Rwanda ilikuwa eneo penye utawala wa kifalme tangu karne ya 16 BK kabla ya kufika kwa ukoloni. Mwanzo wake ni katika eneo la Ziwa la Muhazi. Watawala wenye cheo cha "mwami" kutoka kikundi cha wafugaji (Watutsi) walitanua himaya zao tangu miaka ya karne ya 16 BK hadi kufika eneo la leo hii. Wafugaji wa ng'ombe Watutsi walikalia nchi pamoja na wakulima wa Kihutu na wawindaji Watwaa.
UKOLONI WA KIJERUMANI
Ukoloni ulichelewa kufika Rwanda, mwaka 1890 Ujerumani na Uingereza walipatana ya kuwa Rwanda na Burundi ziwe ni sehemu ya Afrika ya Mashariki ya Kijerumani. Lakini ilikuwa mwaka 1908 tu ya kwamba Wajerumani walimtuma afisa wa kudumu aliyekaa Rwanda kama mwakilishi wa serikali ya Ujerumani. Mwaka 1916 Ubelgiji na Uingereza walivamia Rwanda katika Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia. Baadae ikawa chini ya Ubelgiji pamoja na Burundi kama "Rwanda-Urundi" katika hali ya eneo la kudhaminiwa kutokana na azimio la Shirikisho la Mataifa (UNO).
Utawala wa Wabelgiji ulikuwa wa moja kwa moja na mkali zaidi kuliko wa Wajerumani. Wabelgiji walijaribu kutoa faida ya kiuchumi wakilazimisha wenyeji kupanda mikahawa na kutekeleza kazi za serikali ya kikoloni. Katika utawala wao Wabelgiji walitumia zaidi Watutsi wakiwapa nafasi za elimu na kuwatumia katika shughuli za serikali. Wataalamu wengine huamini ya kwamba siasa hii ilisababisha kukua kwa chuki dhidi ya Watutsi kwa upande wa wakulima Wahutu iliyoleta kumwaga kwa damu baadaye.
Katika miaka ya 1950 ilionekana na kudhihirika ya kwamba ukoloni unaelekea mwisho wake. Uhusiano kati ya Wahutu na Watutsi ukawa vigumu kwa sababu Wabelgiji walibadilisha siasa yao yakupendelea Watutsi wakidai haki zaidi kwa ajili ya Wahutu waliokuwa wengi. Ni hasa wamisionari wa katoliki Mapadre Weupe waliosimama upande wa Wahutu wakiona ndio wagandamizwa.
Mwami Mutara Rudahigwa aliyejiita pia Charles alijaribu kuleta upatanishi kati ya vikundi katika nchi. 1954 aligawa nchi ya kifalme kati ya Wahutu na Watutsi. Lakini alikuwa na wapinzani Watutsi waliomua mwaka 1959. Mtoto wake Mwami Kigeri V. alisimikwa kwenye kiti hicho. Hatua hii ilisababisha ghasia na vurugu nchini kwa sababu Wahutu walidai kuwa na neno katika mabadiliko ya serikali. Mwezi wa Novemba 1959 Mwami Kigeri V. alilazimishwa kuondoka nchini akikimbilia Uganda. Watutsi wenye siasa kali walijaribu kumwua kiongozi wa Mouvement Democratique Republicain (MDR) chama kikubwa cha Wahutu. Wahutu walijibu kwa kuwashambulia na kuua Watutsi. Wabelgiji walitumia wanajeshi wao kupoza hali hiyo nchini Rwanda. Katika uchaguzi wa kwanza wa halmashauri ya tarafa na miji kabla ya uhuru chama cha Parmehutu ndicho kilichopata kura nyingi. Viongozi wa Parmehutu walitangaza serikali mpya mwaka 1961. Uchaguzi wa Bunge ulileta kura ya 77% kwa ajili ya chama cha Parmehutu kilichomchagua kiongozi wake Grégoire Kayibanda kuwa Rais.
Tarehe 01.07.1962 Rwanda ilipata uhuru wake kamili. Wakati huo zaidi ya Watutsi 350,000 tayari walishakuwa wamekimbilia nchi za jirani. Mwaka uliofuata vikundi vya Watutsi kutoka nchi hizo za jirani walijaribu kufanya mapinduzi kwa kushambulia serikali mpya wakitokea uhamishoni. Kitendo hicho kilifuatiwa na uangamizaji wa kwanza wa Watutsi zaidi ya 100,000 waliouawa na Wahutu.
Hata katika miaka iliyofuata mauaji dhidi ya Watutsi iliendelea. Wanasiasa Wahutu walizoea kuita Watusi ndio "Wadudu". Kila kitu kilichokuwa si sawa kilielezwa ni kosa la Watutsi waliokuwa raia bila haki. Idadi kubwa ya Watutsi walikimbia Burundi, Uganda na Tanzania.
Mwaka 1973 Generali Habariyama alimpindua rais Kayibanda na kuanzisha serikali ya kijeshi akijaribu kupatanisha vikundi ndani ya taifa. Lakini hata mwaka uliofuata 1974 mauaji ya Watutsi yalitokea tena.
Mnamo 1990 ilikuwa wazi ya kwamba Rwanda ilikuwa na hali ngumu. Kwa upande moja nchi za mataifa zilisukuma serikali za Afrika kuruhusu kura huru za kisiasa.
Katika Rwanda ongezeko la wakazi lilileta msongamano mkubwa na uhaba wa ardhi ya kilimo na Ufugaji. Uchumi ulikuwa duni, Wakati huohuo wapinzani Wahutu walikusanyika nje ya nchi hiyo kudai demokrasia. Na katika makumi elfu ya watoto wa Watutsi waliokuwa nje ya nchi hiyo, sauti zikasikika zilizodai warudi tena kuijenga Rwanda.
Habyarimana alijaribu kutafuta suluhisho na ungamano wa kitaifa, akaanza kujadiliana na Watutsi wa nje lakini alikutana na upinzani kwa upande wa Wahutu wakali waliochukia uelewano na Watutsi.
Safari ya Kagame na RPF kurudu Rwanda kutoka Uganda.
Oktoba 1990 Watutsi waliokaa Uganda walianzisha chama cha RPF (Rwanda Patriotic Front) wakiwa na wafuasi wahutu wachache wakavamia Rwanda kwa silaha. Kiongozi wao alikuwa Paul Kagame aliyeondoka Rwanda akiwa mtoto wa miaka minne. Alikuwa amejiunga na jeshi la Yoweri Museveni na kupanda ngazi katika jeshi la Uganda hadi kuwa mkuu wa huduma ya usalama ya kijeshi ya Uganda. Walitaka kulazimisha serikali ibadilishe hali ya Watutsi kuwa raia bila haki. Lakini uvamizi huu ulisababisha kuongezeka kwa ukali wa Wahutu dhidi ya Watutsi ndani ya Rwanda na siasa kali kwa upande wa viongozi Wahutu. Kikundi cha kihutu cha Interahamwe kilipewa silaha kujibu mapigo dhidi ya uvamizi wa Kagame, Maelfu ya Watutsi Warwanda waliuawa. Vita kati ya wapinzani kutoka Uganda na jeshi la serikali iliendelea mpakani hadi pande zote mbili zilikutana hapa Arusha Tanzania na kupatana kukoma kwa vita 1992 chini ya uangalizi wa Umoja wa Mataifa na Umoja wa Afrika.
Sehemu ya viongozi Warwanda walijiandaa kutafuta utaratibu mpya lakini wengine walifanya mipango ya kumaliza swali la Watutsi kabisa wakipanga kuua Watutsi wote nchini.
Tarehe. 06.04.1994 rais Habariyama akirudi nchini kutoka safari ya Tanzania, Ndege yake ilipigwa kombora kabla ya kutua ikaanguka chini akafariki. Uwezekano ni mkubwa ya kwamba ni Wahutu wenye msimamo mkali ndio waliomua, lakini wengine walisema ni Jenerali Paul Kagame na RPF yake.
Tendo hili ilikuwa mwanzo wa mauaji ambayo hayakuwahi kutokea Afrika. Viongozi wa Interahamwe, wa jeshi la kitaifa na vikundi vikali vya Kihutu walitekeleza mipango ya kukusanya Watutsi kila mahali na kuwaua. Haiwezekani kuwa na idadi kamili lakini makadirio ya chini yanataja Watutsi 750.000 na Wahutu wasio wakali zaidi ya 100.000 waliuawa na Interahamwe na wanajeshi wa serikali ya Kihutu. Watu walikimbilia na kutafuta hifadhi makanisani lakini hata huko walichinjwa bila neema. Wahutu waliokataa kushiriki katika mauaji waliuawa pia.
RPF chini ya uongozi wa Paul Kagame iliamua kutumia nguvu zote kusimamisha machinjo haya. Kwa miezi miwili mauaji na vita yalienda sambamba hadi RPF iliposhinda Julai 1994 na kuchukua madaraka ya serikali.
Jeshi, Waparmehutu na serikali ya Kihutu walikimbilia Kongo wakiwalazimisha wakazi wengi kuongozana nao hali iliyosababisha kutokea kwa makambi ya wakimbizi makubwa sana katika Kongo ya mashariki yaliyokuwa na idadi ya Wahutu milioni mbili. Walio wengi wamerudi baada ya kuimarika kwa serikali mpya.
Tangu ushindi wa kijeshi mwaka 1994, RPF walianzisha serikali ya umoja wa kitaifa. Rais alikuwa Pasteur Bizimungu mwanasiasa Mhutu aliyeshikamana na RPF Kagame akiwa makamu wake. Baada ya kupinduliwa kwa Bizimungu mwaka 2000 Kagame akawa Rais. 2003 palitokea uchaguzi wa kwanza wa kirai ambapo chama cha RPF chimi ya Jenerali Paul Kagame kilishinda.
Jeshi la Rwanda limeendelea kuwa na vita ndani ya Kongo likipigana na mabaki ya Interahamwe waliokuwa wanashambulia Rwanda mara kwa mara kutoka Kongo.
Kutokana na mauaji hayo ya 1994, mahakama ya kimataifa iliyopo nchini Uholanzi imeendesha hukumu nyingi kwa wahusika wake, vilevile mahaka ya kimataifa ya Arusha nchini Tanzania nayo imeendesha huku stahiki kwa wahusika,
Ndani ya Rwanda mahakama za vijijini zinazoitwa "gachacha" vilevile zimejaribu kutoa hukuma juu ya waliohusija na mauaji ya mwaka 1994.
Mapatano ndani ya Rwanda yamezidi kushamiri, huku Paul Kagame akionsha kuijenga vema Rwanda kwa mkono wa chuma, Mathalani: D.Gasangwa wa EACU arisisitiza kwamba "Sometime in April(2004)" movie, ilikuwa "ETHNIC CLEASING", si HOLOCOSTI!, kama ilivyoandikwa na Wazungu wa Magazeti ya Ulaya. Watu karibu 600,000 waliuawa Rwanda, na hapo Mkoa wa Kivu, Congo.
Afrika ina ujuzi sasa; kama ujuzi wa Kiarabu, Kiswahili, Kilingala, Kiwolof, Kiamharic. Utengamano wa siasa mpya rasima utatupa na fasi ya kujenga inchi mpya kama EACU na Rwanda Kazembe.
Lakini huku mapambazuko mema yakitamalaki Rwanda, Kiongozi wa utawala wa nchi hiyo ndogo, anatajwa kuwa ni miongozi mwa viongozi makupe barani Afrika, ukupe wake sio waufisadi bali ukwasi wenye chembe za kiyunani
Lakini leo yale mabaki ya vikundi vile vya Interahamwe vilivyokimbilia uhamishoni kaskazini mwa Kongo mji wa Goma na Kivu si vikundi vya uasi dhidi ya Rwanda tena bali ni vitendea kazi muhimu dhidi ya upanuzi wa miliki mpya ya Watusi,
Wale watusi waliokimbilia Uganda enzi za Mwami Kigeri V, Inatajwa na kuaminika kuwa Jenerali Paul Kagame, Yoweri Mseveni na Watutsi waliokimbilia Goma baada ya kushika dola zao, walikuja na malengo mujarabu yanayotekelezwa kwa hatua na kwa vipindi virefu sana,
Mpango huo ulikuwa ni kusimika dola imara la Watutsi barani Afrika hasa nchini Kongo katika Goma-Kivu ya Kasiskani mpango siri walioupa jina la "Nchi mpya ya ahadi ya Watutsi". Ni mpango endelevu ulio na lengo la kuwakusanya Watutsi duniani kote na kuwaweka pamoja wakimiliki ardhi na rasilimali zake!
Hili linathibitika katika kile walicho "Mkataba wa kuigawa Kongo" ulisainiwa na Yoweri Mseveni, Paul Kagame na Laurent Kabila akiomba msaada wa kuingia madarakani kwa mtutu wa bunduki,
Naam baada ya Laurent Kabila kuingia madarakani kwamsaada wa Kagame na Mseveni kupitia ule mkataba, Kabila alikataa kuheshimu mkataba ule nakusema yale yalikuwa ni maneno ya porini tu hivyo hawezi kuiuza nchi kwa karatasi za mstuni!
Hapo sasa ndipo tunapoingia kwenye madhila ya Kongo tuliyoyaona tangu mauaji ya L. Kabila na tunayoyashuhudia hii leo chini ya J. Kabila, M23, Kagame na Mseveni
.............................. ...........
MKATABA WA KUIGAWA na KUIUZA KONGO
Kinachoitwa vita vya sasa nchini Kongo ni utekelezaji wa “Makubaliano ya Lemera” ya mwaka 1996 yenye shabaha ya kuigawa nchi hiyo kubwa kuliko yoyote ile Afrika Mashariki na Kati.
Makubaliano yalifanywa kati ya Laurent Desire Kabila, akiwa kiongozi wa chama cha “kuikomboa Kongo” kutoka utawala wa dikteta Mobutu Sese Seko, kwa upande mmoja; na wapiganaji wa Kinyarwanda kutoka Rwanda na Mashariki mwa Kongo.
Makubaliano ambayo yalifanyika kwenye vilima vya Lemera vilivyoko Kivu ya Kusini na kujulikana kwa jina hilo, yalitaka Kabila, baada ya kuwa rais wa Kongo, aruhusu mikoa miwili ya Kivu Kaskazini na Kusini kuwa makazi ya Wanyarwanda wa kabila la Kitutsi.
Taarifa zilizopo zinaonyesha makubaliano yaliandaliwa mapema mjini Kigali na pale Lemera yalikuwa yanazinduliwa tu. Ilikubaliwa wakati huo kwamba hiyo ndiyo ingekuwa “asante” kwa Rwanda “kwa ukombozi wa Kongo.”
Desire Kabila alikuwa tayari amechoka. Kwa takriban miaka 20 alikuwa akipambana na utawala wa Mobutu Sese Seko. Alikuwa amefikia hatua ya kukata tamaa na kutulia jijini Dar es Salaam.
Mwaka 1996, mjini Kigali, Rwanda kilikuwa kimeundwa kikundi cha wapiganaji waliojiita “wapinzani wa dikiteta Mobutu.” Hawa walikuwa Wakongomani na Wanyarwanda kutoka Rwanda na wengine waliokuwa wakiishi mkoa wa Kivu Kusini, Mashariki mwa Kongo.
Katika kundi hilo alikuwemo Mkongomani, Jenerali Andre Kisasi Ngando; askari mtaalam wa kusomea. Anadaiwa kupata mafunzo nchini Cuba, Ujerumani na Bulgaria. Alikuwa akiongoza Wakongomani wapatao 600 katika kikundi hicho.
Wakati kikundi hicho kinataka kuanza vita, kilitaka kuwa na msemaji. Mungu akupe nini! Hakuna uthibitisho wowote, lakini taarifa zinaeleza kiliomba ushauri wa Mwalimu Julius Nyerere “ambaye aliwapa Laurent Desire Kabila kuwa msemaji wa wapiganaji.”
Mwanzoni mwa vita ya kumg’oa Mobutu kikundi hiki kilijulikana kama cha Wanyamulenge. Dunia nzima ikaambiwa na kuaminishwa kuwa hayo yalikuwa “maasi ya Wanyamulenge.”
Wanyamulenge ni watu wanaodaiwa kutoka kwenye vilima vya Mulenge vilivyoko wilaya ya Uvira katika mkoa wa Kivu Kusini. Makabila ya asili ya hapa ni Wavira na Wafuliro. Wanaojiita Wanyamulenge ni Wanyarwanda wakuja.
Vita vilianza kwa propaganda kuu kwamba serikali ya Mobutu haitambui Wanyamulenge ambao walidai ni raia wa Kongo; inawanyanyasa na inawanyima uraia. Haya yalikuwa madai makubwa sana yaliyovuta hisia kali na huruma kwa wapiganaji.
Wapinzani, chini ya Jenerali Andre Kisasi Ngando, na msemaji mkuu wao Laurent Kabila waliteka, kama mchezo, mji mkuu wa Kivu Kaskazini, Goma. Wakavuka Ziwa Kivu na kuingia Kivu Kusini.
Ilikuwa baada ya kukamata mji wa Bukavu, makao makuu ya Kivu Kusini na sehemu nyingi za mkoa huo, wapiganaji wa Kinyarwanda waliingiza pendekezo la rais ajaye wa Kongo, kutoa Kivu Kaskazini na Kusini kwa Rwanda.
Lakini kabla suala hilo nyeti kupewa uzito unaostahili, wapiganaji wa Kinyarwanda, baada ya kuteka Bukavu, wanadaiwa kuanza kupora mali – magari, vifaa vya nyumbani, dawa katika maduka – hatua ambayo ilielezwa kuwa uhamishaji wa mali za wakazi wa Bukavu na maeneo mengine.
Alikuwa Jenerali Ngando anayeripotiwa kupinga uporaji usiomithilika, jambo ambalo lilimletea uhasama kwa baadhi ya wapiganaji. Kuona hivyo, Laurent Kabila akamwasi Ngando.
Ngando anasemekana kuuawa siku chache baada ya kutofautiana na wapiganaji juu ya uporaji. Inaelezwa kuwa alimiminiwa risasi na kuuawa na mwili wake kuchomwa moto katika mbuga ya wanyama ya Virunga.
Kabila aliulizwa mara nyingi juu ya Ngando. Alikuwa na majibu tofauti. Akiwa bado msituni alisema Jenerali Ngando amekamatwa na majeshi ya serikali na mara ametekwa na wanamgambo wa Mai Mai.
Baadaye Kabila alisema Ngando alijeruhiwa na kupelekwa Ujerumani kwa matibabu. Na wakati akiwa rais, aliwaambia waandishi wa habari mjini Kinshasa kuwa Ngando alikuwa askari kama askari wengine na kwamba alikufa kwenye mapambano.
Ilikuwa baada ya kifo cha Jenerali Ngando ndipo Kabila aliingizwa kwenye makubaliano ya kumega Kongo. Kwanza, kikundi cha wapiganaji kiligeuzwa kuwa chama – AFDL – Alliance de front Democratique pour la Liberation du Congo.
Kabila akapanda cheo na kuwa kiongozi wa chama cha ukombozi wa Kongo kutoka kuwa msemaji tu wa wapiganaji.
Baada ya kuundwa kwa AFDL, jina la Wanyamulenge likatoweka kabisa. Wapiganaji wakaitwa waasi wa Kongo. Taarifa zinasema kabla wapiganaji kutoka Bukavu na kuanza safari iliyomfikisha Kabila madarakani, waliingia katika mkataba ambao ndio umekuja kuitwa “Makubaliano ya Lemera.”
Kuna madai kwamba viongozi wakuu wa wakati huo wa baadhi ya nchi walipata nakala ya makubaliano hayo ya kumega Kongo. Miongoni mwa nchi hizo ni Namibia, Uganda, Burundi, Zambia, Ethiopia, Eritrea, Zimbabwe, Angola, Namibia, Sudan na baadhi ya nchi za Ulaya na Marekani.
Imeelezwa kuwa makubaliano ni pamoja na kufanya mikoa ya Kivu Kaskazini na Kusini kutawaliwa na Wanyarwanda wa Kitutsi kutoka mataifa ya Rwanda, Burundi na Uganda; na kwamba utawala huo ambao ungefanya kazi kwa ushirikiano na serikali ya Kabila, ungetekelezwa kwa awamu tatu katika kipindi cha miaka 10 kuanzia 1998.
Chini ya mpango huo, raia wa Kongo, wakazi wa Kivu Kaskazini wangehamishiwa Kivu Kusini, “taratibu na kwa utulivu huku makazi yao yakichukuliwa” na wavamizi.
Imeelezwa kuwa hatua ya kwanza isingekuwa ngumu kwani Rwanda ingedai kuwa inapambana na wanamgambo wa Kihutu walioitwa Interhamwe ambao itaelezwa kuwa wanatishia amani nchini Rwanda. Hivyo ndivyo imekuwa ikifanya hadi sasa.
Makubaliano yanadaiwa kueleza kuwa kuchukuliwa kwa miji ya Goma na Butembo mkoani Kivu Kaskazini, sharti iwe hatua ya kwanza kwa kuwa hayo ndiyo maeneo yenye upinzani mkubwa. Kufanikiwa kwa awamu ya pili, kungetegemea mafanikio ya awamu ya kwanza, makubaliano yanadaiwa kueleza.
Wafuatiliaji wa mahusiano ya Rwanda na Kongo wanasema ingawa mpango huo ulishindikana kutekelezwa kuanzia mwaka 1998, kuingia kwa majeshi ya Rwanda nchini humo hivi sasa, ni utekelezaji wa hatua ya kwanza ya Makubaliano ya Lemera; na tayari miji ya Goma na Butembo iko chini ya kile kinachoitwa “majeshi ya ushirikiano” ya Rwanda na Kongo.
Kwa mujibu wa masimulizi juu ya makubaliano hayo, awamu ya pili ingekuwa kujaza wakazi wa Kaskazini katika Kivu Kusini na kufanya uchaguzi wa serikali za mitaa ambapo wazawa wangeenguliwa, kukosa uongozi na hivyo kunyimwa sauti.
Hatua nyingine ilikuwa kuanzisha benki ya kusaidia wavamizi katika Kivu mbili, kujenga nyumba zipatazo 600,000 na kujiimarisha katika nchi ya kigeni – Kongo.
Imeelezwa kuwa Kabila alikubaliana na masharti ya makubaliano kwa kuwa lengo lake lilikuwa moja tu: Kuingia ikulu ya Kinshasa kwa msaada wowote kutoka kwa yeyote; Mungu au shetani.
Ilikuwa baada ya makubaliano hayo, Kabila alisonga mbele na hatimaye kushinda na kuingia ikulu ya Kinshasa akiwa na wapiganaji wa Rwanda, akiwemo mkuu wa sasa wa majeshi wa Rwanda, James Kabarebe.
Baada ya kuingia ikulu, Kabila anadaiwa kuwageuka wenzake. Ilikuwa baada ya miaka miwili ya urais, alitangaza, tena kwa jeuri, kuwa wageni wote waondoke nchini. Aliongeza kwa kufafanua, kwamba Wanyarwanda warudi kwao na kusema anawashukuru kwa kazi waliyofanya.
Kabila alikuwa tayari amesoma mwelekeo wa makubaliano yake na kuona kuwa yanatoa mwanya kwa kile kilichoitwa “Nchi ya Ahadi” ya Watutsi kutoka Rwanda, Burundi, Uganda, Somalia, Ethiopia, Eritrea na Tanzania.
Alitakiwa atangaze, akiwa rais, kuwa Kivu mbili zote ni makazi ya Watutsi; ili hata wananchi wa Kongo watakaobaki humo, wawe wanafahamu kwamba siyo kwao.
Kabila alinukuliwa akisema kuwa hayo (Makubaliano ya Lemera) ni “makubaliano ya porini” na kwamba yeye hakuwa na madaraka ya kuuza nchi. Alisema hakatai kuwepo mkataba, lakini akataka hilo “lipelekwe kwa wananchi – kupitia bungeni – ili wananchi wenyewe waamue.”
Kilichomshangaza zaidi Kabila, baada ya kutangaza kuwa Wanyarwanda warudi kwao, ni kwamba aliyekuwa wa kwanza kuondoka na kukimbilia Afrika Kusini, alikuwa waziri wake wa mambo ya nje aliyeitwa Bizima Karaha (Bizimana Karahamuheto).
Katika mshangao na labda kejeli, Kabila alisema, “Kumbe nchi ilikuwa imevamiwa! Hata waziri wangu wa mambo ya nje alikuwa Mnyarwanda?”
Hiyo ilifuatiwa na kufukuzwa kwa James Kabarebe aliyekuwa mkuu wa majeshi ya Kongo na sasa mkuu wa majeshi ya Rwanda. Hatua hizi na nyingine, ndizo zilisababisha kutotekelezwa kwa Makubaliano ya Lemera.
Lakini wachunguzi na wafuatiliaji wa mahusiano ya nchi hizi mbili wanasema, makubaliano yameandikwa na yapo; hayajafutika. Kilichofanyika ni “ukaidi wa Kabila” wa kutotaka kutimiza ahadi yake baada ya kuingia ikulu.
Kabila anasemekana alikuwa amesoma kitabu cha Raphael Ntibazokiza kikieleza mahusiano ya Watutsi na wabantu, kiitwacho Plan de la colonisation tutsi au Kivu et region centrale de l’Afrique – Mpango wa ukoloni wa Kitusi katika Kivu na eneo la Afrika ya Kati.
Raphael anaandika, “Mhutu ameumbwa kufanyia kazi watu wengine; hawezi hata kujaribu kupata uongozi. Chukua nafasi zote za mikoa na wilaya na atakayekuwa mtawala ahakikishe kuwa analinda maslahi yetu... Baadaye watakapokuja kustuka, watakuwa wamechelewa…”
Mmoja wa waliokuwa karibu na Laurent Kabila amenukuliwa akisema hakuna kitu kilichomsononesha Kabila kama kauli ifuatayo ndani ya kitabu cha Raphael:
“Tutumie ukarimu wao. Tujinyenyekeze kwao kama sisi ni watumishi wao.
Tukiishachukua nafasi zao tuwatelekeze na ‘kuwalipa ujira wa nyani’- payez-les en monnaie de singe pour montrer leur incapacite – ili kudhihirisha kuwa hawana uwezo.”
Kabila aliuawa kabla hajamaliza kunyukana na Rwanda. Aliuawa na mmoja wa “watoto” wake – vijana wadogo waliokuwa watu wa karibu sana na waliomlinda tangu akiwa msituni.
Kuna maelezo tatanishi juu ya kifo chake. Kuna wanaodai aliyemuua alitumwa na waliokuwa wakitaka atekeleze makubaliano ya Lemera; lakini wengine wanadai ni karata za nchi za Magharibi.
Kwa kuwa Jonas Savimbi aliuawa katika wiki moja tu baada ya kifo cha Kabila, inadaiwa kulikuwa na mkono wa mataifa makubwa; hili likitaka kuingia Kongo na hivyo kuomba msaada wa kuondoshwa kwa Kabila huku likiwezesha kukamatwa na kuuawa kwa Savimbi. Siasa hizi hazijafafanuliwa.
Kuingia kwa Joseph Kabila, anayedaiwa kuwa mtoto wa kufikia wa Laurent Kabila, kunaonekana kuleta mgeuko mwingine kuelekea kule ambako “baba” yake alikataa.
Kinachoitwa makubaliano kati ya serikali ya Rwanda na ile ya Kongo kinaonekana wazi kuwa utekelezaji wa mpango wa awali ambao Laurent Kabila alikataa.
Aidha, kukamatwa kwa Jenerali Laurent Nkundabatware na kuhifadhiwa nchini Rwanda kunaelezwa kuwa sura kamili ya “kuheshimu kazi ya maandalizi aliyokuwa akifanya nchini Kongo.”
Kuna madai kuwa Nkundabatware, Mnyarwanda kutoka Rwanda, lakini Rwanda inasema ni Mkongomani, hakuwa na jeshi lolote nchini Kongo. Aliongoza majeshi ya Rwanda hadi hapo ilipoonekana kuwa mazingira yamekuwa mazuri kwa Rwanda kuingilia kwa kisingizio cha “kufukuza Interhamwe na kuweka usalama mpakani.”
“Hata akipelekwa Kongo leo hii, Kabila atamlinda Jenerali Nkundabatware, labda kama wakuu wa Kongo na Rwanda watakuwa wamegundua kuwa amewasaliti,” kimeeleza chanzo cha habari hizi mjini Goma.
Rwanda imeingia Kongo. Nani ataiondoa? Baadhi ya nchi jirani zimekuwa watazamaji tu wakati nyingine zikiwa katika maandalizi ya kunufaika kutokana na mgogoro wa nchi hii.
Moses Byaruhanga, waziri katika ofisi ya rais (Siasa) nchini Uganda, amesema nchi yake inaunga mkono “shirikisho la Kivu na Kisangani” na kwamba wanasubiri kuona serikali ya Kinshasa inalionaje suala hilo.
Katika siku za karibuni kumekuwa na taarifa za kukamilisha kumegwa kwa mikoa miwili ya Kivu Kaskazini na Kusini kutoka Jamhuri ya Kongo na kuzifanya muungano wa Jamhuri ya Kivu.
Kauli ya msemaji wa ikulu Uganda inaongeza uwezekano wa kuimega Kongo pale inapohusisha jimbo jingine la Kisangani ambako majeshi ya Uganda yanadai kuwinda waasi wa Lord’s Resistance Army (LRA).
Kiongozi wa LRA, Joseph Kony amekuwa akipambana na majeshi ya serikali ya Yoweri Museveni kwa zaidi ya miaka 15. Uganda sasa inadai kuwa Kongo inatumika kama kichaka cha waasi hao.
Kauli ya Uganda haipishani na mipango inayodaiwa kufanywa na Rwanda ingawa Rwanda, kupitia balozi wake mjini Dar es Salaam ilikaririwa ikisema haina mpango wowote wa kuigawa Kongo.
Jumuiya ya kimataifa imetekwa kwa propaganda za Interhamwe, Wanyamulenge, waasi wa LRA na kumbukumbu za mauaji ya kimbari.
Isipokuwa Barrack Obama ambaye angalau amesema anataka Kongo tulivu na kwamba atasaidia kuleta hilo, mataifa mengine, pamoja na Ufaransa, yanataka kuimega Kongo.
Vielelezo:
Moabi KKK/BKK
Yunani
Wikipedia
Tutsi
Hutu
Twa
Paul Kagame
Laurant Kabila
Yoweri Mseveni
MwanaHalisi
Mimi Mwenyewe
Showing posts with label TANZANIA. Show all posts
Showing posts with label TANZANIA. Show all posts
6 May 2016
- 6.5.16
- Evarist Chahali
- TANZANIA
- 1 comment
Bila shaka matokeo ya utafiti huu yatawashangaza watu wa nchi nyingine, lakini sio sie Watanzania, ambao tumebainika kuwa watu wanafiki zaidi kuliko wote duniani. Sio jambo la kushangaza kwa sababu unafiki umekuwa sehemu ya utamaduni wetu.
Na mfano mwepesi wa unafiki wetu ni kuhusu uamuzi wa serikali kuipiga marufuku video ya msanii Snura iitwayo 'Chura' ambayo ilivuka mipaka ya ustaarabu. Awali, watu wengi waliishutumu Serikali kwa kuruhusu video hiyo 'chafu' kuonyeshwa ilhali vikao vya bunge vikizuiwa kuonyeshwa 'live.' Well, japo bunge laendelea 'kufichwa,' lakini serikali imejitutumua na kipiga kufuli video ya 'Chura.'
Lakini hatua hiyo imewakera baadhi ya wenzetu. Wengine wanadai serikali ina vitu muhimu zaidi vya kufanya badala ya kufungia video. Wengine wanadai mbona kuna video chafu zaidi za 'akina Rihanna' kuliko hiyo ya Chura. Wengine wanakwenda mbali na kudai kuwa alichofanya Snura na hao mabinti wa kwenye video ni UBUNIFU. Really?????
Twende kwenye maisha yetu ya kila siku. Tuchukulie mfano vifo. Utakuta watu wanasubiri mpaka mtu afe ndio waanze kumwagia sifa, "Oh marehemu alikuwa mtu mzuri sana, oh marehemu alikuwa mwema sana...RIP...RIP..." Hii tabia ya kuwapenda watu wakifa lakini kuwachukia walipokuwa hai ni nini kama sio UNAFIKI? Angalia Marehemu Kanumba alivyoandamwa wakati wa uhai wake. Msanii aliyefanya kazi kubwa kabisa kuiinua medani ya filamu za Kitanzania aliandamwa mfululizo na hili na lile, huku watu wasio na vipaji ya kitu chochote kile wakigeuka mahakimu na majaji dhidi ya kipaji cha msanii huyo.
Tuangalie huko mitaani tunakoishi na 'makazi yetu mapya' mitandaoni. Huko mitaani, wenzetu wenye umuhimu mkubwa kwa jamii - madaktari, manesi, walimu, nk - hawapewi heshima kubwa kulinganisha na wanayopewa wahalifu kama wauza madawa ya kulevya au wabadhirifu serikalini. Twaita wauza unga WAZUNGU WA UNGA, na wabadhirifu twawaita MAPEDEJEE, VIBOSILE, VIGOGO, na majina mengine ya kuwatukuza, ilhali jina lao stahili ni WAHALIFU.
Nenda mtandaoni, kwa mfano Instagram. Ukiacha wasanii wetu na watu wengine muhimu, watu maarufu zaidi katika mtandao huo kwa Tanzania ni wale wenye kuongoza makundi ya matusi, picha za utupu, majungu, na madudu kama hayo. Sio kwamba hawa 'wameroga' ili kuwa maarufu. Hapana. Umaarufu wao unatokana na Watanzani wengin kupenda vitu hivyo: picha za utupu, majungu, nk.
Angalia wakati wa uchaguzi. Wanasiasa wetu hujiweka karibu kabisa na wananchi. Si ajabu kuona mwanasiasa akiwasalimia wananchi kwa kupiga magoti 'kwa heshima' wakati anaomba kura.Subiri ashinde uchaguzi. Humsikii japo akicheka au kuzomea bungeni. Unaweza kuhisi kuwa asilimia kuwab ya wabunge wetu wanatoka majimbo ya nchi kama Uingereza au Marekani, ambazo zina matatizo machache kwa wapigakura, kwani haiingii akilini kwa mbunge ambaye jimbo lake lina matatizo lukuki awe haonekani bungeni unless kwenye kukusanya posho tu, na akitokea bungeni, si ajabu kuona amepigwa picha huku kachapa usingizi (labda alishindwa kulala kutokana na kuzongwa na mawazo kuhusu jimbo lake?)
Anyway, turudi kwenye utafiti unathibitisha tulivyobobea kwa unafiki. Watafiti kutoka Chuo Kikuu cha Nottingham cha hapa Uingereza waliendesha utafiti wa kupima kushamiri kwa ukiukwaji wa kanuni katika nchi 159 duniani, wakitumia takwimu za kutoka mwaka 2003 kuhusu ubadhirifu katika siasa, ukwepaji kodi na rushwa.
Twende tena mtaani. Kuna suala la ushoga ambalo taarifa zinaeleza kuwa unakua kwa kasi huko nyumbani. Juzi kuna shoga mmoja kafiwa Dar, na inaelezwa kuwa takriban kila mtu maarufu jijini hapo hakukosekana msibani. Lakini sio katika msiba huo tu, nenda Instagram halafu angalia akaunti za mashoga na idadi ya 'followers' wao. Hivi yawezekanaje kama 'ushoga sio tu ni laana bali pia ni kinyume cha sheria za Tanzania,' then shoga awe na 'followers' zaidi ya laki moja? Kwanini kila shughuli ya mastaa wetu haiwi kamili bila uwepo wa mashoga wa 'kukata viuno' kwenye shughuli hiyo?
Habari kamili kuhusu utafiti huo ipo HAPA na kuna MAKALA HII katika gazeti la kila wiki la RAIA MWEMA Toleo la wiki hii imeandika kwa kirefu kuhusu suala hilo
1 Apr 2016
- 1.4.16
- Evarist Chahali
- MAREKANI, MCC, TANZANIA, ZANZIBAR
- No comments
Moja ya masuala yanayotawala anga za habari na
mijadala mbalimbali mtandaoni ni uamuzi wa bodi ya taasisi ya Changamoto ya Milenia
(Millennium Challenge Corporation) ya Marekani kusitisha misaada kwa Tanzania.
Sababu kuu mbili zilizotolewa na bodi hiyo kuhusu uamuzi huo ni marudio ya
uchaguzi huko Zanzibar Machi 20, mwaka huu, ambao licha ya kususiwa na chama
kikuu cha upinzani cha CUF, ulilalamikiwa kwa kiasi kikubwa na nchi wahisani,
ikiwa ni pamoja na Marekani.
Sababu ya pili, kwa mujibu wa bodi hiyo, ni uamuzi wa
serikali ya Tanzania kupitisha Sheria Uhalifu wa Mtandaoni (Cybercrime Act) ya
mwaka 2015 licha ya upinzani mkali dhidi ya muswada wa sheria hiyo,
iliyotafsiriwa kuwa imemlenga kukandamiza uhuru wa habari na haki za binadamu.
Kabla ya kuingia katika uchambuzi huu kiundani,
nieleze mtazamo wangu kuhusu sababu hizo mbili zilizotolewa na bodi ya MCC.
Kwanza, kwa mtazamo wangu, suala la marudio ya uchaguzi wa Zanzibar ni mzaha wa
kidemokrasia, na ni jeraha la kisiasa ambalo historia inaweza kutuhukumu huko
mbeleni. Haihitaji uelewa mkubwa wa siasa za Zanzibar kufahamu kuwa kuna ‘sheria
isiyo rasmi’ kuwa ‘kamwe CUF hawapaswi kutawala Zanzibar.’ Bila kuuma maneno,
hiyo ndo sababu pekee ya kufutwa kwa uchaguzi wa awali (ambao inadaiwa mgombea
wa CUF, Seif Shariff Hamad, alishinda), na kuamiriwa uchaguzi huo urudiwe huku
CCM ikiwekeza nguvu zake zote kuhakikisha inashinda. Hata kama CUF wasingesusia
uchaguzi huo, bado CCM wangeshinda kwa sababu ‘ni lazima iwe hivyo,’ kwa ‘kanuni’
zao.
Je MCC ipo sahihi kutumia kigezo cha Zanzibar
kusitisha misaada yao? Kwa upande mmoja, wapo sahihi. Kwanini? Kwa sababu, hata
katika mahusiano yetu ya kawaida tu kibinadamu, anayekupa msaada anapata ruhusa
pia ya ‘kukutawala’ kwa kukupa masharti ambayo ukiyakiuka, yanaweza kuathiri
mahusiano katika ya mtoa msaada na mpokea msaada. Miongoni mwa masharti ya MCC
ni pamoja na masuala ya demokrasia, na haihitaji kukuna kichwa sana kubaini
kuwa marejeo ya uchaguzi wa Zanzibar, ambayo binafsi ninayaona kuwa ni mzaha wa
kidemokrasia, yamewapa MCC ‘kisingizio chepesi’ hata kama hawangekuwa na sababu
nyingine.
Mgogoro wa muda mrefu wa kisiasa huko Zanzibar ni
zaidi ya jipu. Ni kansa ambayo imeshachafua sura ya Tanzania huko nyuma ambapo
kwa mara ya kwanza tulizalisha wakimbizi baada ya vurugu za uchaguzi mkuu mwaka
wa 2000. Ni kansa ambayo sasa imewapa MCC kisingizio cha kutunyima misaada yao.
Kwa bahati mbaya, au makusudi, hakuna utashi wa kisiasa wa kusaka ufumbuzi wa
kudumu wa mgogoro huo. Kila kiongozi wa CCM, kwa upande wa Bara, anaogopa suala
hilo kwa kuhofia ‘kuvunjikiwa na Muungano mikononi mwake.’
Wanasiasa wa Zanzibar sio tu wanaufahamu udhaifu huo
bali pia wanautumia vema. Wanaendesha siasa zao cha chuki na uhasama watakavyo
wakifahamu fika kuwa hakuna mwana-CCM wa Bara mwenye jeuri ya kuwaingilia.
Sina hakika Zanzibar itaathirika vipi kwa maamuzi ya
MCC kukata misaada, lakini kinachowapa kiburi viongozi wa huko ni kwamba ‘Tanganyika’
haina jeuri ya kuisusa Zanzibar, au kuinyooshea kidole katika mwendelezo wa
siasa za chuki na ubaguzi.
Lakini kwa upande wa pili, hao MCC ni wanafiki tu.
Huhitaji kuwa na uelewa mkubwa wa siasa za kimataifa kutambua unafiki wa
Marekani linapokuja suala la demokrasia. Nchi hiyo ni mshirika mkubwa wa tawala
za kidikteta kama vile huko Misri, Saudi Arabia na kwingineko. Sawa, labda
Zanzibar wamefanya mzaha wa kidemokrasia lakini vipi kuhusu demokrasia isiyopo
kabisa huko Saudi? Well, jibu rahisi ni kwamba Zanzibar na Tanzania sio muhimu ‘kihivyo’
kwa Marekani ilhali taifa hilo linazitegemea mno tawala za kibabe za nchi kama
Misri au Saudi, hususan katika masuala ya ushushushu/mapambano dhidi ya ugaidi
wa kimataifa.
Kuhusu suala la Sheria ya Uhalifu wa Mtandao, hapa
kumesheheni unafiki, na upo wa aina mbili: wa Wamarekani na wa sie Watanzania
wenyewe. Mie ni mfuatiliaji wa karibu wa masuala ya usalama mtandaoni, ambao
kwa namna moja au nyingine unahusiana na hiyo ishu ya Cybercrime Act. Kwa
kifupi tu, Marekani ina sheria kandamizi mno dhidi ya uhuru wa raia mtandaoni.
Naamini ushaskia kuhusu jamaa anayeitwa Edward Snowden (kama hujamsikia, Wasiliana
na Google…haha). Huyu bwana alikuwa mtumishi katika shirika la ushushushu la
Marekani linalohusika na kunasa mawasiliano mbalimbali (NSA – National Security
Agency), na baadaye nafsi yake ilimsuta, akaamua ‘kuingia mitini’ na kumwaga
siri lukuki kuhusu jinsi NSA inavyohujumu haki za raia kimawasiliano. Hawa
jamaa wamekuwa wakinasa mawasiliano ya takriban kila mtu, wakishirikiana kwa
karibu na mashushushu wenzao wa hapa Uingereza, GCHQ, taasisi ya kishushushu
inayohusika na kunasa mawasiliano.
Lakini hata tukiweka kando suala la NSA kunasa
mawasiliano mbalimbali (waliwahi kuzua kasheshe kubwa baada ya mashushushu wa
Ujerumani kubaini kuwa NSA walikuwa wakinasa kwa siri mawasiliano ya Kansela
Angela Markel hadi waliposhtukiwa), mashambulizi ya kigaidi nchini humo mwaka
2001 yalipelekea kuundwa kwa sheria kali kabisa dhidi ya uhuru wa habari na
haki za kibinadamu kwa kisingizio cha usalama wa taifa. Kwahiyo, kwa kifupi, ni
uhuni tu wa Marekani kudai Sheria ya Makosa ya Mtandaoni inakiuka uhuru wa
Watanzania. Sheria zao za wazi na za kificho ni mbaya mara milioni zaidi yetu.
Hata hivyo, katika suala hili la Cybercrime Act, tuna
wanafiki kadhaa huko nyumbani. Kwa kumbukumbu tu, mie nilikuwa mtetezi mkubwa
wa muswada uliozaa sheria hiyo, yaani Cybercrime Bill, na niliunga mkono kwa
nguvu zote jitihada za aliyekuwa Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na
Teknolojia, January Makamba, kuhusu muswada huo.
Hata hivyo, baadhi ya watu wanaoinyooshea kidole
Marekani na wafadhili wengine kuhusu suala la Tanzania kukatiwa misaada
walikuwa mstari wa mbele kuziomba nchi wahisani ziingilie kati kuibana serikali
ili muswada huo usipitishwe kuwa sheria. Sasa kama uamuzi huo wa Marekani
umechangiwa na ‘kelele’ zao hizo, kwanini leo wanalalamika?
Mie niliunga mkono muswada na sheria hiyo kwa sababu
ikitumiwa vema ni nzuri. Hebu nenda Instagram kaangalie uanaharamu unaoendelea
huko, kuanzia picha za uchi, ushoga na kila aina ya laana. Huo sio uhuru wa
habari, ni uwendawazimu ambao kwa hakika ulihitaji sheria kali kuudhibiti.
Na watu waliopita huku na kule kudai sheria hiyo ni
kandamizi na ililenga kuwabana wananchi wasiwasiliane, hawatuambii kama baada
ya sheria hiyo kupitishwa wameshindwa kuwasiliana na watu wengine. Kwa kifupi,
kulikuwa na udanganyifu mkubwa katika kambi ya waliopinga muswada na sheria
hiyo. Walitumia uelewa mdogo wa wananchi wengi kuhusu masuala ya mtandao, na
kuwajenga hofu feki.
Ninakerwa kuona kundi la wanafiki hawa likiilaumu MCC
au Marekani au nchi nyingine wahisani kuhusu suala la kutukatia misaada, kwa
sababu wao walikuwa mstari wa mbele kuhamasisha nchi wahisani zichukue hatua,
na ‘hatua maarufu’ ya wahisani huwa ni kukata misaada. Badala ya kulalamika,
wanafiki hawa wanapaswa kufanya sherehe maana wishes zao zimetimia.
Sasa niangalie upande wa athari za uamuzi huo wa MCC
kukata misaada. Taarifa nyingine zinaeleza kuwa kuna wahisani wengine nao
wamekata misaada japo kuna mkanganyiko kama hatua hiyo ni mwendelezo wa hatua
za huko nyuma au ni mpya.
Tuwe wakweli, kwa watu masikini kama sisi, hatua
yoyote ile ya kutupunguzia msaada wa aina yoyote ile itatuathiri. Hilo
halihitaji uelewa wa jinsi gani misaada inavyofanya kazi au jinsi gani nchi
yetu ilivyo mtegemezi mzoefu wa misaada. Tatizo kubwa hapa kuhusu “kukatiwa
misaada kutatuathiri au hakutatuathiri” ni tofauti zetu za kiitikadi. Kwa kiasi
kikubwa, suala hilo linaangaliwa katika lensi ya u-CCM na u-UKAWA/Upinzani. Kwa
wana-CCM, ni mwendo wa ‘kiburi’ kwenda mbele, kwamba “waende tu na misaada yao,”
au “hela yenyewe ilikuwa ya mradi wa kifisadi wa Symbion,” mara “ah misaada
gani hiyo yenye masharti kibao.” Wanamhadaa nani? Kama misaada hiyo haikuwa na
muhimu, kwanini basi tuliiomba in the first place? Hizi hadithi za sungura
kusema “sizitaki ndizi hizi” baada ya kushindwa kuzikia mgombani.
Kwa upande wa wana-UKAWA/Wapinzani, bila kujali kuwa
wao kama Watanzania ni wahanga watarajiwa wa uamuzi huo wa nchi yetu kukatiwa
misaada, wanakenua meno yote 32 kwa furaha, huku wakiwazodoa wenzao wa CCM kwa
vijembe kama “ndio matunda ya ubabe wenu huko Zanzibar, tuone sasa…” au “mtaisoma
namba” au “mtakula jeuri yenu…”
Ulemavu huu wa kifikra unaosababishwa na kuliangalia
suala la kiuchumi kwa mtizamo fyongo wa itikadi za kisiasa. Naam, suala la
Zanzibar ni la kisiasa, lakini athari za uamuzi wa Marekani/MCC/wahisani ni la
kiuchumi.
Mie sio mchumi ila ninachoelewa fika kuwa uchumi wetu
umekuwa tegemezi tangu tupate uhuru. Kabla ya kuipa kisogo siasa ya Ujamaa na
Kujitegemea, tulikuwa tukapata misaada kutoka kwa marafiki zetu wa mrengo wa
Ukomunisti. Baada ya kuuzika Ujamaa, tumekuwa kama puto linaloyumbishwa na
upepo, tupo radhi kumpigia magoti yeyote anayeweza kutusaidia. Kimsingi, tuna
ombwe la kiitikadi: majukwaani, CCM wanasema sie ni Wajamaa, vitendo vyetu
havipo kwenye Ujamaa wala Ubepari, tupu tupo tu. Huo ndo ukweli mchungu kuhusu
ubabaishaji wetu.
Kwahiyo, tuache kudanganyana kuwa kukatiwa misaada
hakutotuathiri. Huko ni kujipa jeuri tu. Tunachoweza kukubaliana ni kwamba
suala hilo limeshatokea, tumeshakatiwa misaada, na si ajabu wahisani wengine
wakaamua kufata mkumbo na kufanya hivyo pia.
Jukumu letu kubwa kwa sasa sio kuendelea kunyoosheana
vidole bali tuwe kitu kimoja kama taifa bila kujali nani hasa aliyetusababishia
tatizo hili. Ni tatizo la Watanzania wote bila kujali itikadi zao. Uamuzi wa
wahisani kukata misaada utawaathiri wana-CCM wanaodai hautowaathiri kama
ambavyo utawaathiri wna-CUF au Chadema wanaokenua meno yote 32 kufurahia hatua
hiyo. Na utatuathiri (angalau kisaikolojia) hata akina sie ambao itikadi yetu
pekee ni Tanzania yetu. Huo ni ukweli usiopingika: we are all in this together.
Kuna mambo mawili ya kupigiwa mstari. Kwanza, kwa
miaka mingi tumekuwa tukiishi kifahari mno kuliko uwezo wetu. Na kimsingi,
uwezo wetu duni haukupaswa kuwepo kwani sie sio masikini hata kidogo. Tuna kila
aina ya utajiri lakini kuna majambazi walioigeuza Tanzania yetu kuwa kitu cha
kubakwa kila kukicha. Kila mwenye uelewa anafahamu kilichojiri katika takriban miaka
30 iliyopita. Tanzania yetu ilikuwa shamba la bibi, watu wanafisadi wapendavyo
kiasi kwamba kuwa na uchungu na nchi ilionekana kama wendawazimu.
Kwa bahati nzuri, Mwenyezi Mungu amesikia kilio cha
baadhi yetu na sasa tumempata Rais, Dkt John Magufuli, ambaye anaonekana
amedhamiria kurekebisha mwenendo wa mambo. Kikwazo chetu kikubwa kilikuwa
ufisadi, lakini sasa Magufuli ameamua kuvalia njuga kupambana na ufisadi kwa
nguvu zote. Mwanzo ni mgumu lakini angalau dalili za mafanikio zimeanza
kujionyesha. Tumuunge mkono, tuchukie ufisadi, tuongeze uzalendo, tuikwamue
Tanzania yetu, tujikwamue nasi wenyewe, tuache kutafuta njia za mkato za
mafanikio, tufanye kazi, tache majungu na kusaka sifa za kijinga mitandaoni,
tuwajibike.
Twahitaji kujifunga mikanda. Haiwezekani wafadhili
wetu waishi kimasikini ilhali sie wafadhiliwa twaishi kama matajiri. Viongozi
wetu waache kuchuana na wauza unga kushindana jinsi ya kuishi kitajiri,
wawabane wauza unga hao, majangili na maharamia wengine ili tuiokoe Tanzania
yetu.
Je twaweza kujitegemea? Absolutely, lakini
tusidanganyane kuwa twaweza kufanya hivyo ghafla ghafla. Tukumbuke, mtoto
hazaliwi akatembea. Tumekuwa wategemezi mno wa misaada kiasi kwamba tumesahau
kuwa twapaswa kujitegemea. Twahitaji kuchukua na kukubali maamuzi magumu ya
kutuwezesha kujitegemea. Ni kama kumlazimisha mtoto anayetambua aanze kutembea
kwa nguvu. Sio rahisi, lakini tukimkazania anaweza kusimama mwenyewe na baadaye
akaweza hata kukimbia. Hilo linahitaji kujitoka mhanga kwa ajili ya nchi yetu,
sambamba na kuweka mbele uzalendo badala ya maslahi binafsi.
Jambo jingine, kwa hisia zangu, japo suala la Zanzibar
na Cybercrime Act zinatajwa kama sababu za uamuzi wa kutunyima misaada,
ninashawishika kuamini kuwa baadhi ya nchi wahisani hawapendezi na kasi ya Rais
Magufuli kuziba mianya ambayo kimsingi licha ya kuwanufaisha mafisadi wa ndani,
ilikuwa pia inanufaisha taasisi za kifisadi za kimataifa. Wengi wa majambazi
waliokuwa wakitupora fedha zetu mchana kweupe walikuwa hawahifadhi fedha zao
katika benki zetu bali zilizopo kwa hao wahisani wetu. Waweza kudhani huu ni
utani mbaya, lakini jiulize, je kama unamfadhili mtu pesa za kumsaidia yeye na
familia yake, lakini anatumia fedha hizo kununulia bling bling, kuongeza nyumba
ndogo, kufanya matumizi ya anasa, nk kwanini usichukue hatua?
Mfano huo unamaanisha hivi: kwanini wahisani wetu walionekana
kutokerwa na jinsi pesa walizokuwa wanatupatia zikifisadiwa kila kukicha lakini
wakaendelea kutumwagia misaada? Na kwanini sasa, tumempata Magufuli ambaye
amepania kwa dhati kupambana na ufisadi, wahisani wanaanza kuleta ‘longolongo’?
Kuna tunaodhani kuwa hao wahisani wanataka tuendelee
kuwa wategemezi wao milele. Kwa upande mmoja utegemezi wetu unawapa uhuru wa
kukwapua kila raslimali tuliyonayo, na kwa upande mwingine, wananeemesha
taasisi zao za fedha kwa vile mafisadi wetu wa ndani wanahifadhi fedha zao
kwenye taasisi hizo.
Mwisho, tuache porojo, tuache unafiki, tuwe kitu
kimoja, athari za kukatiwa misaada zipo, tukishikamana tutaweza kukabiliana
nazo japo mwanzoni itakuwa ngumu. Yawezekana uamuzi huo wa Wamarekani ukawa ‘blessing
in disguise’ kwa maana ya kutupa ‘wake-up call’ tuanze kujitegemea kwa lazima
badala ya kutembeza bakuli letu huko na kule, kisha kile kidogo kinachopatikana
kikaishia kwenye ujenzi wa mahekalu ya mafisadi, ongezeko la magari yao ya
kifahari, na kutanua ukubwa wa nyumba ndogo zao.
MUNGU IBARIKI TANZANIA
29 Mar 2015
Kwa muda mrefu, baadhi ya watumiaji wa mtandao wa kompyuta (Internet) wamekuwa na wakati mgumu kufuatia kushamiri kwa unyanyasaji mtandaoni, kwa kimombo CYBERBULLYING.
Kwa kiasi kikubwa, tatizo hili linaakisi tabia zetu nje ya mtandao. Mtu aliyezowea kunyanyasa wenzie mtaani, akiingia mtandaoni anaweza kuendeleza tabia hiyo kirahisi. Kadri mtandao unavyozidi kuwa sehemu ya maisha yetu ya kila siku ,ndivyo unavyoakisi maisha yetu 'ya kawaida' nje ya mtandao.
Kwa upande mwingine, mtandao unatoa fursa ya watu wenye tabia tofauti kukutana. Ndio maana si ajabu kukuta mtu mmoja akiweka bandiko kuhusu dini, mwingine akaweka bandiko kuhusu matusi.
Licha ya tabia, mtandao pia huwakutanisha watu wenye sifa tofauti: wapole na wakorofi, wapenda amani na wagomvi, wenye elimu na mbumbumbu, wenye aibu na wasio na mishipa ya aibu, nk.
Kadhalika, mtandao unatoa fursa mbalimbali, nzuri na mbaya. Kwa mfano, mtandao unatuwezesha kuwa karibu na viongozi wa nyanja mbalimbali, kutoka mawaziri hadi viongozi wa taasisi binafsi.Uzuri wa fursa hiyo ni pamoja na kurahisisha mawasiliano baina ya watu wanaotoka 'madaraja' tofauti ya kijamii. Kadhalika, fursa hiyo inatuwezesha kujifunza kutoka kwao, sambamba na kufuatilia masuala mbalimbali ambayo kutokana na nafasi zao yanagusa maisha yetu binafsi au ya jamii kwa ujumla.
Fursa hiyo pia inatuwezesha kuwa karibu na watu mbalimbali, muhimu na wa kawaida. Katika mazingira ya kawaida, ni vigumu kufahamiana na Waziri, kwa mfano, labda kuwe na undugu, kufahamiana au mahusiano kikazi.
Hata hivyo, mtandao pia unatoa fursa 'mbaya.' Binadamu tupo tofauti, kuna wenzetu ambao wakiiona fursa wanaitumia kwa manufaa, lakini kuna wengine sio tu hawataki kujifunza 'mazuri' ya wenzao (ambayo wao hawana) pia hujenga chuki na jitihada za kuwachafua au kuwadhalilisha wenzao wenye 'mazuri.' Kwa mfano, unaweza kukutana na mtu ambaye hakubahatika kupata elimu ya kutosha, au hakusoma kabisa. Anapokutana na mwenye elimu kiasi au ya juu, badala ya kutumia fursa hiyo kama 'darasa nje ya shule' anaanzisha chuki na uhasama usio na manufaa.
Kama dunia ilivyo uwanja wa fujo, ndivyo ilivyo kwa mtandaoni. Kuna mazuri na mabaya. Kuna baadhi yetu ambao tumenufaika sana kwa uwepo wetu mtandaoni, kwa maana ya kutengeneza urafiki na watu muhimu, lakini pia kuna nyakati tumejikuta tukikutana na 'maadui.'
Ofkoz, mtandano sio sehemu ya kubadilisha mawazo, kujifunza au kuuliza maswali tu bali pia ni sehemu ya burudani. Utani ni ruksa lakini utani wenyewe usizidi kiwango. Na kanuni ya mtaani kuwa usimtanie mtu asiyekutania, ina-apply mtandaoni pia.
Kwa bahati mbaya kuna wenzetu ambao hulazimisha utani.Wengine huenda mbali zaidi kwa kulazimisha kumjua mtu zaidi ya anavyojijua yeye mwenyewe.
Kwa bahati nzuri, hatimaye serikali imesikia kilio dhidi ya unyanyasaji wa mtandaoni na Jumanne ijayo inatarajia kuwasilisha muswada kuhusu uhalifu wa mtandaoni ambao pamoja na mambo mengine unaharamisha unyanyasaji wa mtandaoni (cyberbullying)
Katika muswada huo unajulikana kwa kimombo kama The Cyebrcrimes Act, 2015, ibara ya 23 inaharamisha unyanyasaji mtandaoni (cyberbullying) na kutaja adhabu husika.
Muswada unafafanua maana ya cyberbullying, kwamba "mtu hataruhusiwa kuanzisha au kutuma mawasiliano ya kielektroniki kwa kutumia kompyuta kwa mtu mwingine kwa malengo ya 'kumsukuma kwa nguvu' (coerce), kumtisha, kumyanyasa au kumsababishia msongo wa mawazo, na mtu atakayekiuka kipengele hocho atakuwa anafanya kosa, na adhabu yake ni sio chini ya shilingi milioni tatu au kifungo cha sio chini ya mwaka mmoja au adhabu zote pamoja."
Muswada kamili ni huu hapa chini (kwa bahati mbaya au makusudi, watawala wetu hawakuona umuhimu wa kuupatia tafsiri ya Kiswahili)
Wakati muswada huu ni habari njema kwa wahanga wa unyanyaswaji mtandaoni, unatarajiwa pia angalau kupunguza kushamiri kwa matusi na picha zisizofaa mtandaoni. Sio siri kwamba baadhi ya mitandao ya kijamii, hususan Instagram, imegeuka uwanja wa matusi.
Kibaya zaidi, umahiri wa matusi umegeuka moja ya vyanzo vya umaarufu mtandaoni. Kama nilivyobainisha hapo juu,mtandao unatoa fursa 'mbaya' kwa wenzetu wasio na cha kuelimisha, kujadili au hata kujivunia hadharani, na matokeo yake ni kuwabughudhi watu wengine au kubandika picha zisizofaa kama mbinu ya kusaka sifa za kipuuzi.
Hata hivyo, ni muhimu kukumbushana kuwa Tanzania yetu haina uhaba wa sheria.Tatizo kubwa ni katika kuziheshimu na kuzitekeleza. Twaweza kuwa na sheria kali dhidi ya uhalifu wa mtandaoni lakini utekelezaji ukiwa hafifu basi sheria hizo zitabaki maandiko tu vitabuni.
Kadhalika, ni muhimu kutahadharisha kwamba sheria hii ya uhalifu wa mtandaoni isitumiwe vibaya na serikali kuwanyima wananchi uhuru wa mawasiliano, au kibaya zaidi, kuitumia kwa minajili ya kuficha maovu na kuwalinda waovu. Sitarajii kuona sheria hii ikitumika iwapo chombo cha habari kitaibua utovu wa maadili wa kiongozi, kwa mfano.
Mwisho, ni matarajio yangu kuwa vitendo vya uhalifu wa mtandaoni, ikiwa ni pamoja na cyberbullying, vitapungua kufuatia sheria hii, iwapo itapitishwa na bunge. Angalau sasa, cyberbullies watafikiria mara mbili kabla ya kumwaga sumu zao kuwanyanyasa watu wasio na hatia.
14 Aug 2013
- 14.8.13
- Evarist Chahali
- DRC, PAUL KAGAME, Rwanda, TANZANIA, Uganda, Yoweri Museveni
- No comments
Ijue Rwanda, Kagame, Mseveni na Uvamizi wao katika Ardhi ya Kongo
18 Jul 2013
3 Jun 2013
1 Jun 2013
- 1.6.13
- Evarist Chahali
- Rwanda, TANZANIA
- No comments
The Tanzanian Foreign Minister Bernard Membe wondered at Rwandan government strange attitude to overreact on a simple advise given in good faith to the country in full presence of the Rwadan Delegation in Ethiopia saying it is up to them accept or refuse the advise.
The Foreign Minister also stated categorically that the government will not move even an inch to apologize Rwanda since he still believed that engaging the enemies was the best option for Rwanda which he said has failed to to find amicable solution through wars for more than 15engage the rebels in the last 16 years.
Speaking before parliament in Dodoma yesterday, the visibly irked Minister wondered as to why was making lots of politics with a simple advise that a they either dumed to accept or refuse to.
Using the famous quotation used once by the Former Israel Prime Minister, Yizak Rabin Mr Membe said "We negotiate peace with our enemies not our friends" adding that" there is no need for Rwanda to sound an alarm for the advise given in the open table in Ethiopia."
Assah Andrew Mwambene
Po box 9000 Dar es Salaam
Mobile +255782-553737
+255756887880
On 26 May 2013 in
Addis Ababa the UN Secretary General, Mr. Ban Ki-moon and the Chairperson of the
African Union Commission Dr. Nkosazana Dlamini Zuma, convened the
first meeting of the Regional Oversight Mechanism of the Peace,
Security and Cooperation Framework for the DRC and Region. It was at this
important meeting where the President of the United Republic of Tanzania, H.E. Jakaya
Mrisho Kikwete made what many level headed commentators have referred to as candid
and commonsensical remarks about the protracted conflicts in the Great Lakes
Region. President Kikwete - a seasoned and consummate diplomat who has helped
broker many peace deals in Africa - remarked that it was high time Rwanda and
Uganda gave serious attention to peace talks with FDLR and ADF rebels
respectively. He said, and correctly so, that it was evident the barrel of the
gun cannot bring about the ultimate answer as testified by the
recurrence of fighting in our region. He never condoned the role that the FDLR rebels
played in the 1994 genocide. He was being reasonable and pragmatic.
Rwanda should know better
than any other country that there is no way Tanzania would condone or sympathize
with the perpetrators of genocide. To make such insinuations is, quite frankly,
a demonstration of breathtaking ignorance about Tanzania’s enviable and
unparalleled history - the history of speaking out against any forms of crimes
and injustices. Moreover, for Rwanda to make such insinuations is to show just what
a short memory span this country has.
Admittedly, genocide
brought about painful and unforgettable misery to the people of Rwanda but its
spillover effects were felt well beyond its borders. The effects of genocide were
felt right inside Tanzania which had to shoulder the burden of providing for thousands
of Rwandan refugees. By the way, Tanzania has a long history of taking good
care of Rwandan refugees both before and after genocide. The sons and daughters
of the Rwandan refugees benefitted from Tanzania’s generous education system by
studying, for free, at the country’s Universities and many of them are now occupying
high positions in the Government of their motherland.
So given the foregoing, I
have to say that I have been taken aback by our neighbors’ over-reaction to
what was a completely innocuous statement by President Kikwete. Indeed, what the
President said could (and should) have been said by other leaders a long time
ago. What he said is a no-brainer! It is
commonsensical! Negotiations have a much
better chance of resulting into durable peace than the use of force. Thus, I find
the reactions from Rwanda not only disturbing but also objectionable and utterly
impudent! What is even more shocking is the discourteous behavior shown by the Rwanda’s
Foreign Minister. She seems to be getting
too much big for her boots as to suggest that President Kikwete’s statement was
absurd! She even has the audacity to ask that he should retract it. If
anything, I think it is our Foreign Ministry which should summon the Ambassador
of Rwanda in Dar es Salaam and ask him to clarify his Minister’s inadvisable
utterances.
For far too long now the international
community has adopted a softly softly approach with respect to Rwanda and this
has meant that this tiny country gets away with literally everything, even
murder. Rwanda has become like a spoiled child - untouchable and overly
sensitive to everything even the slightest suggestion of censure. Rwanda has a tendency of not taking kindly any
form of criticism whether from within or without. And its leadership comes
across as snobbish and delusional. May be the western countries’ plaudits about
its so called success story have finally got into the heads of Rwandan leaders
so much that they think they know it all.
For Rwanda to say that
they cannot engage in talks with FDLR rebels because of their role in 1994
genocide is to allow themselves to be the captives of the past. History is
replete with numerous instances of former sworn enemies burying their hatchets
and extending an olive branch to one another for the sake of peaceful
coexistence and future prosperity. This happened in South Africa where ANC and
other progressive movements sat down with the perpetrators of one of the most
brutal and inhumane policies in the history of mankind (apartheid) and agreed
to work together in an inclusive and democratic society. Similarly, after many
decades of committing some of the most heinous crimes against the people of
Angola, UNITA is now part of the democratic government of that country. And in
2011, US and its allies initiated direct talks with some elements of the Taliban
in Doha (Qatar), if my memory serves me well.
Rwanda should wake up and
smell the coffee! Being delusional has not worked and won’t work. It is now close to 20 yrs since the 1994 genocide
and during all that time Rwanda has not been able to achieve its objectives
visa vis FDLR rebels through the use of force.
Any sane person in Kigali should see the wisdom of changing the
tactic/strategy which is, for all purposes and intents, what our President said
in the Statement. Rwanda should understand that by calling for direct talks,
Tanzania does not suggest, by any stretch of imagination, that the architects
and executors of genocide should go scot free. Not at all! Talks can, and
indeed should, offer the mechanism of dealing with known perpetrators of
genocide by isolating them from non-perpetrators such as those born after 1994.
This is just one example of approaching talks. I am sure there are many others.
But
talking of genocide, am I wrong in recalling that even President Kagame himself
was once found to be complicit in this crime by a French Magistrate? I recall
that Rwanda’s reaction to this finding was, as we have come to expect, fast and
furious to the extent of severing its diplomatic relations with France. Again,
this goes to show that this “spoiled child” can’t stand any sort of censure or
straight talking. I also recall that as recent as last year a UN report revealed
that Rwanda’s Kagame had committed or assisted in committing genocide in DRC!
Despite
all this compelling evidence, neighbors of Rwanda are still ready to engage
that country in talks. Why can’t Rwanda show the same attitude? And lest he
forgets, Kagame himself and his RPF henchmen come from a background of
rebellion. They were rebels operating from Ugandan forests before taking over
power in 1994. However, despite their “rebels” status they were invited and
took part in the Arusha peace process of the early 1990s.
Finally,
I have a gut feeling that Rwanda doesn’t want FDLR rebels to go away that’s is
why it is vehemently opposing the suggestion of talks which is one sure way of
ending this conflict once and for all. This because, the perpetual presence of
FDLR rebels in DRC gives Rwanda a convenient excuse to interfere in the DRC’s
affairs thereby making the country ungovernable for its own economic and
geopolitical interests. I read somewhere that Rwanda’s army – which is one of
the biggest for a country of that economy and size - is mainly sustained by the
exploitation of DRC’s natural resources. So, Rwanda goes into the DRC on the
pretext that it is in hot pursuit of the FDLR rebels but in actual fact what it
does is to plunder the resources.
And
Rwanda is particularly angry with Tanzania because by being part of MONUSCO in DRC, its misdeeds will be exposed
and curtailed by our non-nonsense troops. So the over-reaction to our
President’s innocuous statement should not be seen in isolation. It is part of
the frustration born out of the uneasy situation which Rwanda finds itself in
as a result of our troops being part of the UN/SADC intervention force in DRC.
I
submit.
Concerned Citizen
1 Aug 2011
- 1.8.11
- Evarist Chahali
- TANZANIA
- No comments
The Biggest Spending Tanzanian Embassies
- Budget 2011/12
Posted June 10th, 2011 by Web Master
A Rapid Analysis of the biggest spending Tanzanian Embassies - Budget 2011/12
Ministry of Foreign Affairs and International Cooperation Budget 2011/12
- UN Missions alone to spend 5,051,259,000/-
- Missions in Europe and Moscow to spend 12,481,913,000/-
- Embassies in four EA capitals allocated 3,746,956,000/-
- The Africa allocation is 10,945,095,000/-
- Administration costs nearly half of ministerial vote
- Salaries for London mission the highest (Pensionable posts & non-pensionable) at 868,142,918/- and Kigali the lowest at 80,201,559/-
Programme 20 - Diplomatic Missions | Tshs |
Permanent Mission to the UN - New York | 2,882,502,000 |
Permanent Mission to the UN - Geneva | 2,168,757,000 |
Embassy of Tanzania - Paris | 2,133,493,000 |
Embassy of Tanzania - London | 2,009,942,000 |
Embassy of Tanzania - Moscow | 1,907,166,000 |
Embassy of Tanzania - Rome | 1,891,547,000 |
Embassy of Tanzania - Berlin | 1,776,946,000 |
Embassy of Tanzania - Washington DC | 1,714,958,000 |
Embassy of Tanzania - Abu Dhabi | 1,710,597,000 |
Embassy of Tanzania - Tokyo | 1,662,626,000 |
Embassy of Tanzania - Nairobi | 1,625,277,000 |
Embassy of Tanzania - Brasilia | 1,532,748,000 |
Embassy of Tanzania - Brussels | 1,465,353,000 |
Embassy of Tanzania - Ottawa | 1,367,032,000 |
Embassy of Tanzania - Beijing | 1,352,422,000 |
Embassy of Tanzania - Stockholm | 1,297,466,000 |
Embassy of Tanzania - Pretoria | 1,269,178,000 |
Embassy of Tanzania - New Delhi | 1,215,144,000 |
Embassy of Tanzania - Kuala Lumpur | 1,160,872,000 |
Embassy of Tanzania - Riyadh | 1,156,879,000 |
Embassy of Tanzania - Addis Ababa | 892,277,000 |
Embassy of Tanzania - Maputo | 873,151,000 |
Embassy of Tanzania - Kampala | 822,513,000 |
Embassy of Tanzania - Kinshasa | 797,422,000 |
Embassy of Tanzania - Abuja | 778,726,000 |
Embassy of Tanzania - Muscat | 765,066,000 |
Embassy of Tanzania - Harare | 722,034,000 |
Embassy of Tanzania - Lusaka | 692,592,000 |
Embassy of Tanzania - Bujumbura | 659,258,000 |
Embassy of Tanzania - Kigali | 639,908,000 |
Embassy of Tanzania - Cairo | 595,191,000 |
Embassy of Tanzania - Lilongwe | 577,568,000 |
TOTAL Programme | 42,116,611,000 |
Administration Programme 10 | 38,486,246,000 |
Total of Vote 34 | 80,602,857,000 |
Less Retention Scheme funds | 14,872,492,146 |
Net total of vote | 65,730,364,854 |
Subscribe to:
Posts (Atom)