30 Apr 2009


Spika wa Bunge, Samuel Sitta amesema kuna maazimio mengi ya Bunge ambayo serikali imekuwa inasuasua kuyatekeleza. Kutokana na hali hiyo, amesema katika mkutano ujao wa Bunge wa bajeti, atatekeleza wajibu wake na serikali isije kumlaumu atakapoanza kutekeleza wajibu huo.

Kauli hiyo ya Spika aliitoa kutokana na majibu yaliyotolewa na serikali kupitia Naibu Waziri wa Miundombinu, Hezekiah Chibulunje, alipokuwa akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Vunjo, Aloyce Kimaro (CCM). Mbunge huyo alitaka serikali kuunda kamati huru ambayo itachunguza na kushughulikia waliohusika kuuza nyumba za serikali na kusababisha hasara. Naibu Waziri huyo alisema serikali inatekeleza maazimio ya Bunge ambayo yalitokana na Mbunge huyo kuwasilisha hoja binafsi bungeni....ENDELEA


HII HAIJATULIA.INA MAANA AWALI SPIKA ALIKUWA HATEKELEZI WAJIBU WAKE IPASAVYO NA NDIO MAANA HALAUMIWI AU...?HALAFU HAYA MAMBO YA LAWAMA YANATOKA WAPI WAKATI SPIKA (NA BUNGE) NA SERIKALI HAWAFANYI MAMBO KWA AJILI YAO BINAFSI BALI UMMA WA WATANZANIA?


HIVI BUNGE LETU LIMEGEUKA KUWA MALI YA SPIKA AU SPIKA NI KIONGOZI TU WA BUNGE?MAANA KAMA KUTAKUWA NA LAWAMA (KAMA ANAVYOTAHADHARISHA SPIKA) BASI ZITAELEKEZWA KWA BUNGE NA SIO SPIKA (AMBAYE PIA NI MBUNGE).


OK,TUWEKE HILO KANDO.JE KUNA HAJA YA KUTAHADHARISHANA KWAMBA MSIPOFANYA HIVI MIE NTAFANYA VILE?KWANI HAKUNA UTARATIBU MAALUM WA KUFUATWA PINDI HALI KAMA HIYO ANAYOZUNGUMZIA SPIKA IKITOKEA?


KUBINAFSISHA-IN THE SENSE KWAMBA NIKISEMA INYESHE ITANYESHA OR VICE VERSA- TAASISI KAMA BUNGE NI HATARI.

0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.