18 Jun 2011




Pinda: SIJUI Waziri Nahodha anaishi hotelini

na Martin Malera, Dodoma

WAZIRI Mkuu, Mizengo Pinda, amesema hajui kama Waziri wa Mambo ya Ndani, Shamsi Vuai Nahodha, anaishi hotelini.

Kauli hiyo aliitoa jana bungeni baada ya kuulizwa swali na mbunge wa Chambani, Salim Hemed Khamis (CUF), alihoji dhamira ya serikali kupunguza matumizi.

Mbunge huyo alihoji kwa nini Waziri Nahodha anakaa hotelini wakati serikali ina nia ya kupunguza matumizi yasiyo ya lazima.

“Kuna mawaziri wanaishi hotelini tangu walipoteuliwa hadi sasa, serikali haioni kama hali hiyo ni kikwazo kwa mafanikio ya Mpango wa Maendeleo wa Miaka Mitano tulioupitisha hivi karibuni Bungenin?” alihoji mbunge huyo.

Akijibu swali hilo, Waziri Mkuu Pinda kwanza alionekana kushangazwa na taarifa hiyo na baadaye alimtaka mbunge huyo ataje majina ya mawaziri anaowajua wanaioshi hotelini hadi sasa tangu walipoteuliwa.

Mbunge huyo alitaja jina la Waziri Nahodha.

Huku akiwa haamini na kumkazia macho Waziri Nahodha, Pinda alijibu kwa kifupi tu: “Basi nimesikia.”

Katika hatua nyingine, Spika Anna Makinda, alimzuia Waziri Mkuu Pinda kujibu maswali ya Mbunge wa Singida Vijijini, Tundu Lisu, na Esther Matiku wote CHADEMA, yaliyohusu mauaji ya raia katika mgodi wa kampuni ya Barrick, Tarime mkoani Mara

CHANZO: Tanzania Daima
Katuni kwa hisani ya Kipanya 

0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.