12 Feb 2009

Ni kweli nimewachapa, mara hii nimewachapwa wakiwa wamefungiwa, wakati mwingine watachapwa hadharani.” Ni kauli ya MKUU wa Wilaya ya Bukoba, Albert Mnali kuthibitisha habari kwamba aliamuru polisi mmoja kuwachapa viboko walimu katika shule tatu za msingi zilizo Bukoba, kutokana na wilaya hiyo kuwa ya mwisho katika matokeo ya darasa la saba. Huu sio udikteta bali DC huyo yaelekea haelewi aliteuliwa kufanya nini wilayani humo.Kwa habari kamili,BONYEZA HAPA

2 comments:

  1. Sina la kusema Kaka. Asante kwako na pole kwao. Ila ninalojiuliza ni ku wa kuna maendeleo gani aliyofanya huko Bukoba? Hivi wakianza kuweka wilaya ya kwanza mpaka ya mwisho ya kwake itakuwa ya ngapi na atachapwa na nani?
    Licha ya kuwa kinyume cha haki, alichofanya huyo mkuu wa wilaya ni udhalilishaji.

    ReplyDelete
  2. Huwa nafika hapa kusoma na kuondoka kimya kimya, leo imebidi niandike maana hiyo habari kwa njia ya picha imefikisha ujumbe asilimia 101% ha ha haa, nimefurahi sana!
    Bado msimamo wangu ni ule ule, kuwachapa walimu haikuwa sahihi. Ipo namna ya kuadhibiana na si kukurupuka tu. DC tayari amefutwa kazi na Raisi.

    ReplyDelete

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.