14 Sept 2018
21 May 2018
- 21.5.18
- Evarist Chahali
- CIA, Kujisomea, Let's Read, Na Tusome, Reading, Ushushushu
- No comments
Kuna msemo usiopendeza kwamba, ukitaka kumficha kitu Mswahili, basi weka kwenye kitabu. Waswahili wengi wanaogopa maandishi kuliko virusi vya UKIMWI, except maandishi hayo yatakapohusu UBUYU, our nation's favourite.
Sasa, kwa vile lawama hazijengi, nimeamua kuendeleza utaratibu niliouanzisha huko Facebook ambapo mara kwa mara nilikuwa nawapatia watu machapisho mbalimbali BURE. Kwahiyo, angalau mara moja kwa wiki, nitakuwa naweka post yenye link ya kupakua kitabu chenye umuhimu kwako. Series hiyo ya vitabu takriban kila wiki ninaipa jina "Let's Read / Na Tusome."
Leo tunaanza na chapisho hili muhimu kuhusu "ushushushu." Ni mwongozo wa Shirika la Ujasusi la Marekani (CIA) kuhusu "kuzuga watu" (trickery) na hadaa (deception). Baadhi yenu mtakuwa mlishakipakua nilipokiweka mara mbili huko Facebook.
Pakua HAPA
Sambamba na vitabu, from time to time nitajitahidi kubandika makala mpya mara nyingi zaidi ya ilivyo sasa ambapo inaweza kupita mwezi mzima bila kubandika post yoyote ile.Tarajia mada za mbinu za kimaisha (life hacks), usalama wa mtandaoni (cybersecurity), nyeNzo za mtandaoni (internet tools), afya, na kadhalika. Hakikisha unatembelea blogu hii mara kwa mara.
21 Apr 2018
Jana ilitolewa taarifa kwa vyombo vya habari kuwa Rais John Magufuli amemteua "Msalika Robert Makungu kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Tabora." Hata hivyo, kwa makusudi, taarifa haikueleza kabla ya uteuzi huo, Makungu alikuwa na wadhifa gani, japo ilieleza kuwa anakwenda mkoani Tabora kuchukua nafasi ya Dokta Thea Ntara ambaye amestaafu.
"Kilichofichwa" kwenye taarifa hiyo ni ukweli kwamba Makungu alikuwa Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa (DDGIS) ambaye aliteuliwa wakati mmoja na Mkurugenzi Mkuu wa Idara hiyo, Dokta Modestus Kipilimba, Agosti mwaka jana.
Japo taarifa husika haikutumia neno "kutumbuliwa," lakini haihitaji ufahamu wa mfumo wa utawala wa Idara ya Usalama wa Taifa kumaizi kwamba kutoka u-Naibu Mkurugenzi Mkuu wa taasisi hiyo nyeti hadi u-Katibu Tawala wa Mkoa ni kushushwa cheo (demotion).
Kwa mujibu wa vyanzo vyangu vya kuaminika ndani ya taasisi hiyo, kilichopelekea hatua hiyo inayoelezwa kuwa ngumu kwa Magufuli ni tofauti kati ya watendaji hao wakuu wa taasisi hiyo, yaani Makungu na aliyekuwa bosi wake, yaani Kipilimba.
Inaelezwa kuwa tofauti kati yao ilikuwa kubwa kiasi cha Kipilimba kutishia kujiuzulu iwapo Magufuli asingechukua hatua dhidi ya Makungu.
Hata hivyo, Makungu alikuwa "mtu wa Magufuli" kwa sababu ni wote wanatoka Kanda ya Ziwa, na ni miongoni mwa "circle ya karibu ya Magufuli" ambayo pamoja na watu wengine, inayojumuisha Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, Katibu Mkuu wa Hazina Dotto James, na aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani, Charles Kitwanga.
Kwahiyo wakati ingetarajiwa Magufuli "angemkumbatia poti wake Makungu" lakini kwa mujibu wa vyanzo vyangu, umuhimu wa Kipilimba kwa Magufuli ni mkubwa zaidi.
Tukio hilo ambalo halikuvuta hisia za wengi hasa kwa vile lilitokea muda mfupi baada ya kupatikana taarifa za kifo cha mlimbwende maarufu Agnes Masogange aliyefariki jijini Dar jana.
Japo wadhifa wa "Naibu Mkurugenzi wa Usalama wa Taifa" (DDGIS) sio wa muda mrefu tangu uanzishwe (Makungu alikuwa mtu wa pili kushika wadhifa huo baada ya Jack Zoka kuwa wa kwanza), kitendo tu cha Mkurugenzi katika taasisi hiyo kutolewa na kupelekwa mkoani ni cha kushangaza na kinaingia moja kwa moja kwenye kumbukumbu za kihistoria.
Hata hivyo, kabla ya Makungu "kutumbuliwa" tayari kuna Mkurugenzi mwingine ambaye aliondolewa kwenye wadhifa wake kama nilivyoripoti kupitia mtandao wa kijamii wa Twitter
#Tanzania Intelligence agency's Director of External Operations removed from her post. Sources indicate her pro-reform stance didn't sit well with anti-reform elements within the highly secretive organisation— Evarist Chahali (@Chahali) March 14, 2018
Kwa mujibu wa taarifa zilizopatikana wakati huo, kuondoka kwa mwanamama huyo kulichangiwa na mtazamo wake wa kutaka mabadiliko ndani ya taasisi hiyo ambao ulikinzana na wahafidhina wasiotaka mabadiliko yoyote kwa taasisi hiyo.
Wakati hayo yanatokea, Zoka, aliyekuwa Balozi wa Tanzania huko Canada nae alitolewa katika wadhifa huo hivi karibuni. Nilieleza kwa kirefu kuhusu tukio hilo katika makala HII
Kama ambavyo Zoka aliandamwa na lawama kwamba alikuwa akiongoza mkakati wa kuhujumu vyama vya upinzani, Makungu pia ametoka katika nafasi hiyo akikabiliwa na lawama kama hizo.
Kwa upande wangu binafsi kama afisa wa zamani katika taasisi hiyo, wakati fulani nililazimika kumwandikia barua Makungu kutokana na taarifa flani zilzonikera. Na katika barua hiyo nilimkumbusha kuwa cheo ni dhamana, na hakina mwamana.
Tatizo kwa wenzetu wengi wanaposhika madaraka ni ile hali ya kujisahau wakidhani watafia wakiwa kwenye madaraka. Hupuuzia ukweli kuwa ipo siku watatoka katika nafasi zinazowapa jeuri na kujikuta "mtaani." Maisha hayatabiriki, leo unalala ukiwa DDGIS kesho unaamka ukiwa RAS.Huyu Robert nilimtumia barua Mei mwaka jana baada ya kusikia taarifa flani zilizonikera. Nikamweleza kuwa haya madaraka hayana mwamana. Ni vitu vya kupita. Sikujua kama karma was waiting to screw him. He's learning the hard way.— Evarist Chahali (@Chahali) April 20, 2018
Hey Daudi Albert Bashite wanna learn something? pic.twitter.com/ScQhR1doWu
Kuhusu iwapo hatua hiyo ya Magufuli kuwa na atahri zozote, kwa sasa ni mapema mno kubashiri. Baadhi ya maafisa waliopo kazini na wastaafu wa Idara ya Usalama wa Taifa walidokeza kwamba taarifa hiyo ya kuondolewa kwa Makungu imewashtua wengi
#Tanzania spoken to couple of current & ex-TISS guys and they all are shocked. It's exceedingly unprecedented for a DDGIS to be demoted to RAS.— Evarist Chahali (@Chahali) April 20, 2018
Even more confusing is fact Makungu was a Magufuli main chap in TISS, with some regarding him as de-facto DGIS and Kipilimba a proxy pic.twitter.com/HTXMHnth9f
Kwa upande mwingine, wakati yote haya yanatokea, haijafahamika hali ikoje kwa "Idara ya Usalama wa Taifa nje ya Idara ya Usalama wa Taifa," yaani kile kikosi kilicho chini ya Daudi Alabert Bashite.
Kwamba Kipilimba ameweza kumn'goa "poti wa Magufuli" Makungu, basi huenda pia akawezesha kung'oka kwa Bashite, mtu anayeutia doa utawala wa Magufuli kwa kila hali.
Ni muhimu pia kujumuisha tweet ya mtu mmoja ambaye hujitambulisha kama Gavana wa zamani wa Benki Kuu, Daudi Balali.
Baada ya mvutano wa kimadaraka ndani ya Usalama wa Taifa, baadaye idara imegawanyika pande mbili na kudhoofu. Magufuli alielezwa wazi kwamba achague kijana wake (Msalika) aondoke na aadhibiwe au DG Kipilimba ajiuzulu. Kipilimba anaungwa mkono na jeshi na wakongwe idarani.— Daudi T. Balali (@daudibalali) April 20, 2018
Nimalizie makala hii kwa kukushauri uwe ukiitembelea blogu hii mara kwa mara upate fursa adimu ya kusoma uchambuzi exclusive kama huu wa leo.
16 Apr 2018
Africa Confidential Toleo la 28 Machi 2018
27 Machi 2018
Hatua
za kidikteta za Magufuli zinakumbana na upinzani unaoongezeka lakini ndio
Ameshika uelekeo huo na anatishia wanaomkosoa
Katikati
ya muhula wake wa kwanza, Rais John Magufuli anakabiliwa na shinikizo. Huku
akikabiliwa na tishio kubwa kutoka Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema),
vikundi vya kiraia, viongozi wa kanisa, na sasa vijana kwenye mitandao ya
kijamii, anaonekana kufurahia mapambano hayo. Dola pia inatishiwa na makundi
yenye silaha yaliyokuwa viongozi wa serikali na chama mkoani Pwani (MKIRU).
Majibu ya serikali kukabiliana na changamoto hizo yametawaliwa na ukatili ambao
haujawahi kuonekana kamwe, na kupelekea kulaaniwa kutoka kila upande.
Kuongezeka
kwa vurugu za kisiasa, hasa wakati wa uchaguzi mdogo wa jimbo la Kinondoni,
kulipelekea lawama dhidi ya utawala wa mabavu wa Magufuli. Ubalozi wa Marekani
ulitaka kufanyike uchunguzi kuhusu utekaji na mauaji ya kiongozi wa upinzani
jijini Dar es Salaam wakati wa kampeni. Umoja wa Ulaya baadaye ulionyesha
wasiwasi wake kuhusu "mwenendo wa hivi karibuni unaotishia kanuni za
demokrasia" baada ya polisi kutumia risasi katika maandamano ya Chadema
katika mkesha wa siku ya kupiga kura Februari 17, hali iliyopelekea majeruhi
watatu na kuuawa kwa mpita njia.
Wiki
mbili baada ya matamko hayo, Wizara ya Mambo ya Nje ilijibu kwa taarifa yenye
kurasa tatu na nusu ikiyahusisha matukio ya huko MKIRU na "vikundi vya
ndani na nje ya nchi vinavyochukizwa na jitihada za Magufuli kuondoa ufisadi,
biashara ya mihadarati, ujangili, ukwepaji kodi na kujenga uwajibikaji."
Vikundi
hivyo vyenye silaha, ambapo baadhi vinadaiwa kuwa na mahusiano na Al-Shabaab ya
Somalia, vimewauwa viongozi wa Chama Cha Mapinduzi na baadhi ya watendaji wa
serikali. Tatizo hilo lilianza tangu mwaka 2014 lakini likafikia kilele mwaka
2017 baada ya operesheni ya kikatili ya vyombo vya dola kushambulia. Serikali
inajaribu kuushawishi umma kwamba maandamano ya amani dhidi ya haki za kiraia
na mauaji hayo ya MKIRU ni pande mbili za kitu kimoja. Ni watu wachache tu
wanaoshawishika kuamini.
Katika
ujumbe wao kwa msimu wa Kwaresma, maaskofu wa Katoliki walionya kwamba kuendelea
kwa ukandamizaji wa kisiasa kutapelekea migawanyiko itakayohatarisha misingi ya
kitaifa ya umoja na mshikamano. Walieleza kwamba kuzuwia shughuli za kisiasa
sio halali na kunakiuka katiba. Kituo ch Demokrasia (TCD), ambacho huvileta
pamoja vyama vya siasa kilitoa tamko la pamoja na viongozi wa Kikristo na
Kiislamu kudai mapitio ya Katiba. Hii ilifuatiwa na kauli ya kuunga mkono ya
vikundi zaidi ya 100 vya kiraia.
Jumapili
ya Majivu Machi 25 ilishuhudia maaskofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri
Tanzania (ELCT) wakitoa tamko kali wakiilaani utekaji watu, utesaji watu,
upoteaji watu, mashambulizi ya silaha dhidi ya wanasiasa, mauaji yanayotokana
na itikadi za kisiasa, vitisho, kesi za kubambikizwa, na unyanyaswaji wa raia
unaofanywa na vyombo vya dola. Pia walitaka katiba mpya iwepo kabla ya uchaguzi
mkuu wa mwaka 2020. "Taifa huongozwa na katiba ambayo ndio msingi wa
sheria zote", walisema. "Haiongozwi na ilani za vyama."
Pia
kuna changamoto za kisheria. Mahakama Kuu inatarajiwa kusikia kesi mbili za
kikatiba zilizoletwa na watetezi wa haki za binadamu ikiwa ni pamoja na Chama
cha Wanasheria TLS, Umoja wa Watetezi wa Haki za Binadamu (the Tanzania Human
Rights Defenders Coalition), na Taasisi ya sheria na haki za binadamu (the
Legal and Human Rights Centre). Kesi zote zinaongozwa na Fatma Karume wa
kampuni ya uwakili ya IMMA, ambayo ofisi zake zilichomwa moto Agosti mwaka
jana. Akiwa anatoka kwenye familia yenye nguvu ya Karume, amekuwa mwiba kwa
utawala uliopo madarakani. TLS inaongizwa na mmoja wa wateja wake, kiongozi wa
Chadema Tundu Lissu, ambaye bado yupo Ubelgiji anakopata matibabu ya majeraha
ya risasi kufuatia jaribio la kumuuwa.
Kumekuwa
na ukosoaji ndani ya CCM pia. Nape Nnauye, mbunge aliyetimuliwa uwaziri mwaka jana,
ametoa wito wa kuifanyia marekebisho Idara ya Usalama wa Taifa (TISS) akieleza
"kwa macho makavu" kuwa kama ambavyo taasisi hiyo imekuwa ikifanya
kazi kwa manufaa ya dola, pia imekuwa ikiitumikia CCM, inaendeshwa kisiasa.
Mbunge
mwingine wa CCM, Hussein Bashe, ambaye awali hakufahamika kuwa na mtazamo huru,
na aliongoza kampeni ya Waziri Mkuu wa zamani Edward Lowassa kuwania urais,
naye ametokea kuwa mtetezi wa uhuru wa kujieleza na mawazo mbadala.
Haya
na matamko mengine yanaashiria demokrasia ya Tanzania ipo katika kipindi
kigumu. Akiongea kwenye shughuli ya TCD ambayo ilipelekea wito wa katiba mpya,
Askofu Benson Bagonza wa Kanisa la Kilutheri alitanabaisha kuwa kamwe hajawahi
kuona polisi wakitumia risasi dhidi ya waandamanaji. "Nini
kimebadilika?" aliulizwa.
Moja
ya majibu kwa swali lake hilo ni "hakuna kikubwa (kilichobadilika)." Kunapokuwa
na upinzani mkali kwenye chaguzi zilizopita, dola na chama tawala vimekuwa
vikikimbilia kwenye ukatili. Kufanya vema kwa Chadema katika uchaguzi mkuu wa
mwaka 2010 kulipelekea angalau miaka miwili ya ukatili. Ilianza Januari 2011
ambapo polisi walitumia risasi dhidi ya maandamano ya wafuasi wa Chadema
Arusha.
Februari
2012, wanaharakati 16 wa haki za binadamu walikamatwa kwa kuunga mkono mgomo wa
madaktari. Agosti mwaka huohuo, polisi walimuua kwa risasi muuza magazeti huko
Morogoro wakati wa maandamano ya Chadema. Mwezi uliofuata, mwandishi wa habari
Daudi Mwangosi aliuawa na polisi kufuatia kupigwa na bomu la kutoa machozi huku
akiwa amekandamizwa chini na polisi. Katika mwezi huohuo, kiongozi wa
maandamano ya madaktari, Steven Ulimboka alitekwa, akateswa na kuachwa ajifie
mwenyewe kwenye msitu nje ya jiji la Dar es Salaam, tukio linalodhaniwa kufanywa
na maafisa wa TISS. Baadaye mwaka huo huo, na pia Mei 2013, njia za kikatili zilitumika
kukabiliana na maandamano yaliyoambana na wimbi kubwa la machafuko katika
historia ya Tanzania.
CCM
inakabiliwa na changamoto kubwa kudumisha utawala wake. Kwa kutoongelea suala
la ufisadi mkubwa (katika kampeni zake za uchaguzi mkuu wa) mwaka 2015, ilitoa
fursa kwa Chadema kupata mafanikio (ya kuridhisha) katika uchaguzi huo. Wimbo
la ukandamizaji linaloendelea hivi sasa, linailenga Chadema, na pia
linachangiwa na hofu kuhusu vikundi vyenye msimamo mkali vyenye silaha (kama
ilivyokuwa huko MKIRU).
Sintofahaumu
hiyo inaweza kueleza ukatili mkubwa uliotumika kukabiliana na kilichokuwa kikijiri
katika mkoa wa Pwani. Miili kadhaa iliyofungwa kwenye 'viroba' iliyokutwa
inaelea maeneo ya (Msasani) Peninsula jijini Dar es Salaam inaashiria jinsi
hali ilivyokuwa.
Wizara
ya Mambo ya Nje ilitoa tamko masaa tu baada ya tovuti ya African Arguments ya
Royal African Society kuchapisha habari iliyoeleza kuhusu matumizi ya silaha za
moto dhidi ya waandamanaji huko wilayani Rufiji katika ofisi za halmashauri ya
mji.
Kwa
kuunganisha vitendo vya vikundi hivyo vilivyokuwa vinavyotumia silaha (huko
MKIRU) na upinzani dhidi ya mageuzi yanayofanywa na Magufuli, inatoa kisingizio
kwa dola kutumia nguvu dhidi ya makundi yote mawili (vikundi vya MKIRU na
upinzani dhidi ya Magufuli).
Mkuu
wa Majeshi Jenerali Venance Mabeyo aliwataka Watanzania kuwa wazalendo dhidi ya
tishio kwa amani, umoja, uhuru na mshikamano. Kichekesho ni kwamba aliyasema
hayo katika maadhimisho ya viongozi waliopambana na utawala wa mkoloni mwaka
1907 katika Vita ya Maji Maji. Jinsi dola inavyopambana na vurugu na upinzani inarejesha
kumbukumbu za jinsi serikali ya mkoloni ilivyopambana na upinzani dhidi yake.
Mafanikio
yoyote ya kuelezea kuhusu tishio linaloukabili demokrasia nchini Tanzania yatategemea
zaidi makundi mbalimbali ndani ya CCM na tabaka tawala. Wanaoonekana kama
wapinzani ndani ya CCM kama Nape na Bashe watabaki ndani ya chama hicho kwa
gharama yoyote, wakicheza mchezo mrefu wa subira hadi uchaguzi mkuu wa mwaka 2025
ambapo inatarajiwa Magufuli atamaliza muda wake.
Viongozi
wa dini – Magufuli anajitambulisha kama Mkatoliki mcha Mungu – wanaweza kufanikiwa
kumshawishi kupunguza matumizi ya vyombo vya dola dhidi ya upinzani. Lakini
wanaharakati na wanasiasa wa upinzani wanafahamu fika kuwa kudhibitiwa kwa
asilimia 100.
MHALAKI (SOCIALITE) AONGOZA MAPAMBANO KUPITIA MTANDAO
WA KIJAMII WA INSTAGRAM
Mashtaka
yanayofunguliwa na taasisi za kiraia na matamko ya viongozi wa dini ni kitu
kimoja, lakini wito wa kufanyika maandamano unaotolewa na bloga mwenye makazi
yake Los Angeles (Marekani), Mange Kimambi, ni changamoto tofauti kabisa kwa
Magufuli. Kimambi amekuwa sura ya hadharani ya wito wa maandamano ya nchi nzima
tarehe 26 Aprili dhidi ya Magufuli.
Akifahamika
zaidi kwa masuala ya fasheni na habari zinazohusu watu maarufu, akaunti ya Instagram
ya Kimambi imekuwa ikihamasisha na kuyapa umaarufu maandamano hayo,
yanayotarajiwa kufanyika siku ya Muungano, ambayo ni kumbukumbu ya Muungano
kati ya Tanganyika na Zanzibar.
Kimambi
anayedhaniwa kuwa anashirikiana na wanaharakati nchini Tanzania, anachukuliwa
kwa uzito mkubwa na mamlaka za nchi hiyo. Akiongea kwenye tukio moja Machi 9
kijijini kwake Chato, Magufuli alisema "tusubiri na tuone wakiandamana, na
watanitambua." Siku chache kabla, Waziri wa Mambo ya Ndani Mwigulu Nchemba
aliwatuhumu waandaaji wa maandamano hayo kuwa wanapanga kuuwa watu na kisha
kuvitupia lawama vyombo vya dola. Maonyo mengine yametolewa na angalau makamanda
wa polisi wa mikoa saba. Inafahamika kuwa viongozi wa serikali na chama
(tawala) wameelekezwa kuhamasisha upinzani dhidi ya maandamano hayo na tayari
watu kadhaa wameshakamatwa.
Kimambi
ni mwanaharakati ambaye haingekuwa rahisi zamani kumtarajia. Alipata umaarufu
mwaka 2009 kupitia blogu yake ya 'U-Turn' ambayo ilikuwa ikisimulia kuhusu
maisha yake kama mhalaki huko Dubai. Baadaye alihamia katika makazi yake ya
sasa, Los Angeles, kabla ya kuanza kuiteka Instagram mwaka 2015, ambapo alimpigia
Magufuli kampeni yenye ufanisi, licha ya yeye kushindwa kuteuliwa kugombea
ubunge jimbo la Kinondoni.
Alimgeuka
Magufuli takriban Mei 2016 ambapo alipinga vikali kusitishwa kwa matangazo ya
moja kwa moja ya vikao vya bunge. Anachanganya upinzani wa kisiasa na nguvu yake
kama mhalaki anayeweza kumjenga au kumbomoa mtu kwa kutumia mitandao ya
kijamii. Awali ilikuwa kuhusu picha zake binafsi na "selfies" lakini
baadaye mabadiliko yakajitokeza. Kufikia mwishoni mwa mwaka 2016, akaunti yake
ikawa sehemu kuu ya harakati za mtandaoni za upinzani dhidi ya serikali, na sehemu
ya kuona nyaraka mbalimbali zilizovuja.
Akaunti
yake imechukua nafasi ya Jamii Forums, jukwaa la maoni mtandaoni lililokuwa
kitovu cha upinzani mtandaoni, na ambalo waanzilishi wake wanakabiliwa na kesi
mahakamani na wamekuwa wakisumbuliwa na mamlaka kwa muda mrefu.
Huku
akiwa na wafuasi zaidi ya milioni 1.4* kwenye Instagram, uwezo wa Kimambi
kuwafikia watu unawazidi wanasiasa wote wa Tanzania, japo kuna shaka kuhusu
maandamano ya April 26. Kujitokeza kwa watu wengi kwenye maandamano hayo
kutategemea uwezo wa waandaaji wake wa maandamano hayo nchini Tanzania, ambao wanaokabiliana
na utawala usio na huruma – polisi watamwaga risasi kwa ajili ya kuuwa, kama ambavyo
wamefanya huko nyuma.
Haitojalisha
hata kama hakuna mtu atayejitokeza kuandamana Aprili 26. Kutoka umbali wa
kilomita 26,000, Kimambi tayari ameweza kufanya zaidi ya kutikisa mkia wa chui
kwa kutumia simu ya mkononi tu. Na laiti ikitokea asalimisha yeye mwenyewe, mara
moja kukamatwa kwake kutakuwa tukio kubwa kabisa litakaloiweka Tanzania kwenye
macho na masikio ya dunia nzima.
MAELEZO
YANGU: Makala hii ni tafsiri ya neno kwa neno ya makala ya gazeti maarufu la duniani
la habari za kuchunguza kuhusu bara la Afrika la AFRICA CONFIDENTIAL Toleo laMachi 28, 2018 lililokuwa na kichwa cha habari "Enemies Without And Within."
Nimejitahidi
kadri nilivyoweza kufanya tafsiri ya karibu kabisa kutoka Kiingereza kwenda
Kiswahili. Ni vigumu kufanya tafsiri timilifu kwa asilimia 100 hasa pale
mwandishi na mtafsiri ni watu wanaoongea lugha mbili tofauti. Ni rahisi kwa mtu
aliyeandika mwenyewe kufanya tafsiri ya alichoandika kuliko kazi hiyo kufanywa
na mtu mwingine.
*
Idadi ya "followers" kwenye akaunti ya Mange kwa sasa ni watu milioni
1.8.
27 Feb 2018
Nianze
makala hii kwa kuwashukuru ndugu nyote mlionitumia salamu za upendo,kunipa pole/kunipa
moyo baada ya jina langu kutajwa miongoni mwa watu 9 wanaodaiwa kuwa hatari kwa
usalama wa Tanzania.
Orodha
hiyo ilitajwa na mtu mmoja anayejiita Cyprian Musiba japo taarifa nilizonazo ni
kwamba jina hilo lina walakini kama lilivyo jina la rafiki yake – na miongoni
mwa watu waliofanikisha press conference yake – Daudi Albert Bashite. Waingereza
wanasema "birds of a feather flock
together."
Kichekesho
ni kwamba mara ya kwanza kumfahamu mtu huyo ni wakati flani aliponitumia ujumbe
kwenye mtandao wa kijamii wa Twitter akinifahamisha kuwa wana gazeti lao
linaitwa 'Tanzanite' na kuniomba niwe nawatumia makala. Nilipuuza ombi hilo kwa
sababu kutoka level ya kuandikia gazeti kubwa kama Raia Mwema kwenda kuandikia
kijigazeti kipya kama hicho cha Tanzanite ingekuwa kujishushia heshima yangu.
Kwa
upande mmoja,tuhuma za huyo mtu hazijanishangaza kwa sababu kadhaa. Kwanza,
tunafahamu fika ugumu wa maisha huko nyumbani, na sio suala la ajabu kuona
baadhi ya watu wakiuza utu wao ili mradi tu "njia ya kwenda msalani isiote
nyasi."
Lakini
pili, kuna jitihada kubwa za kuigeuza Tanzania kuwa kama wilaya ya Kanda ya
Ziwa. Huyo mtoa tuhuma ana asili ya maeneo hayo, na kuna hali inayozidi kuota mizizi
kwa baadhi ya wahuni wanaotoka eneo moja na Magufuli kujiona wana hatimiliki ya
Tanzania yetu.
Jingine
ambalo lilinifanya nipuuze hizo tuhuma za huyo bwege ni ukweli kwamba safari
yangu kimaisha hadi hapa nilipo imepshapitia vilima na mabonde. Nimeshaeleza
mara kadhaa kuhusu janga lililonisibu Februari 2, 2013 ambapo chombo kimoja cha
usalama hapa kilinifahamisha kuwa kuna tishio dhidi ya uhai wangu, tishio from
Tanzania. Na kwa zaidi ya mwaka mzima tangu wakati huo, nikawa ninaishi maisha
ya kutambua kuwa muda wowote ule naweza kudhurika. Licha ya ugumu mkubwa, hali
hiyo ilinipa uzoefu wa kuishi na vitisho.
Lakini
pia, hiyo hatua tu ya huyo mzembe kunituhumu naona kama tusi flani kwangu. Mie
sio wa kutuhumiwa na mtu asiyejulikana kama yeye. Ilipaswa labda awe kigogo
flani wa Usalama wa Taifa, ndo ningeweza kuchukulia suala hilo seriously.
Wanasema "usiongee na mbwa bali ongea na mwenye mbwa."
Hata
hivyo, japo sikushangazwa na tukio hilo la kihuni, nilikerwa na vitu vikuu
vitatu. Kwanza, wakati nina uhakika wa asilimia 100 kuwa huyo bwege ametumwa tu,
nilikerwa mno na uongo wa mchana kweupe uliokuwemo kwenye tuhuma zake. Uongo
huo ni pamoja na kudai kuwa FBI ni shirika la ujasusi la Marekani. Hivi hao
wapuuzi waliomtuma hawakufanya research japo kidogo ya kuwaelewesha kuwa
shirika la ujasusi la Marekani ni CIA na sio FBI?
Halafu
huyo bwege akachapia tena kwa kudai kuwa chama cha Kansela Angela Markel ni CDP
ilhali chama chake ni CDU. Halafu sijui ni mie tu na "macho yangu ya
kishushushu" niliyeona huyo jamaa akiongea kwa kuhema kana kwamba
anakimbizwa, huku amejawa na uoga mkubwa. Hizi njaa zitakuwa watu mwaka huu.
Seriously!
Kingine
kilichonikera ni jinsi huyo bwege alivyopewa umuhimu mkubwa asiostahili. Hivi
kwa mfano hiyo video ya press conference yake ingepuuzwa, nani angejua kuwa
kuwa mwendawazimu flani kuitisha press conference kutuhumu watu kadhaa wenye
heshima zao katika jamii? Kuna nyakati ukimya una nguvu zaidi ya kupigiana
kelele na mtu. So far, huyo mhuni amefanikiwa kufikisha ujumbe wake kwa watu
wengi mno kutokana na sie wenyewe – including tuliotuhumiwa -kumsaidia
kusambaza ujumbe wake muflis. Anyway, by muda huu hizo 15 minutes of fame
zimeshaisha muda wake.
Lakini
pia nilikerwa na ukweli kwamba uhuni wa aina hii ukiachwa tu bila kuchuliwa
hatua unaweza kusababisha madhara makubwa huko mbele. Maana tumeshaona jinsi Bashite
alivyoweza kuvamia studio za Clouds kisha Rais Magufuli bila aibu akamtetea
hadharani na kumsifia kuwa ni mchapakazi. Kwa kifupi, huko ni kusherehesha
uhuni.
Sasa
huyu bwege si mara ya kwanza kuibuka na press conference za kiendawazimu.Last
time aliitisha press conference na kutishia kumfungulia mashtaka shujaa Tundu
Lissu. Katika tukio hilo nilikerwa zaidi na ukweli kwamba kuna viumbe wenye
roho mbaya kama wachawi, ambao hawajatosheka na mateso aliyepitia Lissu baada
ya karibio la kutaka kumuuwa. Mie nimesoma"War Studies" na miongoni
mwa kanuni za vita ni kwamba pindi adui yako akiwa chini basi unatarajiwa kutomdhuru.
Kwahiyo hata kama Lissu ni adui yao, basi angalau wangesubiri apone kwanza
kabla ya kuanza kumwandama namna hiyo
Kwa
taarifa nilizonazo, press conference ya huyo bwege inamhusisha Bashite ambaye
bila shaka ana baraka za baba yake, lakini pia watu wa Kitengo nao wamehusika.
Ni vigumu kujua "kitengo kipi" maana kwa sasa ni kama tuna "Idara
mbili" – hiyo tunayoifahamu na hiyo "kampuni binafsi ya ulinzi wa
JPM/Bashite."
So who is this man Cyprian Musiba?— Evarist Chahali (@Chahali) February 26, 2018
Surely someone was behind his press conference: Is it @MagufuliJP? Bashite or TISS?
I'll have answers soon
| Je mtu huyu Cyprian Musiba ni nani? Kwa hakika ametumwa: Je ametumwa na Magufuli? DAB au Kitengo?
Nitakuwa na majibu karibuni pic.twitter.com/WFsQSi4u0I
Lakini
kubwa zaidi, na hasa ndio lengo la makala hii ni kuwafahamisha Watanzania
wenzangu kwamba tafsiri halisi ya tuhuma zilizotolewa kwenye hiyo press
conference ni kuwafanya ninyi Watanzania hamna akili ya kuweza kubaini nani
hasa ni tishio kwa usalama wa taifa lenu.
Twende
hatua kwa hatua japo kwa umbali mfupi tu.Hivi katika ya hao watu tisa ni yupi
alishiriki kupanga na kutekeleza shambulio la kinyama dhidi ya Lissu? Kibaya
zaidi, Lissu nae yumo katika orodha hiyo.
Je
ni yui kati ya hao tisa alitoa ruhusa kwa askari kumpiga risasi na kumuuwa
binti asiye na hatia Akwilina? Je ni nani kati yetu aliyehusika na mauaji wa
Katibu wa Chadema Kata ya Hananasifu marehemu Daniel na Diwani wa Kata ya Namwawala
Marehemu Luena? Maana kwa matukio haya matatu tu, na pengine la nne ni la
Lissu, inatosha kuonyesha kuwa kuna pattern ya mauaji dhidi ya raia wasio na
hatia. Na kwa vile hakuna jitihada zozote za vyombo vya dola kuwasaka wahusika
na kuwatia nguvuni, yayumkinika kuhisi ushiriki wa serikali ya Magufuli katika
matukio yote hayo.
Sasa
yule bwege kuwaona ninyi Watanzania hamnazo, kwamba "anamudu kuwalisha matango
pori" kwa kudai kuwa huyo na huyu ndiyo tishio kwa usalama wa nchi yetu,
ilhali kila mwenye akili timamu anafahamu bayana kuwa tishio kubwa zaidi kwa
sasa linatoka kwa WATU WASIOJULIKANA.
Je
sie tisa tuliotajwa ndo tumegeuka kuwa "watu wasiojulikana" ambao
sote wenye akili timamu twatambua ndio tishio kwa usalama wa Tanzania?
Ni
rahisi kulitazama suala hilo kama ni uhuni wa huyo mbwa dhidi yetu lakini
kiukweli mbwa huyo kawanyea Watanzania wote wenye akili timamu. Kawafanya hamna
uwezo wa kutofautisha pumba na mchele. Huyu mtu ni adui yenu zaidi ya adui wa
sie aliotutuhumu.
Sasa
je hasira yako dhidi ya mtu huyu na waliomtuma unaionyeshaje? Mie ushauri wangu
ni mwepesi tu: kama una uwezo wa kuwasomea dua mbaya, itakuwa vema. Kama una
utaalamu wa masuala ya asili, basi ni vema pia. Hata ukitukana kimoyomoyo ni
vema pia. Lakini ukipata wasaa wa "kumpa a uso" popote pale – iwe mtandaoni
au mtaani – tafadhali fanya hivyo.
Naamini
kabisa kati ya sie tisa tuliotajwa na huyo bwege, tuna watu walio tayari
kutafuta haki kwa ajili yetu.Na haki si lazima ipatikane mahakamani. Na
mahakama zenyewe hizi zinazoendeshwa kwa rimoti na Magufuli hadi kumfunga Sugu
wala hazina maana. Ombi langu kwenu ni kila aina ya laana dhidi ya mtu huyo, si
kwa sababu labda ana umuhimu flani bali ukweli huo niliyotanabaisha hapo juu
kuwa amewaona ninyi Watanzania kama hamnazo hadi kufikia hatua ya kutuzushia
sie tusio na hatia tuhuma hizo za kuhatarisha usalama ilhali sote tunafahamu
vema akina nani wanaohatarisha usalama wa Tanzania yetu.
Kama
ukinitumia picha wakati unamfanyia kisomo huyo mbwa basi itakuwa vema sana haha
18 Feb 2018
- 18.2.18
- Evarist Chahali
- CCM, CHADEMA, EDWARD LOWASSA, JOHN MAGUFULI, KIKWETE, MAUAJI, MTULIA, SIASA TANZANIA
- No comments
Nianze
makala hii kwa kutoa salamu zangu za pole kwa familia, ndugu, jamaa na marafiki
wa marehemu Daniel John, ambaye hadi alipouawa kinyama alikuwa Katibu wa
Chadema kata ya Hananasifu, na pia kwa familia, ndugu,jamaa na marafiki wa
marehemu Acqulina Akwilin (samahani kama nimekosea jina).
Kwa
mujibu wa maelezo yaliyotolewa na Mwenyekiti wa Chadema Taifa, Freeman Mbowe,
mwili wa marehemu Daniel uliokotwa kwenye ufukwe wa Coco jijini Dar es Salaam
ukiwa na majeraha. Alieleza kuwa awali marehemu alichukuliwa na Land Rover
nyeupe na watu waliohifanya askari polisi, lakini tangu wakati huo Polisi
hawakuwa na taarifa zozote za kiuchunguzi, na hata jitihada za kupatikana mwili
huo zilifanywa na Chadema wenyewe.
DAR: Katibu wa Kata ya Hananasifu(CHADEMA) afariki dunia katika mazingira yenye utata. Mwili wake umekutwa ukiwa na jeraha la Panga kichwani— Jamii Forums (@JamiiForums) February 14, 2018
> Mwenyekiti wa CHADEMA, @freemanmbowetz amelitaka Jeshi la Polisi kufanya uchunguzi | Soma https://t.co/KUeVlyNDlZ#JFLeo pic.twitter.com/KLJ2vstMBL
Kwa upande wa
marehemu Acquilina, kifo chake kilisababishwa na kasumba hatari inayozidi
kuzoeleka kwa watumishi wa vyombo vya dola kufanya mzaha katika matumizi ya
silaha za moto, ambapo katika tukio husika, polisi waliokuwa wakizuwia
maandamano ya wafuasi wa Chadema, walitumia risasi za moto,na moja kati ya
risasi hizo ilipelekea kifo cha binto huyo, ambaye hadi mauti yanamfika alikuwa
mwanafunzi katika Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) akisomea shahada ya
ununuzi na ugavi.
Mwanafunzi afariki baada ya kupigwa risasi Tanzania https://t.co/msRDdKeueE— bbcswahili (@bbcswahili) February 17, 2018
Ni muhimu
kutambua kuwa vifo vyote hivi viwili vingeweza kuepukika laiti utu na ubinadamu
wetu ungewekwa mbele ya chuki za kisiasa. Huhitaji kuwa mjuzi wa uchunguzi wa
mauaji kufahamu kuwa vifo hivyo ni matokeo ya chuki, hujuma, uonevu na kila
aina ya baya dhidi ya chama kikuu cha upinzani, Chadema, kuhusiana na kampeni
za uchaguzi mdogo katika jimbo la Kinondoni, ambalo kama ilivyo kwa jimbo la
Siha, ni "piga ua" kwa CCM ishinde. Yaani chama hicho tawala kilitarajiwa
kutumia kila mbinu kuhakikisha inashinda katika majimbo hayo mawili.
Lakini kabda
sijaingia kwa undani katika mada hii - ambayo lazima nikiri kwamba inanipa
wakati mgumu sana kuiandika kwa sababu nimebanwa na mchanganyiko wa majonzi na
hasira, sambamba na hofu ya kuona taifa langu likisukumwa kuelekea kwenye
upotevu wa amani na mshikamano wetu – naomba kuweka wazi masuala matatu ya
msingi kunihusu mie mwandishi wa mwakala hii.
Kwanza, mimi
licha ya kuwa na makazi nje ya Tanzania kwa takriban miaka 15 sasa bado no Mtanzania.
Utanzania wangu ni haki nilioirithi kutoka kwa wazazi wangu, na itabaki hivyo
milele. Naeleza hili kwa sababu kuwa wabaguzi wanaopenda kutuhukumu Watanzania
tunaoishi huku ughaibuni, na kutaka tuonekane kama Utanzania wetu sio kamili.
Kwa mantiki hiyo, kama Mtanzania, nina kila haki ya kutoa maoni yangu kuhusu
mustakabali wa taifa letu, hususan katika nyakati hizi ambapo kuna dalili za
wanaotaka kulipeleka kubaya taifa letu.
Pili, mwaka 2015
nilishiriki kikamilifu katika kampeni zilizomwingiza madarakani Rais John
Magufuli. Kwa upande mmoja nililazimika kumkampenia Magufuli kwa vile nilikuwa
nina "sababu binafsi" dhidi ya aliyekuwa mpinzani wake mkuu, mgombea
urais wa tiketi ya UKAWA, Edward Lowassa. Wanasema "adui ya adui yako ni
rafiki yako."Kwa upande mwingine, nililipwa kutoa huduma ya ushauri wa
kitaalamu (usadi, yaani consultancy kwa kimombo) hususan kwenye mitandao ya
kijamii. Natanabaisha hili ili asije akakurupuka mtu na kusema "ah
ulishiriki kutupigia kampeni kwa vile tulikupa pesa."
Tatu, huko nyuma
nilikuwa mtumishi wa Idara ya Usalama wa Taifa. Na kabla ya kuanza utumishi
katika taaluma hiyo muhimu na nyeti, nilikula kiapo kwa nchi yangu, kiapo
ambacho nitaishi nacho hadi ninaingia kaburini. Kiapo hicho sio cha kukitumikia
chama flani au viongozi wake bali Tanzania yetu. Nchi ni muhimu kuliko vyama vya siasa au wanasiasa.
Mtu aliyepikwa
na kuiva kwenye taaluma ya uafisa usalama wa taifa, katika nchi yoyote ile, anapaswa
kubaki kuwa mtiifu kwa nchi yake bila kujali yupo ndani au nje ya ajira ya
taasisi inayohusika na usalama wa taifa wa nchi husika.
Wanasema hata
nje ya ajira rasmi, kila mtu aliyewahi kuwa afisa usalama wa taifa anaendeshwa
na "sense of public duty born in
their previous lives" yaani wajibu kwa umma uliozaliwa katika maisha
yao huko nyuma. Jasusi mmoja mstaafu anaeleza “...I have obligations, professional obligations. If there’s a national
security emergency or possible national security issue, I should report it."
“ ‘You know, I have obligations, professional obligations. If there’s a national security emergency or possible national security issue, I should report it.’ ” ~ Steele— Evarist Chahali (@Chahali) February 8, 2018
Kwahiyo, hata
kama "maafisa wenzangu wa zamani" wataamua kukaa kimya kwa sababu
moja au nyingine – wengi wanahofia usalama wa maisha yao – sie wengine hatuwezi
kukaa kimya, hasa kwa vile baadhi yetu tumeshalipa gharama kubwa kwa kelele
zetu. Kukaa kimya ni sawa na kuafiki uhuni unaoendelea ambao ni tishio kwa
usalama wa taifa.
Lakini licha ya
wajibu huo unaotokana na utumishi wetu kwa nchi huko nyuma, Rais Magufuli
amefanikiwa kuvifunga mdomo vyombo vya habari kiasi kwamba haviwezi kusema
lolote kuhusu "mabaya" yake, na amefanikiwa kuvijengea nidhamu ya
uoga vyombo hivyo vya habari kiasi kwamba habari pekee zenye umuhimu kwao ni za
kumtukuza na kumpamba "mungu-mtu" huyo. Kwahiyo na sie tuliopikwa na kuiva kuhusu ujasiri, kujitoa mhanga na kutokuwa waoga tukiufyata na kukaa kimya - ilhali media zetu ndio zishapigwa kufuli - hali itazidi kuwa mbaya.
Rais wa Tanzania John Magufuli ayaonya baadhi ya magazeti nchini humo https://t.co/grUpqa52uq— DW (Kiswahili) (@dw_kiswahili) January 13, 2017
Baada ya kuweka
wazi nafasi yangu, sasa tuangalie kwa kina kinachoendelea huko nyumbani hasa
kuhusiana na uchaguzi mdogo kwenye jimbo la Kinondoni na Siha na kuuawa kwa Daudi
na Acquiline.
Ni muhimu
kutambua kwamba ukandamizaji dhidi ya vyama vya upinzani sio kitu kilichoanza
chini ya utawala wa Magufuli bali hali hiyo imedumu mfululzo tangu kuanzishwa
kwa mfumo wa siasa za vyama vingi mwaka 1992. Labda kilicho tofauti kwa zama
hizi ni "ujasiri" wa Magufuli kutoficha chuki yake dhidi ya vyama vya
upinzani. Yaani angalau akina Mwinyi,Mkapa na Kikwete walikuwa "wanauma na
kupuliza." Kwamba angalau walikuwa na "mshipa wa aibu" na
walijitahidi japo kutowaonea Wapinzani waziwazi.
Kwa wanaojua
"yanayojiri nyuma ya pazia" watakwambia kuwa hujuma dhidi ya vyama
vya upinzani ni miongoni mwa vipaumbele vikubwa kwa CCM na serikali zake, na
hiyo imepelekea kujengeka "symbiotic relationship" kati ya chama
hicho tawala na taasisi za dola, ambapo kila mmoja anategemea uhai wa mwenzie.
Lakini kama kuna
kitu kinachokera zaidi kuhusu hujuma dhidi ya demokrasia ni pale CCM na taasisi
zake hasa za dola wanapoweka mbele maslahi yao mbele ya utu na uhai wa
Watanzania. Na hili halijaanza jana au katika kampeni za chaguzi ndogo katika
majimbo ya Kinondoni na Siha.
Uchaguzi mkuu wa
kwanza wa vyama vingi mwaka 1995 ulihusisha matukio mengi tu ambayo kwa
makusudi hayapo kwenye kumbukumbu za wazi (japo yamehifadhiwa mahala flani).
Lakini kama
wanavyosema "amekula asali sasa anachonga mzinga," baada ya hujuma za
kimyakimya za mwaka 1995 kuzaa matunda, CCM na taasisi zake ikanogewa, na
matokeo yake ni kwamba uchaguzi mkuu uliofuata, mwaka 2000 uliweka doa kubwa
kwa historia ya Tanzania yetu ambapo kwa mara ya kwanza nchi yetu ilizalisha
wakimbizi kufuatia unyama uliofanyika huko Zanzibar na kupelekea vifo kadhaa (idadi halisi ya vifo haijawahi kuwekwa hadharani japo "wenyewe"
walisema zaidi ya watu 19 ndio waliokufa kwenye machafuko hayo. Wasichosema pia
ni idadi ya watu waliobakwa, kuteswa na kuwekwa kizuizini.
Kwamba hujuma
hizo za CCM dhidi ya demokrasia zilipelekea vifo na majeruhi ni kitu kibaya
kabisa. Lakini kitu kingine kibaya ni ukweli kwamba hakuna mtu hata mmoja
aliyechukuliwa hata kutokana na unyAma waliofanyiwa Wazanzibari hao.
Kwa namna ya
kipekee, CCM ikawa kama imepewa ruhusa ya kutumia vyombo vyake vya dola kufanya
lolote itakalo ili ifanikishe hujuma zake dhidi ya Wapinzani na demokrasia kwa
ujumla, kisha iibuke na ushindi.
Uchaguzi Mkuu wa
mwaka 2005 ulikuwa na "uchafu kupindukia." Kundi lililofahamika kama "mtandao"
lilijipenyeza katika kila sekta, kuanzia kwenye vyombo vya habari, taasisi za
dola hadi kwenye taasisi za dini. Yayumkinika kabisa kuhitimisha kwamba
yaliyojiri wakati "mtandao unafanya jitihada za kumwingiza mtu wao
Ikulu" ni mabaya zaidi ya haya tunayoshuhudia sasa tangu Magufuli aingie
madarakani.
Kwanini basi
hayo yaliyojiri kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2005 hayajulikani? Jibu ni
kwamba, wakati mbinu iliyotumika mwaka 1995 na 2000 ilitegemea zaidi vyombo vya
dola, uchaguzi wa mwaka 2005 na 2010 ulitegemea zaidi nguvu ya fedha, nyingi
zikiwa fedha haramu. Na sehemu ya fedha hiyo ilitumika "kununua ukimya" wa wanahabari wengi tu.
Lakini si fedha tu bali pia kuna hujuma mbalimbali – nyingine chafu na za kuchefua – zilizotawala safari za ushindi wa chama tawala kwenye chaguzi hizo.
Lakini si fedha tu bali pia kuna hujuma mbalimbali – nyingine chafu na za kuchefua – zilizotawala safari za ushindi wa chama tawala kwenye chaguzi hizo.
Labda tofauti
nyingine kuhusu mwaka 2005 na 2010 ni ukweli kwamba wakati chaguzi hizo
zilihusisha "kikundi binafsi" yaani hicho cha wanamtandao ambacho
hakikuwa taasisi ya serikali au chama.
Lakini muda wote
huo, CCM ilikuwa kama imepwa ruhusa na Watanzania kuendeleza hujuma zake dhidi
ya Wapinzani na demokrasia kwa ujumla. Hakujawahi na utashi miongoni mwa
Watanzania kutaka kukabiliana kwa dhati za uhuni/uhalifu wa kisiasa. Na kwa
bahati mbaya, kwa vile vipaumbele vya Watanzania wengi ni kwenye
"ubuyu" na "kubeti/mkeka" basi habari mbaya ni uwezekano wa
CCM kuendelea kufanya itakavyo kwa muda mrefu sana.
Sio kama kwa
kubashiri kuwa unyanyasaji wa CCM utaendelea muda mrefu sana ninamaanisha kuwa
nimekata tamaa. Hapana. Ninakuwa mkweli tu. Tatizo ni zaidi ya CCM na uhuni
wake. Watanzania wenyewe ni sehemu ya mfumo unaowezesha CCM kufanya uhuni/uhalifu
huo.
Uchaguzi Mkuu wa
mwaka 2015 ulihusisha pia matuki kadhaa yaliyojiri "nyuma ya pazia."
Na ukitaka kufahamu kuwa Tanzania yetu haijawahi kuhangaishwa na mauaji ya
kisiasa – kuanzia yale ya mwaka 2001 huko Zanzibar hadi haya ya Daudi wa Hananasifu
na dada Acquilina – ni kifo cha Mchungaji Christopher Mtikila.
Mchungaji Mtikila afariki kwa ajali ya gari Chalinze mkoani Pwani | Soma http://t.co/xRXAqextLi #RIPMtikila pic.twitter.com/HoNnzkjy3w— FikraPevu (@FikraPevu) October 4, 2015
Kwahiyo, na
ninaandika haya kwa uchungu mkubwa uliochanganyika na hasira, kuuawa kwa Daudi
na Acquilina kutaishia kuwa moja tu ya matuko yaliyowahi kutokea katika
Tanzania yetu. Tutawasikia wanasiasa wetu wa vyama vya upinzani wakiongea kwa
hisia kubwa. Tutashuhudia pia wanafiki wengi tu miongoni mwa wasanii wetu nao
wakijifanya kuguswa na vifo hivyo, lakini wakiwa makini kuepuka kumuudhi
"Bashite na baba yake" au kuitibua CCM. Tutashuhudia pia kundi la
wanafiki hatari ndani ya CCM wakijifanya kuumizwa na mauaji hayo, na kutaka
uchunguzi ufanyike, ilhali nao ni kondoo waliojivika ngozi ya mbwa mwitu.
Cheap politics + unafiki. Mbwa mwitu wanaojivika ngozi ya kondoo. Inapofika wakati wa kujitoa mhanga kwa minajili ya kuondoa mfumo kandamizi, hawa wanafiki huonyesha rangi yao halisi na kujivika ukada. https://t.co/39aZHTpFQt— Evarist Chahali (@Chahali) February 17, 2018
Bora tu JPM au Polepole ambao wapo honest kuhusu chuki zao kwa Upinzani/Wapinzani kuliko wanafiki "wanaouma na kupuliza." Bora maadui milioni kuliko "rafiki" mmoja mnafiki https://t.co/39aZHTpFQt— Evarist Chahali (@Chahali) February 17, 2018
Kama ambavyo
"mauaji mengine ya kisiasa" yalivyoruhusiwa kupita kimyakimya, ndivyo
unyama huu uliofanywa dhidi ya Daudi na Acquilina utakavyoruhusiwa uishe
kimyakimya.
Kwa upande mmoja
tusitarajie Rais Magufuli awajibike – sio kwa yeye binafsi kujiuzulu kwa sababu
hilo litakuwa kutarajia zaidi ya muujiza – kwa kumtimua Waziri husika na watendaji
katika jeshi la polisi. Kwa upande mwingine, hakuna wa kumshinikiza Rais
Magufuli achukue hatua stahili dhidi ya wahusika.
Na nisingependa
kuuma maneno hapa. Yeye Magufuli mwenyewe ni chanzo muhimu cha siasa hizi za
uhasama zinazoendelea kuitafuna Tanzania yetu. Huyu ni mtu ambaye wala hapati
shida kuonyesha chuki zake za waziwazi dhidi ya Wapinzani, Upinzani na
demokrasia kwa ujumla.
Tufike mahala tuambiane ukweli: @MagufuliJP anaipeleka Tanzania kusikostahili. And that is too bad. But what's even worse ni kwamba asilimia kubwa ya Watanzania wanasubiri miujiza, kwamba siku moja huyu bwana atabadilika. He won't. Worse is yet to come (God forbid)#MarkThisTweet pic.twitter.com/Uy3VnkOKOH— Evarist Chahali (@Chahali) February 17, 2018
Kama ilivyo kwa
madikteta wengine duniani, Magufuli amefanikiwa kwa kiasi kikubwa kutumia
ajenda yake ya ufisadi kama kisingizio cha kusigina haki za binadamu nchini
Tanzania, na kubinya kila fursa ya haki za kidemokrasia na uhuru wa habari. Kama
nilivyoeleza awali, amefanikiwa kuviziba midomo vyombo vya habari na ndio maana
hata habari za kusikitisha kuhusu mauaji ya Daudi na Acquiline hazijaripotiwa
vya kutosha.
Kwa kuviziba
midomo vyombo vya habari Magufuli amefanikiwa kuzuwia "habari asizozipenda"
na ndio maana hadi muda huu ni Watanzania wachache tu wanaofahamu kilichojiri
huko MKIRU katika kilichoitwa "operesheni dhidi ya ugaidi." Kuna siku
yaliyojiri huko – na ambayo yamechangia "kupotea" kwa mwandishi wa
gazeti la Mwananchi Azory Gwanda – yatajulikana hadharani. Haijalishi itachukua
miaka mingapi.
Baraza la Habari Tanzania (MCT) limesema mwandishi wa Mwananchi aliyetekwa, Azory Gwanda alikuwa anafuatilia taarifa za mauaji ya chini kwa chini yaliyokuwa yanaendelea Kibiti— Jamii Forums (@JamiiForums) December 9, 2017
> Wanadhani mazingira haya ndio yatakuwa yamepelekea usalama wake kuwa hatarini#JFLeo pic.twitter.com/HPsQzmc3XI
Lakini
"yaliyojiri MKIRU" ni uthibitisho mwingine wa hicho nilichoeleza hapo
juu kuwa Watanzania wenyewe ndio wanaopaswa kubeba lawama nyingi katika kasumba
ya CCM kutojali uhai katika harakati zake za kukandamiza demokrasia. Kwamba
kama yaliyojiri MKIRU yameachwa yaishe kienyeji, kwanini tutegemee hali tofauti
kwa vifo vya Daudi na Acquiline?
Kama ndugu zetu
wa Chadema (na kila mpenda haki) "wamekubali yaishe" kuhusu kifo cha
Kamanda Mashaka, "kupotea" kwa kada Ben Saanane (hata zile kampeni za
#BringBackBenAlive zimejifia kifo cha asili), na hawasumbuliwi na serikali ya
Magufuli kupuuzia jaribio la mauaji dhidi ya Tundu Lissu, kwanini tutarajie
jipya katika mauaji yaliyofanywa dhidi ya Daudi na Acquiline?
Yaani Mnadhimu
Mkuu wa upinzani anamwagiwa risasi hadharani wakati mkutano wa bunge unaendelea
huko Dodoma, na tunaambiwa kuwa tukio hilo lilitokea katika eneo lenye ulinzi
mkubwa na lenye CCTV, kwanini basi wanaosumbuliwa na tukio hilo wasitafute njia
stahili za japo kuifanya serikali ione aibu na kufanya japo "uchunguzi wa
kizushi"?
Kuhusu hujuma
"za kawaida" za uchaguzi, kama kila aina ya uhuni uliofanywa na CCM
kwenye chaguzi ndogo za madiwani katika kata 43 uliofanyika Novemba mwaka jana uliruhusiwa
upite "kimya kimya" – kwa maana kwamba hakuna hatua zozote zilizochukuliwa
dhidi ya uhuni huo – kwanini basi chaguzi hizi ndogo katika jimbo la Siha na
Kinondoni zilitarajiwa kuwa tofauti?
Na katika hili,
inapaswa wana-Chadema wajiulize kuhusu busara za viongozi wao kuamua kushiriki
katika chaguzi hizo ndogo Siha na Kinondoni ilhali mazingira yaliyokuwepo yalikuwa
yaleyale yaliyopelekea chama hicho kususia chaguzi nyingine ndogo tatu katika
majimbo ya Longido, Singida Kaskazini na Songea Mjini uliofanyika mwezi
uliopita.
Hadi wakati
ninaandika makala hii, tayari Tume ya Uachaguzi ilikuwa imeshamtangaza mgombea
wa CCM jimbo la Siha, Godwin Mollel kuwa mshindi kwa tofauti kubwa tu ya kura dhidi
ya mgombea wa Chadema. Hata kama CCM wameiba kura, ukubwa wa tofauti kati ya
kura za mgombea wao na huyo wa Chadema zinaashiria kuwa chama hicho kikuu cha
upinzani kilipitisha mgombea fyongo.
Mgombea wa CCM, Dk Godwin Mollel ametangazwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuwa mshindi wa Ubunge Jimbo la Siha baada ya kupata kura 25,611 dhidi ya mpinzani wake, Elvis Mosi wa CHADEMA aliyepata kura 5,905 - Mwananchi pic.twitter.com/hG6oT9GUpZ— Kwanza TV (@kwanza_tv) February 18, 2018
Na kama
ilivyotarajiwa mgombea wa CCM jimbo la Kinondoni, Maulid Mtulia, naye ametangazwa mshindi.
Mie mtumishi wako nilishabashiri mapema tu kuwa chama hicho tawala kingeshinda majimbo hayo, "iwe isiwe."
Breaking news: Aliyekuwa Mgombea Ubunge kwa ticket ya CCM, Maulid Mtulia ametangazwa kuibuka mshindi katika uchaguzi mdogo wa marudio wa Jimbo la Kinondoni.— millardayo (@millardayo_) February 18, 2018
Mtulia amepata kura 30,313 dhidi ya mpinzani wake Salum Mwalim (CHADEMA) aliyepata kura 12,353#MillardAyoUPDATES pic.twitter.com/rYsb0Jgbie
Mie mtumishi wako nilishabashiri mapema tu kuwa chama hicho tawala kingeshinda majimbo hayo, "iwe isiwe."
Ushindi kwa
wagombea hao wa CCM ulipaswa kupatikana kwa gharama yoyote kwa sababu laiti wangeshindwa,
kinachoelezwa kama "mkakati wa Magufuli kuua upinzani kwa kununua wabunge na
madiwani wa Upinzani" kingemfanya
achekwe hata huko kwenye chama chake.
Na kwa vile hadi
sasa wabunge na madiwani waliohama upinzani na kujiunga na CCM wamefanikiwa
kurudi madarakani baada ya chama hicho tawala kuwapa fursa ya kuwa wagombea
wake kwenye chaguzi ndogo, na kuwasaidia kwa hali na mali washinde, tutarajie
wabunge na madiwani wengin zaidi kuhama vyama vya upinzani na kujiunga na CCM.
Kisa? "Dili hilo linalipa," kwa CCM na kwa wanasiasa hao wanaohama.
Na unadhani
mbunge au diwani "mwenye moyo mwepesi" akiona jinsi chama chake "kilivyochukulia
poa" yaliyowasibu akina marehemu Mashaka na Daudi, na yaliyowasibu Ben
Saanane na Lissu, kwanini iwe ngumu kwake kushawishika kuhama?
Ningetamani sana
kuhitimisha makala hii kwa kushauri nini kifanyike lakini itakuwa kupoteza muda
wangu na muda wako msomaji. Ni vigumu mno kuwashauri watu waliokubali kwamba
mgao wa umeme ni stahili yao kwa zaidi ya miaka kumi sasa, na ambao kila mara
umeme unaporudi wanashangilia kana kwamba wamepewa upendeleo flani.
Kama Watanzania
wameshindwa kuilazimisha Tanesko iache mgao wa umeme, wataweza kweli
kuilazimisha CCM iache hujuma dhidi ya vyama vya upinzani na demokrasia kwa
ujumla? Ndio maana bila utu wala aibu, chama hicho tawala kinapata ujasiri wa kukifanyia mzaha kifo cha Acquiline ambapo kwa kudai polisi (haohao waliomuua binti huyo) wachukue hatua dhidi ya Mbowe. Utterly disgusting!
Na kama mauaji mbalimbali ya kisiasa huko nyuma yameachwa yapite na kusahaulika, kwanini tutarajie miujiza kwenye mauaji haya ya sasa dhidi ya wapendwa wetu Daudi na Acquline?
@ccm_tanzania This is too low. Kwanini msitumie akili badala ya makalio kutambua mnachofanyia mzaha huu ni uhai wa Mtanzania uliokatishwa kinyama na polisi haohao mnaowapa kinga kwa kumsingizia @freemanmbowetz? Hamna utu wala mshipa wa aibu? Mungu awalaani kwa hili— Evarist Chahali (@Chahali) February 18, 2018
cc @MagufuliJP pic.twitter.com/7lgzKh0ofe
Na kama mauaji mbalimbali ya kisiasa huko nyuma yameachwa yapite na kusahaulika, kwanini tutarajie miujiza kwenye mauaji haya ya sasa dhidi ya wapendwa wetu Daudi na Acquline?
Na ukweli
mchungu ni kwamba Magufuli ataendelea kuwapelekesha Watanzania atakavyo ka
sababu si watangulizi wake -Mwinyi, Mkapa na Kikwete – wenye jeuri ya kumwambia
"Ee bwana ee, huku unakoipeleka nchi siko." Hawawezi kwa sababu nao
ni kama "mateka." Madhambi waliyofanya kwenye tawala zao yanawafanya
wahofie hatma yao pindi wakimkosoa "mungu-mtu" aliyepo madarakani.
Na wakati
wastaafu au watumishi wa zamani wa Idara za Usalama wa Taifa kwenye nchi kama
Marekani wamekuwa mstari wa mbele kukemea kila tendo linalotishia usalama wa
nchi hiyo – kwa mfano 'ndoa' kati ya Rais Donald Trump na Russia – wastaafu wetu
sie hawana jeuri ya kufungua mdomo sio tu kwa vile wanahofia kuathiri posho na
marupurupu yao bali kwa vile nao ni mateka wa "madudu" waliyofanya
walipokuwa madarakani. Ukiwa mchafu unajinyima uhuru wa kukemea uchafu.
James Comey mkuu wa zamani wa FBI na John Brennan mkuu wa zamani wa CIA ni miongoni mwa sauti muhimu kuhusu mustakabali wa taifa la Marekani. Wako wapi "akina Comey na Brennan" wetu kuhusu mustakabali wa Tanzania yetu? pic.twitter.com/DSA0mWYZ8A— Evarist Chahali (@Chahali) February 17, 2018
Basi niishie
hapa kwa kurejea tena salamu zangu za pole kwa familia, ndugu, jamaa na
marafiki wa marehemu Daudi na Acquiline. Ni vigumu kuwaambia maneno yanayotosha
kuwaliwaza lakini la muhimu ni kuendelea kuzikumbuka roho za marehemu hao, hasa
katika kipindi hiki cha Kwaresma ambapo sisi Wakristu tunaadhimisha mateso ya
Bwana Yesu Kristo. Pumziko la Milele awape Bwana, na Mwanga wa Milele
awaangazie, wapumzike kwa amani. Amen
Subscribe to:
Posts (Atom)