Showing posts with label KIKWETE. Show all posts
Showing posts with label KIKWETE. Show all posts

10 Oct 2014

Kwanza soma taarifa ifuatayo kutoka Ikulu kisha tuijadili pamoja
Kweli Tanzania yetu haina uhaba wa mazingaombwe. Lakini hilo dogo, kubwa ni 'akili' za baadhi ya wasaidizi wa Rais. Binafsi nimekuwa mpinzani sana wa hoja kuwa 'tatizo si JKI bali wasaidizi/ watendaji wake,' kigezo changu kikubwa kikiwa 'kwani walimshikia mtutu wa bunduki awateue na kisha kumtahadharisha kuwa akiwatimua pindi watapoboronga watamdhuru'?

Lakini ukiangalia mlolongo wa 'makanusho' yanayotolewa na wasaidizi wa Rais, unaweza kukubaliana na wanaosema kuwa 'wasaidizi/ watendaji wa JK wanamwangusha' (japo siafiki wanaotaka kutumia sababu hiyo kama excuse ya kumsafisha JK mwenyewe.)


Hebu tuichambue kauli hiyo ya Ikulu hatua kwa hatua. Kwanza, Ikulu haikuwahi kukanusha lundo la picha (kama hiyo inayoambatana na kichwa cha habari hii) zilizowekwa mtandaoni zikimwonyesha Rais Kikwete akipokea zawadi ya saa, huku maelezo yakibainisha waziwazi kuwa 'Rais Jakaya Kikwete akipokea zawadi ya saa..." Najua kwanini hawakuhangaika na taarifa hizo za awali: hazikuhusiana na 'utata' unaomkabili mwekezaji aliyetoa zawadi hiyo.
Lakini baada ya gazeti la Raia Mwema kueleza bayana kuwa mwekezaji wa mradi wa treni ya kisasa Dar ndiye huyo alompa zawadi ya saa Rais Kikwete, na kutanabaisha maswali kadhaa yanayouzunguka mradi husika na wasifu wa mwekezaji huyo, Ikulu ikakurupuka na kanusho hili. WALIKUWA WAPI MUDA WOTE HUO?

Mwandishi wa taarifa hiyo ameonyesha ni mtovu wa nidhamu wa kutokana na matumizi ya maneno yasiyopaswa kutoka ofisi iliyopo sehemu 'tukufu' kama Ikulu. Matumizi ya maneno kama "ni habari ya uzushi na UPUUZI..." na  "...kumhusisha Rais na zawadi ya KIPUUZI kama saa..."Huwezi kuita upuuzi habari inayohoji suala la msingi, ambapo logically, mfanyabiashara anaonekana akitoa zawadi kwa Rais (iwe saa au suti), kisha siku chache baadaye mfanyabiashara huyo anatangaza 'mradi wa utata'...Kwanini wananchi (waandishi wa gazeti hilo ni sehemu ya wananchi hao) wasihoji suala hilo ambalo mwandishi wa Ikulu anaona ni la kipuuzi?

Na kwa kinachoweza kuelezwa kama uhuni na si ubabaishaji, taarifa hiyo ya Ikulu imekwepa kabisa kuzungumzia maswali lukuki yanayoiandama kampuni inayomilikiwa na mfanyabiashara huyo, wasifu wa mfanyabiashara mwenyewe, sambamba na 'sintofahamu' lukuki kuhusu uwekezaji huo.

Kimsingi, habari Ikulu 'imejishtukia' tu inapodai "Ni habari ya uzushi na upuuzi. Ni habari inayolenga kumdhalilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete kwamba amepokea zawadi kutoka kwa mtu ambaye anajaribu kupewa kandarasi ya kujenga ya usafiri wa treni jijini DSM na ambaye pia anahusishwa kwenye shughuli nyingine za kibiashara zenye utata huko kwao Marekani."

Kwa wapambe hao wa Rais ni upuuzi na kumdhalilisha Rais kupokea zawadi kutoka kwa mtu ambaye WANAKIRI BAYANA kuwa anahusishwa na shughuli nyingine za kibiashara ZENYE UTATA huko Marekani. 

Kwanini taarifa hiyo isingewekeza nguvu katika 'kumsafisha' Rais kwa 'kujihusisha' na mtu huyo wanayekiri kuwa na shughuli zenye utata, badala ya kung'ang'ania hoja moja tu 'ya kipuuzi' kuhusu 'zawadi ya kipuuzi' ya saa?

Kilicho bayana ni kasumba iliyoota mizizi kwenye utawala wa Kikwete wa kudhani Watanzania wanaishi karne ya 18, hawana access na internet kufuatilia masuala mbalimbali yanayoihusu nchi yao, na hata wakifuatilia na kupatwa na hofu basi wakae kimya!

Suala la msingi si Rais kupewa zawadi, iwe ni Rolex au 'souvenir watch' nyingine, bali ni utata unaozunguka kampuni inayotaka kuwekeza katika mradi wa treni za kisasa, na inayomilikiwa na mtu ambaye anazungukwa na habari zenye utata, na ambaye alimzawadia Rais saa (iwe halisi au souvenir' tu) siku chache kabla ya kutangazwa taarifa za uwekezaji huo. Surely huu sio upuuzi bali ni kuihoji serikali yetu ambayo ina historia 'nzuri tu' ya kuingia mikataba ya 'ajabu ajabu' kama ule wa kitapeli wa Richmond.

Nihitimishe makala hii kwa kuwakumbusha wasaidizi wa Rais Kikwete kwamba Watanzania wana haki ya msingi kuuliza maswali kuhusu masuala yanayohusu taifa lao. Kadhalika, wanahabari wana haki ya kuhoji utata unapojitokeza katika mahusiano ya serikali au viongozi wake (hususan Rais) na watu au taasisi mbalimbali.

By the way, ajira ya mwandishi wa taarifa hiyo inategemea kumtetea bosi wake, na hakuna cha ajabu katika kujitokeza kwake kwa ukali kukanusha taarifa hiyo. Lakini kama wana ujasiri, basi wajibu maswali haya tuliyomuuliza mwekezaji huyo badala ya kung'ang'ania 'hoja ya kipuuzi ya "SIO ROLEX" au kutuhadaa kuwa "saa aliyopewa Rais Kikwete ni mali ya Watanzania" (mbona hawakutangaza kuwa Rais amekabidhiwa saa ambayo ni mali ya Watanzania hadi walipoona habari hiyo kwenye gazeti la Raia Mwema?)

Rais Kikwete amekuwa ajitianabaisha kama muumini wa dhana ya 'open goverment' inayopigia mstari haja ya wananchi kufahamu utendaji kazi wa serikali yao. Lakini wakati huohuo, wasaidizi wake huwa wakali kweli pindi wananchi wanapotaka kufuata dhana hiyo na kuhoji 'maswali magumu' kama hayo yanayouzunguka mradi wa treni za kisasa Dar.

Ni muhimu kwa watendaji wa serikali yetu kutambua kwamba Rais wanayemtumikia ni mwajiriwa wa Watanzania, na kila mwajiriwa anatambua haki ya mwajiri wake kuhoji masuala mbalimbali yanayomtatiza. Tanzania ni yetu sote na si ya kikundi kidogo cha miungu-watu wasiotaka kuuliza 'kulikoni?' hata katika masuala yanayohitaji 'akili ndogo' tu ya ku-Google kuhusu mtu au taasisi flani (kama ilivyo kwa ishu ya 'M/S Shumoja a.k.a Shumake Rails.'


20 Jan 2012


Dk Slaa: Kwa nini sikumsalimia JK 


Thursday, 19 January 2012 20:42
Fredy Azzah 
KATIBU Mkuu wa Chadema Dk Willibrod Slaa  amesema kuwa, hakuweza kusalimiana na Rais Jakaya Kikwete kutokana na Jiografia ya eneo la makaburini lilivyopangwa na watu wa usalama wa taifa pamoja na kamati ya mazishi kutomruhusu kufanya hivyo.

 
Hata hivyo Dk Slaa alisisitiza kuwa, kwa upande wake, kwenye msiba siyo sehemu ya kwenda kwa ajili ya kusalimiana na watu ama kurekebisha mambo yaliyoharibika bali ni sehemu ya kumwombea marehemu.

 “Siyo hulka ya Dk Slaa kutumia misiba kama sehemu ya kusalimiana, wala kutengeza mambo yaliyoharibika, mimi huwa naenda kwenye msiba kwa lengo moja tu la kumwombea marehemu, huwa simtazami hata mtu aliyekaa pembeni yangu,” alisema Dk Slaa alipozungumza kwa njia ya simu  jana.  

Alifafanua kuwa, katika eneo la makaburi kulikuwa na mabanda matano ambayo yalipangwa kwa ajili ya Askofu, Rais, Viongozi wa vyama vya siasa, mwili wa marehemu  na familia na banda jingine lilikuwa la watu wengine waliohudhuria mazishi hayo. 

“Sasa kutoka alipokuwa amekaa Rais mpaka kwenye banda nilipokuwa mimi, kulikuwa na umbali wa karibu  mita 20, sasa mlitaka nikimbie kumsalimia Rais nivunje protokali kisha nikamatwe na usalama wa taifa,” alisema Dk Slaa. Alisema alikuwa mtu wa kwanza kufika makaburini kwa lengo la kuangalia jinsi kaburi la mbunge wa chama chake lilivyochimbwa kisha akaonyeshwa sehemu ya kukaa na watu wa usalama wa taifa.

 Alisema kuwa, hata katika wakati wa kuaga mwili wa Marehemu Regia Mtema, katika ukumbi wa Karejee, kulikuwa na utaratibu kama huo ambapo ilitengwa sehemu ya kukaa Makamu wa Rais, Spika wa Bunge, Kiongozi wa Kambi ya Upinzani na Makamu wake na yeye Dk Slaa akawekewa sehemu yake kama Katibu wa Chama alichokuwa akikitumika marehemu.

 “Mimi sipendi kuweka siasa kwenye mambo kama ya msiba, Dk Slaa siyo kichaa siyo kichaa aanze kukimbia kumsalimia Rais. Katika sehemu kama ile Rais huwa anakuja baada ya watu wote wakiwa wameshakaa, yeye ndiye hupita na kuanza kusalimia watu na hamjaona hata sehemu moja aliponyoosha mkono kunisalimia nikamkwepa,” alisema Dk Slaa:

 “Msiba siyo mahali pa kutengeza urafiki, au kutengeza mambo yaliyo haribika, pale ni ibada tu na kumuombea marehemu siyo sehemu ya kufanya siasa” alisisitiza Dk Slaa. Jana baadhi ya vyombo vya habari viliripoti kuwa, Dk Slaa alishindwa kusalimiana na Rais Jakaya Kikwete katika mazishi ya Regia Mtema yaliyofanyika kijijini kwao Ipangalala Morogoro juzi.Regia alifariki dunia Januari 14 kwa ajali ya gari iliyotokea katika eneo la Ruvu mkoani Pwani.  


CHANZO: Mwananchi

8 Jun 2011






Mafisadi CCM wageuka mbogo

Na Jabir Idrissa - Imechapwa 01 June 2011

SASA ni piga ni kupige ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM). Wanaotuhumiwa kwa ufisadi, wanakataa kujiuzulu, MwanaHALISI limeelezwa.

Taarifa zinasema walipoitwa mbele ya viongozi wakuu wa chama hicho – makamu mwenyekiti Pius Msekwa na katibu mkuu, Wilson Mukama - wanaoitwa na CCM kuwa “watuhumiwa wakuu wa ufisadi nchini,” walishikilia msimamo kuwa hawawezi kujiuzulu kwa kuwa hawana hatia.

Wanaotakiwa kujiuzulu na viongozi wakuu wa CCM ni Edward Lowassa, Rostam Aziz na Andrew Chenge. Mkutano wa kuwashawishi wajiuzulu, ulifanyika Alhamisi na Ijumaa wiki iliyopita katika ofisi ndogo za chama hicho zilizopo Lumumba, Dar es Salaam.
Taarifa zinasema katika mkutano huo, Msekwa na Mukama waliomba Lowasa ajiuzulu ili kukiokoa chama hicho, lakini yeye alipinga kwa hoja kuwa hana hatia.

MwanaHALISI lilipowasiliana na Msekwa kutaka kufahamu kilichojadiliwa katika mkutano wake na viongozi hao, haraka alisema, “…Umetoa wapi habari hizo?”

Alipoelewa ni vyanzo vya ndani ya chama na serikali, Msekwa alisema, “Hayo ni mambo ya ndani ya chama. Hatuwezi kuyaleta magazetini.”
Lowassa alipoulizwa juu ya kuwapo kwa kikao hicho, alisema ni kweli wamekutana. Hata hivyo, alisema hawezi kueleza walichojadili kwenye vyombo vya habari.

Rostam hakupatikana kueleza upande wake. Hata hivyo, MwanaHALISI limeelezwa na mtoa taarifa wake kuwa mbunge huyo wa Ingunga alitoka kwenye ukumbi wa mkutano akiwa amenuna na kuvurumisha “maneno makali.”

Anasema Rostam alitoka pale akiwa amenuna na kusema yeye hana hatia yoyote na kwa hiyo hastahili kushambuliwa. Amesema yote yanayotokea sasa yanatokana na uadui wa siasa za urais wa mwaka 2005 na ule wa 2015.


Hili linatokea wakati uongozi wa juu wa chama hicho ukishindwa kukabidhi barua ya kuwataka watuhumiwa hao wajiuzulu.
Kuchelewa kwa utekelezaji wa maazimio ya kuwawajibisha Lowassa, Rostam na Chenge kumezaa majungu na umbeya. Hivi sasa taarifa zinasema, Mukama anadaiwa kugoma kuandika barua ya kuwataka watuhumiwa hao kuachia nafasi zao za ujumbe wa Halmashauri Kuu ya taifa (NEC) wanazozishikilia.

Baada ya Mukama kugoma kuandika barua hizo kwa hoja kuwa kilichoamuriwa na NEC hakifahamu kwa kuwa alikuwa hajateuliwa, ndipo Nape Nnauye, katibu wa itikadi na uenezi alipoandika barua hizo na kuzipeleka kwa Msekwa.

Naye Msekwa alizipokea barua na kuzirekebisha. Akazirejesha kwa Nape ili azipeleke kwa Mukama kuzisaini. Mukama akagoma. Zikapelekwa kwa mwenyekiti wa chama hicho, Rais Jakaya Kikwete, ambaye taarifa zinasema, “amezifungia kabatini.”

Kwa mujibu wa taarifa za ndani ya kikao hicho, Lowassa alifika Lumumba saa nne asubuhi. Mazungumzo kati yake, Msekwa na Mukama inakadiriwa yalichukua takribani saa moja.

Katika mazungumzo hayo, Msekwa ananukuliwa akimweleza Lowassa “unatakiwa ujiuzulu nyadhifa zako za uongozi katika chama ili kutekeleza maagizo ya NEC na falsafa ya chama ya kujivua gamba.”

Akijibu hoja hiyo, mtoa taarifa anasema Lowassa alijibu, “Kuhusu Richmond (kampuni feki ya kufua umeme wa dahurula), ukweli unafahamika…Katika hili, mimi sina makosa. Rais anafahamu hilo na kila mmoja anajua hivyo.”

Anasema Lowassa alisema kama kuwajibika kwa makosa yaliyotokana na Richmond tayari amefanya hivyo kwa niaba ya chama chake na serikali pale alipoamua kujiuzulu wadhifa wake wa uwaziri mkuu.
Anasema mbali na kueleza hilo, Lowassa alisikika akisema, “nilikutana na Rais Kikwete. Aliyonieleza si haya.”

Alisema Rais Kikwete alimweleza kuwa hakuna maazimio yoyote ya NEC yaliyomtaka kujiuzulu. Akahoji, “Sasa nimwamini nani, ninyi mnaotaka nijiuzulu au rais aliyesema hakuna azimio kama hilo?”

Habari zinasema mara baada ya Lowassa kuwaeleza viongozi wake msimamo juu ya mazungumzo yake na Kikwete, ndipo Msekwa aliposikika akisema, “Lowassa acha mbio za urais.”

Naye Lowassa hakumkawiza Msekwa. Alijibu, “Lini nimetangaza kugombea urais? Lakini hata kama ninataka kufanya hivyo, ni haramu kugombea nafasi hiyo? Je, kuna mliowaandaa?”

Ni kauli hiyo ya Lowassa, iliyomshutua Msekwa na kusema, “Hapana. Hapana. Hakuna tuliyemuandaa…Haya mambo ya urais yatatuvuruga.”
Akihitimisha hoja zake kabla ya kumalizika kwa mkutano huo, mtoa taarifa anasema Lowassa alikitaka chama chake kuisaidia serikali kutekeleza wajibu wake kwa wananchi, badala ya kufanyia kazi kile alichoita, “majungu ya wanasiasa.”

Naye Chenge taarifa zinasema aliwaambia viongozi aliokutana nao kuwa yeye si fisadi na hafahamu maana ya ufisadi. Akataka kama tuhuma wanazomtuhumu wanaweza kuzithibitisha wamfikishe mahakamani ili aweze kujitetea. Hakuna maelezo ya ziada.

Hata hivyo, watu waliokaribu na kiongozi huyo wanasema, Chenge amejipanga kuhakisha kwamba hang’oki katika kiti chake cha NEC; ikibidi kuondolewa kwa nguvu ametishia kuondoka CCM na kujiunga na upinzani.

Kwa upande wa Rostam Aziz, taarifa zinasema alitakiwa kujiuzulu ujumbe wa NEC kwa tuhuma za kuingiza nchini kampuni feki ya Richmond na baadaye Dowans.

Mtoa taarifa anasema, mara baada ya kuelezwa tuhuma hizo, Rostam alihoji, “Haya ni maamuzi ya NEC?” Naye Msekwa akajibu, “NEC imetaka chama kijivue gamba kuanzia ngazi ya taifa hadi chini kwa kuondoa watu wote wanaotuhumiwa ufisadi.”

Habari zinasema, katika mazungumzo kati ya viongozi hao na Rostam, hakuna mahali popote ambapo Msekwa na Mukama walitaja ushiriki wa mbunge huyo wa Igunga, katika wizi wa fedha za umma kupitia kampuni ya Kagoda Agriculture Limited.

Kampuni ya Kagoda ni miongoni mwa makampuni 22 yaliyothibitika kuchota mabilioni ya shilingi kwenye akaunti ya madeni ya nje (EPA) ndani ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Gazeti hili limeshindwa kufahamu mara moja kilichosababisha Msekwa na wenzake kushindwa kumweleza Rostam ushiriki wake katika Kagoda. Hata hivyo, kwa zaidi ya miaka minne sasa, CCM imekuwa ikituhumiwa kunufaika na fedha za EPA hasa Sh. 40 bilioni zilizoibwa na Kagoda.

Wakati suala hilo likichukua sura hiyo, taarifa zilizofikia gazeti hili zinasema baadhi ya vigogo wa chama hicho wamepanga kupeleka hoja katika vikao vijavyo vya (CC) na (NEC) kushinikiza kufukuzwa ndani ya chama hicho wanaoitwa, “wasaliti ndani ya chama.”

Wanaopangiwa mkakati wa kufukuzwa ni spika wa zamani wa Bunge, Samwel Sitta na mbunge wa Kyela, Dk. Harrison Mwakyembe wanaotuhumiwa kuanzisha Chama cha Jamii (CCJ) wakati wakiwa bado wanachama na viongozi wa CCM.

Wengine ni Nape Nnauye, Victor Mwambalaswa na Daniel Porokwa.
Habari kutoka ndani ya CCM zinawanukuu makada mawili; rais mstaafu, na mjumbe mmoja wa NEC wakitaka chama chao kuwafukuza waasisi wa CCJ kwa kukosa uaminifu.

MwanaHALISI limeelezwa na aliyekuwa naibu katibu mkuu wa CCJ, Dickson Ng’hily kwamba Sitta na Mwakyembe waliokuwa waanzilishi wa chama hicho, walimkatiza masomo yake nchini Afrika Kusini ili kusaidia kupatikana usajili wa chama hicho.

Ng’hily ambaye mahojiano yake yatachapishwa kikamilifu katika toleo lijalo amesema, aliyemwingiza yeye CCJ ni Sitta na Dk. Mwakyembe na anasikitishwa na hatua ya viongozi hao kutaka kuficha ukweli.

“Hawa watu ndio waanzilishi hasa wa CCJ. Mimi na Makonda tulipewa jukumu la kutafuta usajili wa chama. Lakini naona wenzangu wameamua kuficha ukweli kwa maslahi binafsi. Hii si sahihi,” ameeleza.

Ng’hily anaonyesha nyaraka za muhtasari wa vikao walivyoshiriki viongozi wakuu wa CHADEMA, John Mnyika, Anthony Komu na Tundu Lissu kuwa ni miongoni mwa watu walioshiriki katika majadiliano ya kuunganisha nguvu kati ya CCJ ya Sitta na CHADEMA.

“Tulikubaliana kama CCJ itakosa usajili, basi mheshimiwa Sitta atagombvea urais kupitia CHADEMA. Lakini kama tutafanikiwa kusajili chama chetu, basi Sitta angegombea urais kupitia CCJ na CHADEMA wangetuunga mkono,” anaeleza Ng’hily.

Kuibuka kwa Ng’hily kuelezea ushiriki wa Sitta na Dk. Mwakyembe katika kuanzisha na kusimamia usajili wa CCJ kumekuja wiki tatu baada ya Fred Mpendazoe kumtaja Nape Nnauye kuwa ni miongoni mwa waanzilishi wa kwanza wa CCJ.

Mpendazoe aliuambia mkutano mkubwa wa hadhara mjini Njombe kuwa yeye, Sitta na Mwakyembe ndio walianzisha CCJ; bali yeye alitangulia kutoka CCM ili kurahisisha usajili wa chama hicho. Wenzake walikuwa wamfuate baadaye.

CHANZO: Mwanahalisi

4 Apr 2011


Magufuli atamba mbele ya Rais
• Atoa onyo la bomoabomoa kwa wakazi Dar

na Bakari Kimwanga

SIKU chache baada ya Rais Jakaya Kikwete kumtaka Waziri wa Ujenzi, John Magufuli, aache ubabe katika kutekeleza zoezi la bomoabomoa, jana waziri huyo alitoa onyo mbele yake akiwataka wakazi wa Tegeta jijini Dar es Salaam hasa waliokuwa katika hifadhi ya barabara ya Mwenge hadi Tegeta, wahame wenyewe kabla hajachukua hatua za kuwaondoa kwa nguvu.

Magufuli aliyasema hayo jijini Dar es Salaam jana huku Rais Kikwete mwenyewe akiwa pembeni yake, wakati wa sherehe za uzinduzi wa mradi wa upanuzi wa barabara hiyo yenye urefu wa kilometa 12.9 inayojengwa kwa msaada wa serikali ya Japan kupitia shirika lake la maendeo (JICA).

Waziri huyo makeke alisema katu hataacha kusimamia sheria namba 18 ya mwaka 2007 ambayo ilisainiwa na Rais mwenyewe ambayo inakataza watu kuingilia eneo la hifadhi ya barabara kwa kujenga makazi au kufanya biashara.

“Mheshiwa Rais, hata wakileta malalamiko kwako usiwasikilize, kwani sheria namba 18 uliyoisaini inakataza….naahidi kuisimamia na kuwepo kwa Makatapila katika eneo la Tegeta sasa ni ishara tosha kwa wakazi waliovamia hifadhi ya barabara kuondoka wenyewe kabla sijaanza kuwaondoa kwa nguvu!”

“Mradi huu utachukua miezi 27 kuanzia mwezi Februari na unatarajiwa kukamilika Mei, 2013 na utagharimu shilingi bilioni 88 na fedha zote ni msaada toka serikali ya Japan,” alisema Magufuli.

Barabara hiyo inapanuliwa kwa kiwango cha lami na itakuwa na njia nne na vituo rasmi vya mabasi 22.

Aidha, alieleza kuwa hatua ya Rais Kikwete kumteua kushika wadhifa huo ni msukumo tosha kwa yeye na wasaidizi wake kuhakikisha wanasimamia sheria na ikiwa kutatokea utata Naibu Waziri wake, Harrison Mwakyembe, kwa kushirikiana na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Hebert Mrango, wanaweza kuutatua kwani wao ni wanasheria kitaaluma.

Awali akizindua mradi huo, Rais Kikwete aliiagiza wizara hiyo kukishughulikia mara moja kile alichokiita “genge la watu waliojipanga kuidhulumu serikali na wananchi” kwa kuwalipa mabilioni ya fedha makandarasi ambao ujenzi wao wa barabara ni wa kiwango hafifu na cha chini.

Pia aliiagiza Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kuacha mara moja kugawa maeneo ya wazi na badala yake iyasimamie ipasavyo maeneo hayo yakiwamo yale ya watoto kuchezea kwa kuzuia kabisa ujenzi katika maeneo hayo.

Hata hivyo agizo hilo la Rais Kikwete linaonekana limechelewa sana kwani tayari kuna tuhuma na malalamiko mengi yanayoonyesha kuwa tayari maeneo mengi ya wazi yamekwishagawiwa kwa watu binafsi wenye uwezo kinyume cha taratibu, huku ikielezwa kuwa wahusika bado hawajachukuliwa hatua.

“Tumejitahidi kupandisha bajeti ya barabara mwaka 2006; ilikuwa bilioni 470 na hivi sasa tumepanda hadi trilioni 1.3 ili kuimarisha miundombinu ya barabara za ndani.”

“Wizara na Tanroads sasa msifanye malipo kwa watu ambao ujenzi wao ni wa kiwango cha chini na msipokee barabara ambayo iko chini ya kiwango ili kuongeza ufanisi wa barabara zetu jamani,” alisema Rais Kikwete.

Alisema kukamilika kwa upanuzi wa barabara ya Mwenge hadi Tegeta kutapunguza msongamano jiji la Dar es Salaam ambao kila mara umekuwa ukisumbua wakazi wa jiji.




5 Mar 2011


Tunaposema kuna ombwe la uongozi kwenye Serikali ya Rais Jakaya Kikwete baadhi ya vichwa panzi wanatuita wachochezi.Sasa unapoona Waziri anauchapa usingizi kwenye mkutano wa kimataifa,huku bosi wake akiwa kando,basi sijui tusemeje!!!

Na tunaposema Kikwete ni kiongozi dhaifu sio kama ni uchochezi,majungu au chuki binafsi.Hivi kama Rais anashindwa kumkemea Waziri wake kwa kulala kwenye mkutano tunaoambiwa una umuhimu mkubwa kwa nchi yetu (hadi imelazimu mkuu wa nchi aende mwenyewe badala ya kuwakilishwa na Makamu wake,Waziri Mkuu au Waziri wa Nishati na Madini)atamudu vipi kukemea wabaka uchumi ambao baadhi yao ni watu wake wa karibu waliochangia harakati zake za kuukwaa Urais?

Na kuna umuhimu gani kwa fedha ya walipa kodi kugharamia safari ya Ngeleja ambaye anaishia kulala mkutanoni badala ya kutuwakilisha?Au Kikwete amelazimika kwenda mwenyewe badala ya kumwacha Ngeleja pekee kwa vile alijua kuwa waziri wake huyo ataishia kuuchapa usingizi mkutanoni?

Kutegemea watu wa aina hii wanaweza kumsaidia Mtanzania kuondokana na umasikini wa kutupa ni sawa na kutegemea kugema damu kwenye jiwe.Na ukiona waziri mzima pasi haya anachapa usingizi huku Rais wake akiwa kando basi ujue wazi kuwa si akina Richmond na Dowans tu waliomudu kutuingiza mkenge bali tutarajie mengi zaidi.Unadhani kama Ngeleja anathubutu kuuchapa usingizi katika mkutano wa kimataifa unaouhusu maslahi ya nchi,hali inakuwaje wakati anashughulikia maslahi ya nchi ofisini mwake?Sintoshangaa kusikia kuna mikataba ya kuhamisha madini yetu ikisainiwa huku waziri yuko fofofo usingizini

Au Ngeleja ameanzisha mashindano ya kuchapa usingizi dhidi ya Mbunge wa CCM Kapteni John Komba,ambaye kama inavyoonekana pichani chini,alifumwa akiwakilisha wapiga kura wa jimbo lake kwa kuchapa usingizi Bungeni Dodoma



Picha kwa hisani ya Jamii Forums

24 Feb 2011


Katika harakati zake duni za kujinasua uhusika wake katika suala la ujambazi wa Dowans,Rais Jakaya Kikwete alijaribu kuwahadaa Watanzania kwa kudai,pamoja na mambo mengine,kuwa "hawajui wamiliki wa Dowans".

Na kwa bahati nzuri kwake,vyombo vyetu vya habari vikaishia kumnukuu tu.Lakini kwa minajili ya kufupisha makala hii(na kupunguza maumivu yanayotokanayo) tuweke kando kuangalia namna Kikwete alivyotengeneza mazingira ya ujio wa Dowans kupitia majambazi wengine wa Richmond.Hapa namaanisha kauli yake kuwa tatizo la umeme lingekuwa historia baada ya ujio wa mitambo ya kuzalisha umeme kutoka Marekani (na tukaishia kuletewa mitambo garasa)

Hatimaye mwarabu Adawi aliyekimbia ukombozi wa Mzanzibari,amediriki kuja na kutufanyia kila aina ya vituko (kukataa kupigwa picha,nk) na kutangaza hadharani kuwa yeye ndio mmiliki wa Dowans.Na kama kututukana Watanzania,akadai kuwa anaweza kuangalia uwezekano wa kupunguza FIDIA ANAYOPASWA KULIPWA KWA KUTUIBIA (yale yale ya vibaka wanaomkaba mtu kisha kumpigia ukelele wa "mwizi,mwizi...")

Adawi ambaye Kikwete anadai hamjui (japo anamjua sana kwani wana mahusiano ya "kifamilia")ameweza kutia mguu Ikulu na kuongea na Makamu wa Rais Gharib Bilali (anayekaimu urais katika kipindi hiki ambacho Kikwete yuko kwenye mizunguko yake).

Japo tunajua kuwa Ikulu yetu imegeuzwa kijiwe cha mafisadi ambao wana uhuru wa kutembelea mahala hapo patakatifu kila wanapojisikia lakini kwa Adawi kupewa nafasi ya kukutana na Rais (kwa maana ya anayekaimu nafasi hiyo),na mkutano huo kufanywa siri,inaashiria kuwa Kikwete na serikali yake sio tu anamjua Adawi bali pia anamtumikia.

Sintashangaa kusikia kuwa Kikwete aliamua kwenda Mauritania ili kumwezesha Adawi afanye uhuni wake kisha ahitimishe ziara yake kwa maongezi na kaimu wa Kikwete (Gharib Bilali).Na sintoshangaa kusikia kwamba kabla ya kurejea Tanzania,maswahiba hao wawili (Kikwete na Adawi) wakakutana faragha kujadili kuendeleza ujambazi wa Dowans.

Na hata tukiweka kando ujio wa Adawi,kauli ya Kikwete kuwa hawajui wamiliki wa Dowans ilhali majina ya wamiliki hao yapo BRELA (na Waziri Ngeleja alishayaweka hadharani kabla Kikwete hajatoa utetezi wake feki) inatosha kuwafahamisha Watanzania kuwa Rais wao ameshindwa kazi.How come Waziri ajue kile ambacho Rais hakijui?Je kama anashindwa kujua jambo dogo tu kama rekodi ndogo tu iliyopo BRELA atawezaje kujua na hatimaye kushughulikia matatizo ya Watanzania takriban milioni 50?

Tusipofumbuka macho kama wenzetu wa Tunisia,Misri,Libya na kwingineko wanakopambana na tawala dhalimu tunaweza kuishia kuwa koloni la Adawi,yaani mwarabu huyo kuongoza nchi yetu kwa kutumia remote control in the form of Kikwete.

24 Dec 2010


Majuzi,msomaji mmoja wa blogu hii alinitumia maoni ambapo pamoja na mambo mengine aliashiria kuwa nina chuki dhidi ya Rais Jakaya Kikwete.Msomaji huyo aliyejitambulisha kuwa mkazi wa hapa Glasgow alidai (namnukuu) "...I know you hate JK because whatever happens to him you have a negative view, even a tyre puncture...",yaani kwa Kiswahili,"najua unamchukia JK kwa vile chochote kinachotokea kwake wewe una mtizamo hasi,hata pancha ya tairi".Hii ndio mitizamo ya Watanzania wenzetu ambao licha ya kubahatika kuwa nje ya nchi,hususan nchi zilizoendelea kama hapa Uingereza,bado wana mitizamo mgando ambayo kwa kiasi kikubwa imechangia kutufanya hata miaka 49 baada ya uhuru kutamani mkoloni arejee.

Yah,huwezi kuwalaumu wanaotama mkoloni arejee japo mie si mmoja wao.Hivi tunawezaje kuelezea namna Watanzania wanavypelekeshwa kama watoto wadogo tena yatima siku chache tu baada ya Kikwete na CCM yake kupita huku na kule kuahidi neema,only for madudu and more madudu kuibuka kila kukicha?Unajua,angalau mkoloni alipotupelekesha alikuwa na excuse (japo isiyokubalika) kwamba yeye hakuwa Mtanganyika,na hakuwa na uchungu na nchi yetu.Na kwa wanaokumbuka vizuri somo la historia wanafahamu bayana kuwa ujio wa mkoloni ulikuwa kwa minajili ya kuendeleza nchi zao za asili,yaani kukwapua raslimali zetu kwa ajili ya viwanda vyao,kupata masoko ya bidhaa zao na eneo la makazi kwa nguvukazi ya ziada katika nchi hizo za wakoloni.Sasa ondoa neno mkoloni kisha weka neno FISADI,na yayumkinika kuhitimisha kuwa angalau mkoloni alikuwa na ajenda ya maendeleo huko kwao japo at our expense.Mafisadi nao wana ajenda za maendeleo pia,ila ni katika kutunisha akaunti zao kwenye mabenki ya hukohuko kwa wakoloni,kuongeza idadi ya nyumba ndogo zao (isomeke ufuska au uzinzi),kuongeza idadi ya mahekalu yao na magari ya kifahari,na sasa ajenda mpya ya kuimarisha himaya zao kwa kutumbukiza kila mwanafamilia na ndugu wa karibu kwenye siasa ili pindi baba akiondoka madarakani basi mwana amrithi kuzuia uwezekano wa baba mtu kukaliwa kooni kwa madudu aliyofanya akiwa madarakani.

Nimelazimika kuandika makala hii sio kwa minajili ya kumjibu huyo msomaji wangu wa hapa Glasgow bali ni baada ya kusoma toleo la mtandaoni la gazeti la Mwananchi ambapo kuna habari kuwa Tanesco wametangaza tena mgao wa umeme nchi nzima.Hivi sio majuzi tu shirika hilo lilitangaza mwisho wa mgao wa umeme?Tuwe wakweli,hivi uhuni huu wa Tanesco,ambao mie natafsiri kuwa ni uhuni wa serikali iliyopo madarakani,utaendelea hadi lini?So far,hakuna taarifa za wazi kuhusu athari za mgao wa umeme lakini haihitaji sayansi ya roketi au dissertation ya quantum physics kumaizi kwamba mgao huo una madhara makubwa mno kwa uchumi wa taifa na kwa maisha ya walalahoi kwa ujumla (vigogo licha ya kunufaika na ufisadi unaowawezesha kuuza jenereta kila mgao unapotangazwa lakini pia hawaathiriki kwa vile majumbani na maofisini kwao kuna jenereta zinazoendeshwa na fedha za kodi za walalahoi).

Hatuwezi kuilaumu Tanesco pekee kuhusiana na uhuni huu kwani ni siri ya wazi kuwa shirika hilo na sekta ya nishati kwa ujumla vimegeuzwa kitegauchumi kizuri kwa mafisadi.Majuzi tu tumesikia majambazi wa Richmond wakijiandaa kurejeshewa fedha walizotuibia ambapo watalipwa fidia ya mabilioni kwa mgongo wa binamu zao wa Dowans.Hatuwezi kumwepusha Kikwete na CCM yake na ufisadi huu kwa vile licha ya madudu hayo kushika hatamu wakati wa utawala wake,sasa tunafahamu kuwa amekuwa akiwakingia kifua mafisadi wasichukuliwe hatua za kisheria (thanks to nyaraka za siri za kidiplomasia zilizovujishwa na mtandao wa WikiLeaks).Kwa wale ambao hawajabahatika kusoma habari hizo,kuna nyaraka kutoka ubalozi wa Marekani hapo Dar zilizobeba maongezi kati ya bosi wa Takukuru Edward Hoseah na afisa ubalozi wa Marekani ambapo Hoseah alinukuliwa akieleza bayana kwamba Kikwete alishinikiza baadhi ya mafisadi wasichukuliwe hatua.Japo bosi huyo wa Takukuru amejaribu kuruka kimanga na kukana tuhuma hizo,kila mwenye akili timamu anafahamu kuwa ufisadi unashamiri Tanzania kwa vile Kikwete ameshindwa kuwachukulia hatua mafisadi papa licha ya madaraka lukuki aliyorundikiwa na Katiba.

Baadhi yetu tuliwaasa Watanzania wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu uliopita majuzi kwamba kuirejesha tena madarakani serikali ya Kikwete ni sawa na kumwaga chumvi kwenye kidonda kibichi,na matokeo yake ndio haya.Wakati tunaelekea mwezi wa pili tangu Kikwete atangazwe mshindi,hakuna lolote la maana lililokwishafanyika kuashiria kuwa kiongozi huyo ana ajenda mpya tofauti na zile zilizotawala miaka mitano iliyopita,kubwa ikiwa na kushamiri kwa ufisadi na uimarishaji himaya za mafisadi huko nyumbani.

Sawa,makosa yameshafanyika kwa kumrejesha Kikwete na CCM yake madarakani lakini hiyo isiwe sababu ya kuendelea kunung'unika kimoyomoyo huku nchi yetu ikizidi kuteketea.Umefika wakati Watanzania wasikubali kupelekeshwa namna hii.Kwanini Kikwete asibanwe kuhusu tatizo la umeme licha ya ahadi zake za mara kwa mara kuwa tatizo hilo lingekuwa historia?Au alimaanisha kuwa tatizo hilo litaendelea kuwa la kihistoria?

Nimesikia taarifa za mpango wa Chadema kuandaa maandamano ya nchi nzima kupinga kuongezwa bei ya umeme.Yaani licha ya mgao wa kila kukicha bado Tanesco wanataka kuongeza bei?Yayumkinika kuhisi kuwa wazo hilo la ongezeko la bei ya umeme ni la kifisadi lenye lengo la kupata fedha za kuwafidia mafisadi wa Richmond/Dowans.Ni muhimu kwa kila Mtanzania mzalendo kuunga mkono mpango huo wa maandamano ya amani ili kufikisha ujumbe kwa Kikwete na serikali yake kuwa Watanzania wamechoka kupelekeshwa.Hata hivyo,kama maandamano ya kuwapongeza wabunge wa upinzani yalizuiliwa na polisi,sidhani kama serikali itaridhia maandamano hayo ya kupinga ongezeko la bei ya umeme.

Mwisho,tuna choices mbili tu:kuchukua hatua sasa kabla hatujafika mahala ambapo hata tukichukua hatua itakuwa sawa na kutwanga maji kwenye gunia,au tusubiri kusoma rambirambi kuhusu nchi yetu hapo 2015.

5 Sept 2010


Inaudhi na kukasirisha kuona gazeti la serikali,Habari Leo,likijipachika jukumu la kumuua kisiasa mgombea wa Chadema Dokta Wilbroad Slaa kama ambavyo imekuwa ikifanywa na magazeti ya Habari Corporation na Changamoto,na mengineyo yanayofadhiliwa na mafisadi.

Gazeti hilo limeandika kwa kirefu kuhusu anayedaiwa kuwa mume wa mwenza wa sasa wa Dkt Slaa,Josephine Mushumbusi.Ungetegemea gazeti hilo linaloendeshwa kwa fedha za walipa kodi wa Kitanzania pasipo kujali itikadi zao za kisiasa,lingetafakari kwa makini madhara ya habari hiyo.Wanajua sana wanachofanya,na yayumkinika kuamini kuwa serikali inayoongozwa na mgombea wa CCM,Jakaya Kikwete,imeridhia uchapishaji wa habari za aina hiyo.

Kuna msemo wa busara unaoasa "WANAOISHI KWENYE NYUMBA ZA VIOO WASIRUSHE MAWE".Mantiki ya msemo huo ni kwamba kama una wasifu wenye mawaa ya aina moja au nyingine then si wazo jema kuwachafua watu wengine.Wengi wetu tunafahamu "ishu binafsi" za viongozi wa CCM ikiwa ni pamoja na Kikwete mwenyewe.Hazizungumzwi hadharani kwa kuwatunzia heshima viongozi hao lakini inaelekea katika kutapatapa kwao baada ya kugundua hawamwezi Dokta Slaa kwa hoja,wameamua kuhamia kwenye character assassination.

Majukwaani,Kikwete na CCM yake wanajifanya kuhubiri umuhimu wa kampeni za kistaarabu lakini pembeni wanaruhusu raslimali za umma zitumike kumchafua Dokta Slaa.Kikwete alichukua hatua za haraka pale mtandao maarufu wa Ze Utamu ulipochapisha picha zinazomhusu lakini anaruhusu gazeti la serikali litumike kumwandama Dkt Slaa.

Na kwa kuonyesha unazi,kuna mahala katika habari hiyo ambapo pasi aibu wameandika (nanukuu) "Na wakati Mahimbo akiwa njia panda akishindwa kujua hatima ya ndoa yake, Dk. Slaa, Padri msomi `amelitangazia’ taifa mbele ya mikutano ya kampeni ya chama chake cha Chadema kuwa Josephine ndiye mke wake mtarajiwa..." 

Hivi Mhariri wa Habari Leo hafahamu kuwa Dkt Slaa sio Padri bali aliwahi kushika nafasi hiyo na kuiacha?

Blogu hii inamshauri Kikwete akemee mkakati huu mufilisi wa character assassination.Wengi wanafahamu kwa undani maisha ya Kikwete tangu akiwa Waziri,na wanajua vema maisha yake binafsi ndani na nje ya nchi.Asijivunie vyombo vya dola kumlinda pindi kibao kitapogeuzwa upande wake.Ni bora Dokta Slaa anayetangaza hadharani kuhusu uhusiano wake na Josephine kuliko kashfa lukuki zinazohifadhiwa kuhusu viongozi wa CCM kwa vile tu tunawaheshimu na tuna mambo muhimu zaidi ya kuzungumzia kuliko maisha binafsi ya viongozi wetu.

I repeat: Those who live in glass houses shouldn't throw stones!!!



22 Aug 2006

KULIKONI UGHAIBUNI-21

Asalam aleykum,

Leo nina jambo muhimu sana kuhusiana na maslahi ya Taifa letu.Nawaomba wasomaji wapendwa tuwe pamoja kwa makini ili tusipoteane njiani na hatimaye kuleta tafsiri potofu ya ninachotaka kuzunguzia.Natanguliza rai-au niite tahadhari-kwa vile mada yangu ya leo ni nyeti,na ni kuhusu suala ambalo mara nyingi limekuwa likikwepwa na watu wengi.Lakini kabla sijaingia kwa undani,nielezee uzoefu wangu mimi mwenyewe katika suala hilo.

Kwa wafuatiliaji wa makala hii watatambua kwamba mara zote huwa naanza na asalam aleykum.Nimezowea sana kuwasalimia ndugu zangu kwa namna hiyo.Pengine ni kwa vile nimewahi kukaa miji ambayo salamu hiyo inatumika sana,au pengine wengi wa marafiki zangu ni Waislam.Robo ya elimu yangu ya msingi niliipata mkoani Kigoma katika kitongoji cha Ujiji.Nakumbuka kuna wakati flani katika darasa nililokuwa nasoma tulikuwa Wakristo watatu tu na waliosalia (nadhani zaidi ya silimia 90) walikuwa Waislam.Niliwahi kufundisha sekondari flani mjini Tanga na takribani robo tatu ya wanafunzi wangu walikuwa Waislam pia.Na nikipiga hesabu ya harakaharaka,katika marafiki zangu kumi bora saba ni Waislam.Hata siku moja,tangu nikiwa Kigoma,Tanga,Dar na kwengineko sikuwahi kujiona nimezungukwa na watu tofauti nami ambaye ni Mkristo Mkatoliki.Wanafunzi wenzangu,wanafunzi niliowafundisha na marafiki zangu walinichukulia kama Mtanzania mwenzao japo tulikuwa tunatoka madhehebu tofauti.Na hivi karibuni nilipokuja huko nyumbani kwa utafiti wa PhD nayosoma,wengi wa niliohojiana nao walikuwa Waislam.Sikuwahi kupata matatizo yoyote hata pale nilipokutana na wanaoitwa mujahidina.Katika levo ya familia,kaka-binamu yangu mmoja ambaye ni Mkatoliki wa kwenda kanisani kila Jumapili ana mke ambaye ni Mwislam wa swala tano.Uzoefu wangu huo mdogo unatoa picha moja muhimu:Watanzania tumekuwa tukijichanganya sana bila kujali tofauti zetu za kidini.Nikisema kujichanganya namaanisha kujumuika pamoja na sio vinginevyo.

Kuanzia kwenye miaka ya 80 kulianza kujitokeza dalili zilizoashiria kwamba mambo si shwari sana katika eneo la dini nchini.Tunakumbuka uvunjaji wa mabucha ya nguruwe,matukio kwenye msikiti wa Mwembechai,mihadhara ya kidini,suala la Ustaadh Dibagula na mengineyo.Wapo waliosema kwamba kulikuwa na kikundi cha watu wachache kilichokuwa kinachochea vurugu za kidini kuganga njaa zao.Wapo pia waliokuwa wanadai kuwa vurugu za kidini zilikuwa na sura ya kisiasa huku mara kadhaa chama cha CUF kikibebeshwa lawama.Yayumkinika kusema kuwa japo viongozi wetu walikuwa wakikemea vurugu hizo hakukuwa na jitihada za makusudi za kubaini chanzo hasa ni nini.Wanataaluma wetu nao kwa namna flani wamekuwa wakilikwepa suala hili pengine kwa vile linagusa hisia za wengi au pengine kutokana na hisia kwamba matokeo ya tafiti zinahusu migogoro ya kidini huweza kuchangia kuleta utata zaidi badala ya ufumbuzi wa matatizo.Mwalimu wangu wa zamani katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam,Dr John Sivalon alichapisha kitabu ambacho kilitokana na thesis yake kuhusu mahusiano kati ya Kanisa Katoliki na Serikali ya Tanzania.Bila kuingia kwa undani kujadili kitabu hicho cha mhadhiri huyo wa Kimarekani ambaye pia ni Padre,ukweli ni kwamba kimekuwa ni nyenzo muhimu katika mihadhara na mijadala ya kidini nchini,japo sina hakika kama kimesaidia katika kuwa sehemu ya utatuzi wa matatizo yaliyopo.

Hebu sasa niingie kwenye ishu yenyewe.Katika siku za hivi karibuni kumekuwa na mijadala inayoendelea kwenye forums mbalimbali za Watanzania kwenye internet.Suala hilo ambalo limegusa hisia zangu ni madai kwamba Rais Jakaya Kikwete amekuwa akiwapendelea Waislam katika teuzi mbalimbali anazoendelea kuzifanya tangu aingie madarakani.Na pengine kinachotajwa zaidi ni ule uteuzi wake wa kwanza wa mabalozi wa mwanzo (akina Adadi na wengineo) ambao kwa mujibu wa majina yao wote ni Waislam.Pengine bila kudadisi sifa za walioteuliwa,wanaolalamika wakaangalia dini zao.Teuzi nyingine nazo zimeendelea kuzua mijadala isiyo rasmi japo sina uhakika kama na huko nyumbani nako hali ni kama hii niliyoiona kwenye mtandao.Ila niliona kwenye mtandao makala mbili tofauti ambazo nadhani zilitolewa kwenye magazeti ya huko nyumbani ambapo mwandishi mmoja mkongwe alikuwa akijibu hoja za mwanasiasa flani ambaye nadhani pia ni kiongozi wa kidini,na mada yenyewe ilikuwa ni hiyohiyo eti Kikwete anawapendelea Waislam.

Mimi siamini kabisa kwamba yeyote kati ya aliyeteuliwa-iwe kwenye uwaziri,unaibu waziri,wakuu wa mikoa,wakurugenzi na kadhalika-wamepewa dhamana zao kutokana na Uislam au Ukristo wao.Unajua kwa miaka mingi sisi tumekuwa Watanzania kwanza halafu ndio vinafuatia vitu kama Ukristo au Undamba wangu.Na ndio maana kule Ujiji,Tanga,Dar na kwingineko nilikokuwa sikuwahi kupata matatizo na waliokuwa karibu nami kwa vile cha muhimu kwetu haikuwa dini au kabila bali urafiki au mahusiano yetu kikazi.Na naamini kabisa kuwa Kikwete ni Mtanzania kwanza,na anaongoza Watanzania kwa misingi ya umoja wao na sio tofauti za kidini,na kwa mantiki hyo hata anapochagua viongozi haangalia dini bali sifa za wateuliwa.

Hata hivyo,kuna matatizo kadhaa yanayohusiana na suala la dini nchini.Tusijidanganye kwamba hatufahamu kuwa kumekuwa na manung’uniko miongoni mwa Waislam kuhusu usawa katika sekta ya elimu na ajira.Iwapo chanzo cha tatizo hilo ni sera za kibaguzi za wakoloni au kuna mbinu za makusudi za kuchochea matatizo hayo,hiyo sio muhimu sana kama ilivyo kwa umuhimu wa serikali,taasisi mbalimbali,wanataaluma na wananchi kwa ujumla kulitafutia ufumbuzi tatizo hilo.Matokeo ya awali ya utafiti wangu unaohusu harakati za Waislam nchini yanathibitisha kwamba matatizo yapo na yanajulikana ila kinachokosekana ni jitihada za makusudi za kupata ufumbuzi wa kudumu.Habari nzuri ni kwamba,hilo (la kupata ufumbuzi) linawezekana iwapo busara zitatumika na wadau kujumuishwa kwa karibu.Namalizia kwa kusisitiza kwamba wanaoleta madai ya udini wanatumia haki yao ya kikatiba kutoa mawazo yao,japo siafikiani nao.Hivi mtu anapooa au kuolewa na mtu anayetoka naye dini moja anaitwa mdini?Hapana.Kitakachojadiliwa hapo ni sifa za huyo mume au mke.Hivyohivyo,Jakaya hawezi kuitwa mdini pindi akichagua Muislam kama yeye alimradi ana sifa zinazostahili.

Alamsiki

18 Jun 2006

KULIKONI UGHAIBUNI:

Asalam aleykum,

Mwaka juzi gazeti maarufu duniani la TIME lilimtangaza George W.Bush kuwa “mtu wa mwaka (2004)” –au “Person of the Year” kwa lugha ya kwa mama.Katika uchambuzi wake kuhusu Bush,gazeti hilo lilimnukuu Rais huyo wa Marekani akisema kwamba “inapotokea kuwa hoja au mawazo yako yanazua mjadala au upinzani basi ni dalili kwamba yana uzito…kwa maana yangekuwa ya kipuuzi wala watu wasingejishughulisha nayo.”Alikuwa anazungumzia upinzani anaokumbana nao katika utendaji wa kazi zake za kila siku.Sio siri kuwa Bush anachukiwa na watu wengi hata ndani ya nchi yake.Lakini japo mie sio shabiki wake,namhusudu kwa jinsi anavyoweza kufanya mawazo yake yakubalike hata kwa wale ambao aidha hawayapendi au hawaafikiani nae.

Mwaka jana wakati nakuja huko nyumba,nilibahatika kukaa kiti kimoja na mama mmoja wa Kimarekani.Ni mtu mwongeaji sana,nami niliitumia nafasi hiyo kumdadisi siasa za Marekani hasa kuhusu mgawanyiko mkubwa wa kiitikadi nchini humo baina ya wale wa mrengo wa kulia(conservatives) na wale wa mrengo wa kushoto (liberals).Mwanamama huyo ambaye alinifahaisha baadaye kuwa ni mwanaharakati wa mazingira,alieleza kuwa kwa kiasi kikubwa mgawanyiko huo unachangiwa na siasa za Bush na maswahiba zake kama Dick Cheney,Donald Rumsfield,Paul Wolfowitz,na wengineo ambao wanajulikana kiitikadi kama “neo-conservatives” (sijui wanaitwaje kwa lugha yetu ya Taifa!).Miongoni mwa imani za hawa jamaa ni kuhakikisha kuwa Marekani inatumia ipasavyo nafasi yake kama Taifa lenye nguvu kabisa duniani.Kwa maana hiyo,ni “haki” yake kutumia “ubabe” wake kikamilifu ikiwa ni pamoja na kuvamia zile nchi zinazoonekana kuwa “korofi”.Ipo siku nitawazungumzia kwa kirefu jamaa hawa ambao takriban wote ni wadau wa taasisi moja isiyo ya kiserikali iitwayo “The Project for The New American Century” (Mradi wa Karne Mpya ya Marekani,kwa tafsiri isiyo rasmi).Turudi kwa yule mama.Basi akanambia kuwa japo yeye binafsi ni mpinzani wa Bush na hao neo-conservatives wenzake kuna wakati huwa “anamzimia sana” kutokana na jinsi anavyoweza kufanya maamuzi yake yatekelezwe hata pale kwenye upinzani mkubwa.Waingereza wana msemo “kama humuwezi unayeshindana nae basi bora uungane nae tu,”na ndio maana hata wale wasioafikiana na Bush mwishowe hujikuta hawana jinsi bali kuendana na mawazo au maamuzi yake.

Muda mfupi uliopita nilipata ujumbe kutoka kwa rafiki yangu flani aliyeko huko nyumbani akinijulisha kuwa kuna mwandishi mmoja ameandika makala katika gazeti flani la kila siku (la hapo Bongo) kupingana nami katika hoja ya makala yangu moja ya hivi ambayo nilimfananisha Rais Jakaya Kikwete na kiongozi wa chama cha Conservatives cha hapa Uingereza,David Cameron.Kwa mujibu wa ujumbe niliopata,mwandishi huyo aliyepingana nami anadai sikuwa sahihi kuwalinganisha wanasiasa hao .Kwa bahati mbaya hadi natayarisha makala hii nilikuwa sijapata hoja zote zilizotolewa kukosoa makala yangu.Kwa mantiki hiyo itakuwa vigumu kujibu hoja baada ya hoja bali nachoweza kusema kwanza ni kwamba makala ya mwandishi huyo ni uthibitisho tosha kuwa gazeti hili la KULIKONI ni kipenzi cha wengi,na ndio maana linazaa hoja na makala katika magazeti mengine.Pili,kama gazeti la TIME lilivyomnukuu Bush naamini makala yangu hiyo ilikuwa na uzito ndio maana ikamsukuma mwandishi huyo kuijadili japo hakuafikiana na nilichokiandika,kwa kuwa laiti ingekuwa ya kipuuzi asingepoteza muda wake kupingana nayo.”

Kwa faida ya mwandishi huyo,Kikwete anashabihiana sana na David Cameron katika maeneo flani.Kwa mfano,wote wawili wako katika vyama ambavyo kabla ya wao kushika hatamu za uongozi kwa kiasi flani vilikuwa vinaonekana kama ni vya “wateule wachache” tu.Ushindi wa tsunami kwa Kikwete ni dalili tosha kuwa hata baadhi ya wanachama wa vyama vya upinzani walimpigia kura kuonyesha kuwa kuteuliwa kwake kuwa mgombea urais kuliiongezea nguvu CCM.Hoja nyingine japo inaweza kuwa si nzito sana ni kwamba wanasiasa hao wana sifa inayofanana ya kuwa handsome,na kwa taarifa yako u-handsome unalipa sana kwenye siasa.Lakini kingine ni lugha zao wanazotumia.Wanaongea lugha za watu wa kawaida wa mtaani,yaani wanajua wananchi wanatarajia nini kwao.Ndio,Cameron anafuata siasa za mrengo wa kulia kuelekea kati (right-centre) na Kikwete kama mwana CCM nadhani atakuwa ni wa siasa za mrengo wa kushoto kuelekea kati (left-centre),na japo Cameron ni Mwingereza na Kikwete ni Mtanzania,la muhimu hapa ni jinsi wananchi wanavyowahusudu kutokana na utendaji wao.Kura za maoni hapa Uingereza zinaonyesha kuwa Cameron amempiku Tony Blair kwa kupendwa na wananchi na naamini kuwa hata kama Watanzania wataamshwa usingizini kupiga kura za maoni,Kikwete ataibuka kidedea kwa sana.Kwenye siasa umaarufu wa mwanasiasa haugemei sana kwenye itikadi zake au chama chake,sehemu aliyozaliwa au umri wake bali kukubalika kwake miongoni mwa wananchi,na hicho ndicho kilichonipelekea kuwafananisha wanasiasa hao.

Mwisho,siamini kuwa mwandishi wa makala hiyo alikuwa anatafuta umaarufu kupitia makala yangu au gazeti hili la KULIKONI,bali alikuwa anatumia haki yake ya kikatiba kutoa mawazo yake.Nampa changamoto aendelee kusoma gazeti hili ilimradi isiwe kwa nia ya kupinga kila kitu hata kama ameishiwa na hoja.Kama alivyoimba Mista Two (Joseph Mbilinyi) kwenye wimbo wake “Sugu” kwamba huwezi kuizuia mvua kunyesha,KULIKONI ni kama jua na mvua,halizuiliki.

Alamsiki.

KULIKONI UGHAIBUNI:

Asalam aleykum wasomaji wapendwa wa gazeti hili.

Leo tuzungumzie muziki.Muda mfupi uliopita nilikuwa nasoma makala flani kumhusu msanii wa kizazi kipya Albert Mangwea.Yalikuwa ni mahojiano kati ya msaanii huyo na tovuti ya Darhotwire.com.Niliguswa sana na kilio cha msanii huyo ambacho kimekuwa pia kikisikika kutoka kwa takribani kila msanii wa Bongofleva.Kuna wajanja flani,(hapana,hawa si wajanja,bali ni WEZI) ambao wamekuwa wakiwanyonya vijana wetu bila hata chembe ya huruma.Wezi hawa wanafahamika zaidi kwa jina la “wadosi”.Binafsi sijui kwanini wanaitwa wadosi lakini la muhimu hawa sio jina wanaloitwa bali unyonyaji wanaowafanyia wasanii wetu.

Pengine kabla ya kujadili wizi wa mchana mweupe unaofanywa na wadosi hao,tuangalie maendeleo ya Bongofleva huko nyumbani na huku Ughaibuni.Mimi ni mfuatiliaji sana wa mambo yanayotokea huko Bongo. “Ibada” yangu ya kila asubuhi inaanza kwa kutembelea tovuti za ki-Tanzania ili kujua yanayojiri huko.Sasa,kabla ya kuja huko mwaka jana mwishoni mwa mwaka jana nilikuwa nahisi kuwa habari kwamba Bongofleva imeikamata Tanzania kwa “kasi ya tsunami” ni porojo tu.Lakini nilipokuja nilishihudia mwenyewe jinsi gani hatimaye nyimbo zinazotengenezwa na kuimbwa na Watanzania zilivyokamata soko na mioyo ya wapenzi wa muziki.Wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu nilibahatika kushuhudia tamasha la “Piga Kura au Upigike” kwenye viwanja vya Biafra Kinondoni.Licha ya picha kadhaa nilizochukua kwa ajili ya kuwajulisha marafiki zangu hapa,nilijionea jinsi gani watu wa rika mbalimbali wanavyovutiwa na kazi za wasanii wa muziki wa kizazi kipya.Nadiriki kuamini kuwa mashabiki waliofika viwanja hivyo walikuwa wanawakilisha karibu kila kona ya jiji la Dar es Salaam.Kitu kingine nilichobaini ni kwamba jinsi gani wasanii wanavyotumika katika masuala ya muhiu kwa Taifa.

Nakumbuka niliwahi kusoma katika gazeti moja la huko nyumbani kwamba msanii Juma Nature “alimfunika” mwenyeji wake-mgombea aliyemwalika msanii huyo katika kampeni zake.Yaani watu walikuwa na kiu zaidi ya kusikia muziki wa Nature kuliko hotuba ya mheshimiwa huyo.Na pengine umati kubwa uliojitokeza kwenye mkutano huo ulifuata buridani hiyo ya bure.Yayumkinika kusema kuwa mchango wa wasanii katika kufanikisha uchaguzi,na hata kuwapatia ushindi baadhi ya wagombea,ulikuwa mkubwa.Kwa bahati mbaya,au pengine kwa makusudi,baada ya kukamilisha kazi ya kuhamasisha jamii kuhusu uchaguzi na wagombea,wasanii wetu wamerudi kulekule walikokuwa:wamesahauliwa na wanaendelea kunyonywa.

Napenda kuwafumbua macho wasanii wetu kwa kuwaambia kuwa muziki wao huku guhaibuni unauzika sana miongoni mwa watu waliotoka Afrika Mashariki.Wamuulize Banana Zorro aliyealikwa hapo London kwenye pati ya Muungano,wamuulize Mr Nice,Ray C na TID,na Profesa J ambaye nasikia amewachengua vilivyo huko Sweden na Holland.Wasanii wa nyumbani wakija huku wanababaikiwa kama vile akina Shaggy au Sean Paul wanavyobabaikiwa wakija huko nyumbani.Lakini,safari za nje sio jambo la kukurupuka tu,ni kitu kinachotaka maandalizi.Kwa mantiki hiyo si lazima kusafiri ili kunufaika na kazi za sanaa bali hata kutafuta namna ya kupenyeza muziki katika soko la kimataifa kunaweza sana kuwainua wasanii wetu.Hivi wasanii wetu wanajua kuwa CD zao huku zinauzwa hadi paundi 10 (zaidi ya shs 24,000/=)?Nimesoma kwenye internet kwamba tarehe 12/06/2006 kampuni moja iitwayo Townsend Records itatoa CD iitwayo Bongoflava (Swahili Rap from Tanzania) ambayo itauzwa paundi 10.99 (takriban shs 27,000/= kwa exchange rate za leo).Sijui kama na hawa ni wadosi au la,lakini huo ni uthibitisho kuwa Bongoflava ina soko zuri tu kuhu Ughaibuni.Na watu wanapenda kweli kazi za wasanii wa nyumbani.Niliporudi kutoka Tanzania jamaa zangu kibao walikuwa wananiulizia kama nimekuja na CD za Bongofleva.Kila mmoja anasema wanaposikia wasanii wetu wanakumbuka sana nyumbani.

Mheshimiwa Kikwete alinukuliwa akiwataka Watanzania walioko nje kuwasaidia wenzao walio nyumbani hasa katika nafasi za masomo.Ujumbe huo unaweza pia kupanuliwa na kuwahusisha wasanii wa nyumbani,kwa maana kuwa Watanzania walio nje hasa wale wenye upeo na mambo ya muziki wawasaidie wasanii wetu wa nyumbani kwa namna yoyote ile inayowezekana.Lakini ili hilo liwezekane wasanii wetu hawana budi “kuchangamka.”Wanaoitwa “wadosi” wanawanyonya na kuwaibia kwa vile wanajua dhahiri kuwa wasanii hao hawana njia mbadala.Jamani,dunia siku hizi imekuwa kama kijiji (japo ni kinadharia) na unachohitaji ni kwenda tu kwenye internet cafĂ© na kuperuza kurasa za mtandao kujua wapi unaweza kupata huduma au kuuza ulichonacho kwa mtu aliye bara jingine.Hapa ndipo umuhimu wa shule (elimu) unapojidhihirisha.Lakini hata kama shule haipandi,si unaweza kumwomba rafiki yako akusaidie kutafuta soko la kazi zako za sanaa nje ya nchi?

Serikali inapaswa kuwasaidia wasanii wetu kwa kuipa meno sheria ya hatimiliki.Sambamba na hilo ni wasanii wenyewe kusimama kidete kutetea maslahi yao badala ya kuendelea kulalamika au kufikiria kuingia kwenye fani nyingine kukwepa wizi wa kazi zao.Pia wasione aibu kuomba msaada kwa wenzao walio nje.Mwisho naiomba serikali ipanue vita dhidi ya wala rushwa na majambazi na kujumuisha “wadosi” pia.

Alamsiki

KULIKONI UGHAIBUNI

Asalam aleykum,

Siku za nyuma niliahidi kwamba iko siku nitawaletea stori kuhusu “mateja” wa huku Ughaibuni.Ndio,tatizo la matumizi ya madawa ya kulevya linawaumiza vichwa watu kadhaa huku Ughaibuni.Kuna vijana wadogo kabisa ambao wanashawishika kujiingiza katika kubwia unga.Ni vigumu kutabiri mafanikio ya jitihada za serikali na taasisi mbalimbali katika mapambano yao dhidi ya ulevi huo haramu na hatari.

Hivi karibuni nilipewa habari za kusikitisha sana.Kijana mmoja mwenye umri usiozidi miaka 18 alikutwa amekufa huku sindano aliyoitumia kujidungia adawa ya ulevya ikiwa inaning’inia kwenye mkono wake.Huyo kijana namfahamu vizuri kwa vile siku moja aliwahi kufika hapa ninapoishi akiwa ameongozana na rafiki yangu mmoja mwenye asili ya Afrika Mashariki.Kilichonivutia zaidi kuhusu kijana huyo ni kauli zake ambazo lazima nikiri kuwa mara nyingi kwa hapa zinatolewa na wanasiasa kuliko wananchi wa kawaida.Alikuwa akionyesha kuchukizwa kwake na watu wanaowabagua wenzao kwa vile tu ni wageni au wana rangi tofauti na wao.Kimsingi,alikuwa akilaani suala zima la ubaguzi.Kwa umri wake mdogo,nilimwona kama ni mtu mwenye upeo mkubwa sana.Kwa wakati huo sikujua kabisa kuwa pamoja na busara zake,kijana huyo alikuwa akiweka rehani roho yake kwa kubwia unga.Pengine lishe bora na huduma mbalimbali zinazopatikana kirahisi ndizo zilikuwa zinamsaidia kuficha “uteja” wake,kwani kama tujuavyo wengi si vigumu kumtambua m-bwia unga kwa kumwangalia tu.

Alienisimulia kuhusu mauti yaliyomkumba kijana huyo alinijulisha kwamba aliemletea marehemu madawa hayo ya kulevya alikuwa ni rafiki yake ambae walikuwa wanasoma darasa moja.Kwa lugha nyingine,wawili hao walishirikiana katika kuleta mauti ya mmoja wao.Huo ni ushirika wa mauti,na hilo ndio linanipeleka kwenye mada yangu ya pili kuhusu ujambazi uliotokea hivi karibuni pale Ubungo uliopelekea vifo na majeraha kwa waliosalimika.

Kuonyesha yeye ni kiongozi anaewajali mno wananchi wake,matra baada ya kurejea nchini akitoka ziarani kusini mwa Afrika,Rais Jakaya Kikwete alikwenda kuwajulia hali waliojeruhiwa na majambazi katika tukio hilo la Ubungo.Mheshimiwa Kikwete alinukuliwa na vyombo vya habari akisema kwamba anaamini kuwa kulikuwa na njama ndani ya benki iliyoibiwa fedha hizo kwa vile isingekuwa rahisi kwa majambazi hayo kuvamia tu gari lenye fedha bila kuwa na taarifa sahihi.Wafanyakazi waliohusika kuvujisha taarifa za fedha hizo kwa majambazi watakuwa hawana tofauti na yule kijana aliempelekea unga rafiki yake na hatimaye kumsababisha mauti.Waliovujisha taarifa hizo walikuwa na ushirika wa mauti na majambazi waliofanya unyama huo.Hivi tunapokuwa kazini si huwa tunaunda kitu kama undugu kwa vile muda mwingi tunautumia tukiwa pamoja na pengine kushirikiana katika mambo ya nyumbani kama vile harusi na misiba?Sasa unapotoa taarifa kwa majambazi wenye silaha za moto ili kuwawezesha kuvamia gari ambalo mfanyakazi mwenzio yupo humo si ni kama unamtengenezea mauti mwenzio?Jamani,hivi fedha zinatupeleka kupoteza utu wetu na kutothamini uhai wa wenzetu!Kwa hakika walioshiriki kwa namna yoyote katika kufanikisha uporaji huo wanastahili kusakwa kwa udi na uvumba na hatimaye kupatiwa kibano wanachostahili.Kwa “waliouza ishu” hiyo kwa majambazi wanakuwa wametenda dhambi kuu mbili:kuwasaliti wafanyakazi wenzao ambao aidha waliuawa au kujeruhiwa,na pia walishiriki katika ujambazi huo kwa vile wao ndio hasa waanzilishi wa mpango mzima.Hiyo si kusema kwamba majambazi waliohusika hawana hatia,lakini iwapo waliotoa taarifa hizo wasingewajulisha majambazi kwamba siku flani,muda flani,katika gari flani kutakuwa na shilingi bilioni moja ni dhahiri kwamba tukio hilo lisingetokea.

Kwa upande mwingine,ni muhimu kwa taasisi zetu za fedha kuwa makini zaidi wanaposafirisha fedha kutoka sehemu moja kwenda nyingine.Hivi kweli benki kama NMB inashindwa kununua gari moja ambalo ni maalumu kwa ajili ya kusafirishia fedha?Uzuri wa magari kama hayo ni kwamba licha ya kutoa usalama mkubwa kwa mali inayosafirishwa,maisha ya wanaosafirisha mali hiyo nayo yanakuwa salama zaidi ukilinganisha na magari ya kawaida.Natambua kuwa yapo makampuni binafsi ya ulinzi ambayo yanamiliki magari ya aina hiyo.Lakini siwezi kuilaumu NMB moja kwa moja kwa kutokodi huduma hiyo kwa vile kumbukumbu zinaonyesha kuwa siku za nyuma walinzi wasio waadilifu walishawahi kuingia mitini na mamilioni ya fedha wakiwa katika gari maalumu la kusafirishia fedha.

Hata hivyo,kuwa na gari maalumu la kusafirishia fedha bila kuwa na watumishi waadilifu ni sawa na kulala ukiwa kwenye chandarua chenye dawa lakini kimekufunika kuanzia kichwani hadi kiunoni tu,na hapohapo kuamini kuwa unawadhibiti mbu.Uaminifu,uadilifu na kuthamini maisha ya wenzetu ni vitu muhimu sana na lazima kwa kila Mtanzania.

Alamsiki

17 Apr 2006

KULIKONI UGHAIBUNI:

Kabla ya yote sina budi kuanza kwa kumpongeza Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete kwa kutimiza siku 100 tangu achaguliwe kuwa Rais wa serikali ya awamu ya nne huko nyumbani.Si huko nyumbani tu ambako wananchi wengi wameridhika na utendaji wa Mheshimiwa na serikali yake bali hata huku Ughaibuni.Kuna dalili nyingi zinazoonyesha kwamba nchi yetu inaweza kurudisha heshima yake ambayo kwa kiwango kikubwa ilikuwa imepotea ndani na nje ya nchi.

Siku moja nikiwa kibaruani hapa napoishi nilikutana na jamaa mmoja ambaye nilipomfahaisha kuwa mimi ni Mtanzania alionyesha kuwa na shauku ya kuongea nami.Huyo jamaa alinifahamisha kuwa yeye ni Mskotishi ambaye miaka michache alipata fursa ya kutembelea Tanzania kufanya mchanganuo wa mradi flani uliokuwa ufadhiliwe na wahisani wa kimataifa.Jamaa alianza kwa kuniuliza kwanini Tanzania ni nchi masikini wakati ina utajiri kibao wa asili.Nikajifanya kama sikulielewa swali lake na kumtaka anifafanulie huo anaoita utajiri.Akanitolea mlolongo wa vitu:madini,misitu,ardhi yenye rutuba,maziwa na mito kadhaa,mbuga za wanyama (na hapo akaniambia kuwa Selous ni mojawapo ya mbuga za asili kubwa kabisa duniani),mlima Kilimanjaro,na kikubwa zaidi ya vyote,AMANI.Sio siri,nilibaki nang’ang’aa macho tu bila ya kuwa na jibu la haraka la swali lake la msingi:kwanini Tanzania ni miongoni mwa nchi masikini sana duniani wakati ina utajiri lukuki?

Jamaa akaendelea kunikalia kooni.Akanipa mfano hai wa uzoefu wake kuhusu Tanzania.Nilisema hapo mwanzo kuwa huyo jamaa alikuja hapa kwa ajili ya mradi flani.Alidai kuwa wakati yeye na wenzake wakiwa wanaandaa mambo flani kuhusu mradi huo,wakakumbana na mambo ambayo yeye aliyaona ya ajabu sana kwa mtizamo wake.Alieleza kuwa katika ofisi zaidi ya moja walikutana na watendaji wa serikali ambao waliwaomba “ma-TX” hao kuongeza gharama halisi za mradi huo kwa makubaliano ya “teni pasenti” pindi fungu la fedha likitoka.Huyo jamaa na wenzake walionekana kushangazwa sana na tabia ya watendaji hao wa serikali walioonekana kuwa hawakuwa na uchungu wowote na nchi yao wala kujali umuhimu wa mradi huo kwa Taifa lao.Jamaa anadai wao walikataa ofa hizo (kama ni kweli au la mimi sijui) na picha aliyobaki nayo ni kwamba wabomoaji wa Tanzania kwa kiasi kikubwa ni Watanzania wenyewe.

Nimeelezea stori ya Mskotishi huyo kubainisha jambo ambalo haliitaji mtu kutoka nje kutuelezea.Ni wangapi tunaojua kwamba wapo watendaji ambao kwa teni pasenti wanatoa vibali vya kazi kwa wageni wasiostahili kuwepo bila kujali kuwa wanaweza kuwa magaidi?Au wale wanaotoa vibali vya ujenzi kwa makandarasi wasio na sifa na hatimaye kuhatarisha maisha ya watuamiaji wa majengo hayo?Au wale wanaruhusu bidhaa mbovu,ikiwa ni pamoja na chakula,kuingia nchini bila kujali athari kwa afya za watumiaji?Orodha ni ndefu.

Ndio maana Watanzania wengi walio huku Ughaibuni walifurahishwa sana na kauli ya Mheshimiwa Kikwete kuwa atakula sahani moja na watu wanaofanya kazi za umma na kutanguliza maslahi yao binafsi badala ya ya yale ya Taifa ikiwa pamoja na wale wanaosaini mikataba bomu zaidi ya ile ya baadhi ya machifu wetu enzi za ukoloni.Ni dhahiri kuwa nchi yetu iko katika nafasi ambayo haistahili kuwepo.Nchi yetu haipaswi kuwa masikini wa kutupwa wakati tuna rasilimali kibao.

Salamu za wabongo walioko huko kwenda kwa Mheshimiwa Kikwete ni kwamba akaze uzi na kutowalea wazembe kama ilivyokuwa huko nyuma.Mtu akiboronga atimuliwe mara moja.Kuunda tume kuichunguza tume iliyofanya ubadhirifu wakati inachunguza ubadhirifu wa fedha uliofanywa na tume nyingine ni kupoteza fedha tu.Wazembe watimuliwe na ikiwezekana wafikishwe kwenye vyombo vya sheria haraka iwezekanavyo.Historia inaonyesha kuwa binadamu tuna tabia ya kuogopa mambo yanayoweza kuhatarisha nafasi zetu nzuri.Kiongozi anaeteuliwa kuchukua nafasi ya mwenzie alietimuliwa kutokana na utendaji mbovu ana nafasi kubwa ya kuwa mtendaji mzuri kwa vile anajua akiboronga yatamkumba yaliyompata aliyemtangua.

Mwisho,wabongo walioko huku “wanakupa tano” Mheshimiwa Kikwete na serikali yako huku wakitarajia kuwa dhamira yako ya kurudisha heshima ya nchi yetu itatimia.

Alamsiki

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.