7 Mar 2020


#Thread: katika vitu ambavyo namshukuru sana Mungu ni kunijalia uwezo wa kutumia vema akili yangu. Sote tuna akili lakini kinachotutofautisha ni uwezo wa akili husika na jinsi tunavyotumia uwezo huo pindi mtu anapokuwa nao. 

Katika #thread hii nitakueleza baadhi ya "mbinu zangu"

Binafsi nina "bahati tatu" hivi zinazonisaidia. Kwanza, udogoni nililazimishwa na mmoja wa watu wawili muhimu kabisa katika maisha yangu, marehemu baba yangu Mzee Chahali (mwingine ni mama yangu marehemu Mama Chahali), kuhusu matumizi chanya ya "akili"

Sambamba na hilo, marehemu baba alinishurutisha kwa kutumia mbinu mbalimbali, kujenga uwezo kiakili na kuhakikisha kuwa sio tu uwezo huo unatumia vema bali "naumwagilia maji" au/na "kuua mlo" ili uzidi kunawiri na kuwa na ufanisi zaidi. 

Moja ya silaha muhimu aliyonipatia ni MANENO. Alinifundisha "kijeshi" sio tu jinsi ya KUSOMA bali pia "kusoma kwa ufanisi." Yaani kwa kifupi, husomi ili kusoma tu au kusoma ili kuelewa tu bali unasoma ili ulichosoma kiwe na impact flani kupitia wewe msomaji

Nakumbuka kitabu cha kwanza kusomewa na marehemu baba ni cha mmoja cha watunzi bora kabisa wa riwaya kimataifa, James Hadley Chase. Kitabu husika kinaitwa "Come Easy Go Easy."
Baada ya kunisimulia kitabu hicho, marehemu baba alinishurutisha nami nikisome kisha niwasimulie kaka na dada zangu. Hiki ndio kitabu cha kwanza kabisa cha Kiingereza kwa mie kukisoma. Na tangu hapo, kusoma kumekuwa kama basic need kwangu. 

Kitu cha pili kuhusu MANENO ambacho marehemu baba alinisistiza mno ni KUANDIKA. Na cha tatu ni KUSIKILIZA. Na cha nne ni KUONGEA. Kwahiyo kama upo nami hadi hapa, nyenzo kuu NNE za MANENO nilizopatiwa na "Chahali Sr," ni
1. KUSOMA
2. KUANDIKA
3. KUSIKILIZA
4. KUONGEA

Fastforward miaka kadhaa mbele nikabahatika kuingia Kitengo (siku nafsi ikinituma nitaelea jinsi nilivyoingia huko japo it is now irrelevant). Pamoja na mambo mengi niliyopata huku, kubwa na la muhimu zaidi linahusu taaluma yenyewe: INTELIJENSIA

Kwa kimombo ni INTELLIGENCE, yaani AKILI. Naam, sio tu taaluma hiyo yahitaji watu wenye uwezo wa hali ya juu kiakili bali pia nayo huwajengea watu hao uwezo zaidi wa kuwa na akili, na jinsi ya kuitumia vema akili hiyo. Unfortunately, #MATAGA hawakupata fursa hii. Kwa kifupi, mwana-intelijensia bora anapaswa
KUSOMA sana
KUSIKILIZA sana
KUANDIKA sana (taarifa za kiusalama)
KUONGEA sana (si kuropoka bali kuongea na watu muhimu). Kuna msemo wa kishushushu kuwa "ni silika kwa majasusi kuongea na kila mtu."

Kama wanavyosema kuwa "once a teacher always a teacher," kwenye intelijensia nako ni hivyo hivyo, once a spy always a spy." Kwahiyo, hayo mahitaji ya "kusoma sana, kusikiliza sana, kuandika sana na kuongea sana" sasa ni sehemu ya maisha yangu ya kila siku

Enewei lengo la #thread hii sio kukusimulia historia yangu balikukutaji baadhi ya nyenzo nazotumia kutunza na kuboresha uwezo wa kiakili. Siwezi kusema "nina uwezo mkubwa wa akili," maana wa kunihukumu ni watu kama wewe unayesoma #thread hii

Nikijihukumu nitajipendelea/ntajionea
Nyenzo ya kwanza, ofkoz ni KUSOMA. Nasoma mno. Lakini kama nilivyofundishwa na marehemu Mzee Chahali, nasoma si kwa ajili ya kuelewa tu bali piakwa ajili ya kuelimisha, kuhabarisha na pengine kuburudisha (inapobidi)

Nyenzo nyingine ni KUSIKILIZA watu. Na moja ya sababu yamie kufolo watu wachache sana kwenye akaunti zangu za mitandao ya kijamii ni kujijengea mazingira mazuri ya KUSIKILIZA vizuri watu/vitu mbalimbali. Again, kusikiliza huku si kwa ajili yangu tu bali ajili ya jamii pia

Nyenzo nyingine ni KUONGEA. Naongea na watu wengi sana. Takriban kila wiki ninawasiliana na watu 5,000 hivi kupitia vijarida vyangu mbalimbali. Na pindi nikichapisha makala kwenye blogu zangu mbili, naweza kujikuta "naongea" na watu hadi 10,000 kwa wiki. 

Lakini mengi ya maongezi yangu ni kwa kutumia maandishi zaidi kuliko "maneno kutoka mdomoni." Japo naandika sana, mwenyewe hujitambulisha zaidi kama "mwanamaongezi," kwa kimombo "conversationalist."

Na nyenzo nyingine ni huko KUANDIKA. Kama nilivyotanabaisha hapo juu, maandiko yangu hulenga zaidi KUFUNDISHA na/au KUHABARISHA japo from time to timehuwa nachomekea kuburidisha pia. 

Lakini sipendi kuitwa MWANDISHI bali najiona MWANAMAONGEZI (conversationalist)

Ukifanya ku-search "@chahali #Tools" utakutana na lundo la nyenzo mbalimbali kwa ajili ya kada mbalimbali. Nyingi ni nyenzo za mitandao ya kijamii (social media tools) lakini pia kuna nyenzo za ushushushu, usalama wa mtandaoni, journalism, nk
Moja ya mbinu ninazotumia kufahamu nyenzo hizo ni kwa kutumia "mbinu mbalimbali za kutafuta vitu" (hususan mtandaoni). 

Kwa mfano, jinsi ya kutumia alama ya reli kutafuta kitu kwenye mitandao ya kijamii. Mfano, kuandika #Tools kwenye Twitter search. Kingine kinachonisaida sana ni KUALAMISHA. 

Sijui "uelewa wako wa Kiswahili ni mkubwa kiasi gani," ila kama hufahamu maana ya "kualamaisha,," jibu ni "ku-bookmark." Na Twitter ina kitufe maalum kwa ajili ya kualamisha
Kanuni yangu ni hii: kila ninapokutana na kitu chochote kile ninachodhani kina umuhimu, lazima nikialamishe. Iwe ni tweet, video, picha, habari, nukuu, just almost certainly anything and everything. Nina lundo la apps za kualamisha. 

Ukiniuliza niapps zipi zilizo bora zaidi kualamisha (kwa simu za Android) nitakutajia hizi
Evenote
Google Keep
Pocket
Microsoft OneNote
Insapaper
Zoho Notebook
Nyenzo ninazotumia sana kwenye mitandao ya kijamii hususan hapa Twitter ni za kufanya AUTOMATION. Hii inamaanisha, kwa lugha nyepesi, kuifanya app itekeleze majukumu bila wewe kuwepo kwenye app hiyo. 

Kwa mfano, muda mwingi mie sipo Twitter, na nyingi ya tweets zangu huji-post zenyewe.Nachofanya ni kuandika tweets usiku kisha nazipangia muda wakuji-post. 

Mfano halisi ni hizo "motivational quotes" za kila siku. Huwa nazipangia kuji-post 6am, 8am,12pm,2pm na 4pm UK Time. Apps zinazoniwezesha kufanya hivyo ni
Hootsuite
Buffer
Post It Later
Everypost
Crowdfire
Recurpost,

Pia web apps nazotumia ni Tweetsmap na Twittimer
Sambamba na apps hizo kwa ajili ya ku-automate posts, pia ninatumia nyenzo moja bora kabisa iitwayo IFTTT. Kirefu chake ni "If This Then That," yaani "kama hivi basi vile."
Natumia IFTTT kufanya mambo mengi. Kwa mfano nikiposti kitu bloguni kwangu nimeielekeza IFTTT ifanye kupost chapisho hilo hapa Twitter. 

Kadhalika, nimeielekeza IFTTT kuwa niki-like post basi ialamishe post hiyo kwenye app ya Evernote. Nimeielekeza pia kuwa nikipost #NenoLaLeoKiroho huko Pinterest basi ifanye kupost hapa insta pia. 

Pia naitumia IFTTT "kufuatilia watu ninaohitaji kuwafuatilia kwa sababu zangu binafsi." Kwa mfano, mlengwa akinitaja kwenye twiti, IFTTT inahifadhi twiti hiyo kwenye app flani 😊

Kuhusu hizi #thread, nikiwa na muda naandika thread husika kwa kuunganisha twiti kama mnyororo. Lakini muda ukiwa tight, natumia web app iitwayo Chir App ambayo ni ya bure au Hypefury ambayo ni ya kulipia.
Nimalizie #thread kwa kukutajia nyenzo ambayo kwenye taaluma ya masoko inaitwa NICHE. Ni hivi, kama ambavyo huwezi kwenda chuoni na kusoma kila kozi au somo, ndivyo maisha ya mtandaoni yanavyostahili kuwa. 

Usipokuwa na "mkazo" kwenye mada/sekta (niche) flani unaweza kuyumba
Kwangu, nina "niche" kadhaa ambazo ndio "zinaniweka kwenye mitandao ya kijamii."

Niche hizo ni siasa kwa ujumla (zaidi za Tanzania), teknolojia hususan usalama wa mtandaoni na ufanisi katika matumizi ya mitandao ya kijamii. Vilevile "personal development yaani "jinsi ya kuwa mtu bora." Niche nyingine ni lugha ya Kiswahili na uandishi wa vitabu. 

Je wewe "niche" yako ni ipi?

0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.