Showing posts with label USTAARAB. Show all posts
Showing posts with label USTAARAB. Show all posts

13 Jul 2010

Kuna tofauti moja ya msingi katika Twitter na Facebook (social media nazizipendelea zaidi),nayo ni namna watu wawili wanavyounganishwa na huduma hizo.Wakati nikiomba kuunganishwa na mtumiaji wa Facebook,na kukubaliwa inamaanisha nitaweza kuona profile yake na updates mbalimbali,kwenye Twitter habari ni tofauti.Nikiamua "kumfuata" (following) mtu,haimaanishi kuwa mtu huyo automatically naye "atanifuata".

Lakini katika mazingira ya kawaida,na pengine kistaarabu,kama mtu ameamua "kukufuata" huko Twitter,unapungukiwa nini ukirejesha "fadhila" kwa kumfuata mtu huyo?Au ndio usupastaa kwamba wanaokufuata ni wengi kuliko unaowafuata?Ofkoz,inaweza kuwa vigumu "kumfuata" kila "anayekufuata" ukiwa na "wafuasi" maelfu kadhaa lakini si vigumu kama wafuasi wako ni mia na kitu tu.

Naandika haya nikitambua kuwa uamuzi wa mtu kukufuata ni suala la mtu binafsi.Na kwa vile mtu ahajalazimishwa kumfuata mtu mwingine inaweza kupelekea hoja yangu kuonekana haina umuhimu.Nachojaribu kupigia mstari hapa ni ustaarab wetu wa Kiafrika.Katika mazingira ya kawaida,kama jana nilikutana nawe nikakusalimu,leo pia tumekutana nikakusalimu na kesho inakuwa hivyohivyo,basi kistaarabu inatarajiwa kuwa kesho kutwa nawe utaanzisha salamu.Kinyume cha hivyo,tafsiri itakuwa aidha unaringa au huhitaji salamu yangu.Ni katika mantiki hiyohiyo,kama mtu ameamua kukufuata (hata kama wewe ni maarufu mara elfu kuliko huyo mfuasi) basi ni tarajio la mfuasi huyo kuwa nawe utamfuata.Si lazima lakini ni katika masuala ya ustaarab tu.

Kama unaafikiana nami,basi pengine fanya jambo la kupendezesha roho za wale wanaokufuata lakini wewe hujaamua kuwafuata:WAFUATE PIA.Haigharimu chochote,haikupunguzii umaarufu ulionao,na zaidi,itakufanya uonekane huna dharau.

Ni ushauri wa bure tu.

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.