3 Nov 2008

Nyumbani kwa Obama kijijini Kogelo,Kenya.

Kwa mujibu wa ripota wa CNN aliyeko kijiji cha Kogelo huko Kenya,ambacho kinahusiana kwa karibu sana na asili ya Barack Obama,kuna kundi la viumbe-hai wanaoombea mgombea wa urais huyo asishinde kesho ili viumbe hao wasalimike.Hao ni ng'ombe ambao wanaandaliwa kwa ajili ya sherehe kubwa pindi Obama atapotangazwa mshindi.Ni dhahiri kwamba asiposhinda,ng'ombe hao nao watasalimika.Who would you  have felt more sorry for?

Wakati ng'ombe hao wakisubiri hatima yao,sangoma mmoja kijijini hapo ametabiri kuwa Obama atashinda uchaguzi huo wa kesho.Of course,sangoma huyo-John Radima-sio pundit wa major TV networks au pollster kutoka Gallup,lakini ameweza kukamata attention ya vyombo vya habari vya kimataifa.

Kwa upande wa grandmother wa Obama,yeye anasema hawezi ku-take things for granted hadi hapo mshindi atapotangazwa,na anafuatilia kwa karibu maendeleo ya mjukuu wake kwenye runinga inayotumia solar power kwa vile hakuna umeme katika makazi yake.Sarah Onyango Obama,wenye miaka 86,anasema kwamba katika soka huwezi kutabiri ushindi mpaka goli lipatikane.Wakati bibi Sarah (pichani chini) akisubiria kwa hamu matokeo ya kesho,upanuzi wa uwanja wa ndege wa Kisumu umewafanya baadhi ya watu kutania kwamba huenda ni maandalizi ya ujio wa Air Force One ikiwa na Obama.


0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.