15 Jun 2013




Habari zilizotufikia hivi punde bomu limelipuka katika eneo la Soweto mkoani Arusha kwenye mkutano wa Chadema leo, na kusababisha watu wanne  kufariki  Dunia.

Mlipuko huo umetokea majira ya saa 12:00 na  majeruhi ni zaidi ya 10 wamekimbizwa katika Hospitali ya Mount Meru STK 8493 kwa matibabu zaidi.

Bomu hilo ambalo lilikuwa limetegewa katika mkutano huo lilipuka na kusababisha mauti na kujeruhi watu zaidi 10.

Pia gari limevunjwa vioo na wananchi kwa madai ya kwamba limeshindwa kuokoa maisha ya majeruhi.
 
Inaonekana bomu lilitegwa karibu na gari la matangazo, Mtoto aliyelipukiwa na bomu amefariki uwanjani.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Liberatus Abbas amesema kwamba watu wawili ndio wamepoteza maisha.




0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.