6 May 2016

Bila shaka matokeo ya utafiti huu yatawashangaza watu wa nchi nyingine, lakini sio sie Watanzania, ambao tumebainika kuwa watu wanafiki zaidi kuliko wote duniani. Sio jambo la kushangaza kwa sababu unafiki umekuwa sehemu ya utamaduni wetu.

Na mfano mwepesi wa unafiki wetu ni kuhusu uamuzi wa serikali kuipiga marufuku video ya msanii Snura iitwayo 'Chura' ambayo ilivuka mipaka ya ustaarabu. Awali, watu wengi waliishutumu Serikali kwa kuruhusu video hiyo 'chafu' kuonyeshwa ilhali vikao vya bunge vikizuiwa kuonyeshwa 'live.' Well, japo bunge laendelea 'kufichwa,' lakini serikali imejitutumua na kipiga kufuli video ya 'Chura.'

Lakini hatua hiyo imewakera baadhi ya wenzetu. Wengine wanadai serikali ina vitu muhimu zaidi vya kufanya badala ya kufungia video. Wengine wanadai mbona kuna video chafu zaidi za 'akina Rihanna' kuliko hiyo ya Chura. Wengine wanakwenda mbali na kudai kuwa alichofanya Snura na hao mabinti wa kwenye video ni UBUNIFU. Really?????

Twende kwenye maisha yetu ya kila siku. Tuchukulie mfano vifo. Utakuta watu wanasubiri mpaka mtu afe ndio waanze kumwagia sifa, "Oh marehemu alikuwa mtu mzuri sana, oh marehemu alikuwa mwema sana...RIP...RIP..." Hii tabia ya kuwapenda watu wakifa lakini kuwachukia walipokuwa hai ni nini kama sio UNAFIKI? Angalia Marehemu Kanumba alivyoandamwa wakati wa uhai wake. Msanii aliyefanya kazi kubwa kabisa kuiinua medani ya filamu za Kitanzania aliandamwa mfululizo na hili na lile, huku watu wasio na vipaji ya kitu chochote kile wakigeuka mahakimu na majaji dhidi ya kipaji cha msanii huyo. 

Tuangalie huko mitaani tunakoishi na 'makazi yetu mapya' mitandaoni. Huko mitaani, wenzetu wenye umuhimu mkubwa kwa jamii - madaktari, manesi, walimu, nk -  hawapewi heshima kubwa kulinganisha na wanayopewa wahalifu kama wauza madawa ya kulevya au wabadhirifu serikalini. Twaita wauza unga WAZUNGU WA UNGA, na wabadhirifu twawaita MAPEDEJEE, VIBOSILE, VIGOGO, na majina mengine ya kuwatukuza, ilhali jina lao stahili ni WAHALIFU. 

Nenda mtandaoni, kwa mfano Instagram. Ukiacha wasanii wetu na watu wengine muhimu, watu maarufu zaidi katika mtandao huo kwa Tanzania ni wale wenye kuongoza makundi ya matusi, picha za utupu, majungu, na madudu kama hayo. Sio kwamba hawa 'wameroga' ili kuwa maarufu. Hapana. Umaarufu wao unatokana na Watanzani wengin kupenda vitu hivyo: picha za utupu, majungu, nk.

Angalia wakati wa uchaguzi. Wanasiasa wetu hujiweka karibu kabisa na wananchi. Si ajabu kuona mwanasiasa akiwasalimia wananchi kwa kupiga magoti 'kwa heshima' wakati anaomba kura.Subiri ashinde uchaguzi. Humsikii japo akicheka au kuzomea bungeni. Unaweza kuhisi kuwa asilimia kuwab ya wabunge wetu wanatoka majimbo ya nchi kama Uingereza au Marekani, ambazo zina matatizo machache kwa wapigakura, kwani haiingii akilini kwa mbunge ambaye jimbo lake lina matatizo lukuki awe haonekani bungeni unless kwenye kukusanya posho tu, na akitokea bungeni, si ajabu kuona amepigwa picha huku kachapa usingizi (labda alishindwa kulala kutokana na kuzongwa na mawazo kuhusu jimbo lake?)

Anyway, turudi kwenye utafiti unathibitisha tulivyobobea kwa unafiki. Watafiti kutoka Chuo Kikuu cha Nottingham cha hapa Uingereza waliendesha utafiti wa kupima kushamiri kwa ukiukwaji wa kanuni katika nchi 159 duniani, wakitumia takwimu za kutoka mwaka 2003 kuhusu ubadhirifu katika siasa, ukwepaji kodi na rushwa.

Twende tena mtaani. Kuna suala la ushoga ambalo taarifa zinaeleza kuwa unakua kwa kasi huko nyumbani. Juzi kuna shoga mmoja kafiwa Dar, na inaelezwa kuwa takriban kila mtu maarufu jijini hapo hakukosekana msibani. Lakini sio katika msiba huo tu, nenda Instagram halafu angalia akaunti za mashoga na idadi ya 'followers' wao. Hivi yawezekanaje kama 'ushoga sio tu ni laana bali pia ni kinyume cha sheria za Tanzania,' then shoga awe na 'followers' zaidi ya laki moja? Kwanini kila shughuli ya mastaa wetu haiwi kamili bila uwepo wa mashoga wa 'kukata viuno' kwenye shughuli hiyo?


Habari kamili kuhusu utafiti huo ipo HAPA na kuna MAKALA HII katika gazeti la kila wiki la RAIA MWEMA Toleo la wiki hii imeandika kwa kirefu kuhusu suala hilo

1 comment:

  1. Kwenye hili wala hata hawaja kosea kabisa... watanzania ni wanafiki wakutupwa... wapo sawa kabisa.

    Ukiingia kwenye siasa ndio kabisa majanga... nadhani ujaguzi wa mwaka jana ulionyesha ni jinsi gani tulivyo wanafiki. Ni yayo tu.. asante kwa Makala nzuri Chahali.

    Ni mimi, Ally

    Connect with me on twitter @ally_eh of find me at allymsangi.com

    ReplyDelete

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.