15 Jul 2016

Anaitwa Karrima Carter, mwanadada mwenye asili ya Tanzania mwenye makazi yake hapa Uingereza. Kwa miaka kadhaa amekuwa akijitolea kukusanya misaada mbalimbali kwa ajili ya kuyasaidia makundi yenye uhitaji huko Tanzania. Tayari ametoa misaada kwa shule mbalimbali za msingi na sekondari katika maeneo mbalimbali ya Tanzania, anaendesha vituo vya kulea watoto yatima na kusaidia wazee. 

Tukio hili pichani ni mfululizo wa matukio anayofanya kabla ya kuelekea Tanzania wiki ijayo kukabidhi misaada kadhaa kwa makundi mbalimbali yenye uhitaji, ikiwa ni pamoja na kuambatana na wahisani kutoka hapa Uingereza kwenye hafla kwenye kituo cha yatima huko Bagamoyo, sambamba na uzinduzi wa vyoo kadhaa katika shule ya msingi Ilala.

Blogu hii inafuatilia kwa karibu jtihada za mwanadada huyu hasa ikizingatiwa kuwa kuna makundi mengi yenye uhitaji huko nyumbani ilhali suala la kujitolea bado halijapata mwamko miongoni mwa Watanzania wengi. 

Chini ni baadhi ya picha za kikundi cha watoto wa Kiingereza walioshiriki katika shughuli hiyo kwa 'kujipaka rangi usoni' (face painting) na kuigiza tamthilia maarufu ya Simba the Lion kwa lugha mbalimbali ikiwa pamoja na Kiswahili. Licha ya kushiriki kukusanya michango, watoto hao pia wanachangia kuwasaidia watoto wenzao huko Tanzania, kwa uratibu wa Karrima.

Waweza kuangalia video mbalimbali kwenye ukurasa wake wa Facebook HAPA au kwenye akaunti yake ya Instagram HAPA.














0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.