Showing posts with label MEMORABLE EVENTS. Show all posts
Showing posts with label MEMORABLE EVENTS. Show all posts

7 Aug 2009



Kwa mfumo wa tarehe za "kwetu" tunaanza na tarehe kisha mwezi,tofauti na wenzetu wa kwa Obama ambao wanaanza na mwenzi kisha tarehe.Yaani,kwa hapa,na kama ilivyo huko nyumbani TZ,ni tarehe 07/08/09 japo kwa wenzetu wa US itaandikwa 08/07/09.Basi,leo mchana kulikuwa na tukio adimu katika uhai wa wengi.Kama inavyoonekana pichani juu,kuna muda saa na kaelnda ilisomeka 1-2-3-4-5-6-7-8-9,yaani saa 12 na dk 34 na sekunde 56 tarehe 7 mwezi wa nane mwaka 2009 (12:34:56 7/8/9).Ulikumbuka kuhusu tukio hili?

MHAMASISHA VITA DHIDI YA MAFUA YA NGURUWE NAYE AAMBUKIZWA....


Na the funny side ya "maadhimisho" hayo ni habari hapa Uingereza kwamba jamaa aliyetumika katika tangazo la "Wizara" ya Afya katika runinga kuhamasisha jamii dhidi ya mafua ya nguruwe (swine flu) nae ameambukizwa ugonjwa huo.Msanii Davidi McCusker (pichani juu).Hata hivyo,lililo dhahiri ni kwamba maambukizo hayo hayana mahusiano na ushiriki wa msaanii huyo David McCusker katika tangazo hilo.

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.