayohusika na Hesabu za Umma, aliwahakikishia wanahabari kwamba katika miaka kumi toka tukio hilo la 1999 vyombo vya serikali dhidi ya rushwa vimebadilika na kuimarika. “Matumizi halali ya fedha yatakahakikisha pesa zitatumika kujenga elimu,” alisema Mbuge huyo wa Bariadi Mashariki.

Toka SFO ilipoamuru BAE Systems ilipe faini kwa mahakama na fidia kwa Tanzania yametokea pia madai kwamba wapo walioandikia BAE barua pepe kuwa wasiilipe serikali ya Tanzania pesa hizo.
Wabunge wanasisitiza pesa zitaendeleza elimu.

Mbunge Maalum, Angellah Kairuki ambaye ni pia Naibu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Haki na Utawala, alielezea kwamba ingawa pesa hizo zinaonekana nyingi lakini hazitasuluhisha matatizo yote ya elimu nchini, mathalan, kuongeza mishahara ya waalimu.
Alitoa mifano ya ukosefu wa madaftari, vyoo na vitabu vya kusaidia waalimu kufundisha. Mifano hiyo inayolenga shule za msingi na sekondari inatokana na matizo makubwa ya wanafunzi kujisaidia porini na kukosa vifaa muhimu vya elimu.

Mbunge Mussa Zungu wa Ilala, na vile vile Naibu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge inayohusika na Ulinzi, Usalama na Mambo ya Nje, alikumbusha kwamba tatizo halikuanzwa na Watanzania. “Ni suala lililoamuliwa na mahakama ya Uingereza; sisi tuchohitaji ni kuendeleza elimu.”

Habari imeandikiwa na Freddy Macha akishirikiana Jestina George pamoja na
URBAN PULSE CREATIVE

MUNGU IBARIKI AFRIKA, MUNGU IBARIKI TANZANIA

Na kwa kumalizia,tuache kumchosha Mungu kwa kutaka aibariki nchi yetu ilhali sie wenyewe hatujibidiishi kuifanya Tanzania kuwa lulu ya Afrika na pengine dunia kwa ujumla.Au tunamtaka Mungu aibariki nchi yetu ili mambo yakizidi kwenda mrama tumlaumu yeye badala ya kujilaumu kwa uzembe wetu?

Pia naomba kutoa wito kwa wanahabari wenzangu (hoping hamto-mind kukosolewa),let's go beyond the "photo-op" cancer inayowasumbua wengi wa wanahabari wenzetu huko nyumbani.Picha ni muhimu lakini la muhimu zaidi ni kuwabana viongozi wababaishaji kila wanapojipendekeza kuleta porojo zao.Mtakumbukwa kwa kuuwakilisha umma vyema na sio picha.Sorry guys,I think you could have done better than just reporting what they said.You just gave them a free pass na pengine bado hawaamini kama wamesalimika kuulizwa maswali magumu na Watanzania waliopo "dunia ya kwanza".

24 Jun 2011

Waziri Mkuu Pinda akimwaga machozi Bungeni mwaka 2009
Kwa kifupi tu,Jaji mtajwa katika habari ifuatayo hastahili kuendelea na wadhifa wake.Hili ndio tatizo la kuteua majaji weeeengi mpaka wababaishaji kama hawa wanapata fursa.Pia habari hii imenikumbusha lile tukio la Waziri Mkuu Mizengo Pinda kulia Bungeni alipobanwa kuhusu kauli yake kuhusu wauaji wa maalbino (aliropoka kuwa wauaji hao nawe wauawe)

Jaji aangua kilio akijitetea
Thursday, 23 June 2011 21:49

Hadija Jumanne
JAJI Atuganile Flora Ngwale wa Mahakama Kuu, Kanda ya Dar es Salaam kitengo cha Ardhi, jana alishindwa kujitetea kuhusu kushindwa kwake kujaza fomu zinazohusu mali na madeni yake, kwa mujibu wa sheria ya maadili ya viongozi wa umma.

Jaji huyo alishindwa kufanya hivyo mbele ya Baraza la Maadili ambako aliangua kilio na hivyo kusababisha wanasheria kushindwa kumhoji.

Hali hiyo ililazimisha baraza kusitisha usikilizaji wa shauri hilo.Wakati akiangua kilio, jaji huyo alilieleza baraza kwamba alishindwa kujaza fomu hizo na kuomba msamaha.Wakati akiangua kilio, jaji huo alisema "sina mali yoyote, kazi ndio maisha yangu, watoto wangu wanategemea kazi hii siwezi kudharau mtu, naomba mnisamehe, nimejifunza Mungu wangu,"alisema jaji huyo.

Jaji Ngwale alisimama katika baraza hilo ili kuanza kujitetea, lakini ghafla aliangua kilio kwa sauti ya juu huku akiomba baraza hilo limuonee huruma kwa kutojaza fomu."Ni kweli sijajaza fomu na kama kuna mtu aliniona nimejaza fomu hizi ajitokeze ndani ya baraza hili la maadili," alisema.

"Kazi hii ndio maisha yangu, kazi hii ndio faraja ya watoto wangu hivyo naitegemea sana sina mali zozote za kunitesa na kuniita katika Baraza la Maadili,"alisema Ngwale huku akimwaga machozi.

Baada ya Barazakuona Jaji Ngwale ameshindwa kujitetea kwa njia ya mdomo, lilimtaka atoe utetezi wake kwa njia ya maandishi na kulazimika kusitisha kuendelea na shauri hilo.Mbali na baraza hilo kusitisha kuendelea kusikiliza shauri hilo, pia wanasheria wa sekretarieti ya maadili na hawakupata nafasi ya kumhoji Jaji Ngwale kutoka na hali hiyo.

Baada ya baraza hilo kusitisha kuendelea kusikiliza shauri hilo walimuomba jaji huyo aondoke mbele ya baraza hilo, lakini jaji huyo alikaidi agizo la wanasheria hao na badala yake aliendelea kulia mpaka baraza hilo lilipomuomba mmoja wa wanasheria ambembeleze na baada ya kubembelezwa alikubali kwenda kutoa maelezo yake kwa njia ya maandishi na baadaye aliruhusiwa kuondoka.

Baraza hilo litaendelea leo kwa ajili ya kuhoji watu wanne ambao hawakujaza fomu hizo za maadili ya umma mwaka jana, miongoni mwa watu hao watakaohojiwa ni pamoja na Diwani wa Kata ya Kanazi Mathias Bisoma Mgatta, Mkurugenzi wa Shirika la Hifadhi ya Jamii la Taifa (NSSF), Crecencius Magori.

Wengine ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kikosi cha Usalama Barabarani, Tafiki Mwanza, Francis Bayona Katunzi na Diwani wa Mpanda mjini Ally Juma Nsokolo.

CHANZO: Mwananchi

7 Jun 2011


Ama kwa hakika Rais Jakaya Kikwete anaweza kabisa kushinda tuzo ya kuiongozi mbabaishaji aliyepindukia.Hivi inahitaji rocket science kwa mkuu wa nchi kufahamu majina ya viongozi wa dini wanaojihusisha na uuzaji wa madawa ya kulevya,kisha akayakalia majina hayo hadi kwenye halfa ya kidini na kulalamika BADALA YA kuchukua hatua stahili?Hata askari mgambo angeweza kuchukua hatua katika tuhuma kama hii kwa kuliripoti kwa vyombo vya dola.

Kikwete ni mbabaishaji,period.Nasema hivyo kwani hii si mara yake ya kwanza kukurupuka na kauli zake tunazoweza kabisa kuziita za kizushi akidai anawafahamu wahalifu.Mwaka 2006,mara tu baada ya kuukwaa urais kwa nguvu za wanamtandao (ambao baadhi yao leo wanaitwa magamba),Kikwete alifanya kituko kwa kudai sio tu anawafahamu wala rushwa bali anawafahamu kwa majina.Badala ya kuchukua hatua stahili,yeye akatoa deadline kuwa wajirekebishe la sivyo watamwona mbaya.

Ni dhahiri wala rushwa waliamua kumpuuza,na yeye mwenyewe ameamua kupuuza deadline hiyo kwani hadi leo hajaigusia tena.Ukidhani kuwa labda amejifunza lolote kuhusu tabia hiyo ya uropokaji,baadaye alifanya ziara Bandarini Dar na kudai tena kuwa anawafahamu watu wanaosaidia kukwepa ushuru bandarini hapo,na kwamba atawasilisha majina kwa wahusika ili wachukuliwe hatua.Kwa vile ubabaishaji uko damuni kwake,hakuweza kuwasilisha majina hayo wala kuchukua hatua stahili.

Sasa sijui ni kucnganganyikiwa au mwendelezo wa ubabaishaji,safari hii kakurupuka tena na uzushi mwingine akidai kuwa baadhi ya viongozi wa dini wanashiriki kwenye biashara haramu ya madawa ya kulevya.Hivi jamani,Rais mzima anasubiri hadi aalikwe kwenye sherehe ya kidini ndio atangaze kuwa anafahamu viongozi wa dini wanaojihusisha na uhalifu?Ina maana Kikwete hajui majukumu yake kama Rais wa Tanzania ni pamoja na kulinda sheria sambamba na kuchukua hatua dhidi ya wanaovunja sheria (including wazungu wa unga)?

Lakini safari hii,ubabaishaji wake unaweza kumtokea puani baada ya viongozi wa dini kumpa masaa 48 (hadi muda huu yatakuwa yamebaki kama 24 hivi) kuwataja hadharani viongozi hao wa dini anaodai wanashiriki katika biashara ya madawa ya kulevya.Na wamemtega vizuri kwelikweli kwa kumwambia aidha ataje majina hayo ndani ya masaa 48 au jamii imhukumu kuwa ni mnafiki na mzushi.

Soma habari husika hapa chini

JK awapasha viongozi wa dini
• Asema wapo wanaouza dawa za kulevya
na Stephano Mango, Songea

RAIS Jakaya Kikwete, amewaonya viongozi wa madhehebu mbalimbali ya dini nchini kuacha tabia ya kushiriki biashara ya kuuza dawa za kulevya na badala yake washirikiane na viongozi wa serikali kuidhibiti biashara hiyo haramu.

Alitoa kauli hiyo jana alipokuwa akihutubia waumini wa Kanisa Katoliki Jimbo la Mbinga wakati wa ibada maalumu ya kupewa daraja la uaskofu na kusimikwa kwa askofu wa jimbo hilo, Mhashamu John Ndimbo, katika kanisa la kiaskofu la Mtakatifu Killian iliyohudhuriwa pia na Rais mstaafu wa awamu ya tatu, Benjamini Mkapa.

Alisema baadhi ya viongozi hao wamekuwa wakishiriki kufanya biashara hiyo ya dawa za kulevya kwa kuwatumia vijana ambao huwafanyia mipango ya kuwatafutia hati za kusafiria (Passport) kwenda nchi za nje.

Badala yake Rais Kikwete amewataka viongozi hao nchini kuikemea biashara hiyo na kujenga uhusiano mzuri na vyombo vya dola katika kuhakikisha biashara hiyo inakomeshwa kwa kuwafichua wahusika wanaoifanya ili wachukuliwe hatua za kisheria.

“Inasikitisha sana na kutisha, biashara hii haramu sasa inawavutia hata watumishi wa Mungu, taifa letu litaharibika tusipokuwa makini katika hili kwani baadhi yenu tumewakamata.

“Kwa kauli zenu kemeeni jambo hili kwa kuelimisha jamii hususan vijana waweze kuepuka na matumizi ya dawa hizi,” alisema Rais Kikwete

Chanzo: Tanzania Daima

Maaskofu CCT wampa Rais Kikwete saa 48 kuwataja Viongozi wa Dini "wauza unga"
06/06/2011

L-R: Kadinali Pengo, Rais Kikwete, Askofu John Ndimbo (picha: C.Sikapundwa)Katika taarifa ya habari iliyosomwa leo saa mbili usiku kupitia kituo cha runinga cha ITV, imetamkwa kuwa Maaskofu wa Jumuiya ya Kikristo Tanzania, CCT, wamempa Rais Kikwete saa 48 za kuwataja kwa majina viongozi wote wa Dini anaowatuhumu kuhusuka na biashara haramu ya madawa ya kulenya "unga".

Maaskofu hao wamesema endapo Rais atashindwa kufanya hivyo, basi itachukuliwa kwamba siyo mkweli.

Agizo la CCT lilitolewa na Mwenyekiti wake taifa, Askofu Peter Kitula jijini Dar es Salaam katika mkutano na waandishi wa habari linasema, “Tunampa saa 48 rais awataje kwa majina viongozi hao ambao yeye anadai wanajihusisha na kuuza dawa na kama atashindwa kufanya hivyo tunamtafsiri ni mwongo na mzushi... Tunasikitishwa na kushangazwa kwa kauli hiyo na tunamheshimu kama kiongozi wa nchi, hivyo tunampa masaa hayo awataje kwa majina” alisema Kaimu Mwenyekiti wa CCT, Askofu Mokiwa akichangia hoja.

Kauli ya Rais kuhusu viongozi wa dini kuhusika na biashara ya madawa ya kulevya inanukuliwa kuwa ilitamkwa siku ya Jumapili, Juni 5, 2011 wakati akiwa aalipowahutubia waumini wa Kanisa Katoliki la Jimbo la Mbinga wakati wa ibada maalumu ya kuwekwa wakfu na kupewa daraja la uaskofu na hatimaye kusimikwa kuwa Askofu wa jimbo la Mbinga, Mhashamu John Ndimbo.

Misa hiyo ilifanyika katika Kanisa la Kiaskofu la Mtakatifu Killian na kuhudhuriwa na Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa pamoja na mkewe, Anna Mkapa.

Rais Kikwete amenukuliwa na vyombo vya habari (1), (2), (3), (4), (5), (6) ... kuwa alisema ,“Inasikitisha sana na kutisha biashara hii haramu sasa inawavutia hata watumishi wa Mungu, Taifa letu litaharibika tusipokuwa makini katika hili, baadhi yenu tumewakamata,”... “Kauli zenu kemeeni jambo hili kwa kuelimisha jamii hususani vijana waweze kuepuka na matumizi ya madawa ya kulevya.”

Kwamba, baadhi ya viongozi hao wamekuwa wakishiriki kufanya biashara ya madawa ya kulevya kwa kuwatumia vijana ambapo huwafanyia mipango ya kuwatafutia hati na pasi za kusafiria kwenda nchi za nje kufanya biashara hiyo. Rais akawataka viongozi wa dini nchini kuikemea biashara hiyo na kujenga uhusiano mzuri na vyombo vya dola katika kuhakikisha biashara hiyo inakomeshwa kwa kuwafichua wahusika wanaoifanya ili wachukuliwe hatua za kisheria.

Wakahoji, ikiwa Rais anawafahamu viongozi wa dini wanaohusika na biashara ya kuuza "unga" iweje ashinde kuwachukulia hatua za kisheria ikiwemo kuwakamata na kufunguliwa mashitaka?

Walisema viongozi wa dini wanalo jukumu la kutetea na haki mbalimbali za wananchi, na kuionya Serikali pale inapokosea.

CHANZO: Wavuti

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.