23 Sept 2011


Hatimaye mfungwa maarufu kuliko wote nchini Tanzania kwa miaka ya hivi karibuni,Bwana Amatus Liyumba ameachiwa huru leo.Haijafahamika kama amemaliza kifungo,au amepewa msamaha wa Rais au muda wa kipindi cha maigizo umekwisha.

Na kwa vile fisadi huyu ameachiwa,je wewe mlipakodi umenufaika vipi na kifungo chake?Sikuwahi kusikia kuwa fedha alizokwiba zilitaifishwa,ikimaanisha kwamba anaweza kabisa kutumia jeuri ya fedha hizo kwa kufuru ya kukufanya utamani angeendelea kuzeekea jela.

Na kwa vile habari za kifungo chake huko jela zilikuwa za siri,hatuna uhakika kuwa alikuwa mfungwa wa kawaida-kwa maana ya kutopewa huduma za ki-V.I.P au hata kuwa analala nyumbani kisha asubuhi anarejea jela.

Anyway,kwa sasa habari ndio hiyo.

0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.