Showing posts with label Watanzania Marekani. Show all posts
Showing posts with label Watanzania Marekani. Show all posts

16 Aug 2012

5 Aug 2012


Makada wa CCM wakiwa na kadi za  uwanachama kwa wanachama wapya  katika futari ya pamoja ilioandaliwa na tawi la CCM DMV Jana Ijumaa Aug 3, 2012 katika ukumbi wa Hillandale Park iliyopo Silver Spring, Maryland Nchini Marekani.

Mwenyekiti wa tawi la CCM DMV Loveness Mamuya akipata picha na tikiti maji lililochongwa kwa longo ya Chama cha CCM, katika futari ya pamoja ilioandaliwa na tawi la CCM DMV Jana Ijumaa Aug 3, 2012 katika ukumbi wa Hillandale Park iliyopo Silver Spring, Maryland Nchini Marekani.

Tikiti maji lililochongwa kwa longo ya Chama cha Mapenduzi CCM

  
Baadhi ya waTanzania mbali mbali waliohudhuria kwenye futari hiyo ilioandaliwa na tawi la CCM DMV

Baadhi ya waTanzania waliovalia rangi za chama cha CCM wakiwa kwenye futari ya pamoja ilioandaliwa na tawi la CCM DMV, Jana Ijumaa Aug 3, 2012 katika ukumbi wa Hillandale Park iliopo Silver Spring, Maryland Nchini Marekani.

  Makada wa CCM Tawi la DMV shoto Mbunifu wa Ma Winny Casey Khanga Wrap Designer, pamoja na Peter Ligate (Picha ya kulia) wakiwa katika mpango mzima wa futari ya pamoja ilioandaliwa na wanatawi la CCM DMV

Watanzania  waliojumuika  kwenye futari ya pamoja ilioandaliwa na tawi la CCM DMV, Jana Ijumaa Aug 3, 2012 katika ukumbi wa Hillandale Park iliopo Silver Spring, Maryland Nchini Marekani.

  
Mwenyekiti wa tawi la CCM DMV Loveness Mamuya akiwakaribisha rasmi  wageni walikwa  kwenye futari ya pamoja ilioandaliwa na tawi la CCM DMV, Jana Ijumaa Aug 3, 2012 katika ukumbi wa Hillandale Park iliopo Silver Spring, Maryland Nchini Marekani.


Baadhi ya wanachama wa  CCM Tawi la DMV wakipata picha ya pamoja baada ya futari walioiyanda 


Wanachama wa  CCM Tawi la DMV na baadhi ya wageni wawili kutoka Londan Uingereza

Wageni wawili majirani wapendanao kutoka jijini London pia walihudhuria katika futari hiyo ilioandaliwa na  ilioandaliwa na tawi la CCM DMV Jana Ijumaa Aug 3, 2012 katika ukumbi wa Hillandale Park iliyopo Silver Spring, Maryland Nchini Marekani


Katibu wa CCM DMV Jacob Kinyemi, kushoto akipata picha ya pamoja na  Halima baada ya kumkabidhi rasmi kadi ya uwanachama wa CCM, Jana Ijumaa  na kuwa mwanachama rasmi wa CCM



Chanzo: SWAHILIVILLA

12 May 2012

5 Feb 2012

Viongozi wa Chadema jana tarehe 4 Februari 2012 wamekutana na kufanya Mazungumzo na Watanzania wanaoishi Washington DC . Katika msafara huo ambao umeongozwa na Mwenyekiti wa Chadema Mheshimiwa Freeman Mbowe na Mbunge wa Nyamagana na Waziri kivuli wa Mambo ya nje Mheshimiwa Ezekiel Wenje, wameongelea mambo mbalimbali ikiwemo suala la Mipango ya Maendeleo ya Chama na Mikakati ya kujiandaa na chaguzi zijazo hususani uchaguzi mkuu wa mwaka 2015.

Hali kadhalika wakazi hao wa Washington DC wametumia fursa hiyo kumuuliza maswali mbalimbali hususani suala la upatikanaji wa Katiba mpya. Akichangia katika mjadala huo Prof N. Boazi amewakumbusha viongozi hao umuhimu wa kuwa na katiba mpya ambayo itampunguzia madaraka Rais tofauti na sasa inayompa Rais  madaraka  makubwa na kunyima fursa kwa wengine.


Pia wakazi wa Washington DC walimuuliza Mheshimiwa Freeman Mbowe kuhusu suala la mgomo wa madaktari unaoendelea. Akijibu suala hili Mheshimiwa mbowe amesema kuwa alipata nafasi ya kuwasiliana na Viongozi wa mgomo huo lakini walimjibu kwamba hawataki kulifanya suala hilo la Mgomo kuonekana la kisiasa kwa kuwahusisha Chadema.



Mheshimiwa Freeman Mbowe akiwahudubia Watanzania wanaoishi  Washington DC jana jumamosi Feb, 4 2011 Nchini Marekani




 Wakazi wa Washington DC wakimsikiliza Mheshimiwa Freeman Mbowe kwa makini katika mkutano huo.




Mbunge wa Nyamagana na Waziri kivuli wa Mambo ya nje Mheshimiwa Ezekiel Wenje akiongea katika mkutano huo.


Baada ya Mheshimiwa Freeman Mbowe na  Ezekiel Wenje kuongea,  Watanzania waliohudhuria walipata nafasi ya kuliza masuali, na  moja ya maswali aliyoulizwa Mhe Freeman Mbowe ni ile dhana kuwa CHADEMA ni "chama cha waChagga na matajiri". Hapa chini anafafanua dhana zote hizo na ile aliyosema iliwahi kusambaa kuwa ni "chama cha waKristo"


CHANZO: Swahilivilla. Shukrani pia kwa Mzee wa Changamoto Mubelwa Bandio kwa kunitumia kiungo (link)

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.