4 Jun 2013

1 c2a93
2 f62f0
3 2ee6a
4 64345
5 d0206

6 22b50
7 4b4d8
8 7ac7f
9 38e5a
10 16480
11 cfaf2
12 af5ae
13 78606
14 c3197
15 d40a2
16 27144
17 cdc7f
18 05b65
19 a08de
20 ce3f7

3 Jun 2013



THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS

Telephone: 255-22-2114512, 2116898
E-mail:  [email protected]
              [email protected]             

Fax: 255-22-2113425


PRESIDENT’S OFFICE,
      THE STATE HOUSE,
              P.O. BOX 9120,  
DAR ES SALAAM.
Tanzania.
 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Ban Ki Moon ampongeza Rais Kikwete kuhusu njia mpya ya kuleta amani DRC

KATIBU Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN) Mheshimiwa Ban Ki Moon amempongeza na kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete kwa kutoa mapendekezo muhimu na murua ya aina yake ya kuanza kutafuta amani ya kudumu katika eneo la Maziwa Makuu kwa njia ya mazungumzo badala ya kutegemea mapambano ya silaha peke yake.

Aidha, Katbu Mkuu huyo wa UN ameishukuru Tanzania kwa kuchangia askari wa kuunda Brigedi Maalum ya Kusimamia Amani katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC) na pia kutoa kamanda wa Brigedi hiyo.

Vile vile, Mheshimiwa Ban Ki Moon amemwomba Rais Kikwete kuendelea kuunga mkono jitihada za kuleta amani na utulivu katika DRC na eneo lote la maziwa makuu kupitia Mchakato wa Kanda wa Kusimamia Amani (Regional Oversight Mechanism) katika eneo hilo.

Mheshimiwa Ban Ki Moon ametoa shukrani na pongezi hizo kwa Rais Kikwete wakati viongozi hao walipokutana leo, Jumapili, Juni 2, 2013, kwa mazungumzo wakati wa Mkutano wa Tano wa Tokyo Kuhusu Maendeleo ya Afrika (TICAD V) unaoendelea mjini Yokohama, Japan.

Wakati wa mazungumzo hayo kwenye Hoteli ya Intercontinental ambako viongozi hao wamefikia, Mheshimiwa  Ban Ki Moon amemwambia Rais Kikwete: “Nakushukuru sana Mheshimiwa Rais kwa mchango wako mzuri kwenye mkutano wetu wa Jumapili asubuhi mjini Addis Ababa. Yako yalikuwa mapendekezo bora zaidi na mapya katika mkutano wetu mzuri. Asante sana kwa kuunga mkono Mchakato wa Kanda wa Kusimamia Amani katika eneo la Maziwa Makuu. Tunaomba uendeleaa kuunga mkono Mchakato huu.”

Ameongeza Katibu Mkuu wa UN: “Nilipokuwa Goma karibuni nilikutana na Jenerali kutoka Tanzania ambaye ni Kamanda wa Brigedi Maalum ya Kulinda Amani katika DRC iliyoko chini ya Umoja wa Mataifa. Tunakushukuru sana kwa kuchangia Brigedi hii na tunakushukuru sana kwa kukubali kutoa Kamanda wa Brigedi hii.”
Katibu Mkuu Ban Ki Moon pia amemwalika Rais Kikwete kushiriki katika kikao kijacho cha Mchakato kilichopangwa kufanyika kwenye Umoja wa Mataifa Septemba mwaka huu wakati wa Mkutano wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kwa mwaka huu.

“Nakusudia kuitisha kikao kingine cha Mchakato wetu katika wiki kati ya Septemba 20 na 27, mwaka huu, 2013 wakatiwa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa na napenda kukualika ushiriki katika kikao hiki muhimu sana katika jitihada zetu za kuleta amani katika eneo la Maziwa Makuu na hasa katika Congo,” Mheshimiwa Ban Ki Moon amemwambia Rais Kikwete.

Rais Kikwete amemwambia Katibu Mkuu wa UN kuwa anaendelea kuamini kuwa matumizi ya nguvu za kijeshi na askari peke yake hayataweza kuleta amani katika eneo la Maziwa Makuu ikiwamo DRC.“Huu ndio msimamo ambao niliueleza katika mkutano ule wa Jumapili iliyopita mjini Addis Ababa hata kama baadhi ya watu hawakufurahishwa sana na msimamo huu.”

Tumekuwa tunajaribu kutumia nguvu kuleta amani katika DRC tokea mwaka 1997 na bado mpaka sasa hatujafanikiwa kuleta amani ya kudumu katika nchi hii jirani – tokea wakati huo tumejaribu kuunga mkono uasi mmoja baada ya mwingine lakini bado tuko pale pale na ndiyo maana naamini kuwa wakati umefika wa kuelekeza nguvu zetu katika mazungumzo ya hatua tatu kama nilivyoelekeza katika mkutano ule wa wiki iliyopita.”

Viongozi hao wawili pia wamejadili hali ilivyo katika Madagascar na maandalizi ya uchaguzi mkuu nchini humo. Aidha, viongozi hao wawili walijadili maendeleo ya kisiasa katika Zimbabwe ambako Katibu Mpya imepitishwa na sasa maandalizi yanafanywa kwa ajili ya uchaguzi mkuu nchini humo.

Rais Kikwete ambaye ni Mwenyekiti wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya Jumuia ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) ametoa ufafanuzi wa ndani kuhusu jitihada ambazo zimekuwa  zinafanywa na Asasi yake kuhusu suala la Madagascar baada ya kuwa ameombwa na Mheshimiwa Ban Ki Moon kuhusu jitihada hizo.

Rais Kikwete amemwambia Mheshimiwa Ban Ki Moon kuwa viongozi wa SADC watakutana mjini Maputo, Mozambique wiki ijayo kujadili matukio ya karibuni katika Madagascar na maendeleo ya kisissa katika Zimbabwe.

Mapema leo, Rais Kikwete amekutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Uchumi, Biashara na Viwanda (METI) wa Japan Mheshimiwa Toshimitsu Motegi.
Katika mkutano huo, Mheshimiwa Motegi ameomba Serikali ya Tanzania kuyasaidia makampuni ya Japan ambayo yanajaribu kuwekeza katika uchumi wa Tanzania. 

Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.

2 Juni, 2013



2 Jun 2013




1 Jun 2013

Tanzanian Foreign Minister Bernard Membe has wondered at Rwanda's strange atitude to over react on a simple advice given in good faith on how to engage  and find amicable solution to negative forces in Eastern DRC, saying it is up to Rwandan Government to accept or turn down the advice...FOR MORE, CLICK HERE
http://www.tanzaniangovernment.blogspot.co.uk/


The Tanzanian Foreign Minister Bernard Membe wondered at Rwandan government strange attitude to overreact on a simple advise given in good faith to the country in full presence of the Rwadan Delegation in Ethiopia saying it is up to them accept or refuse the advise.

The Foreign Minister also stated categorically that the government will not move even an inch to apologize Rwanda since he still believed that engaging the enemies was the best option for Rwanda which he said has failed to to find amicable solution through wars for more than 15engage the rebels in the last 16 years.

Speaking before parliament in Dodoma yesterday, the visibly irked Minister wondered as to why was making lots of politics with a simple advise that a they either dumed to accept or refuse to.

Using the famous quotation used once by the Former Israel Prime Minister, Yizak Rabin Mr Membe said "We negotiate peace with our enemies not our friends" adding that" there is no need for Rwanda to sound an alarm for the advise given in the open table in Ethiopia."
Assah Andrew Mwambene
Po box 9000 Dar es Salaam
Mobile +255782-553737
+255756887880



On 26 May 2013 in Addis Ababa the UN Secretary General, Mr. Ban Ki-moon and the Chairperson of the African Union Commission Dr. Nkosazana Dlamini Zuma, convened the first meeting of the Regional Oversight Mechanism of the Peace, Security and Cooperation Framework for the DRC and Region. It was at this important meeting where the President of the United Republic of Tanzania, H.E. Jakaya Mrisho Kikwete made what many level headed commentators have referred to as candid and commonsensical remarks about the protracted conflicts in the Great Lakes Region. President Kikwete - a seasoned and consummate diplomat who has helped broker many peace deals in Africa - remarked that it was high time Rwanda and Uganda gave serious attention to peace talks with FDLR and ADF rebels respectively. He said, and correctly so, that it was evident the barrel of the gun cannot bring about the ultimate answer as testified by the recurrence of fighting in our region. He never condoned the role that the FDLR rebels played in the 1994 genocide. He was being reasonable and pragmatic. 

Rwanda should know better than any other country that there is no way Tanzania would condone or sympathize with the perpetrators of genocide. To make such insinuations is, quite frankly, a demonstration of breathtaking ignorance about Tanzania’s enviable and unparalleled history - the history of speaking out against any forms of crimes and injustices. Moreover, for Rwanda to make such insinuations is to show just what a short memory span this country has.

Admittedly, genocide brought about painful and unforgettable misery to the people of Rwanda but its spillover effects were felt well beyond its borders. The effects of genocide were felt right inside Tanzania which had to shoulder the burden of providing for thousands of Rwandan refugees. By the way, Tanzania has a long history of taking good care of Rwandan refugees both before and after genocide. The sons and daughters of the Rwandan refugees benefitted from Tanzania’s generous education system by studying, for free, at the country’s Universities and many of them are now occupying high positions in the Government of their motherland.

So given the foregoing, I have to say that I have been taken aback by our neighbors’ over-reaction to what was a completely innocuous statement by President Kikwete. Indeed, what the President said could (and should) have been said by other leaders a long time ago. What he said is a no-brainer!  It is commonsensical!  Negotiations have a much better chance of resulting into durable peace than the use of force. Thus, I find the reactions from Rwanda not only disturbing but also objectionable and utterly impudent! What is even more shocking is the discourteous behavior shown by the Rwanda’s Foreign Minister.  She seems to be getting too much big for her boots as to suggest that President Kikwete’s statement was absurd! She even has the audacity to ask that he should retract it. If anything, I think it is our Foreign Ministry which should summon the Ambassador of Rwanda in Dar es Salaam and ask him to clarify his Minister’s inadvisable utterances.

For far too long now the international community has adopted a softly softly approach with respect to Rwanda and this has meant that this tiny country gets away with literally everything, even murder. Rwanda has become like a spoiled child - untouchable and overly sensitive to everything even the slightest suggestion of censure.  Rwanda has a tendency of not taking kindly any form of criticism whether from within or without. And its leadership comes across as snobbish and delusional. May be the western countries’ plaudits about its so called success story have finally got into the heads of Rwandan leaders so much that they think they know it all.

For Rwanda to say that they cannot engage in talks with FDLR rebels because of their role in 1994 genocide is to allow themselves to be the captives of the past. History is replete with numerous instances of former sworn enemies burying their hatchets and extending an olive branch to one another for the sake of peaceful coexistence and future prosperity. This happened in South Africa where ANC and other progressive movements sat down with the perpetrators of one of the most brutal and inhumane policies in the history of mankind (apartheid) and agreed to work together in an inclusive and democratic society. Similarly, after many decades of committing some of the most heinous crimes against the people of Angola, UNITA is now part of the democratic government of that country. And in 2011, US and its allies initiated direct talks with some elements of the Taliban in Doha (Qatar), if my memory serves me well.
Rwanda should wake up and smell the coffee! Being delusional has not worked and won’t work.  It is now close to 20 yrs since the 1994 genocide and during all that time Rwanda has not been able to achieve its objectives visa vis FDLR rebels through the use of force.  Any sane person in Kigali should see the wisdom of changing the tactic/strategy which is, for all purposes and intents, what our President said in the Statement. Rwanda should understand that by calling for direct talks, Tanzania does not suggest, by any stretch of imagination, that the architects and executors of genocide should go scot free. Not at all! Talks can, and indeed should, offer the mechanism of dealing with known perpetrators of genocide by isolating them from non-perpetrators such as those born after 1994. This is just one example of approaching talks. I am sure there are many others.

But talking of genocide, am I wrong in recalling that even President Kagame himself was once found to be complicit in this crime by a French Magistrate? I recall that Rwanda’s reaction to this finding was, as we have come to expect, fast and furious to the extent of severing its diplomatic relations with France. Again, this goes to show that this “spoiled child” can’t stand any sort of censure or straight talking. I also recall that as recent as last year a UN report revealed that Rwanda’s Kagame had committed or assisted in committing genocide in DRC!

Despite all this compelling evidence, neighbors of Rwanda are still ready to engage that country in talks. Why can’t Rwanda show the same attitude? And lest he forgets, Kagame himself and his RPF henchmen come from a background of rebellion. They were rebels operating from Ugandan forests before taking over power in 1994. However, despite their “rebels” status they were invited and took part in the Arusha peace process of the early 1990s. 

Finally, I have a gut feeling that Rwanda doesn’t want FDLR rebels to go away that’s is why it is vehemently opposing the suggestion of talks which is one sure way of ending this conflict once and for all. This because, the perpetual presence of FDLR rebels in DRC gives Rwanda a convenient excuse to interfere in the DRC’s affairs thereby making the country ungovernable for its own economic and geopolitical interests. I read somewhere that Rwanda’s army – which is one of the biggest for a country of that economy and size - is mainly sustained by the exploitation of DRC’s natural resources. So, Rwanda goes into the DRC on the pretext that it is in hot pursuit of the FDLR rebels but in actual fact what it does is to plunder the resources.

And Rwanda is particularly angry with Tanzania because by being part of MONUSCO in DRC, its misdeeds will be exposed and curtailed by our non-nonsense troops. So the over-reaction to our President’s innocuous statement should not be seen in isolation. It is part of the frustration born out of the uneasy situation which Rwanda finds itself in as a result of our troops being part of the UN/SADC intervention force in DRC.
I submit.
Concerned Citizen




30 May 2013

Magufuli amkana Sitta, asema hana ubia naye urais 2015


Siku chache baada ya Waziri wa Afrika Mashariki Samuel Sitta kumhusisha Dk John Magufuli na kundi la urais la mwaka 2015, Waziri huyo wa Ujenzi, ameibuka na kupinga kauli hiyo, akisisitiza hafikirii kuwania nafasi hiyo.
Waziri Sitta alinukuliwa na gazeti hili juzi akieleza kuwa wakati ukifika, yeye na rafiki zake Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, Waziri wa Ujenzi, Dk Magufuli na Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe, watachagua mmoja wao watakayeona anafaa kuwania urais katika Uchaguzi Mkuu wa 2015. Alisema hayo juzi kwenye Kongamano la Mawasiliano katika Nyanja za Digitali la wanafunzi wa Idara ya Uhusiano na Masoko, Chuo Kikuu cha St. Augustine (SAUT), Mwanza.
Kabla ya hapo alikuwa amewataja rafiki zake hao wakati wa hafla ya kuchangia Kanisa Katoliki, Josephine Bakita, Parokia ya Igoma, Mwanza, Jumapili iliyopita.
Alisema hatagombea tena ubunge mwaka 2015, baada ya kuwa katika ulingo wa siasa kwa miaka 35 na badala yake ataangalia namna nyingine ya kuwatumikia wananchi huku akigusia mchakato wa kuwania urais ambao alieleza anamwachia Mungu.
“Kwa ubunge nimekwishawaeleza inatosha, sitagombea tena kwani miaka 35 inatosha, … lakini hatima yangu ni nini siwezi kujua lakini nina afya nzuri na mmoja wa wanasiasa wakongwe, wenye afya nzuri, mnaona ninavyopendeza... kwa urais namwachia Mungu tutaona,” alisema Sitta.
Kauli ya Magufuli
Akizungumza na gazeti hili nje ya ukumbi wa Bunge jana, Dk Magufuli alisema haelewi msingi wa kauli ya waziri mwenzake huyo, kwani hajui chochote katika mtandao wa urais alioutaja.
Magufuli alisisitiza kusema hana kundi, hakuwahi kuzungumza wala kuhudhuria vikao vya kundi lolote, na kwamba kundi lake ni CCM na Mwenyekiti wake ni Jakaya Kikwete.
“Sina kundi. Sijawahi kuwa na kundi na sitarajii kuwa na kundi lolote. Ninachojua kundi langu ni CCM na kiongozi wake ni mwenyekiti wake, Rais Kikwete,” alisema Dk Magufuli.
Hata hivyo, Dk Magufuli pia alipuuza taarifa kuwa alichangia harambee hiyo akisema, “Si kweli, Mwanza sijatoa hata senti na hata siku ilipofanyika hafla hiyo, nilikuwa Dar es Salaam katika mkutano na makandarasi.” Licha ya kutajwa kuwa miongoni mwa vinara wa urais 2015, Magufuli alieleza kuwa hakuwahi kuzungumza na Sitta suala hilo linalohusu makundi ya urais mwaka 2015.
CHANZO: Mwananchi
WAKATI HAYO YAKITOKEA, JANA PIA ILIKUWA SIKU CHUNGU  KWA SITTA,KAMA INAVYOONYESHA HABARI HII HAPA CHINI
Wassira amvaa Sitta
WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Rais Mahusiano na Uratibu, Stephen Wassira, amemtaka waziri wa ushirikiano wa Afrika Mashariki Samwel Sitta, aweke wazi njia anazotumia kupambana na ufisadi nchini ambazo mawaziri wengine wa serikali ya CCM hawawezi kuzitumia.

Wakati Wassira akitaka ufafanuzi huo, Waziri wa Katiba na Sheria Mathias Chikawe kwa upande wake alikataa kuzungumzia mbinu anazotumia Samwel Sitta kwa kile alichoeleza kuwa hawezi kuongelea masuala ya serikali na mtu asiyemjua.

Wassira na Chikawe walitoa kauli hiyo jana wakati gazeti hili lilipotaka maoni yao juu ya kauli ya Sitta iliyonukuliwa na baadhi ya vyombo vya habari akisema kuwa katika serikali nzima ni mawaziri wanne waliojipambanua kupambana na ufasadi na kutetea wanyonge.

Wassira alisema kwa sasa hawezi kuchangia jambo lolote juu ya kauli hiyo ya Sitta kwa kuwa hajaliona katika vyombo vya habari au kumsikia waziri huyo akisema hadharani.

Alisema kama kauli hiyo imetolewa na Sitta ni vema angefafanua mbinu anazotumia ili wengine waige.
“Mimi siwezi kuzungumzia hayo; mmeyasema nyie pia ingekuwa ni vema kama angeulizwa Sitta mwenyewe na atueleze mbinu zake tuone na wengine wanafanya nini,” alisema Wassira.

Alipoulizwa kama majina yaliyotajwa ni miongoni mwa makundi yanayodaiwa kujipanga ndani ya Chama cha Mapinduzi (CCM), kwa ajili ya urais wa 2015; Wassira alisisitiza jambo hilo aulizwe Sitta.

Kwa upande wake Waziri wa Katiba na Sheria Mathias Chikawe, alipopigiwa simu kwa ajili ya ufafanuzi wa kauli hiyo, alikataa kuzungumzia jambo lolote kwa madai kuwa alishajeruhiwa kwa kutoa habari kwa njia ya simu.

“Sitaki na sizungumzi mambo ya serikali na mtu nisiyemjua tena katika simu…siku moja alinipigia mtu akasema anatoka Daily News nilipompa habari akaandika anavyojua na ikaniletea matatizo, kwanza kwa sasa niko Arusha,” alisema Chikawe na kukata simu.

Juzi wakati Waziri Sitta, akishiriki harambee ya kuchangia ujenzi wa Kanisa la Mtakatifu Joseph katika Parokia ya Igoma jijini Mwanza, aliwataka Watanzania kujihadhari na watu wasio waadilifu katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwaka 2015.

Alisema watuhumiwa wa kashfa ya ufisadi wa kampuni ya kufua umeme ya Richmond na Dowans ni hatari na hawastahili kuungwa mkono katika uongozi.

Alisema kutokana na hali hiyo ya ufisadi yeye pamoja na mawaziri wengine watatu wako pamoja katika fikra za kupambana na vitendo vya kifisadi, uonevu na mikataba tata.

Aliwataja mawaziri hao kuwa ni Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Benard Membe, pamoja na Waziri wa Ujenzi, Dk. John Magufuli.


1 847ab
2 25864
3 a8154
4 03915

5 18a07
6 6e516
7 490c3
8 fc79a
9 6a000
10 34db5
11 7e585
12 86883
13 9c617
14 a7531
15 a5327
16 d6902
 CHANZO: Mjengwa

29 May 2013


Tarehe kama hii, miaka mitano uliyopita,mama mpendwa Adelina Mapango, uliagana nasi. Nikisema 'uliagana nasi' inaweza kutafsiriwa kana kwamba ulipata nafasi ya kutuaga.Nilikuja huko nyumbani kukuuguza Februari 2008, lakini tangu nilipokuona pale Muhimbili hadi tarehe 29 Mei 2008 hukuwahi japo kuniambia neno moja la mwisho.Nakumbuka ulivyokuwa ukiniangalia kwa upendo wako mkubwa,nakumbuka pia tabasamu lako licha ya maumivu makubwa uliyokuwa nayo.Lakini kila nilipojaribu angalau kusikia neno lako moja tu,haikuwezekana hadi siku unafariki.

Mama mpendwa, kabla ya kifo chako sikuwahi kuelewa maana ya kufiwa na mzazi au mtu wa karibu.Sasa sio tu naelewa bali kila siku ya Mungu tangu siku ulipotutoka imekuwa kama ndoto mbaya ambayo natamani iishe ili hali irejee kuwa kama zamani.Kwa bahati mbaya, ndoto hiyo mbaya ni ukweli (hali halisi), na hadi sasa matarajio kuwa kuna siku nitaamka na kukuona au kukusikia ukiwa hai yanazidi kufifia.Kwa kifupi,mama mpendwa,hadi leo bado napata shida kuamini na kukubali kuwa haupo nasi.

Nyakati mbili ngumu zaidi kwangu ni wakati ninapofanya sala kabla ya kulala ambapo wakati wa uhai wako nilikuwa nikisali "Ee Bwana uijalie familia yangu yani Baba na Mama..." lakini sasa inabidi nimtaje Baba pekee.Pia wakati wa uhai wako,nilijenga utaratibu kwamba nikipiga simu naanza kuongea na Baba kisha anapitisha simu kwako tunaanza kutia stori mbalimbali.Sasa,mama,nikimaliza kuongea na Baba huwa najikuta nasahau kuwa haupo hapo nyumbani,na kumwambia Baba akupe simu...then nakumbuka haupo.Naishia kutoa machozi.

Nikiwa mbinafsi,nitaangalia tu jinsi ninavyopata shida kukabiliana na ukweli kuwa hauko nasi.Lakini kuna rafiki yako kipenzi Baba Mzee Chahali ambaye yeye amekuwa mtu tofauti kabisa tangu ulipoondoka.Kama unavyokumbuka,baba ni mtu mkimya,mwenye marafiki wachache, na rafiki yake mkuu ulikuwa wewe.Sasa tangu uondoke,baba amekuwa mnyonge kupita kiasi.Kibaya zaid, ameendelea kudai labda yeye ndio angestahili kutangulia mbele ya haki kwa vile alikuwa amekuzidi kiumri.Kwa hakika, baba ameendelea kuwa katika wakati mgumu sana licha ya sapoti kubwa tunayompatia.

Lakini pia kuna rafiki zako wapenda Kulwa na Doto (Peter na Paul). Pengine kwa vile wao ni last borns, walikuwa wakikuchukulia zaidi ya mzazi, ulikuwa kama bibi yao, shangazi yao, na kikubwa zaidi, rafiki yao.Kila ninapoongea na wadogo zangu hawa najiskia kutokwa na machozi.Kimsingi, sidhani kama waliwahi kuwaza kuwa na maisha bila ya uwepo wako mama.

Familia yote kwa ujumla inakukumbuka sana mama.Nina mkanda wa video niliowarekodi wewe na baba mlipokuwa mnaadhimisha miaka 50 ya ndoa yenu mwaka 2005,lakini kila nikijaribu kuuangalia najikuta nabubujikwa na machozi.Katika mkanda huo uliongea mambo mengi ya msingi kuhusu maisha.Kuna nyakati nataka kuuangalia ili nirejee wosia wako lakini nashindwa kwa sababu ya uchungu.

Mama nilikupenda sana,ninakupenda sana,na nitaendelea kukupenda milele.Kwangu, japo hupo nasi kimwili,lakini unaendelea kuishi nasi kiroho.Nitazidi kukukumbuka kwa sala kila siku,na ninaamini huko uliko unapata faraja kila ninapotenda mambo kwa kuzingatia mafundisho yako.

WE MISS YOU SO MUCH MAMA MPENDWA

PUMZIKO LA MILELE AKUPE EE BWANA NA MWANGA WA MILELE AKUANGAZIE UPUMZIKE KWA AMANI AMINA

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.