24 May 2016

Sakata la kutumbuliwa kwa aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani, Charles Kitwanga, linazidi kutawala vichwa vya habari, huku maendeleo mapya yakiashiria kuwa kuna mengi yanayoweza kuwa yanaendelea 'nyuma ya pazia.'

Jana, watu waliojitambulisha kama 'wana-jimbo wa Misungwi' walitoa tamko kwa waandishi wa habari. Hebu ndugu msomaji mpendwa, fanya kulisoma tamko hilo kwanza, kisha bingirika nami kwa uchambuzi zaidi, and trust me, sintokuangusha haha!

First thing first, hawa 'wana-jimbo wa Misungwi' WAMETUMWA NA NANI? Ninauliza hivyo kwa sababu hisia yangu ya sita inanituma kuamini kuwa hawajajitolea wenyewe tu kutoa tamko hilo. Hawa wametumwa, no doubt about that. Lakini hatujui nani kawatuma.

Kwa kuitegemea tena hisia yangu ya sita, yayumkinika kuhisi kuwa hao 'wana-jimbo' ni wapambe tu wa Kitwanga. Twende mbali zaidi, ninahisi watu hao ni sawa na spika tu ya kumwezesha Kitwanga asikike.. 

Tetesi zinaeleza kuwa Kitwanga alikuwa 'mtu wa kinywaji' kitambo sasa. Na kwa wenzetu ambao hawajawahi kugusa kinywaji, ukweli upo hivi: hakuna mtu anayeitwa 'mnywaji wa muda mrefu.' Mtu wa aina hiyo ni MLEVI. Period. Na ulevi, japo si dhambi au kinyume cha sheria, una athari zake. Kuna mlolongo mrefu wa jinsi ulevi ulivyobomoa maisha ya watu mbalimbali. Kwahiyo, tukiafikiana kuwa Kitwanga ni mlevi, basi ilikuwa suala la muda tu kabla haijamlipukia. Kwa lugha nyingine, Bwana Kitwanga alikuwa kama time-bomb, muda wowote ule lingetokea la kutokea.

Mengi yameshaongewa tangu Kitwanga atumbuliwe na Rais Magufuli hapo juzi, makubwa zaidi yakiwa ni pamoja na madai kuwa ishu hiyo ni mcheoz wa kuigiza. Kwamba kutumbuliwa kwa Kitwanga ni mkakati wa makusudi wa kuiua ishu ya Lugumi. 

Siafikiani na mtazamo huo kwa sababu kama kweli Magufuli alikuwa anataka kumuokoa rafiki yake alikuwa na njia nyingi tu, moja ya wazi ikiwa ni 'kuziba masikio,' kwa maana ya kupuuza kelele za waliotaka Kitwanga atumbuliwe.

Wengine wanadai kuwa kweli Kitwanga alikuwa amelewa, lakini hakulewa kwa hiari yake bali 'kinywaji chake kilifanyiwa utaalam,' wakijaribu kutushawishi kuwa Kitwanga alihujumiwa. 

Hizi ni hisia tu zisizo na uthibithso wowote. Jamaa alikuwa 'chapombe,' na wanaomfahamu hawashangazwi na hilo tukio la majuzi au kutumbuliwa kwake. Pombe sio chai, siku ya siku lazima itamwadhiri mtu.

Madai mengine ambayo yanahusiana na hayo ya 'kinywaji cha Kitwanga kufanyiziwa' yanauhusisha utawala wa Awamu ya Nne ya Rais Jakaya Kikwete, ambako ndiko suala la Lugumi lilianzia. In fact, hizo tuhuma za 'kinywaji cha Kitwanga kufanyiziwa' zinawahusu baadhi ya watu waliokuwa karibu na utawala huo. 

Na kama msomaji ulivyoona katika 'tamko la wana-jimbo wa Misungwi' hapo juu, mmiliki wa Kampuni ya Lugumi, Said Lugumi na mtoto wa Rais Kikwete, Ridhiwani, wametajwa kuwa miongoni mwa wanaomhujumu Kitwanga.

Sawa, ishu ya ufisadi wa Lugumi ipo complex lakini kudai kuwa akina Lugumi na Ridhiwani ndo waliomfanyizia Kitwanga hadi akaishia kutimuliwa na Rais Magufuli ni hisia tu zisizo na mantiki. Haina mantiki kwa vile haiingii akilini jinsi gani hao jamaa wangemudu kumhujumu Kitwanga na wakati huohuo kumshinikiza Magufuli amchukulie hatua.

Kwa upande mwingine, Spika Job Ndugai, amejiingiza matatizoni 'kitoto' kwa kauli yake isiyo na busara ianyoashiria kuwa 'ulevi wa Kitwanga ni cha mtoto, kuna waheshimiwa wanavuta bangi na kubwia unga.' Really? Yaani Spika anawafahamu waheshimiwa wanaotenda makosa ya jinai lakini anawahifadhi!? 

Sasa, inasemekana baadhi ya wabunge wameamua kumkalia kooni awataje hao 'wabunge wavuta bangi na wala unga' na ajieleze kwanini hakuwaripoti kwa mamlaka husika.

Kadhalika, baadhi ya 'wazushi' wanamtaka Waziri Mkuu Kassim Majaliwa kuonyesha uthibitosho kuwa kweli Kitwanga alikuwa 'njwii' siku ile pale Bungeni hadi Rais Magufuli kuchukua hatua ya kumtumbua. Nadhani hii inalenga kumpima ubavu tu Waziri Mkuu Majaliwa kwani kila aliyeona Kitwanga akijibu swlai pale Bungeni hatoshindwa kujua kuwa alikuwa amelewa

Anyway, blogu hii inaendelea kufuatilia ishu hiyo, pamoja na ishu nyingine mbalimbali katika jamii yetu. Pia, kesho, makala yangu katika toleo la wiki hii la jarida la Raia Mwema inajadili kwa kirefu kuhusu suala hilo la Kitwanga kutumbuliwa. Usikose kupata nakala yako.

0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.