29 Feb 2008

Hivi ukiwa na glasi yenye maziwa yenye ujazo unaofikia nusu ya glasi hiyo,utasema iko HALF FULL au HALF EMPTY?Au,unapokwenda kazini,shuleni,kwenye mizinguko,nk je unakuwa umetoka NJE ya makazi yako au umetoka NDANI ya makazi yako?Haya ni maswali yanayohusiana na mantiki na maana ya kauli.Nimekuchokoza ili utafakari hoja hii:je vita dhidi ya ugaidi (war on terror) imefanikiwa-hata kama ni kwa kiasi kidogo-huko Mashariki ya Kati na Ghuba au ndio imeifanya dunia kuwa sayari hatari zaidi kwa maisha ya binadamu?

Hebu tuangalie Iraki ya Saddam Hussein na hii ya baada ya uvamizi wa Marekani na washirika wake.Wakati wa utawala wa Saddam,hakukuwa na demokrasia ya aina yeyote ile,kauli ya dikteta huyo ilikuwa na nguvu pengine zaidi ya kauli ya Mungu.Lakini pamoja na hayo,Wairak kwa kiasi kikubwa hawakuwa na hofu ya kuwa kwenye mkusanyiko kwa kuhofia kulipuliwa na suicide bombers,hatukuwahi kusikia jina la mtu aitwaye Muqtada al Sadr,hakukuwa na kitu kiitwacho Al Qaeda in Iraq,huduma za muhimu kama maji,umeme,barabara,nk zilikuwa zikipatikana kwa wingi,utajiri wa mafuta ulisaidia kuifanya nchi kuwa yenye nguvu,na kadhalika na kadhalika.Baada ya uvamizi wa Marekani na washirika wake,demokrasia imepatikana na watu wamepiga kura japo kwa hofu ya suicide bombers na snipers waliotapakaa nchini humo.Hata hivyo,uvamizi huo umezaa "majimbo mapya" ikiwa ni pamoja na lile lililopachikwa jina la "pembetatu ya kifo" (Triangle of Death),umeibua vikundi kama Mehdi Army,uliwavutia watu kama Zarqawi,umekosesha huduma nyingi muhimu kama maji,umeme,barabara na uhaba wa mafuta licha ya nchi hiyo kuwa mzalishaji mkubwa wa mafuta na,kama Obama alivyomjibu McCain-baada ya kutupiwa kijembe kwamba (Obama) ni dhaifu kwa kudai kwamba hakuna Al-Qaeda nchini Irak-hivi sasa kuna kitu kiitwacho Al-Qeada in Iraq.Je Iraki chini ya Saddam ni bora zaidi kuliko hii ya sasa au ni vice versa?Tunarudi kulekule kwenye "mwenye nyumba ametoka ndani au ametoka nje."

Bush na neocons wenzake walikuwa na sababu muhimu za kuivamia Afghanistan baada ya mashambulizi ya Septemba 11,2001.Hakuna wakati ambao kiongozi wa nchi anatakiwa kuonyesha msimamo kama pale linapotokea jambo la kutikisa nchi.Kama utamaduni huu utazingatiwa basi si ajabu kelele za wanaolialia kuwa wameonewa kwenye sakata la Richmond na BoT/EPA zikasikika kutoka Segerea,Keko,Ukonga au hata wakiwa deathrow huko Isanga,japo I doubt).Nadhani kila Mmarekani alisapoti uvamizi dhidi ya Taliban huko Afghanistan hasa kwa kuzingatia usemi "akuanzae mmalize."Lakini kabla mission ya Afghanistan haijazaa matunda yaliyotarajiwa,na Osama bin Laden na mpambe wake Zawahiri wakiendeleza ngebe zao,Bush na neocons wenzake wakaamua kumalizia kiporo cha Joji Bush Mkubwa cha kumng'oa Saddam kwa kisingizio cha WMD.Haya,Saddam aliondoka madarakani na hatimaye kunyongwa lakini Irak imetokea kuwa sumaku ya magaidi kuliko ilivyokuwa kipindi cha dikteta huyo.Pia chuki dhidi ya taifa la Marekani imekua maradufu katika Muslim World.So far,taarifa kutoka Afghanistan zinaonyesha dalili za mission impossible.

Anyway,hiyo ndio siasa:ubabaishaji,udanganyifu,utapeli,uzushi,kuzinguana na lolote lile linaloweza kumfanya mwanafunzi wa siasa kama mie kujiuliza nyakati flani kama hiki nachosoma kina umuhimu wowote.Well,at the end of the day,"kinacho-matter" ni shahada uliyonayo na si shahada kwenye fani gani (in most cases,watu huwa hawaulizi Profesa Othman Haroub,Issa Shivji au Mwandosya ni wahitimu wa fani gani....)In simple words,Politics sucks!



0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.