17 May 2009


NIMEKUTANA NA HABARI ILIYONISHTUA KIDOGO,KWAMBA MMOJA WA WANA-CCM WALIOOMBA KUGOMBEA KITI CHA UBUNGE KATIKA UCHAGUZI MDOGO WA JIMBO LA BUSANDA,DONALD MAX, AMEREJESHEWA GHARAMA ALIZOTUMIA WAKATI WA KUJIPIGIA DEBE.INADAIWA HILO LIMEFANYIKA ILI AWEZE KUSHIRIKI KWENYE KAMPENI ZA MGOMBEA ALIYEPITISHWA NA CCM,LORENCIA BUKWIMBA.

KWA MUJIBU WA GAZETI LA Mwananchi:


Taarifa...za ndani zilisema kukubali kwa Max kupanda jukwaani, kunatokana na makubaliano ya faragha baina yake na Malecela kwa niaba ya Kikwete ambaye aliagiza arejeshewe gharama zake za kampeni katika mchakato wa kura za maoni...Kutokana na makubaliano hayo CCM kiliagizwa kusaka fedha za kumrudishia Max ambazo zililetwa na mbunge mmoja wa Kanda ya Magharibi, ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu na Halmashauri Kuu, ambaye imeelezwa aliingia Geita kimya kimya na kufanya mazungumzo naye.

NASEMA HABARI HIYO IMENISHTUA "KIDOGO" KWA VILE CCM SI NGENI KATIKA ULIMWENGU WA MAIGIZO YA KISIASA.KWA MFANO,TUME YA MAADILI YA CHAMA HICHO BADO IKO CHINI YA UONGOZI WA MZEE WA VIJISENTI,MWANASIASA AMBAYE MAADILI YAKE YA UONGOZI NI QUESTIONABLE KUTOKANA NA TUHUMA ZA KUJILIMBIZIA VIJISENTI HAPO JERSEY.

LAKINI INAPOFIKIA HATUA YA CHAMA HICHO KUREJESHA GHARAMA ZA MGOMBEA ALIYESHINDWA KWENYE NOMINATION PROCESS INAMWAGA ZEGE ZAIDI KWENYE UKWELI KWAMBA CHAMA HICHO TAWALA KINA UHABA MKUBWA ZA BUSARA ZA UONGOZI.HIVI KUREJESHA GHARAMA HIZO KUNA TOFAUTI GANI NA KUMHONGA MWANASIASA HUYO ILI APANDE JUKWAANI?HIVI,TUKIAMINI KUWA HABARI HIZO NI ZA KWELI,CCM ITOE FEDHA HIZO KISHA MAX APANDE JUKWAANI KUMNADI MGOMBEA BUKWIMBA,KISHA CHAMA HICHO KISHINDWE KWENYE UCHAGUZI (WHICH IS POSSIBLE KAMA KUTAKUWA NA UCHAGUZI HURU NA HAKI)........FILL IN THE BLANKS,MZALENDO MWENZANGU.

KAMA LEO CCM INADIRIKI KUTOA FEDHA KUMSHAWISHI MAX APANDE JUKWAANI,ITASHINDWAJE KUWAPA FADHILA MAFISADI KATIKA UCHAGUZI WA MWAKANI IWAPO CHAMA HICHO KITAELEKEA KUSHINDWA?HAYA YALITOKEA 2005,NA NDIO VYANZO VYA SKANDALI ZA EPA NA NYINGINEZO.SIJUI INGEKUWAJE LAITI MAREHEMU BABA WA TAIFA ANGERUDI DUNIANI NA KUKUTA CHAMA ALICHOKIASISI KINAFANYA UTUMBO KAMA HUU!

0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.