Showing posts with label VACATION PICS. Show all posts
Showing posts with label VACATION PICS. Show all posts

18 Sept 2008

KIDATU MACHANICAL AU MECHANICAL?

22 Apr 2008

NINA LUNDO LA PICHA LAKINI LEO INTERNET IKO SLOW SANA.KEEP ON VISITING THE BLOG FOR MORE PICS.PICHA TATU ZA CHINI NI KUTOKA HOSPITALI YA MTAKATIFU FRANCIS IFAKARA (KUNA SANAMU YA MTAKATIFU HUYO KATIKA PICHA YA TATU).PICHA YA NNE NI MAHINDI YALIYOANIKWA KWENYE LAMI.SIJUI NDIO TEKNOLOJIA AU VIPI LAKINI THE IDEA IS SIMPLE:LAMI INAPATA JOTO UPESI NA KWA KUANIKA MAHINDI KWENYE LAMI BASI YANAKAUKA UPESI,NA MASUALA YA UGALI YANAWEZEKANA NDANI YA MUDA ULIOPANGWA.HIKI NI KIPINDI CHA MAVUNO,KWAHIYO NADHANI VIBAKA WA MAHINDI SIO WENGI.SIDHANI KAMA KATIKA KIPINDI CHA NJAA VIBAKA WATAYANUSURU MAHINDI YALIYOANIKWA BARABARANI.




21 Apr 2008

Makala yangu katika toleo la wiki hii la gazeti la Raia Mwema inaelezea kwa kirefu nightmare niliyokumbana nayo baada ya kuingia mkenge wa kusafiri "first class" ya Tazara.Hiyo ilikuwa wakati naelekea nyumbani Ifakara mkoani Morogoro.Baada ya mateso ya hiari huko Tazara,nikaamua usafiri wa kurudi Dar uwe kwa njia ya Barabara.Nadhani picha zifuatazo zinatosha kukueleza namna Maisha Bora kwa kila Mtanzania yanavyowezekana.Kuna jamaa aliyeziona picha hizi kabla sijaziposti amenitania kwamba heri wale ambao "nyumbani" ni Dar es Salaam na si Ifakara,et al kwani hawahitaji Tazara wala matrekta ya kuvuta mabasi.Nikamuuliza iwapo Dar es Salaam anayozungumzia ni ya Oysterbay na Upanga au ile ya Mwananyamala kwa Ali Maua au Mbagala Kibondemaji...kwani alijibu!?
















Bilionea mwenye vijisenti,Andrew Chenge amejiuzulu,na Braza Ditto amefariki.Hizo ndizo habari zinazovuma hapa Dar tangu asubuhi.Hii ya kifo cha Ditto niliisikia jana.Na kama ilivyo kawaida,kila mmoja anasema lake ila kwa vile blogu hii si ya udaku,naomba nisiorodheshe conspirancy theories lukuki zinazovuma hapa jijini.Anyway,kuna picha kadhaa nilizozikamata maeneo mbalimbali.Nyingi zinajieleza zenyewe
























KIZA KWENYE PLATFORM YA TAZARA



















HAPO JUU NI CHOO CHA FIRST CLASS CABIN TAZARA

















HAPO JUU NI BUFFET COACH TAZARA



















HUYO UTINGO KAZI YAKE NI KUSHUKA KWENYE FOLENI NA KUWEKA GOGO ILI LORI LISIGONGE MAGARI YA NYUMA.KWA HAKIKA UDEREVA WA BOGNO UNAHITAJI ZAIDI YA LESENI:SALA NA BAHATI NI MUHIMU PIA KUHAKIKISHA UNAMALIZA SALAMA SIKU YAKO BARABARANI.THE SAME LORRY BELOW.




































HAPO JUU NA CHINI NI KIZA KWENYE PLATFORM YA TAZARA.


















HAPO CHINI NI ENEO LA MIZIGO TAZARA






















HAPO CHINI NI KITUO CHA MAFUTA MTANI.VIKO LUKUKI LAKINI BEI INAZIDI KUPAA.INAWEKEKANA ILE KANUNI YA DEMAND NA SUPPLY HAIFANYI KAZI KWENYE SUALA LA MAFUTA!

















BELOW IS A LORRY TO AND FROM HELL

18 Apr 2008

Katika picha hapo chini,treni ikikatiza kwenye railway crossing hapo jana.Almanusura itokee ajali mbaya laitimzalendo mmoja asingemshtua dreva kwamba anaona moshi wa treni kwa mbali.Yaani hakuna namna kwa mwenye gari kufahamu awapo kwenye railway crossing iwapo garimoshi linakuja au la.














Picha ya chini ni kwa ajili ya tafakuru:hivi hayo maisha bora kwa kila Mtanzania yatawezekana vipi kwa mkazi wa nyumba hiyo pichani ilhani akina Chenge wanadai dola milioni moja za ufisadi ni vijisenti?Hii ndio Bongo


15 Apr 2008

MASHABIKI WA SOKA WA IFAKARA WAKIFUATILIA MECHI KATI YA TAIFA STARS NA HARAMBEE STARS YA KENYA
HUYU NYAU ANAJARIBU KU-GOOGLE NENO "UFISADI"
HIKI NI CHOO NDANI YA BEHEWA LA DARAJA LA KWANZA LA TAZARA.EVER HEARD OF A TRAIN FROM/TO HELL?
UFISADI KUTOKA CHINA: HII NI PIRACY YA DARAJA LA KWANZA (ZAIDI YA LILE LA TAZARA).MOVIES TAKRIBAN 40 ZIMELUNDIKWA KWENYE DISC MOJA.BEI MAELEWANO.HI SAMPLE NILINUNUA KWA SHS 5000.NAOMBA KUSISITIZA KUWA NILINUNUA ITEM HII KWA AJILI YA KUKUONYESHA WEWE MSOMAJI WA BLOG HII,NA SIO KUWANUFAISHA MAFISADI.TRUST ME!
UFISADI,CHINESE STYLE
HIVI UNAWEZA KU-GUESS HAPO NI WAPI?I DONT THINK SO.NI RAHISI ZAIDI KU-EXTRACT DAMU KUTOKA KWENYE JIWE KULIKO KUPATA JIBU SAHIHI KWENYE KIJISWALI HIKI.ANYWAY,HAPO NI KWENYE PLATFORM YA KUONDOKEA,STESHENI KUU YA TAZARA DAR ES SALAAM,NA HILO DUDE KULIA NDIO TRENI LA KWENDA ZAMBIA.MWANGA HAPO NI HAFIFU ZAIDI YA ZILE DISCO LIGHTS ZA KIZAMANI.NDANI YA HILO DUDE LIITWALO TRENI NI ADHABU FROM THE MOMENT UNAINGIA TILL UPOTEREMKA UENDAKO ("KUTEREMKA" IS A POLITE WORD,"KURUKA" WOULD BE MORE PRECISE)
ANGALIA KWA MAKINI "TAIFA LA KESHO" (WATOTO) WAKIFUATILIA MECHI YA TIMU YETU YA TAIFA HUKUWAKIWA WAMEKAA CHINI.HAPA NI IFAKARA.RUNINGA ZIPO MADUKANI LAKINI NI AFFORDABLE KWA WATU WACHACHE.UNYANYASAJI WA WATOTO HAPA NYUMBANI UNAPASWA KUTANGAZA JANGA LA KITAIFA.NOBODY SEEMS TO CARE JAPO KUNA WIZARA INAYOHUSIKA NA MASUALA HAYA.NA HAKUNA SEHEMU NZURI YA KUPIMA POROJO ZAMAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA KAMA HUKU UPCOUNTRY.

MORE PICS LATER,STAY TUNED!

6 Apr 2008

Pata burudani ya picha zaidi kutoka Bongo
Lounge ya hoteli ya Kempinski

Kempinski kwa ndani,kwa hakika wanastahili pongezi kwa namna palivyoboreshwa.
Msikiti wa Kichangani Magomeni.Jirani na msikiti huuu,kuna makutano ya barabara za Morogoro na Kawawa.Eneo hilo ni maarufu sana kwa vibaka wababe wanaopora madereva.Ni zaidi ya kosa la jinai kusimamisha gari eneo hilo huku kioo kikiwa chini au nusu.
Makutano ya barabara za Morogoro na Bibi Titi.
Kasi ya majengo mapya ni kubwa katika maeneo mengi ya Dar.Hata hivyo,wananchi wengi wanalalamika kuwa hali ya maisha inazidi kuwa ngumu.
Sehemu hii inapendeza.Kwa muda nilijiskia kama niko Scotland vile.Hapa ni Kilimanjaro Hotel Kempinski.

Kempinski

Hakuna sheria muhimu ya uendeshaji gari mitaa ya Kariakoo zaidi ya ubabe.Ukifuata taratibu za usalama barabarani utaishia kugongwa,kuporwa au kulala hapohapo.
Mbinde za driving mitaa ya Kariakoo
Leo ni Jumapili na foleni katika barabara nyingi ni pungufu
I wish kila siku barabara zingekuwa nyeupe namna hii.
Msikiti wa Kichangani Magomeni
Millennium Towers.Eneo hili kuna internet cafe ambayo ni kimbilio la wengi wanaotegemea wireless connection.Pia ni mahala unapoweza kugongana na jamaa mbalimbali mliopoteana kutokana na kwenda nje kusaka hili au lile
Hii joint inaitwa "SAMAKI SAMAKI".The name tells it all...it's all about fish,fish and even more fish...Jana tulipewa ofa ya bure ya dagaa wa kukaanga.Yaani.... ndio mambo ya home sweet home hayo!However,dont let these nice pics fool you,mapambano ya maisha hapa yanataka ujasiri...na ukiwa jijini hapa inaweza kuwa rahisi kufahamu kwanini UFISADI unashamiri.The going seems to be getting tougher and tougher,forcing some folks to try to make the tough get going.
Barabara nyeupe
Barabara nyeupe pyee
Mitaa ya Kariakoo







Wakati unasubiri batch nyingine ya picha kutoka hapa,hebu pata burudani kutoka kwa Common featuring Dwelle katika track ya The People

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.