Showing posts with label DINI. Show all posts
Showing posts with label DINI. Show all posts

13 Feb 2013

Peter Turkson (Ghana, 64) is the top African candidate. Head of the Vatican justice and peace bureau, he is spokesman for the Church's social conscience and backs world financial reform. He showed a video criticizing Muslims at a recent Vatican synod, raising doubts about how he sees Islam.

Kadrinali Peter Turkson ambaye ni Mghana anatajwa kuwa miongoni mwa wanaoweza kumrithi Papa Benedikti wa 16 ambaye atajiuzulu mwisho wa mwezi huu. Iwapo Turkson atafanikiwa kuwa Papa, atakuwa mtu mweusi wa kwanza kushika nafasi hiyo ya ukuu wa Kanisa Katoliki.Moja ya mambo yanayozungumzwa kuhusu Kardinali huyo ni mtizamo wake kuhusu kukua kwa Uislamu duniani.Licha ya kuongea lugha yake ya asili ya Fante na lugha nyingine za asili za Ghana, Kadrinali Turkson anaongea pia Kiingereza, Kifaransa,Kitaliano,Kijerumani na Kiyahudi.Pia anafahamu Kigiriki na Kilatini.

'Papabili' (Mapapa watarajiwa) wengine ni kama ifuatavyo

Luis Tagle (Philippines, 55) has a charisma often compared to that of the late Pope John Paul. He is also close to Pope Benedict after working with him at the International Theological Commission. While he has many fans, he only became a cardinal in 2012 and conclaves are wary of young candidates.
Kardinali Luis Tagle wa Ufilipino

Angelo Scola (Italy, 71) is archbishop of Milan, a springboard to the papacy, and is many Italians' bet to win. An expert on bioethics, he also knows Islam as head of a foundation to promote Muslim-Christian understanding. His dense oratory could put off cardinals seeking a charismatic communicator.
Kardinali Angelo Scola wa Italia

Christoph Schoenborn (Austria, 67) is a former student of Pope Benedict with a pastoral touch the pontiff lacks. The Vienna archbishop has ranked as papal material since editing the Church catechism in the 1990s. But some cautious reform stands and strong dissent by some Austrian priests could hurt him.
Kardinali Christoph Schoenborn wa Austria

Odilo Pedro Scherer (Brazilia, 63) ranks as Latin America's strongest candidate. Archbishop of Sao Paolo, largest diocese in the largest Catholic country, he is conservative in his country but would rank as a moderate elsewhere. The rapid growth of Protestant churches in Brazil could count against him.
Kardinali Odilo Pedro Scherer wa Brazili

Leonardo Sandri (Argentina, 69) is a "transatlantic" figure born in Buenos Aires to Italian parents. He held the third-highest Vatican post as its chief of staff in 2000-2007. But he has no pastoral experience and his job overseeing eastern churches is not a power position in Rome.
Kardinali Leonardo Sandri wa Ajentina

Gianfranco Ravasi (Italy, 70) has been Vatican culture minister since 2007 and represents the Church to the worlds of art, science, culture and even to atheists. This profile could hurt him if cardinals decide they need an experienced pastor rather than another professor as pope.
Kardinali Ginafranco Ravasi wa Italia

Marc Ouellet (Canada, 68) is effectively the Vatican's top staff director as head of the Congregation for Bishops. He once said becoming pope "would be a nightmare." Though well connected within the Curia, the widespread secularism of his native Quebec could work against him.
Kardinali Marc Ouellet wa Kanada

Timothy Dolan, (USA, 62) became the voice of U.S. Catholicism after being named archbishop of New York in 2009. His humor and dynamism have impressed the Vatican, where both are often missing. But cardinals are wary of a "superpower pope" and his back-slapping style may be too American for some.
Kardinali Timothy Dolan wa Marekani

Joao Braz de Aviz (Brazil, 65) brought fresh air to the Vatican department for religious congregations when he took over in 2011. He supports the preference for the poor in Latin America's liberation theology, but not the excesses of its advocates. Possible drawbacks include his low profile.
Kardinali Joao Braz de Aviz wa Brazil

Kardinali Peter Erdo wa Hungary

Mwafrika mwingine anayetajwa kuwa anaweza kuwa mrithi wa Papa Benedikti wa 16 ni Kardinali Francis Arinze wa Nigeria (pichani chini)




11 Mar 2008

MAKALA HII YANGU ILITOKA KATIKA GAZETI LA MTANZANIA TAREHE 07 MACHI 2008

Unafiki wa viongozi wetu wa dini

na evarist chahali, uskochi

MADA yangu ya leo, najua dhahiri itawakera wateule wachache wa aina fulani. Lakini kabla ya kuwapasha, naomba nizungumzie suala la imani na dini hapa ninapoishi Ughaibuni.

Nilipofika hapa kwa mara ya kwanza, nilionyeshwa majengo kadhaa ambayo huko nyuma yalikuwa Makanisa, lakini sasa yamegeuzwa kuwa kumbi za disko na klabu za usiku.

Na hao walioyageuza Makanisa hayo kuwa sehemu za starehe, wala hawakujishughulisha kabisa katika kubadili mwonekano wake, bali wameyaacha yatoe ushuhuda kuwa huko nyuma yalikuwa sehemu za ibada.

Nilipofanya udadisi kwa wenyeji, niliambiwa kwamba makanisa hayo yaliuzwa baada ya kuwa matupu kutokana na ukosefu wa waumini. Wengi wa waumini wa makanisa ya mji huu ninaoishi, ni ama wahamiaji waliotoka nje ya nchi hii kama mimi, na au vikongwe vya hapa hapa.

Binafsi, sina majibu ya moja kwa moja kwamba tatizo la hawa wenzetu ni nini. Hata hivyo, ninachofahamu ni kwamba kuna watu kadhaa ambao wanajitambulisha kuwa hawana dini, na au hawaamini kuwapo kwa Mungu.

Imani ni suala la mtu binafsi, na hivyo pengine si mwafaka kuhoji kwa nini fulani anaamini, ama haamini kuwapo au kutokuwapo kwa Mungu.Ingawa binafsi, ni muumini kwa aina fulani, huwa sisiti kuwasifu wale wasiowaumini wa dini yoyote, lakini wasioona aibu kuelezea msimamo wao wa kidini. Kwa lugha nyingine, watu hao si wanafiki. Wanaeleza bayana kile wanachokiamini na kutokiamini.

Kuna tatizo la msingi huko nyumbani, ingawa natambua dhahiri kwamba watu wengi hawapendi kujadili mambo ya dini kwa sababu ile ile ya unafiki!

Baadhi ya viongozi wetu wa dini, wamekuwa mstari wa mbele kukemea wale ambao wanakwenda kinyume na imani zao, lakini viongozi hao hao wakishiriki kwenye maovu wanayoyakemea.

Ndiyo, tunatambua kwamba mara nyingi viongozi wetu wa dini wana wafadhili wao nje ya nchi. Lakini hicho si kigezo cha wao kuishi maisha tofauti kabisa na wafuasi wao.

Utakuta katika kijiji fulani ambacho kimegubikwa kabisa na umasikini, kiongozi fulani wa dini yeye akiishi kama yuko peponi. Na bila huruma, huyo huyo anayeishi maisha kama ya peponi katikati ya waumini masikini, kwa kutumia kisingizio cha maandiko matakatifu, anawashurutisha waumini wake kujipigapiga ili kuongeza sadaka wanazotoa.

Kinachokera zaidi, ni hili suala la baadhi ya viongozi wa madhehebu fulani kuwa na watoto mitaani, huku sheria za madhehebu yao zikiwa haziwaruhusu kufanya hivyo.

Tatizo hili ni sugu sana, hususan maeneo ya vijijini. Kinachosikitisha ni ukweli kwamba waumini wanafahamu kwamba kiongozi wao wa dini, anaishi kinyume na maadili ya huduma yake, lakini hawachukui hatua yoyote zaidi ya kulalamika chini chini.

Binafsi, ninayo mifano hai ya baadhi ya viongozi wa madhehebu yangu ambao wana watoto lukuki mitaani. Baadhi yao wanatoa huduma kwa wazazi wa watoto wao hao, lakini wengine wamewatelekeza kabisa.

Hawa watu ni wanafiki ambao hawastahili kuachwa waendeleze uhuni kwa kisingizio kwamba daraja walilofikia, haliwezi kutenguliwa.

Mitume wetu waliishi maisha ya uadilifu, ambayo yalishabihiana kwa asilimia 100 na kile walichokuwa wakikihubiri. Na si katika suala la uzinzi pekee, bali hata kwenye dili za kibiashara.Majanga kama ya ukimwi yataondoka vipi iwapo baadhi ya wale wanaopaswa kukemea vitendo vya ngono, kwa vile vinavunja amri ya Mungu, nao ni washirika wa vitendo hivyo?

Pamoja na mapungufu waliyonayo baadhi ya viongozi wa dini, hivi karibuni tumeshuhudia wengi wakijitokeza kuungana na Watanzania wenzao kukemea masuala yanayohatarisha umoja wa kitaifa.

Suala ambalo baadhi ya viongozi hao wa dini wanastahili pongezi, ni katika kukemea vitendo vya kifisadi, ingawa tatizo linakuwapo, pale msimamo huo unapokuwa wa kiongozi mmoja zaidi, badala ya kuwa msimamo wa taasisi ya dini.

Katika hili, napenda nichukue fursa hii kumpongeza Askofu Mkuu mpya wa Kanisa la Anglikana Tanzania, ambaye ameweka bayana msimamo wake dhidi ya vitendo vya kifisadi. Hiyo inatia moyo sana!

Licha ya kukemea ufisadi na maovu mengine katika jamii, asasi za dini zinaweza kubadili tabia za waumini wao kwa kuwawekea vikwazo vya aina fulani. Taratibu za aina hiyo, zipo katika baadhi ya imani, kwa mfano, Wakatoliki, ambao muumini akikiuka kanuni fulani, anazuiwa kushiriki baadhi ya sakramenti.

Kwa nini basi tunaendelea kujumuika na mafisadi makanisani, na au misikitini ilhali matendo yao yanalenga kutuumiza kimaisha? Nafahamu kuwa dini zote zinahimiza upendo, lakini hiyo si sababu ya kutowabana wale wasio na upendo kwa Watanzania wenzao.

Inawezekana kwamba kikwazo kikubwa kwa dini zetu kuwa mstari wa mbele katika kukemea maovu na kubadili tabia za wanaokwenda kinyume na maadili ya kimwili na kiroho, ni hofu ya usafi wa baadhi ya viongozi wa dini hizo, kama nilivyoeleza mwanzoni mwa makala haya.Tatizo hilo linaweza kupatiwa ufumbuzi iwapo viongozi wa madhehebu wataepuka mtindo wa kulindana, na hivyo kuchukua hatua kali kwa walio chini yao, ambao wanakwenda kinyume cha kanuni na taratibu za madhehebu.

Ni wazi kwamba viongozi waadilifu wa dini, hawawezi kuogopa kumnyooshea kidole fisadi fulani, kwa kuwa hata kama fisadi huyo atataka kulipa kisasi, atajikuta hana jambo lolote analoweza kulitumia kushusha heshima ya kiongozi wa dini aliyemkemea.

Busara za Kiswahili zinatueleza kwamba kujikwaa si kuanguka, na hata kuanguka si mwisho wa safari. Wito wangu kwa viongozi wetu wa dini, ni kuongeza jitihada za kuwahudumia waumini wao kiroho na kimwili.

Ni muhimu kwa viongozi hao kuishi kama Mitume ambao mafundisho yao yalikubalika na kuvuta watu wengi, kwa vile wao wenyewe walikuwa waadilifu na mifano bora ya kuigwa na wanadamu.




Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.