11 Sept 2014

Teknolojia ya kuhifadhi mafaili imetoka mbali, na kwa sasa ipo mbali pia. Zamani hizo, nyenzo kuu ya kuhifadhi mafaili ilikuwa CD-ROM,ambayo hatimaye ilipoteza umaarufu kwa USB Drives ambazo japo kimsingi bado zinatumika kwa wingi lakini umaarufu wake umepungua baada ya ujio wa kinachoitwa 'Cloud storage.' Hii ni teknolojia ya kuhifadhi mafaili 'hewani.' Uzuri wa teknolojia hii upo kwatika urahisi wa kulifikia faili lako kwani huhitaji kutembea na CD-ROM au USB Drive ili u-download faili lako. Kwa kuiba msemo wa mjini, Cloud Storage ndio 'habari ya mujini' kwa sasa.

Kimsingi, teknolojia hii ya kuhifadhi mafaili 'hewani' inahusisha ku-upload faili katika tovuti au app flani, na pili ukilihitaji faili husika basi unachofanya ni kwenda katika tovuti au app husika na ku-download faili hilo popote pale.Kwahiyo unaweza ku-save faili lako kwa kutumia simu kisha ukaweza kuli-download kwa kutumia PC au Tablet yako kwa aida kwenda kwenye tovuti husika au app yenye faili hilo.

Miongoni mwa tovuti/apps maarufu zinazotumia teknolojia ya Cloud storage ni pamoja na OneDrive ya Microsoft.OneDrive imekuwa ikichuana na tovuti/apps nyingine maarufu kama vile Google Drive,










Sasa kuna habari njema, nayo ni kwamba OneDrive imeongeza fursa ya kuhjifadhi mafaili kutoka 2 GB hadi 10GB...bure buleshi. Ifahamike kuwa nyingi  ya huduma hizo za cloud storage hutoa fursa ya wastani tu bure na iwapo mtumiaji atahitaji storage kubwa zaidi hulazimika kulipia.

Natumaini makala hii itakusaidia kupiga hatua katika teknolojia ya uhifadhi mafaili ambapo badala ya kutembea na CD-ROMs au USB Drives kila wakati, sasa waweza ku-upload mafaili yako mtandaoni au kwa kutumia apps za huduma hizo hapo juu (na zipo lukuki mtandaoni) na kuwezesha ku-access mafaili yako mahala popote pale.

0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.