4 Sept 2012



Septemba 2, 2012: Pichani JUU: CCM inafanya mkutano wahadhara huko Bububu, Zanzibar licha ya Serikali "kusitisha shughuli zote za kisiasa ili kupisha sensa ya watu na makazi."

Septemba 2, 2012 Pichani CHINI,mwandishi wa habari wa kituo cha TV cha Channel Ten,Daudi Mwangosi akipata kipigo kutokakwa FFU kwa "kosa" la kufanya coverage ya KIKAO CHA NDANI cha Chadema huko Nyololo,Iringa,ambacho Polisi sio tu walikizuwia kwa SABABU ZILEZILE ZILIZORUHUSU MKUTANO WA HADHARA JIMBONI BUBUBU bali walipiga,kujeruhi wananchi wasio na hatia na HATIMAYE KUMUUA mwandishi Daudi Mwangosi ."



Mheshimiwa Rais, damu za wananchi wasio na hatia wanaouawa na polisi kwa "kosa la kutumia haki zao za kikatiba za freedom of association" hazitapotea bure. Polisi waliua Arusha,lakini hiyo haikuzuwia wanachama na wapenzi wa Chadema kukusanyika Morogoro ambapo polisi waliua tena.Hata hivyo,kifo hicho hakikuwatisha wana-Chadema kukusanyika tawini kwao huko Nyololo ambapo baada ya unyanyasaji wa hali ya juu,polisiwaliua tena.

Hivi Mheshimiwa Rais hujifunzi kitu kutoka kwenye JEURI hii? Labda umesahau kuwa hata tawala dhalimu kabisa za kikomunisti huko Ulaya Mashariki zilijidanganya kuwa ukatili na unyama wavyombo vya dola utazidumisha (tawala hizo) milele,lakini wakati ulipofika zilisambaratika.Na huko Afrika ya Kusini,makaburu walitawala kwa mtutu wa bunduki lakini hawakuweza kuzuwia kuanguka kwa mfumo wa kibaguzi.

Mwanafalsafa Karl Marx aliwahi kuusia kuwa "mnyonge hana cha kupoteza zaidi ya minyororo." Wakati mafisadi wanaishi kwa hofu ya kunyang'anywa walichotupora, wanyonge wasio na uhakika na mloujao wanaishi kwa matumaini tu.Lakini kuishi huko kwa matumaini kunaweza kuwa silaha yenye nguvu kuliko vipigo,risasi na unyama wa FFU.

Watu wameichoka CCM na ni wazi kuwa vitisho na mauaji ya raia yasiyo na hatia hayawezi kushusha chuki hiyo.Sana sana inawaongezea tu sababu ya kukichukia chama hicho. 2015 si mbali.CCM inaweza kung'olewa madarakani.Ni vema,Mheshimiwa Rais,ukaanza kutafakari hatmayako pindi hao wanyonge wanaonyanyaswa sasa wakishika madaraka.

Watanzania wana kila sababu ya kuichukia CCM lakini inaonekana kana kwamba chama hicho kinasaka sababu nzito zaidi.Sijui ni kuishiwa na uwezo wa kuongoza au ndio kimezeeka na kinasaka namna ya kujipeleka kaburini,lakini kilicho wazi ni kuwa kila tone la damu linalomwagika kutokana na unyama wa polisi wetu ni sawa na lita nyingi za petroli kuchochea moto wa mabadiliko.


0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.