4 Apr 2015


Kabla ya kuingia kwa undani kuhusu mada hii, ni muhimu kutanabaisha kuwa uchambuzi huu wa kitaalam (kiintelijensia) unatokana na mchanganyiko wa hisia na facts.Lakini pengine ni muhimu pia kueleza kuhusu nilivyofikia hitimisho lililopelekea kichwa cha habari hapo juu.

Tabia nzuri: Miaka kadhaa wakati nikiwa mtumishi katika taasisi flani huko Tanzania, mkuu wangu wa kazi ambaye pia alikuwa mmoja wa viongozi wakuu wa taasisi hiyo alivutiwa sana na mtizamo wangu wa kutilia mashaka kila jambo. Sio tu kwa vile mtizamo huo uliendana na mafunzo yanayohusu kazi hiyo bali pia ulikuwa na mafanikio. Moja ya kanuni kuu za kazi hiyo ni 'usiamini kitu chochote' sambamba na 'kumini vitu kwaweza kukuletea matatizo au hata kuuawa.' Kwahiyo, kila jambo liliangaliwa kwa pande mbili, huku swali kubwa likiwa 'what if.' Kwa kifupi, mtizamo huo ulisaidia sana kutambua 'ubaya uliojificha katika uzuri.'

Tabia mbaya: Wanasema ukishakuwa mwalimu unabaki mwalimu milele. Nami kwa kiasi kikubwa nimejikuta katika hali hiyo. Uzoefu na ujuzi nilioupata katika kazi hiyo umenifanya niwe mtu wa kutoamini vitu kirahisi, na hata nikiamini bado ninakuwa na wasiwasi flani. Kwa 'maisha ya mtaani,' tabia hiyo ina madhara yake. Kwa mfano, inaathiri relationships kwa kiasi flani maana ili uhusiano uwe imara sharti kuwa na kuaminiana. Kadhalika, jamii inaweza kuniona kama prophet of doom, yaani mtu anayehubiri majanga. Ni rahisi pia kulaumiwa kuwa ni 'mtu wa kuongelea mabaya tu' pale ambapo wengi wanadhani panastahili sifa.

Bottom line: Kinachohitajika ni uwiano kati ya kuamini vitu/watu kwa kuzingatia facts na hisia, kwa uande mmoja, na kutilia shaka vitu/watu kwa kuzingatia facts na hisia. Hili ni rahisi kuliongea lakini pengine ni guu kulitenda hasa kama hisia zinatawala zaidi ya facts, hususan kama hisia zenyewe ni zile zinazofahamika kitaalam kama 'hisia ya sita' (6th sense, yaani zisizotumia kuona, kusikia,kugusa,kulamba,kunusa na kuona)

Baada ya utangulizi huo, tuingie kwenye mada husika. Kuna sababu kadhaa za kimazingira zinazonipa wasiwasi kwamba Tanzania yetu inaweza kukumbwa na shambulio la kigaidi, wakati huu wa sikukuu ya Pasaka au huko mbeleni. Hapa chini, ninabainisha sababu hizo.

Tukio la ugaidi Garisa, nchini Kenya:

Juzi, magaidi wa Al-Shabaab walifanya shambulio kubwa la ugaidi katika mji wa Garisa, uliopo mpakani mwa Kenya na Somalia.Shambulio hilo limepelekea vifo vya watu takriban 150 huku taarifa mbalimbali zikionyesha uwezekano wa kuwepo idadi kubwa zaidi ya waliouawa. 

Awali, nilikuwa upande wa watetezi wa serikali ya Kenya na vyombo vya usalama vya nchi hiyo katika lawama kwamba walizembea kuchukua tahadhari. Hoja yangu kuu ilikuwa kwamba kupewa taarifa kuhusu ugaidi ni kitu kimoja, kuweza kuzifanyia kazi taarifa hizo na kuweza kuzuwia ugaidi ni kitu kingine kabisa. Hata hivyo, utetezi huo umepungua baada ya kupatikana taarifa mbalimbali zinazoashiria mapungufu makubwa ya serikali ya Kenya na taasisi za Usalama nchini humo kukabiliana na tetesi walizopewa kuhusu uwezekano wa shambulio hilo la kigaidi.

Tukiweka kando kilichojiri nchini Kenya lakini tukitilia maanani ukweli kuwa nchi hiyo ilitahadharishwa kabla ya tukio hilo, kwa Tanzania hali ni tofauti. Hadi sasa hakuna taarifa rasmi ya uwezekano wa kutokea shambulio la ugaidi.

Hata hivyo, ni muhimu kutambua kuwa Kenya ina ushairikiano mkubwa zaidi na taasisi za kiusalama za mataifa makubwa zaidi ya Tanzania, hasa ikizingatiwa kuwa Marekani, kwa mfano, ina 'base' yake ya kijeshi nchini humo (Manda Bay


Kwa maana hiyo, tahadharani ya Wamarekani kwa Kenya sio tu kwa maslahi ya Kenya bali ya Wamarekani pia. 

Hitimisho: Kwa kufanikiwa kufanya shambulio kubwa kabisa nchi Kenya, ikiwa ni takriban mwaka na nusu baada ya kufanya shambuli jingine la ugaidi kwenye supamaketi ya Westgate jijini Nairobi, magaidi wa Al-Qaeda wanaweza kushawishika kupanua kampeni yao ya uharamia hadi Uganda (ambako tayari kuna tishio kama ninavyoeleza hapo chini) na hata Tanzania (kwa sababu nitazobainisha mbeleni katika makala hii)

Uwezekano wa shambulio la kigaidi Uganda:

Machi 25 mwaka huu, Marekani ilitoa tahadhari kwa Uganda kuhusu uwezekano wa shambulio la kigaidi nchini humo. Kama ilivyo kwa Kenya, Marekani ina maslahi yake nchini Uganda ambako  inarusha ndege zake za upelelezi (PC 12) kutoka Entebbe, Kwahiyo usalama kwa Uganda una maslahi kwa Marekani pia.

Hitimisho: Iwapo Al-Shabaab watafanikiwa kutimiza uovu wao kuishambulia Uganda (Mungu aepushe hili), wanaweza kupata motisho wa kutanua zaidi kampeni yao hadi Tanzania hasa kwa kuzingatia kuwa kundi hilo la kigaidi linaziona nchi hizi tatu kama kikwazo kikubwa kwa uhai wake. 

Shaka ya ugaidi nchini Tanzania:

Moja ya matatizo makubwa ya kufahamu ukubwa au udogo wa tishio la ugaidi nchini Tanznaia ni siasa. Kwa muda mrefu, chama tawala CCM kimekuwa kikiutumia ugaidi kama kisingizio cha kudhibiti vyama vya upinzani na baadhi ya viongozi wake. Kwa minajili hiyo, hata serikali ikitoa taarifa sahihi kuhusu uwezekano wa tishio la ugaidi, kuna uwezekano wa wananchi wengi kudhani hiyo ni siasa tu.

Kana kwamba hiyo haitoshi, mwaka huu Tanzania itafanya uchaguzi mkuu wa Rais na wabunge hapo Oktoba. Japo haijazoeleka sana, historia inaonyesha kuwa angalau katika uchaguzi mkuu mmoja uliopita zilisikika taarifa za 'tishio la usalama' kutoka kwa nchi jirani. Mbinu hii hutumiwa na vyama tawala kujenga hofu ya kiusalama kwa wapigakura, na kuwaunganisha chini ya mwavuli wa chama kilichopo madarakani. Kwa mantiki hiyo, iwapo kutakuwa na taarifa za tishio la ugaidi, yayumkinika kuhisi baadhi ya wananchi wakatafrisi kuwa ni mbinu tu ya CCM kuelekea kwenye uchaguzi mkuu.

Lakini tatizo kubwa zaidi kwa sasa ni imani ndogo ya wananchi kwa serikali ya Rais Jakaya Kikwete na nyingi ya taasisi za serikali yake. Uhaba huo wa imani unatokana na mchanganyiko wa hisia za ushahidi wa matukio yaliyopita. Kutokana na kuandamwa mno na kashfa za ufisadi, kumeanza kujengeka imani miongoni mwa Watanzania kuwa serikali yao ni ya kifisadi pia.

Matumizi mabaya ya 'taarifa za kiintelijensia' yamewafanya Watanzania wengi kuwa na hisia kuwa 'taarifa za intelijensia' ni mbinu ya serikali kuwadhibiti. Mara kadhaa,Jeshi la Polisi nchini humo limekuwa likipiga marufuku maandamano ya kisiasa au kijamii kwa kisingizio cha 'taarifa za kiintelijensia.' Hivi karibuni, zilipatikana taarifa za mapigano makali kati ya jeshi la polisi wakishirikiana na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) dhidi ya 'magaidi' kwenye mapango ya Amboni mjini Tanga. Mchanganyiko wa taarifa za kukanganya na imani haba ya wananchi kwa jeshi hilo vilipelekea tukio hilo kuonekana kama 'mchezo wa kuigiza.'


Lakini licha ya kasoro hizo zinazoihusu serikali na taasisi zake, kuna tatizo jingine linalohusu vyombo vya habari vya nchi hiyo. Utiriri wa magazeti ya udaku na uhaba wa uandishi wa kiuchunguzi katika 'magazeti makini' umekuwa ukichangia mkanganyiko katika kubaini ukweli na porojo. Mfano mzuri ni tukio hilo la Amboni ambalo kwa kiasi flani liligeuka kama mfululizo 'series' ya mchezo wa kuigiza, huku magazeti ya udaku yakiwa na 'habari' nyingi zaidi ya 'magazeti makini.'

Hali hiyo yaweza kuwa inachangiwa na mahusiano hafifu kati ya taasisi za dola na vyombo vya habari, sambamba na mazowea ya taasisi hizo kutoa tu taarifa pasipo kurhusu maswali kutoka kwa wanahabari. Ukosefu wa taarifa sahihi, sambamba na ugumu wa kupata taarifa hizo huchangia 'udaku' kuziba ombwe husika.

Tukiweka kando kasoro hizo hapo juu, hadi sasa kuna mabo yafuatayo ambayo yanaweza kuwashawishi magaidi kuvamia Tanzania.

1. Mgogoro wa muda mrefu kuhusu uanzishwaji wa mahakama ya kadhi: Japo hadi muda huu suala hili limeendelea kuwagawa Watanzania kwa njia za mijadala na kwa amani, yayumkinika kuhisi kuwa magaidi wanaweza kulitumia kama kisingizio cha kuishambulia Tanzania. Cha kutia hofu ni ukweli kwamba sio tu suala hili limedumua kwa muda mrefu, hasa baada ya chama tawala CCM kuahidi katika Ilani yake ya Uchaguzi Mkuu mwaka 2005 kuwa itaanzisha mahakama hiyo lakini imeshindwa kufanya hivyo hadi leo, bali pia uamuzi usio wa busara wa kuupeleka Bungeni  Muswada wa Uanzishwaji Mahakama ya Kadhi kisha kuuondoa. Kana kwamba hiyo haitoshi, majuzi Rais Kikwete alikaririwa akidai kuwa serikali haina mpango wa kuanzisha mahakama hiyo, na badala yake jukumu hilo linabaki kwa Waislamu wenyewe. Haihitaji uelewa wa sheria kujiuliza kwamba kama suala hilo lilikuwa la Waislamu wenyewe, lilipelekwa Bungeni kwa minajili gani?

Licha ya mjadala huo wa uanzishwaji wa mahakama ya kadhi kuendelea kwa amani, mjadala kuhusu suala hilo umewagawa viongozi wa dini (Wakristo na Waislamu) na kwa kiasi flani umerejesha mgogoro kati ya baadhi ya viongozi wa Kiislam na serikali, sambamba na kuleta sintofahamu miongoni mwa baadhi ya wanasiasa.

2. Vitisho bayana kutoka kwa watu wanaodai ni magaidi.

Hivi karibuni ilipatikana video nchini Tanzania ambapo mtu mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Kaisi Bin Abdallah alidai kuwa kundi lao limekuwa na mafanikio katika ugaidi wa kudhuru polisi na vituo vya polisi. Video hii chini inajieleza yenyewe.



Licha ya 'mapungufu kadhaa' katika video hiyo, ambayo yanaweza kutupa imani kuwa ni porojo tu, kwa kuzingatia nilichokitanabaisha mwanzoni mwa makala hii, yawezekana tishio lililo kwenye video hiyo ni la kweli. Na hili ni moja ya matatizo ya kukabiliana na tishio la ugaidi: kuchukulia taarifa kuwa ni serious au kuzipuuza.

Hofu kuhusu uwezekano wa matukio ya ugaidi nchini Tanzania ilithibitishwa na kauli ya hivi karibuni ya Rais Kikwete kuwa mashambulizi ya hivi karibuni dhidi ya vituo vya polisi katika maeneo mbalimbali nchini humo yana uhusiano wa ugaidi, japo hakubainisha iwapo kuna uhusika wa makundi ya kigaidi ya kimataifa au la.

3. Taarifa za kimataifa:

Hadi muda huu hakuna taarifa za moja kwa moja zinazoashiria uwezekano wa tukio la ugaidi nchini Tanzania. Hata hivyo, bado kuna hali ya tahadhari wa wastani kuhusu uwezekano wa shambulio la kigaidi. Wakati serikali ya Canada inaeleza kuwa haina 'ushauri unaohusu taifa (Tanzania) zima, inawashauri raia wake kuchukua tahadhari kubwa kuhusiana na ugaidi. Kwa upande wake, Serikali ya Uingereza inatoa angalizo la jumla tu japo inatahadharisha kuhusu tishio la ugaidi wa Al-Shabaab kwa eneo  la Afrika Mashariki (ikiwa ni pamoja na Tanzania). Serikali ya Marekani inatoa ushauri wa jumla tu kwa kurejea matukio ya uvunjiafu wa amani huko nyuma.

Hata hivyo, ripoti iliyotolewa LEO na taasisi ya HTH Worldwide kuhusu risks zinazoikabili Tanzania, ugaidi unatajwa kuwa ni tishio la kuamika, japo uwezekano wa kutokea shambulizi la ugaidi ni wa wastani.

Pengine taarifa ya kuogofya zaidi ni ile iliyobainisha uwepo wa jitihada za kundi la kigaidi la ISIS kutaka kujiimarisha katika eneo la Afrika Mashariki, ikiwa ni pamoja na Tanzania. Kwa mujibu wa taarifa hiyo, ISIS inajaribu kujenga ushirikiano na Al-Shabaab kwa minajili ya kuwa na infulence katika eneo la Afrika Mashariki.

Kadhalika, majuzi zimepatikana taarifa kutoka Kenya kuhusu mwanamke mmoja wa Kitanzania aliyekamatwa na wenzie wawili Wakenya wakijaribu kwenda Somalia kuwa wenza wa magaidi wa Al-Shabaab.


 Tukio hilo linaakisi kinachotokea katika nchi mbalimbali za huku Magharibi ambapo mabinti kadhaa wamekuwa wakitorokea Syria kwenda kuwa 'wenza' wa magaidi wa ISIS.

Hitimisho:

Ni vigumu kwa kuwa na hakika ya asilimia 100 iwapo magaidi watafanya shambulio au la. Kwa upande mmoja, magaidi wana muda wote wanaohitaji kabla ya kutimiza azma yao, yaani wanaweza kusubiri kwa muda mrefu, ilhali vyombo vya dola havina faida hiyo kwani vinatakiwa kuwa makini muda wote.

Kuna msemo maarufu kuhusu ugaidi, kwamba wakati magaidi wanahitaji DAKIKA MOJA TU kutimiza uovu wao, vyombo vya usalama vinahitaji KILA SEKUNDE YA DAKIKA kuwazuwia magaidi husika.

Na japo uwepo wa taarifa za uhakika kuhusu uwezekano wa shambulio la kigaidi unaweza kusaidia jitihada za kukabiliana na magaidi husika, ukweli mchungu ni kwamba, kuwa na taarifa ni kitu kimoja, uwezo wa kuzitumia taarifa hizo ni kitu kingine.

Wakati huu tunaungana na wenzetu wa Kenya kulaani unyama wa Al-Shabaab, ni muhimu kuchukua tahadhari mahususi ili kuweza kukabiliana na uwezekano wa magaidi hao kushambulia Tanzania. La muhimu zaidi ni umoja na mshikamano, ambao kwa hakika unapotea kwa kasi, na haja ya haraka kwa Serikali kurejejesha imani ya wananchi kwake. Kingine ni umuhimu wa kuweka kando siasa katika masuala nyeti kama haya..

Kubwa zaidi ya yote ni la kitaalamu zaidi. Wakati serikali ya Tanzania imekuwa ikitegemea zaidi msaada wa kimataifa katika kuiimarisha kiuwezo Idara ya Usalama wa Taifa, ni muhimu jitihada za ndani pia zielekezwe katika kuijengea uwezo wa kukabiliana na matishio mbalimbali ya usalama wa taifa, ikiwa ni pamoja na ugaidi. Kwa uelewa wangu, uwezo wa vitengo vya kuzuwia ugaidi na kitengo cha kupambana na ujasusi unaathiriwa na mapungufu ya kimfumo na kisera, sambamba na nafasi ya maafisa wa Idara hiyo kwenye balozi za Tanzania nje ya nchi 'kubweteka' na teuzi zinazodaiwa kufanywa kwa misingi ya undugu,urafiki au kujuana.

Mwisho, tishio la ugaidi sio la kufikirika. Lipo, na kwa bahati mbaya, mazingira ya kulirutubisha tishio hilo yapo pia. 

3 Apr 2015

Takriban watu 150 wameuawa katika shambulizi lililofanywa na kikundi cha kigaidi cha Al-Shabaab, katika eneo la Garisa, nchini Kenya. Katika tukio hilo la kinyama lililotokea saa 11 asubuhi kwenye Chuo Kikuu cha Garisa, magaidi hao waliwapiga risasi na kuwachinja wanafunzi Wakristo.baada ya kuwazidi nguvu walinzi.
Masked gunmen stormed the Garissa University College campus, in Kenya's north-east, yesterday
Kwa mujibu wa gazeti la Daily Mail la hapa Uingereza, idadi ya waliouawa inafikia 147 na majeruhi ni 79 huku watu 500 wakiokolewa. Wengi wa waliouawa na wanafunzi wa chuo hicho, pamoja na polisi wawili,mwanajeshi mmoja na walinzi wawili.



Kenyan soldiers and police officers pictured at Garissa University College in Kenya where 147 people were murdered by terrorists yesterday

Waziri wa Mambo ya Ndani wa Kenya, Joseph Nkaissery , alieleza kuwa magaidi wanne walijifunga mabomu, na polisi walipowapiga risasi, walilipuka kama mabomu ambapo vipande vya mabomu hayo viliwahjeruhi polisi.
Kenyan police officers, pictured, take cover across from the university during the terrorist gun attack

Maafisa wa usalama katika eneo la tukio walieleza kwamba mateka kadhaa waliokolewa, na magaidi wanne waliokuwa na bunduki aina ya AK-47 waliuawa.
Kenyan security officials at the scene said dozens of hostages were freed and four of the gunmen were killed
Jana usiku, Kituo cha Operesheni ya Uokoaji Kitaifa kilieleza kwamba idadi ya wanafunzi wote, wazima na waliouawa sasa inafahamika.
Students fled the area, some of them without shoes, after the al-Shabaab terrorists launched their attack

Just last week, the Chief Security Officer at the University of Nairobi feared an attack was imminent and issued a security warning - but it is unclear whether the same information was relayed to Garissa officials 

Students ran for their lives as the terrorists launched their attack on the college campus in Kenya yesterday

Escape: Students pictured fleeing from the university. The death toll rose to 147 as the siege ended last night

Some of the students did not have time to dress as they fled for their lives when faced by the gunmen

Distraught: Paramedics help a woman injured during the attack on the Garissa University College campus

Shambulizi hilo linaelezwa kuwa baya zaidi nchini humo katika miaka 17 baada ya shambulizi jingine kubwa la kigaidi  mwaka 1998 kwenye Ubalozi wa Marekani nchini humo ambalo lilipelekea vifo zaidi ya 200.
Heavily armed soldiers pictured outside the Garissa University College campus where 147 people were murdered

Safety: A student hostage is escorted out of Garissa University College after Kenya Defence Forces ended a siege by terrorist gunmen

A Kenyan soldier runs for cover near Garissa University College's perimeter wall where 147 people have been killed

Rescued: A woman is led to safety from the building where she was held hostage by al-Shabaab terrorists





An injured man on a stretcher is taken to Kenyatta National Hospital following the attack by al-Shabaab terrorists

Medical treatment: An injured man arrived at Kenyatta National Hospital in Kenya's capital, Nairobi following the raid by terrorists



Tukio hilo la jana limetokea katika Juma Kuu, kipindi cha majonzi katika kalenda ya Wakristo. Jana ilikuwa Alhamisi Kuu ambayo kwa mujibu wa taratibu za baadhi ya madhehebu ya Kikristo, ni siku ya maungamo. Leo, Ijumaa Kuu, ni siku ya maadhimisho ya kusulubiwa kwa Yesu Kristo msalabani na hatimaye kufa. Jumapili ijayo ni Pasaka ambapo Wakaristo wanaadhimisha ufufuo wa Yesu Kristo.
A Kenya Defence Forces soldier carries a machine gun outside Garissa University College on April 2 2015

Captured: The Kenyan military launched a major security operation and detained one terrorist trying to escape

A Kenya Defence Forces tank driven outside Garissa University College. Al-Shabaab terrorists raided the campus shortly after 5am local time yesterday, overwhelming guards and killing anyone they suspected of being a Christian

Kenyan police managed to arrest one of the terror suspects, right, after he tried to flee from the campus

The death toll rose to 147 tonight and the siege ended, according to the country's disaster response agency. A total of 79 were injured, 587 were led to safety


Most of those killed were students but two police officers, one soldier and two watchmen are among the dead

Tragedy: Last night, officials confirmed the security operation is now over but the death toll has reached 147

Gunfire: A Kenya Defense Force soldier takes cover near the perimeter wall of Garissa University College

Kenyan soldiers took cover as heavy gunfire continued at Garissa University College in Kenya yesterday

Kenyan security officials at the scene said dozens of hostages were freed and four of the gunmen were killed

A Kenyan soldier takes cover as shots are fired in front of Garissa University College in Garissa town, located near the border with Somalia

Maafisa usalama wa Kenya walieleza kuwa gaidi mmoja alikamatwa wakati anajaribu kutoroka. Kadhalika, serikali ya nchi hiyo imetangaza zawadi ya Shilingi za Kenya Milioni  20 kwa atakayewezesha kukamatwa kwa Mohammed Mohamud, anayejulikana pia kama Dulyadin, au Gamadhere, ambaye anatuhumiwa kupanga shambulizi hilo.

A £145,000 reward has been offered for information leading to the capture of Mohamed Mohamud, who is believed to have masterminded the attack

Wanausalama nchini humo wanaamini kuwa gaidi huyo ni mkuu wa operesheni za kigaidi wa kundi la Al-Shaabab.Inaaminika kuwa gaidi huyo ametumia muda mwingi kuwafunza magaidi watarajiwa kwenye madrasa mbalimbali.Pia anatuhumiwa kuhususika na shambulizi jingine la kigaidi lililotokea Novemba 22 mwaka jana huko Mkka, nchini humo, ambapo watu 28 waliuawa.
A Kenyan soldier takes cover as shots are fired in front of Garissa University College in Garissa town, located near the border with Somalia
Mkuu wa Polisi, Joseph Boinet, alitangaza amri ya kutotembea ovyo kuanzia saa 12 unusu jioni hadi saa 12 unusu asubuhi.katika mikoa minne inayopakana na Somalia kama tahadhari ya kiusalama.

Chuo kilichokumbwa na shambulizi hilo kina takriban wanafunzi 887 wanaoishi katika mabweni sita



Mmoja wa mashuhuda wa tukio hilo, Collin Wetangula, Makamu Mwenyekiti wa Serikali ya Wanafunzi chuni hapo, alieleza kuwa yeye na wenzake waliposikia milio ya bunduki walijificha kwa kujifungia chumbani.

"Nilisikia milio ya bunduki, lakini hakuna mtu aliyepiga kelele, kwa hofu ya kuwashtua wanaofanya shambulio hilo."

"Watu hao waliokuwa wakifyatua risasi walikuwa wanasema 'sisi ni Al-Shabaab'"

Wetangula alieleza zaidi alisikia magaidi hao wakihoji wanachuo kuhusu dini zao (kama ni Waislam au Wakristo). Alisema, "Ukiwaambia wewe ni Mkristo, walikupiga risasi hapohapo. Kila mlio wa bunduki ulinifanya nijisikie kama nakufa."

"Baadaye tulipochungulia dirishani tuliwaona watu wenye sare za jeshi ambao baadaye walijitambulisha kuwa ni maafisa wa jeshi la Kenya."
Kenyan authorities have airlifted some of the wounded to Nairobi for treatment following the attack yesterday morning

Msemaji wa magaidi wa Al-Shbaab alitangaza kuwa kundi lake linahusika na shambulizi hilo. Sheikh Abdiasis Abu Musab, 'msemaji wa operesheni za kijeshi za Al-Shabaab,' alisema, "Tuliwachambua watu, na kuwaachia huru Waislam.Kuna miili mingi ya Wakristo, na tunawashikilia wengine kadhaa."

Rais Uhuru Kenyatta alieleza baadaye kuwa anaharakisha ajira ya askari 10000 ili kukabiliana na tishio la magaidi hao.
Treatment: Paramedics attend to an injured Kenyan student as she is wheeled into Kenyatta National Hospital in Nairobi
Wiki iliyopita, Afisa Mkuu wa Usalama katika Chuo Kikuu cha Nairobi alitoa tahadhari ya uwezekano wa shambulio la kigaidi lakini bado haijafahamika kuwa iwapo taarifa hizo zilitolewa kwa Chuo Kikuu cha Garisa pia.

Wounded: A man with a leg injury arrived at hospital in Kenya's capital. The death toll has risen to 147

Grace Kai, mwanafunzi wa Chuo cha Ualimu cha Garisa, alieleza kuwa walipewa tahadhari kuwa kuna uwezekano wa kutokea shambulio la kigaidi. Alisema, "Sura ngeni zilionekana Garisa, na kulikuwa na hisia ni magaidi."

"Jumatatu, Mkuu wa Chuo alitupa tahadhari...kwamba kuna sura ngeni zimeonekana maeneo ya chuoni hapo."
Kenyan officials had warned that al-Shabaab were suspected of planning a major assault on the college 
"Kisha Jumanne, tuliruhusiwa kurejea majumbani, na chuo kufungwa., lakini kampasi iliendelea kuwa wazi...na sasa wameshambulia."

CHANZO: The Mail Online


1 Apr 2015


Pengine kabla ya kueleza kwanini naunga mkono muswada wa kudhibiti uhalifu wa mtandaoni (The Cyber Crime Bill),ni vema nikaeleza background yangu kidogo ili kutanabaisha sio tu ninavyothamini uhuru wa habari bali pia nilivyonufaika nao.

Nilianza uandishi kwenye vyombo vya habari mwaka 1996,mwaka mmojabaada ya kujiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.Aliyenishawishi kuingia kwenye fani hiyo ni mwanahabari mkongwe, Albert Memba.Nikiwa mwaka wa pili, na yeye mwaka wa kwanza chuoni hapo, Memba aligundua kuwa 'utani wa busara' niliokuwa nikifanya eneo la 'kijiweni' (nyuma ya ukumbi wa mihadhara ya Sanaa -ATB,mkabala ya Maktaba Kuu ya chuo hicho) ungeweza kunipatia fursa katika gazeti 'lisilo serious.'

Nikafuata ushauri wake na kuanza kuandika 'unajimu wa utani' katika gazeti la 'udaku' la SANIFU lililokuwa linamilikiwa na kampuni ya Business Times, wachapishaji wa gazeti la Majira.Sanifu ni gazeti la kwanza kabisa la udaku Tanzania. Gazeti hilo lilinipa safu (column) niliyoipa jina 'nyota za Ustaadh Bonge.' Nyota hizo licha ya kutumia alama za unajimu kama 'Mshale' (Sagittarius), Ng'e (Scorpio),nk hazikuwa na ukweli wowote zaidi ya burudani. Kwa mfano, ungeweza kukutana na utabiri 'wa kisanii' kama huu: "Wiki hii utakumbwa na nuksi itakayokuletea ulaji mbeleni.Mwanao atagongwa na gari la ubalozi wa Marekani,lakini hatoumia.Ubalozi huo utakufidia kwa kukupatia viza ya kuishi Marekani.Usimzuwie mwanao kucheza barabarani."

Sio siri, watu wengi tu walivutiwa na 'Nyota za Ustaadh Bonge' na hii ilipelekea mie kupewa jina la utani la Ustaadh Bonge kwa muda wote niliokuwa hapo Mlimani (UDSM), na hadi leo, baadhi ya marafiki zangu wananiita Bonge.

Baada ya gazeti la Sanifu 'kufa' nilijiunga na gazeti jingine la udaku la Komesha, na baadaye Kasheshe, magazeti yaliyokuwa yanamilikiwa na kampuni ya IPP. Huko nako niliendeleza safu ya 'Nyota za Ustaadh Bonge.'

Hatimaye niliamua kuachana na magazeti ya udaku na kuhamia kwenye magazeti yenye 'serious news.' Nikafanikiwa kupata safu kwenye gazeti la KULIKONI,na safu hiyo ndio iliyopelekea jina la blogu hii yaani KULIKONI UGHAIBUNI ambalo lilikuwa jina la safu yangu katika gazeti hilo.Lengo la awali la blogu hii niliyoianzisha mwaka 2006 lilikuwa kuwapatia fursa wasomaji wa gazeti la Kulikoni walio nje ya Tanzania kusoma makala zangu kwa vile gazeti hilo halikuwepo mtandaoni.

Ni katika uandishi wa makala katika gazeti la Kulikoni ndipo nilipojitengenezea matatizo makubwa baada ya kuandika makala moja mwishoni mwa mwezi Oktoba 2006 ambapo nilikemea jitihada za aliyekuwa Waziri Mkuu wakati huo, Edward Lowassa, kukwamisha mjadala wa sakata ya Richmond. Makala hiyo ilipelekea Press Secretary wa Lowassa, Said Nguba, kunikaripia vikali hadharani. Mwendelezo wa sakata hilo hatimaye ulipelekea mwisho wa ajira yangu serikalini mwaka 2008.

Baadaye nikapewa safu katika gazeti la MTANZANIA,ambapo safu yangu ilijulikana kama MTANZANIA UGHAIBUNI. Lilipoanzishwa jarida la RAIA MWEMA, nikafanikiwa kupata safu, ambayo niliita RAIA MWEMA UGHAIBUNI, ambayo imedumu kwa miaka kadhaa hadi hivi leo.

Kwahiyo kwa kuangalia background hii utabaini kuwa sio tu nimeutumia vema uhuru wa habari bali pia nimenufaika nao vya kutosha.Nitakuwa mtu wa mwisho kuwa kikwazo cha uhuru huo kwani nami ni mnufaika mkubwa.

Nirejee kwenye mada halisi ya makala hii.Sababu kuu zinazonifanya niunge mkono muswada wa kudhibiti uhalifu wa mtandaoni ni TATU:

Kwanza, KITAALUMA/KITAALAM: Kwa zaidi ya miaka 10 huko nyuma, nilisomea na hatimaye kufanya kazi katika sekta ya usalama. Japo kimsingi kwa sasa si mwajiriwa katika taasisi ya usalama, nina interest kubwa kuhusu stadi na taaluma hiyo, ndani na nje ya Tanzania. Licha ya kujihusisha na usalama kwa maana ya intelijensia, pia nina interest kubwa kuhusu usalama wa mtandaoni hususan uhalifu wa mtandaoni (cybercrime). 

Sambamba na hilo, nimekuwa nikiutumia sana mtandao kwa minajili ya kupashana habari.Licha ya blogu hii, nimekuwa nikiweka mabandiko katika mitandao mingine ya kijamii kama vile Tumblr, Google+, Facebook, Instagram, Pinterest na hata Jamii Forums. Kutokana na uwepo wangu mkubwa mtandaoni, nimelazimika kufuatilia kwa karibu umuhimu wa usalama mtandaoni ikiwa ni pamoja na njia na nyenzo za kujikinga na wahalifu wa mtandaoni, sambamba na kuhabarisha masuala mbalimbali yanayohusiana na suala hilo.

Vilevile, kwa miaka ya hivi karibuni nimepata interest mpya ya software hususan za simu, kwa maana ya maendeleo na matumizi ya apps mbalimbali, pamoja na masuala ya teknolojia kwa ujumla.Katika hilo, nimelazimika pia kufuatilia usalama wa software mbalimbali, za kompyuta na simu.

Kwahiyo, uzoefu wangu mdogo kitaaluma/kitaalam unanituma kuunga mkono umuhimuwa muswada huo hasa kwa vile suala la kompyuta kwa ujumla bado ni geni kwa Watanzania wengi, na hiyo inaota fursa kwa wahalifu wa mtandaoni kufanya hujuma zao kirahisi.Lakini pia hali hiyo inapelekea matumizi yasiyofaa ya teknolojia hiyo ngeni.

Kiintelijensia, kama ilivyosikika hivi karibuni, kuna jitihada za makundi ya kigaidi ya ISIS na Al-Shabaab kufanya hujuma eneo la Afrika Mashariki ikiwamo Tanzania. Kwa bahati mbaya, mtandao umekuwa nyenzo muhimu ya vikundi vya kigaidi, hususan ISIS, katika harakati zao za kidhalimu. Na hivi karibuni tumesikia matukio mbalimbali yanayoelezwa kuwa ya kigaidi huko nyumbani. Hatuwezi kupuuzia taarifa hizi kwa sababu ugaidi, kama ilivyo kifo au tukio la wizi/ujambazi, hausubiri kualikwa.Unatokea tu. Kwahiyo ni muhimu kuchukua hatua za tahadhari ikiwa ni pamoja na kudhibiti matumizi ya kompyuta kwa minajili ya kufanya uhalifu. Naomba kusisitiza kuwa huu ni mtizamo wa kitaalam (kiinteliujensia) zaidi, na pengine si rahisi sana kueleweka.

Pili, KIJAMII: Ni ukweli usiopingika kuwa Tanzania yetu inaweza kuwa inashika nafasi ya juu kabisa katiika matumizi yasiyofaa ya mtandao.Ninaamini kuwa wengi wetu tumeshuhudia utitiri wa blogu za ngono mtandaoni. Ashakum si matusi, uki-Google 'picha za uchi' utakumbana na mlolongo wa mambo yasiyoendana na mila na desturi zetu.

Kama kuna sehemu inayotoa ushahidi mkubwa wa matumizi mabaya ya mtandao kwa Tanzania yetu basi ni INSTAGRAM.Huko imekuwa 'dunia uwanja wa fujo.' Kama si mzoefu wa matusi basi dakika chache tu katika mtandao huo utakutana na kila aina ya matusi. Wenyewe wameanzisha 'timu' za kusapoti au kupinga watu flani maarufu, na kwa hakika lugha inayotumika huko inachefua. Busara pekee hazitoshi kuwadhibiti watu hawa.Dawa pekee ni kuwa na sheria, sio tu ya kuwakumbusha umuhimu wa kuzingatia maadili bali pia kuwazuwia kuendeleza maovu yao.Ifike mahala, kabla mtu hajabandika picha za uchi ajiulize mara mbili iwapo hatochukuliwa sheria.

Matumizi ya simu za kisasa zenye kamera yamechangia 'kumfanya kila mwenye simu kuwa paparazi,' na katika hili, tumekuwa tukishuhudia picha zisizofaa kabisa mitandaoni.Hivi ni mara ngapi tumekwazwa na picha za maiti kwenye mitandao ya kijamii? Ni mara ngapi tumeitaka serikali kuchukua hatua dhidi ya uhuni wa kubandika picha zisizofaa mtandaoni? Naam, serikali imesikia kilio chetu kwa kuleta muswada wa kuzwia uhalifu wa mtandaoni ili kupata sheria itakayosaidia angalau kupunguza kadhia hiyo inayokera wengi.

Pia kuna blog zisizo za picha za ngono lakini zinazosababisha utengano mkubwa katika jamii. Ukimtkana mtu kwa mdomo unaweza kusahau na hata huyo aliyetukanwa anaweza kusahau, lakini mtandao wa kompyuta (internet) hausahau kitu. Uki-Google jina langu, moja ya mambo utakayokutana nayo ni 'ugomvi' wangu wa zamani sana na gazeti moja huko Tanzania uliotokana na mimi kulilaumu kwa kutumia picha za uongo kuhalalisha habari waliyochapiusha.Japo ugomvi huo uliisha miaka mingi iliyopita na wahusika ni marafiki zangu kwa sasa, na tumeshasdahau yaliyopita, lakini internet bado inakumbuka.

Sasa blogu zinazoendekeza matusi, kuchafuana, uzushi na vitu kama hivyo sio tu zinawathiri wahanga kwa muda huo wa tukio lakini zinaweka kumbukumbu ya milele mtandaoni...kwa sababu mtandao hausahau kitu. Tuendelee kuvumilia uhuru huu usio na ukomo wa kumchafua mtu yeyote kwa vile tu mlikorofishana? 

Baba wa Taifa aliwahi kutuusia kuwa "Uhuru bila utii ni ujinga" na "uhuru usio na mipaka ni uwendawazimu." Sasa pasipo sheria ya kudhibiti ujinga na uwendawazimu huu unaotokana na dhana fyongo kuwa 'hakuna anayeniona ninapobandika mabaya mtandaoni' tutaendelea kuumizana.

Tatu, sababu BINAFSI: Japo sitaki kuwa mbinafsi kwa maana ya 'kuunga mokono muswada huu kwa sababu mie pia ni mhanga' lakini pia sitaki kuwa mnafiki kwa kukwepa ukweli kwamba nimeshawahi kuwa mhanga wa matumizi mabaya ya uhuru mtandaoni. Mfano mmoja halisi ni kilipotokea kifo cha binti mmoja aliyekuwa miongoni mwa watumiaji mahiri wa mtandao wa kijamii wa Twitter, Marehemu Betty Ndejembi (Mungu aiweke roho yake mahali pema peponi). Kwa vile kabla ya tukio hilo la kusikitisha nilikuwa nikihamasisha upinziani dhidi ya unyanyasaji mtandaoni, kifo cha marehemu Betty kilinipa changamoto mpya, hasa ikizingatiwa kuwa siku chache kabla ya kukutana na mauti, binti huyo alinyanyaswa vya kutosha huko Twitter. Kwahiyo haikuwa jambo la kushangaza nilipoungana na baadhi ya wanaharakati kutumia hashtag #StopCyberbullying.

Lakini kwa sababu ambazo hadi leo sizielewi, lilijitokeza kundi katika mtandao huo sio tu kupambana na jitihada hizo za kukemea unyanyasaji mtandaoni bali pia kunichafua kwa maana ya jitihada kuonyesha kuwa eti nami ni mnyanyasaji pia huko mtandaoni. Kama kuna kitu kiliniuma na kinaendelea kuniuma hadi leo ni pale mmoja wa watu hao aliponiita MUUAJI. Yaani kuhamasisha mapambano dhidi ya unyanyasaji mtandaoni ni sawa na UUAJI? Ningeweza kumburuza mtu huyo mahakamani kwa kosa la kunidhalilisha (defamation) lakini ukosefu wa sheria halisi inayohusu unyanyasaji mtandaoni (cyberbullying) ungeweza kuniathiri.

Ni rahisi kuzungumzia 'uhuru usio na ukomo' kwa jamii iwapo hujawahi kuwa mhanga wa matumizi ya uhuru huo. Naomba nisieleweke vibaya.Siungi mkono muswada huo kwa vile tu mie ni mhanga huko nyuma, au utakomoa watu flani, lakini pia kuna sababu nyingine muhimu kama nilivyobainisha hapo juu.

MWISHO, japo ninatambua umuhimu wa wananchi kushirikishwa katika utungaji wa sheria zinazowahusu, na pia ninaafikiana na hoja ya kutoharakisha miswada inayohitaji ushirikishwaji wa umma, ninaunga mkono muswada huo kwa sababu UNAHITAJIKA SASA. Na kwa hakika umechelewa sana. Hatuwezi kuendelea kuvumilia matumizi mabaya ya mtandao wa kompyuta kwa kisingizio cha uhuru wa habari. Hatuwezi kuendelea kuvumilia picha za ngono na maiti zikiwekwa hadharani kama mapambo.Jamii yeyote yenye kuzingatia maadili inapaswa kuchukua hatua kali dhidi ya vitendo kama hivyo. Hatuwezi kuwatengenezea mazingira mazuri magaidi kwa kisingizio cha 'umbeya si dhambi.' Madhara ya kutochukua hatua ni makubwa kuliko kuchukua hatua.

Mie ninaweza kuwa mhanga wa sheria hiyo (ikipitishwa) hasa kwa vile ni mtumiaji mkubwa wa mtandao, na pia mkosoaji wa serikali ninapoona inastahili kukosolewa. Ni kweli kwamba sheria hiyo ikipitishwa inaweza kudhuru hata watu wasio na hatia.Lakini katika hili, tatizo si sheria bali CORRUPTION. Tunapozungumzia corruption hatumaanishi tu kuhonga au kuhongwa fedha, bali hata kupindisha sheria kwa maslahi binafsi au kukomoana.Sasa katika hilo, tuna tatizo katika nyingi ya sheria zetu.Ni wangapi wanaporwa viwanja kutokana na corruption katika sheria na sekta ya ardhi? Ni wangapi wapo gerezani muda huu kwa sababu tu walishindwa kuhonga polis au hakimu? Ni vigumu kwa sheria yoyote kuwa na ufanisi katika mfumo corrupt.Ni jukumu letu sote kupambana na corruption ili sheria zenye maslahi kwa jamii zisiishie kuathiri wasio na hatia.

Muswada huu ni kwa maslahi ya kila Mtanzania. Kama wewe si mhalifu wa mtandaoni, sheria hii haitokudhuru. As to itatumika vibaya na serikali, tatizo hapo sio sheria husika bali corruption.Kuna sheria nyingi tu na pengine kali zaidi ya hii tarajiwa, kwa mfano Sheria ya Usalama wa Taifa 1970, Sheria ya Idara ya Usalama wa Taifa 1996 na Sheria ya Kuzuwia vitendo vya Ugaidi ya mwaka 2002, zinazoweza kutumika vibaya kutokana na corruption. Sina hakika wangapi miongoni mwa wanaopinga muswada wa Cybercrime wameshakuwa wahanga wa 'matumizi mabaya' ya sheria hizo kali kuliko hii tarajiwa.

Hofu yetu dhidi ya matumizi mabaya ya sheria isiwe sababu ya kutokuwa na sheria kabisa. Tusielemee kwenye hofu yetu tu bali tutambue kuwa takriban kila siku kuna victims kadhaa kutokana na ukosefu wa sheria ya kudhibiti uhalifu wa mtandaoni.

ANGALIZO: Huu ni mtizamo wangu binafsi na unaweza kuonekana fyongo kwa mwingine.Twaweza kujadiliana pasipo haja ya 'kupigana.'

MUNGU IBARIKI TANZANIA




Kuanzia leo April Mosi, Watanzania wanaokuja hapa Uingereza hawatahitaji viza kufuatia uamuzi uliotolewa jana na kutangazwa na 'Wizara ya Mambo ya Ndani' ya hapa (Home Office) Hatua hiyo ni sehemu ya mkakati wa Uingereza kushirikianana nchi kadhaa za jumuiya ya madola, ikiwemo Tanzania, katika maeneo kadhaa ya kiuchumi.

Kwa habari zaidi BONYEZA HAPA

29 Mar 2015



Kwa muda mrefu, baadhi ya watumiaji wa mtandao wa kompyuta (Internet) wamekuwa na wakati mgumu kufuatia kushamiri kwa unyanyasaji mtandaoni, kwa kimombo CYBERBULLYING.

Kwa kiasi kikubwa, tatizo hili linaakisi tabia zetu nje ya mtandao. Mtu aliyezowea kunyanyasa wenzie mtaani, akiingia mtandaoni anaweza kuendeleza tabia hiyo kirahisi. Kadri mtandao unavyozidi kuwa sehemu ya maisha yetu ya kila siku ,ndivyo unavyoakisi maisha yetu 'ya kawaida' nje ya mtandao. 

Kwa upande mwingine, mtandao unatoa fursa ya watu wenye tabia tofauti kukutana. Ndio maana si ajabu kukuta mtu mmoja akiweka bandiko kuhusu dini, mwingine akaweka bandiko kuhusu matusi.

Licha ya tabia, mtandao pia huwakutanisha watu wenye sifa tofauti: wapole na wakorofi, wapenda amani na wagomvi, wenye elimu na mbumbumbu, wenye aibu na wasio na mishipa ya aibu, nk. 

Kadhalika, mtandao unatoa fursa mbalimbali, nzuri na mbaya. Kwa mfano, mtandao unatuwezesha kuwa karibu na viongozi wa nyanja mbalimbali, kutoka mawaziri hadi viongozi wa taasisi binafsi.Uzuri wa fursa hiyo ni pamoja na kurahisisha mawasiliano baina ya watu wanaotoka 'madaraja' tofauti ya kijamii. Kadhalika, fursa hiyo inatuwezesha kujifunza kutoka kwao, sambamba na kufuatilia masuala mbalimbali ambayo kutokana na nafasi zao yanagusa maisha yetu binafsi au ya jamii kwa ujumla.

Fursa hiyo pia inatuwezesha kuwa karibu na watu mbalimbali, muhimu na wa kawaida. Katika mazingira ya kawaida, ni vigumu kufahamiana na Waziri, kwa mfano, labda kuwe na undugu, kufahamiana au mahusiano kikazi.

Hata hivyo, mtandao pia unatoa fursa 'mbaya.' Binadamu tupo tofauti, kuna wenzetu ambao wakiiona fursa wanaitumia kwa manufaa, lakini kuna wengine sio tu hawataki kujifunza 'mazuri' ya wenzao (ambayo wao hawana) pia hujenga chuki na jitihada za kuwachafua au kuwadhalilisha wenzao wenye 'mazuri.' Kwa mfano, unaweza kukutana na mtu ambaye hakubahatika kupata elimu ya kutosha, au hakusoma kabisa. Anapokutana na mwenye elimu kiasi au ya juu, badala ya kutumia fursa hiyo kama 'darasa nje ya shule' anaanzisha chuki na uhasama usio na manufaa.

Kama dunia ilivyo uwanja wa fujo, ndivyo ilivyo kwa mtandaoni. Kuna mazuri na mabaya. Kuna baadhi yetu ambao tumenufaika sana kwa uwepo wetu mtandaoni, kwa maana ya kutengeneza urafiki na watu muhimu, lakini pia kuna nyakati tumejikuta tukikutana na 'maadui.'

Ofkoz, mtandano sio sehemu ya kubadilisha mawazo, kujifunza au kuuliza maswali tu bali pia ni sehemu ya burudani. Utani ni ruksa lakini utani wenyewe usizidi kiwango. Na kanuni ya mtaani kuwa usimtanie mtu asiyekutania, ina-apply mtandaoni pia.

Kwa bahati mbaya kuna wenzetu ambao hulazimisha utani.Wengine huenda mbali zaidi kwa kulazimisha kumjua mtu zaidi ya anavyojijua yeye mwenyewe.

Kwa bahati nzuri, hatimaye serikali imesikia kilio dhidi ya unyanyasaji wa mtandaoni na Jumanne ijayo inatarajia kuwasilisha muswada kuhusu uhalifu wa mtandaoni ambao pamoja na mambo mengine unaharamisha unyanyasaji wa mtandaoni (cyberbullying) 

Katika muswada huo unajulikana kwa kimombo kama The Cyebrcrimes Act, 2015, ibara ya 23 inaharamisha unyanyasaji mtandaoni (cyberbullying) na kutaja adhabu husika. 

Muswada unafafanua maana ya cyberbullying, kwamba "mtu hataruhusiwa kuanzisha au kutuma mawasiliano ya kielektroniki kwa kutumia kompyuta kwa mtu mwingine kwa malengo ya 'kumsukuma kwa nguvu' (coerce), kumtisha, kumyanyasa au kumsababishia msongo wa mawazo, na mtu atakayekiuka kipengele hocho atakuwa anafanya kosa, na adhabu yake ni sio chini ya shilingi milioni tatu au kifungo cha sio chini ya mwaka mmoja au adhabu zote pamoja."  

Muswada kamili ni huu hapa chini (kwa bahati mbaya au makusudi, watawala wetu hawakuona umuhimu wa kuupatia tafsiri ya Kiswahili)



Wakati muswada huu ni habari njema kwa wahanga wa unyanyaswaji mtandaoni, unatarajiwa pia angalau kupunguza kushamiri kwa matusi na picha zisizofaa mtandaoni. Sio siri kwamba baadhi ya mitandao ya kijamii, hususan Instagram, imegeuka uwanja wa matusi.

Kibaya zaidi, umahiri wa matusi umegeuka moja ya vyanzo vya umaarufu mtandaoni. Kama nilivyobainisha hapo juu,mtandao unatoa fursa 'mbaya' kwa wenzetu  wasio  na cha kuelimisha, kujadili au hata kujivunia hadharani, na matokeo yake ni kuwabughudhi watu wengine au kubandika picha zisizofaa kama mbinu ya kusaka sifa za kipuuzi.

Hata hivyo, ni muhimu kukumbushana kuwa Tanzania yetu haina uhaba wa sheria.Tatizo kubwa ni katika kuziheshimu na kuzitekeleza. Twaweza kuwa na sheria kali dhidi ya uhalifu wa mtandaoni lakini utekelezaji ukiwa hafifu basi sheria hizo zitabaki maandiko tu vitabuni.

Kadhalika, ni muhimu kutahadharisha kwamba sheria hii ya uhalifu wa mtandaoni isitumiwe vibaya na serikali kuwanyima wananchi uhuru wa mawasiliano, au kibaya zaidi, kuitumia kwa minajili ya kuficha maovu na kuwalinda waovu. Sitarajii kuona sheria hii ikitumika iwapo chombo cha habari kitaibua utovu wa maadili wa kiongozi, kwa mfano.

Mwisho, ni matarajio yangu kuwa vitendo vya uhalifu wa mtandaoni, ikiwa ni pamoja na cyberbullying, vitapungua kufuatia sheria hii, iwapo itapitishwa na bunge. Angalau sasa, cyberbullies watafikiria mara mbili kabla ya kumwaga sumu zao kuwanyanyasa watu wasio na hatia.

26 Mar 2015

The United States said on Wednesday it had information of “possible terrorist threats” to locations frequented by Westerners in Uganda’s capital, Kampala, and warned that an attack could take place soon.
The U.S. Embassy in Kampala issued the warning in a statement posted on its website.
"The U.S Embassy has received information of possible terrorist threats to locations where Westerners, including U.S. citizens, congregate in Kampala, and that an attack may take place soon," it said.
"Out of an abundance of caution, the U.S. mission has canceled some non-essential events scheduled at local hotels in the coming days," it added.
Uganda is a close security ally of the United States in East Africa. The embassy issued similar alerts last year about possible attacks in Uganda.
The embassy cautioned that foreigners staying in or visiting hotels should expect increased security sweeps.
Uganda is one of the countries that contributes forces to an African Union peacekeeping mission battling the Islamist militant group al Shabaab in Somalia.
Al Shabaab, which is aligned with al Qaeda, attacked a shopping mall in Nairobi, capital of neighboring Kenya, in 2013. In 2010, it bombed sports bars in Uganda where people were watching soccer’s World Cup on television. Dozens were killed in both attacks.
SOURCE: Matthew Aid



Naibu Waziri wa Afya wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar,Mohamed Thabit Kombo akimpongeza Mwenyekiti wa Mfuko huo,Doris Mollel kwa kuona jukumu la kusaidia jamii katika kuokoa maisha ya watoto njiti.






Naibu Waziri wa Afya wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar,Mohamed Thabit Kombo akizungumza wakati wa hafla ya kutambulisha Mfuko wa Doris Mollel,iliyofanyika kwenye Hoteli ya Hyatt Regency,jijini Dar es salaam.




Mwenyekiti wa Mfuko huo,Doris Mollel akizungumza na wageni waalikwa waliofika kwenye hafla ya kutambulisha Mfuko wa Doris Mollel,uliofanyika kwenye Hoteli ya Hyatt Regency,jijini Dar es salaam.



Naibu Waziri wa Afya wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar,Mohamed Thabit Kombo (pili kushoto),Balozi Mwanaid Maajar (kulia),Mwenyekiti wa Mfuko huo,Doris Mollel (katikati) pamoja na wadau wengine wa Mfuko huo wakishiriki kwa pamoja kukata keki,kuashiria uzinduzi rasmi wa Mfuko wa Doris Mollel,uliofanyika kwenye Hoteli ya Hyatt Regency,jijini Dar es salaam.



Sehemu ya Wageni waalikwa katika hafla ya kutambulisha Mfuko wa Doris Mollel,iliyofanyika kwenye Hoteli ya Hyatt Regency,jijini Dar es salaam.



Picha ya pamoja na baadhi ya wadau waliohudhulia hafla hiyo.


Kutoka kulia ni HEENA ambaye ni mmoja kati ya washirika wakubwa wa mfuko huo, wakiwa wameshikana mikono na muanzilishi wa mfuko huo miss DORIS MOLLEL pamoja meneja wa mfuko huo RAHAB MBISE mara baada ya kuzindualiwa kwa mfuko huo jijini Dar es samaam


Meneja wa mfuko huo RAHAB MBISE akizungumza wakati wa uzinduzi huo uliofanyika jjini Dar es salaam




Mrembo wa singida aliyeshika nafasi ya tatu katika mashindano ya miss tanzania mwaka wa 2014 DORIS MOLEL leo amezindua rasmi rasmi DORIS MOLEL foundation ambayo ni mahususi kwa ajili ya kusaidia watoto ambao wamekuwa wanazaliwa wakiwa bado hawajatimia NJITI ambapo amewataka watu mbalimbali kujitokeza kumpa saport katika shighuli hiyo.

Uzinduzi huo ambao umefanyika leo jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na viongozi pamoja na wadau wanaohusika katika kuwasaidia watoto hao. wengi wamepongeza jitihada zinazoonyeshwa na mrembo huyo kwani watoto wanaozaliwa wakiwa na tatizo hilo wamekuwa wakusahaulika sana nchini tanzania jambo ambalo limetajwa kuwaadhiri watoto hao pamoja na wazazi wao.

Akizungumza katika uzinduzi huo, Mrembo DORIS ambaye ni mmoja  kati ya watu walioathiriwa na tatizo hilo (alizaliwa akiwa njiti) alisema kuwa ameamua kuwasaidia watoto na wazazi  wenye matatizo hayo baada ya yeye kupitia katika kipindi kama hicho ambapo alisema kunahitajika msaada mkubwa kutoka kwa watu wa mbalimbali.

Mimi nilizaliwa nikiwa njiti nilikuwa sijafikisha uzito halali wa kuzaliwa lakini nilizaliwa na mama akanisaidia hadi leo hii mnaniona hapa ni miss Tanzania na ni mtu nayekubalika na jamii,hivyo nimeona kuna haja ya kuwasaidia watoto kama mimi ambao wamezaliwa hivyo ili waweze kukua na afya njema na baadaye kutimiza malengo ya maisha yao,”alisema mrembo huyo.

Alisema kuwa baada ya kuchaguliwa kuwa mrembo namba tatu wa Tanzania alifikiria kitu cha kufanya ili arudishe shukrani kwa Watanzania na baada ya kutembea katika maeneo mbalimbali aligundua kuwa watoto wanaokumbwa na matatizo hayo bado wamekuwa hawapewi kipaumbele katika kusaidiwa jambo ambalo limemsukuma yeye kuanza kufanya mchakato huo.

Aidha alisema kuwa ipo haja ya serikali pamoja na wadau mbalimbali kuunga mkono jitihada hizo kwa lengo la kuokoa kizazi kikubwa ambacho kinazaliwa na matatizo kama hayo ambapo kwa takwimu zinaonyesha kuwa zaidi ya watoto laki mbili wanazaliwa wakiwa njiti kwa mwaka nchini Tanzania.

Uzinduzi huo uliambatana na  uchangiaji wa mfuko huo kwa ajili ya kuwasaidia watoto hao, ambapo watu mbalimbali wachangia na kuwaomba Watanzania wengine kuendelea kumsaidia mrembo huyo kuhakikisha kuwa anatimiza lengo lake.

Baadhi ya watu waliojitokeza kumpa nguvu katika shughuli hiyo leo ni pamoja na muandaaji wa mashindani ya miss tanzania ambapo ndiko mrembo huyo alikotokea bwana hashimu lundenga, Mwenyekiti mstaafu wa Bodi ya Shirika la Usafiri Dar es Salaam (UDA) Mzee Iddi Simba, Naibu Waziri wa Afya wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mohamed Thabit Kombo pamoja na viongozi mbalimbali kutoka Bara na Viusiwani




Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.