12 Oct 2016

Moja ya kazi ambayo inapendwa na kutamaniwa na watu wengi mno DUNIANI ni Uafisa Usalama wa Taifa, kwa jina jingine USHUSHUSHU.

Kuipenda au kuitamani fani hiyo kunachangiwa na ukweli kwamba, kwa upande mmoja ni eneo ambalo limekuwa maarufu mno kwenye filamu, na kwa hakika watu wengi wanapenda filamu za kishushushu.Ni nani asiyependa filamu za James Bond? Au series kama 24 na Homeland zinazohusu fani ya ushushushu?

Lakini licha ya filamu, kuna lundo la vitabu vya riwaya za kuhusu matukio halisi (non- fiction) au ya kutunga (fiction), na vingi ya vitabu hivyo ni 'vitamu' ukivisoma. Na sote twafahamu kuwa moja ya vitabu vilivyokuwa na bado vina umaarufu mkubwa mno nchini Tanzania ni vya Willy Gamba, shushushu mhusika katika vitabu vya Marehemu Eristablus Musiba.

Binafsi nilitamani kuwa shushushu nilipokuwa mtoto mdogo tu. Marehemu baba alikuwa na tabia ya kutusimulia kuhusu vitabu alivyosoma. Na kitabu cha kwanza hakikuwa cha kishushushu, bali story tu, kilichoandikwa na James Hadley Chase, "Come Easy Go Easy."

Baadaye alitusimulia kuhusu kitabu kimoja na James Bond, japo sikikumbuki jina. Kwa mara ya kwanza ndio nikafahamu kuwa kuwa watu wanaitwa 'ma-spy' na wanafanya kazi hiyo ya ushushushu. Fast forward miaka kadhaa baadaye, nikakutana na vitabu vya Willy Gamba, kuanzia "Njama," "Kikomo," "Kikosi cha Kisasi" na kadhalika.Kwa kweli kusoma vitabu hivyo vilikuwa kama kuangalia filamu. Tangu wakati huo nikatamani kuwa Willy Gamba.

Anyway, japo ushushushu kama tunavyoufahamu ni kwa ajili ya masuala ya usalama wa taifa, mbinu zinazotumiwa na mashushushu kusaka habari zinatumika katika maeneo mengine pia. Eneo linalotumia mbinu zinazoshibihiana zaidi na ushushushu ni uandishi wa habari.

Lakini eneo ambalo linanufaika na mbinu mbalimbali za kishushushu ni maisha yetu ya kila siku. Kwamba kuna mbinu mbalimbali za kishushushu ambazo zinaweza kumsaidia mtu wa kuwaida kufanikisha azma kama vile pale inapotokea mwenza mmoja kuhisi kuwa mwenzio anamsaliti au kupima uaminifu wa mwenza wako, kufahamu yanayoendelea 'behind the scene' katika masuala mbalimbali ya kimaisha,nk.

Je unahisi kuwa girlfirend/ boyfriend wako anaku-cheat? Je wahisi kuwa mumeo/mke 'anachepuka? Je unahisi kuwa binti yenu ameanza 'michezo michafu'? Je unahisi kuwa mtoto wenu wa kiume kaanza kujihusisha na makundi yasiyofaa? Je mshirika wako wa kibiashara ana ajenda ya siri dhidi yako? 

Ili uweze kupata majibu ya uhakika au yanayokaribiana na uhakika inabidi uwe shushushu, sio kwa ajili ya usalama wa taifa bali kwa ajili yako wewe mwenyewe au na mwenza wako au familia yako, nk.

Anza safari ya kujifunza ushushushu kwa kununua kitabu changu kuhusu taaluma ya Uafisa Usalama wa Taifa, kitabu pekee katika historia ya Tanzania, kinachoeleza kwa undani kuhusu taaluma hiyo. Ukifuatilia 'comments' za waliokwishasoma kitabu hicho utabaini kuwa wengi wamejifunza kutumia mbinu za kishushushu katika maisha yao binafsi.

Kwa wakazi wa Dar, unaweza kununua kitabu hicho na kuletewa hadi nyumbani, kazini, sehemu ya biashara, shuleni/chuoni, au hata kijiweni au pub.

Maduka ya vitabu jijini Dar na mikoani yanayouza kitabu hicho ni kama ifuatavyo


KARIBUNI SANA



0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.