1 Aug 2011


Familia yenye furaha: Kushoto ni Baba mtoto Jordan (15),akifuatiwa na  mama mtoto Tia (14) na kichanga  Gracie,na nyuma ni babu kijana  Shem (29) na kulia ni bibi kijana  Kelly (30)

Kwa namna ilivyozoeleka,unaposikia "babu" au "bibi" unadhani pasi wasi kuwa mtajwa ni aliyekula chumvi nyingi,na huenda umri wake upo kwenye miaka ya 50 na kuendelea.Na sia ajbu ana mvi lukuki.

Hali si hivyo kwa Shem Davies,kijana mwenye umri wa miaka 29 ambaye wiki hii amekuwa "Babu Kijana Zaidi nchini Uingereza."Davies,ambaye hana kazi (unemployed),amefanikiwa kupata mjukuu baada ya bintiye wa kike aitwaye Tia (umri miaka 14!!) kujifungua mtoto aitwaye Gracie.
Baba na mwana:  Shem na mwanaye Tia na kijukuu Gracie

Kuzaliwa kwa Tia (miaka 14 iliyopita) ni matokeo ya uhusiano wa kimapenzi kati ya Shem na mwandani wake wa zamani aitwaye Kelly John mwenye umri wa miaka 30 sasa.

Kuchanganya madawa zaidi,kijana aliyezaa na Tia (mama mtoto mwenye miaka 14) naye ni serengeri boy wa miaka 15 tu!Kwa jina anaitwa Jordan Williams (pichani chini akiwa na mzazi mwenzie na kichanga chao)

Kwahiyo mjukuu amepatikana kwa mama mwenye miaka 14 na baba mwenye miaka 15,na ana babu wa miaka 29 na bibi wa miaka 30!

Lakini ukiangalia kwenye picha zinazoambatana na habari hii itakuwia vigumu kutambua umri wa wahusika wa Isidingo hii.Tatizo ni kwamba ni vigumu sana kukadiria umri wa hawa "wazungu."

Uingereza ni miongoni mwa nchi zinazoongoza kwa mabinti wanaojifungua kabla ya kutimiza miaka 18.

CHANZO: Daily Mail

0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.