tag:blogger.com,1999:blog-26327165.post3814269620754366187..comments2023-12-12T11:46:45.188+00:00Comments on Kulikoni Ughaibuni : Nova Kambota: VIVA KAMANDA LOWASSAEvarist Chahalihttp://www.blogger.com/profile/08220429042701710191noreply@blogger.comBlogger2125tag:blogger.com,1999:blog-26327165.post-22452234129174453892011-12-11T03:48:14.844+00:002011-12-11T03:48:14.844+00:00Kambota nitakubota, hata kama kiroboto,
Yote unayo...Kambota nitakubota, hata kama kiroboto,<br />Yote unayolumbata, si chochote ni kokoto,<br />Huna mpaka na kata, nijuacho u limpyoto,<br />Kambota acha unywanywa, naona unatumiwa.<br /><br />Lowassa bado fisadi, hata mmpambe vipi,<br />Kambota wewe hasidi, watumika kama nepi,<br />wajiona wafaidi, kumbe kesho ni makapi,<br />Kambota acha unywanywa, Lowassa akutumia.<br /><br />Wauliza nalipwaje, Nani huyo anilipe?<br />Sijalipwa hata punje, mie mwezio si kupe,<br />Shurti mi nijikunje, niishi si kwa mahepe,<br />Kabota acha ushamba, Lowassa atakuponza.<br /><br />Naijua Richmond, Richmond ni Lowassa,<br />Kikwete ni Richmond, Richmond ni mkasa,<br />Kambota nawe ni bundi, Richmond takutesa,<br />Japo wachumia tumbo, Kambota acha ujuha.<br /><br />Utajaliwa ja ng’oda, Siku yako ikifika<br />Ja ng’oda utakonda, Lowassa akikutoka<br />Ukuuishie ukuda, ubaki kulalamika<br />Fisadi hana rafiki, Jifunze kwake Lowassa<br /><br />Mambo yalipombana, Kikwete kaumuumbua,<br />Hawa marafiki sana, Itakuwa wewe bua,<br />Leo sana wajiona, ujinga wakusumbua,<br />Kambota acha ujuha, Lowassa hasafishiki.<br /><br />Huna mpaka na nune, Kambota wala jaani,<br />Leo wewe ujivune, kumbe wenda majilini,<br />Sema sana utukane, itafika arobaini,<br />Kambota acha ujuha, Lowassa hasafishiki.<br /><br />Kaditamati natua, mbele sitaendelea,<br />Kwa hapa naomba dua, wadudi anisikia,<br />Ninamuomba mulua, Kambota aone jua,<br />Kambota chumia tumbo, hebu tumia ubongo.<br /><br />Nkwazi MhangoAnonymousnoreply@blogger.comtag:blogger.com,1999:blog-26327165.post-35648338340526846302011-12-11T01:16:51.361+00:002011-12-11T01:16:51.361+00:00Chahali umenisononesha. Umeingiwa na nini hadi una...Chahali umenisononesha. Umeingiwa na nini hadi unampamba huyu fisadi wa kunuka? Sikuamini kuona naweka shairi langu la kumjibu huyu mtoto changudoa wa maadili wa Lowassa na ukalifuta. Kweli binadamu si viumbe wa kuamini. Hata hii futa kwa maslahi yako. Ila jua legacy uliyokwisha ijenga ina thamani kuliko hiyo hongo ya mabaki ya ufisadi.<br />Nkwazi MhangoAnonymousnoreply@blogger.com