18 Sept 2011

Umoja Wa Bloggers Wa Kitanzania
September 17, 2011

Dear Tanzanian Bloggers,

Do you guys have a union? Why don't you create a Tanzania bloggers union? Haya ni maswali nimekua nikiulizwa na watu mara kwa mara…Kila muda kidogo huwa napokea email inayohusu hili jambo. Nimejitahidi sana kukaa mbali na hii topic lakini kila ninavyofunga macho ndio emails zinazidi kuuliza lini umoja utaanzwisha? Je upo umoja wa watanzania.

Mimi kukaa mbali na hili suala na kuwajibu watu ni kuwa mimi naamini umoja wa kitu chochote unaanzishwa na watu kwa mapenzi yao. Na umoja huo ni lazima uwe na malengo na faida za kuwa mwanachama katika umoja huo. Bila hilo kutakua hakuna maana ya kuwa na umoja au hata ukiwepo hautadumu. Halafu lingine lililokua linanifanya mimi niwe mbali na hii issue ni kuwa mimi sina blog. Ni hivi karibuni tu ndio nimefufua blog yangu ambayo nilikua nayo zamani lakini sikuiendelezaga baada ya kupokea email ya kijana wa miaka 14 akiniambia huwa anafuatilia sana Tanzanian blog awards site na ameona kuwa ninahamasisha sana watu wawe na moyo wa kupenda kuwa na blogs lakini hajaona blog yangu. Hiyo ndio ilikua aha moment yangu. Nikakumbuka ule msemo unaosema “Talk the talk and walk the walk.”.

Anyway baada ya kufikiri sana nimeona kwa vile sasa hivi technology inaweza kuwakutanisha watu kwa urahisi kutoka pande zote za ulimwengu hivyo inaweza kuwa rahisi kwa wale watakaopenda kujiunga kuweza kuwasiliana na kujadili mambo yao kwa urahisi. Na kwa vile kama tunavyofahamu muda sio mrefu Google+ itakua inapatikana kwa kila mtu na itakua inaweza kuwaunganisha watu 10 kwa wakati mmoja hivyo nikafikiria labda kwa kutumia technology hii kuna kitu cha maana kinaweza kufanyika.

Kwa muda huu mfupi nimepata experience kubwa sana kuhusu blogs za watanzania walioko ndani na nje ya Tanzania. Kuna baadhi ya bloggers nimeweza kufahamiana nao katika personal level. Ila baada ya kuongea na wengi ni kuwa sasa hivi nikiwa nasoma blog yeyote ambapo mwandishi wake yupo Tanzania nasoma na kuiangalia tofauti na kama nilivyokua naangalia hapo nyuma. Well, blog yeyote ni lazima kuipa heshima kwa blogger anayeiandika bila kujali yupo wapi lakini baada ya kuongea na bloggers wengi nimegundua mazingira na vitendea kazi wanavyotumia kuili kuweza kufanya blog zao ziwe nzrui ni taabu sana. Blogs nyingi ni nzuri na zina idea nzuir lakini hao bloggers wakiulelezea jinsi wanavyofanya kuweza kupost chochote unakaa chini na kujiuliza WHY and always don't take things for granted.

Hivi mnafahamu kuna bloggers wengine mpaka leo wanatumia internet cafés kumaintain blogs zao. Just imagine mtu anaacha kuingia kwenye internet café ajisomee kwenye net mambo anayotaka anakalia kuweka blog ili mimi na wewe tusome yale anayoyapost. Kuna watu wengine bado wanatumia computers za kazini kublog na watu hao wameniambia kuwa huwa wanawahi kazini mapema ili watumie computer za kazi kabla muda wa kazi haujaanza. Wengine wanaskip lunch breaks zao ili watumie huo muda kublog. Na kuna baadhi wameniambia wao wanaruhusiwa kwenda na nyumbani na laptop za kazini lakini huyo mmoja alinichekesha…It is not a a laughable issue lakini alisema laptop battery charge yake ni ndogo sana sometimes akiwa kwenye daladala anatumia kidogo by the time akifika nyumbani battery imeisha na nyumbani hakuna umeme. Hivyo anakua yupo na laptop lakini hawezi kufanya chochote nayo.

Yaani kuna mambo mengi sana ambayo nimekaa nikajiuliza how can we help? Ndio nikasema once tukishajua watu wangapi wanapenda au watajiunga then agenda inayofuata ni kuweka fundraising. Siku hizi kuna online fundraising sites nyingi tu ambazo huwa tunaweza kuanzisha na zinaonyesha how much watu wamecontribute na baada ya hapo…Kuna off lease laptop very reasonable price zinaweza kupatikana na kusaidia bloggers wa kitanzania who are really in need. Kuna mambo mengi sana kama sio hawa bloggers wa kawaida kuweka wengine wetu wala tusingeweza kuona wala kufahamu. Sasa what is our appreciation? Kama tusipotafuta njia ya kusaidiana nani atakuja kutusaidia? Hata tukiweza kukusanya na kununua moja ni better than nothing. Ni bora kulikokukaa tu na kusema kila mtu atajisaidia mwenyewe.

That is why I am presenting this to you guys …Email me for any suggestions and how we can do and then we will start from there….

Mimi nilichokua nafikiria kwa kuanza kila bara atokee mtu mmoja takayependa kuwa mwenyekiti wa bloggers walioko huko..Hao watu watawasiliana ana kuchagua mwenzyekiti wa wate..Na kama watu watakua wengi basi kuwe na msaidizi na katibu katika kila bara..Kama ni wachache basi itajulikana baadaye jinsi ya kufanya. I don't think kutahitajika cashier mpaka huko mbele kukishaundwa kitu cha maana. Na nadahani itakua fair hao viongozi wawe at least wamekua na blog kwa zaidi ya miaka miwili.

Mimi nipo willing to organise and help to put together this baada ya hapo nitawaachia wanaochagulia na kubakia as a just mwanachama. Hivyo nimeweka hiyo form hapo ili nione ni watu wanagapi wanataka kujiunga. Kwa sababau hatakwenye hii newsletter kuna mambo naona hayanihusu mimi kuyatuma na hayo mambo yangekua vizuri yakitumwa kwa bloggers kma wangekua na umoja.

Na labda niweke clear kama watu wakipatikana huo umoja sio lazima Kwa kila blogger kujiunga. Na pia kujiunga au kutojiunga haitasababisha mtu kuingia katika mashindano yetu au la. This will be two separate things as I said before nikishaweza kusaidia kuput together kama kuna vitu vya kuforward kwa viongozi I will do that and step aside.

Kuna vitu vingi vitaweza kufanyika kwa bloggers vikiwa under umoja wa bloggers.

Okay nasubiri kusikia kutoka kwenu.. Na form ya kutaka kufahamu ni watu wangapi watapenda kujiunga nimeiweka kwenye hiyo site...

Pauline
Founder, Tanzanian Blogs Awards



2 comments:

  1. HAPA HATUSEMI SANA MAANA TUTAONEKANA WAJUAJI

    ReplyDelete
  2. Hahaha!Anonymous ushaskia ule wimbo unaosema 2SEMA USIOGOPE SEMA"?Usiogope kutoa mawazo yako.Atakayekuona mjuaji ana matatizo yake binafsi

    ReplyDelete

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.