11 Aug 2009


Kuna tamasha kubwa la kimataifa linaloendelea jijini Glasgow.Wenyewe wanaliita World Pipe Band Championships.Ni mashindano ya bendi za kupuliza filimbi kama zile za brass band (pipes).Kumejitokeza mgogoro wa kiplomasia baada ya Wakala ya Mipaka ya Uingereza (UK Border Agency) kuwanyima viza wanabendi ya kupuliza filimbi kutoka Pakistan.Licha ya bendi hiyo inayojulikana kama Lahore Piping Band,msafara wa wafanyabiashara kutoka Pakistan nao umenyimwa viza.Kinachochochea zaidi songombingo hilo ni ukweli kwamba Glasgow na Lahore ni miji pacha (twin cities).

0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.