Showing posts with label EGYPT. Show all posts
Showing posts with label EGYPT. Show all posts

12 Feb 2011


Serikali ya Uswisi imetangaza kutaifisha mali zote za Dikteta Hosni Mubarak,ambaye jioni hii ameng'olewa madarakani na nguvu ya umma.Kwa mujibu wa vyombo vya habari vya kimataifa,haijafahamika iwapo serikali za Uingereza,Marekani na nchi nyingine za Magharibi ambako Mubarak ana mali zake (na kujichumia utajiri unaokadiriwa kufikiwa dola za Kimarekani Bilioni 70) nazo zitachukua hatua kama hiyo ya Uswisi au la.Je mafisadi wetu huko nyumbani wanajifunza lolote katika sakata hili?
I just hope they do!

11 Feb 2011

Habari zaidi baadaye

4 Feb 2011


Kuna jitihada zinazofanyika huko nchini Misri katika jitihada za kumaliza machafuko yaliyodumu kwa zaidi ya siku 10 sasa kushinikiza kung'oka madarakani kwa Rais Hosni Mubarak.Jitihada hizo zinafanywa na kundi linalojumisha "Kamati ya Watu wa Busara" (ni kama Wazee wa Busara lakini sio kama wale walioimbwa na kundi la Wachuja Nafaka ).Watu hawa wenye heshima zao katika taifa hilo wanajaribu kuepusha maafa zaidi ambapo inaelezwa kuwa hadi sasa zaidi ya watu 300 wameshauawa.Kwa mfano,miongoni mwa mambo waliyojaribu kuishauri Serikali ya Mubarak ni kuangalia uwezekano wa Rais huyu kubaki na cheo cha heshima (figure head) lakini majukumu ya kuendesha nchi yakabidhiwe kwa Makamu wa Rais.Kadhalika,walidai kuwa wanaweza kushawishi kundi la Muslim Brotherhood lisisimamishe mgombea iwapo Serikali ya Mubarak itakubali kuitisha uchaguzi.

Ukiangalia mwenendo wa mambo huko nyumbani,ni dhahiri nasi tunahitaji Wazee wa Busara wa kukutana na Rais Jakaya Kikwete,angalau kumwamsha katika lindi la usingizi unaomkabili na kumfahamisha kuwa taifa letu linaelekea kusikostahili.Tunaweza kujidanganya kuwa yanayotokea Misri hayawezi kutokea kwetu lakini ukweli ni kwamba mazingira yaliyopelekea mbinde huko Misri,Tunisia,na sasa Yemen na Sudan (kwa kiasi flani) pia yapo huko nyumbani.Umasikini wa kupindukia ambao unapuuzwa na watawala wanaozidi kujirundikia utajiri,sambamba na kupora raslimali za umma;ukosefu wa ajira;utawala wa kibabe (rejea mauaji ya raia wasio na hatia huko Arusha na Mbeya,sambamba na nguvu kubwa kupita kiasi zinazotumiwa na vyombo vya dola kudhibiti maandamano ya amani),to mention but a few.

Unfortunately,wazee aliotuachia Baba wa Taifa ndio dizaini ya akina Kingunge-watetezi wakubwa wa ufisadi.Kuna watu kama Rais Mstaafu Ali Hassan Mwinyi,Mawaziri Wakuu Wastaafu kama Warioba na Cleopa Msuya,na wanasiasa kama akina Joseph Butiku lakini hawa wote wanakwazwa na tatizo lilelile linaloikwamisha Tanzania yetu: kuweka maslahi ya kisiasa mbele ya maslahi ya taifa.Angalau Warioba amejaribu mara kadhaa kuzungumza "kwa niaba ya umma" lakini mafisadi wakaanza kumuundia zengwe.

Nalazimika kupigia mstari umuhimu wa kuwatumia Wazee wa Busara kumwamsha Kikwete kwa vile inaelekea Rais wetu anajifanya haelewi kinachoendelea kwenye maisha ya Watanzania wengi.Yoote aliyoahidi wakati wa kampeni zake za mwaka 2005,na kisha kuyarejea tena wakati za kampeni za mwaka jana yanaelekea kuwa yamesahaulika kama sio kupuuzwa.

Majuzi nilityumiwa comment na msomaji mmoja aliyenishutumu kwa kile alichoita "kuchochea vurugu" na kudai mie nahamasisha yanayotokea Misri na Tunisia yatokee Tanzania pia ilhali mie mwenyewe niko nje ya nchi.Mpuuzi huyu anajifanya haelewi kwamba kuwa nje ya nchi hakumaanishi Utanzania wangu unakuwa nusu.Afterall,nina ndugu,jamaa na marafiki wanaoteseka kutokana na hayo nayopigia kelele kila siku.

Na hata blogu hii ikikaa kimya,au wazalendo wa mtandao kama Jamii Forums nao wakinyamaza,ukweli unabaki kuwa siku moja Watanzania wanaweza kusema this is too much,liwalo na liwe.Mwanafalsafa Karl Marx aliwahi kutuasa kuwa masikini hana cha kupoteza (akiamua liwalo na liwe) except minyororo anayobebeshwa na watawala dhalimu.

Tuna uchaguzi mmoja tu: kubadilisha hali ya mambo kwa njia za amani ama sivyo yanayojiri mahala kwingineko yanaweza kutokea kwetu pia.Sio suala la kuombea au unabii wa maangamizi bali huo ni ukweli mchungu.Hakuna namna ya kumaliza ugonjwa pasipo tiba.

Na kwa Kikwete na jamaa zake,ni muhimu kujifunza katika yanayoendelea huko Tunisia,Misri,Jordan,Yemen na Sudan.Kuendelea kuwakumbatia mafisadi wanaokwangua uchumi wetu kila kukicha ni jambo lisilokubalika hata chembe.

TUSIPOZIBA UFA TUTAJENGA UKUTA

28 Jan 2011












Chanzo: The Guardian

KAMA TUNISIA WALIFANIKIWA,MISRI NAO WANAWEZA KUFANIKIWA.KAMA TUNISIA NA MISRI WAMEDIRIKI,WAANZANIA NAO WANAWEZA.PENYE NIA PANA NJIA.IT CAN BE DONE IF WE ALL PLAY OUR PARTS.

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.