7 Nov 2009


SIKU moja baada ya mjadala wa Richmond kuahirishwa bungeni, baadhi ya wabunge wamesema serikali imechangia kuchelewesha suala hilo ili kukwepa fedheha na kuonya kwamba ujanja huo hautaisaidia.

Wakati wabunge wakitoa kauli hiyo, Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), sasa wanajiandaa kuishtaki serikali kwa wananchi ili waihukumu kwa kuikumbatia Richmond.

Wabunge waliozungumza kwa nyakati tofauti na Mwananchi Jumapili jana, walisema licha ya kuendelea kuupiga kalenda mjadala, bado wanaisubiri ripoti ya Richmond kwa hamu na kwamba hawatalala mpaka kieleweke.

Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Kudumu ya Nishati na Madini, William Shellukindo alisema hajui kilichotokea hata ripoti hiyo ikaahirishwa tena.

"Siku mbili za mwisho sikuwa bungeni, niko nyumbani nimefiwa na mtoto wangu¦, sijui kilichotokea mpaka waahirishe ripoti hiyo katika Bunge hili, alisema Shellukindo...ENDELEA KUSOMA HAPA

CHANZO: Mwananchi

SABABU NYINGINE YA KUINYIMA CCM KURA HAPO MWAKANI.ZIPO NYINGI LAKINI HII INASUKUMA HATA WALE WALIOKUNYWA MAJI YA BENDERA YA CCM.BUNGE LENYEWE HALINA MENO,MIKWARA MIIIINGI KABLA YA VIKAO (PENGINE KATIKA KUHALALISHA MARUPURUPU YAO MANONO) NA WANAHABARI WETU WANADAKIA KILELE HIZO TO AN EXTENT YA KUKUAMINISHA KUWA SAFARI HII WEZI WA RICHMOND HAW

0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.