7 Mar 2008

Wengine wanasema Ukimwi ni miongoni mwa dalili kuwa mwisho wa dunia u-karibu.Huwezi kuwalaumu wanaodhani hivyo kwani tatizo hili limekuwa likiendelea kusumbua miaka nenda miaka rudi pasipo dalili ya ufumbuzi.Ni nafuu zaidi kwa waathirika walio kwenye nchi zilizoendelea ambao licha ya kupatiwa misaada ya tiba na ushauri nasaha,wana nafuu zaidi katika matatizo mengine yanayozizunguka jamii katika nchi masikini ikiwa ni pamoja na ufisadi wa raslimali na ngono,masangoma matapeli,unyanyapaa,nk.Inawezekana tiba ya ukimwi ikapatikana mapema kabla ya tiba ya ufisadi huko nyumbani?Anyway,blogu ya Illseed ina habari inayoweza kuleta matumaini kwa mamilioni ya waathirika wa HIV/AIDS.Soma habari hiyo kwa KUBONYEZA HAPA.

0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.