5 Sept 2010


Inaudhi na kukasirisha kuona gazeti la serikali,Habari Leo,likijipachika jukumu la kumuua kisiasa mgombea wa Chadema Dokta Wilbroad Slaa kama ambavyo imekuwa ikifanywa na magazeti ya Habari Corporation na Changamoto,na mengineyo yanayofadhiliwa na mafisadi.

Gazeti hilo limeandika kwa kirefu kuhusu anayedaiwa kuwa mume wa mwenza wa sasa wa Dkt Slaa,Josephine Mushumbusi.Ungetegemea gazeti hilo linaloendeshwa kwa fedha za walipa kodi wa Kitanzania pasipo kujali itikadi zao za kisiasa,lingetafakari kwa makini madhara ya habari hiyo.Wanajua sana wanachofanya,na yayumkinika kuamini kuwa serikali inayoongozwa na mgombea wa CCM,Jakaya Kikwete,imeridhia uchapishaji wa habari za aina hiyo.

Kuna msemo wa busara unaoasa "WANAOISHI KWENYE NYUMBA ZA VIOO WASIRUSHE MAWE".Mantiki ya msemo huo ni kwamba kama una wasifu wenye mawaa ya aina moja au nyingine then si wazo jema kuwachafua watu wengine.Wengi wetu tunafahamu "ishu binafsi" za viongozi wa CCM ikiwa ni pamoja na Kikwete mwenyewe.Hazizungumzwi hadharani kwa kuwatunzia heshima viongozi hao lakini inaelekea katika kutapatapa kwao baada ya kugundua hawamwezi Dokta Slaa kwa hoja,wameamua kuhamia kwenye character assassination.

Majukwaani,Kikwete na CCM yake wanajifanya kuhubiri umuhimu wa kampeni za kistaarabu lakini pembeni wanaruhusu raslimali za umma zitumike kumchafua Dokta Slaa.Kikwete alichukua hatua za haraka pale mtandao maarufu wa Ze Utamu ulipochapisha picha zinazomhusu lakini anaruhusu gazeti la serikali litumike kumwandama Dkt Slaa.

Na kwa kuonyesha unazi,kuna mahala katika habari hiyo ambapo pasi aibu wameandika (nanukuu) "Na wakati Mahimbo akiwa njia panda akishindwa kujua hatima ya ndoa yake, Dk. Slaa, Padri msomi `amelitangazia’ taifa mbele ya mikutano ya kampeni ya chama chake cha Chadema kuwa Josephine ndiye mke wake mtarajiwa..." 

Hivi Mhariri wa Habari Leo hafahamu kuwa Dkt Slaa sio Padri bali aliwahi kushika nafasi hiyo na kuiacha?

Blogu hii inamshauri Kikwete akemee mkakati huu mufilisi wa character assassination.Wengi wanafahamu kwa undani maisha ya Kikwete tangu akiwa Waziri,na wanajua vema maisha yake binafsi ndani na nje ya nchi.Asijivunie vyombo vya dola kumlinda pindi kibao kitapogeuzwa upande wake.Ni bora Dokta Slaa anayetangaza hadharani kuhusu uhusiano wake na Josephine kuliko kashfa lukuki zinazohifadhiwa kuhusu viongozi wa CCM kwa vile tu tunawaheshimu na tuna mambo muhimu zaidi ya kuzungumzia kuliko maisha binafsi ya viongozi wetu.

I repeat: Those who live in glass houses shouldn't throw stones!!!



0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.