16 May 2009


Na Leon Bahati

MAKAMU wa Rais wa Kenya, Kalonzo Musyoka amekiri kuwa mlima Kilimanjaro umekuwa ukiisaidia nchi yake kukuza sekta ya utalii kutokana na Wakenya wengi kuutumia katika kujitangaza hasa wawapo kwenye nchi za ulaya.

Pamoja na kufaidika huko, alisema kuwa hiyo haifuti ukweli kwamba mlima huo mrefu kuliko yote Afrika, upo Tanzania, ingawa pia huweza kuonekana kutokea Kenya.

Musyoka alisema hayo kwenye hafla fupi ya chakula cha mchana alichoandaliwa na mwenyeji wake, Makamu wa Rais wa Tanzania, Dk Ali Mohamed Shein.

“Wakenya wanapoenda Ulaya wanawaambia wazungu: Njooni Kenya ili muone mlima Kilimanjaro,” alisema Musyoka katika ziara hiyo ya kiserikali kwa mwaliko wa Tanzania...
endelea

CHANZO: Mwananchi


WELL,HUWEZI KUWALAUMU IWAPO SIE "WENYE MLIMA HUO" TUNAENDEKEZA ZAIDI POLITIKI KULIKO KUTANGAZA VIVUTIO VYETU.WANAOPEWA DHAMANA YA KUTANGAZA RASLIMALI ZETU WAKO BIZE ZAIDI NA "TENI PASENTI" YA MIKATABA YA MATANGAZO KULIKO UFANISI WA MATANGAZO HAYO.

0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.