10 Feb 2017


Kwamba Idara yetu ya Usalama wa Taifa imekuwa ikibebeshwa lawama mbalimbali kwa takriban 'kila baya' linaloihusu Tanzania yetu, sio siri. Ni kitu cha wazi ambacho ninaamini hata wana-Usalama wetu pia wanakifahamu.

Hata hivyo, kwa kiasi kikubwa lawama hizo huchangiwa na uelewa mdogo au usiopo kabisa kuhusu dhamana muhimu ya taasisi za usalama wa taifa kwa nchi husika, na jinsi taasisi hizo zinavyofanya kazi muda wote kuhakikisha usalama wa nchi husika.

Lakini pengine kabla ya kuingia kiundani kuhusu mada yangu, nigusie maongezi yangu na jamaa yangu mmoja, shushushu mstaafu kutoka nchi moja ya Afrika Magharibi. Jana aliamua 'kunifungukia,' kwanini mtu mwenye umri wa kati kama yeye ni 'shushushu mstaafu' (tumezowea kuona wastaafu wakiwa watu wenye miaka 50 na kuendelea, lakini huyo bwana ni wa umri wa miaka thelathini na kitu tu).

Alinidokeza kwa kifupi kuwa alilazimika 'kutoroka' nchini kwake baada ya kufeli kwa jaribio la mapinduzi katika taifa analotoka ambalo huko nyuma lilikuwa kama linapendelea zaidi mapinduzi kuliko chaguzi.  Alidai kuwa "mapinduzi hayo yalikuwa ni kwa minajili ya kuikwamua nchi hiyo kutoka katika nira ya utawala wa kidikteta wa kijeshi."

Hadi kufikia hatua hiyo ya maongezi hayo, ilitokana na huyo jamaa kuwa alitembelea kwenye ukurasa wangu wa Facebook, na kuona matangazo ya kitabu changu kuhusu taaluma ya Uafisa Usalama wa Taifa (USHUSHUSHU). Awali hakuelewa kitabu kinahusu nini kwa sababu maelezo yote kuhusu kitabu hicho yapo kwa Kiswahili, na yeye haielewi lugha hiyo. Alichofanya ni "kuomba msaada wa Google Translate," na akaweza kufahamu kitabu hicho kinahusu nini.

Akanambia kuwa amevutiwa sana na kitabu hicho kwa sababu kwa Bara la Afrika lina uhaba mkubwa mno wa katika fasihi simulizi kuhusu taaluma ya Uafisa Usalama wa Taifa. Na akanishauri nianze haraka iwezekanavyo kukitafsiri kitabu hicho kwa lugha ya Kiingereza ili kiweze kuwafikia wana-Usalama wengi zaidi katika nchi mbalimbali zenye uhaba mkubwa wa maandiko ya wazi kuhusu taaluma yao.

Japo sijawahi kuliongelea hili hadharani, moja ya mafanikio mkaubwa mno ya kitabu hiki yamekuwa katika wananchi wa kawaida kuielewa Idara ya Usalama wa Taifa kwa mtazamo chanya zaidi, hasa kutokana na maelezo ya kina ya kazi za taasisi hiyo muhimu kabisa kwa ustawi na uhai wa taifa lolote lile.

Angalia pongezi za msomaji mmoja wa kitabu hicho


Na kwa hakika, licha ya kuandika kitabu hicho kwa ajili ya jamii kwa ujumla, walengwa wakuu pia ni maafisa usalama wa taifa popote pale walipo. Kwa umahiri mkubwa, kitabu kimeepuka 'kuandika yasiyopaswa kuandikwa,' na kuwekea mkazo katika maoeneo ambayo licha ya kujenga ufahamu, yanasaidia kuwaelimisha raia kuwa Idara za Usalama wa Taifa ni kama roho na pumzi za taifa lolote lile. 


Naomba kutumia fursa hii kuwakaribisha ndugu zangu wa Idara ya Usalama wa Taifa kukinunua kitabu hiki kwa minajili ya kujielimisha, sambamba na kupata mtazamo wa 'akina sie' ambao ni wadau wa sekta ya Usalama wa Taifa. 

Kadhalika, kitabu hiki ni dedicated kwa Maafisa wa Usalama wa Taifa popote pale walipo, hasa kwa kutambua safari ndefu na ngumu waliyopitia hadi kufika walipo sasa, na "kuwa kwao macho masaa 24 ya siku 365 za mwaka" kwa minajili ya usalama wa mataifa yao. 


Kwa walio nje ya Tanzania, kitabu kinapatikana www.chahalibooks.com na AMAZON 

Kwa Tanzania, kitabu kinapatikana katika maduka ya vitabu yafuatayo


DAR ES SALAAM:

TPH BOOKSHOP, 24 Samora Street jirani na Sapna (Simu 0687-238-126/ 0759-390-082);
GENERAL BOOKSELLERS, Mtaa wa Mkwepu (Simu MAMA MEENA 0784-887-871)
DAR ES SALAAM BOOSHOP, Mtaa wa Makunganya (Simu MR MPONDA 0657-827-172)
MLIMANI BOOKSHOP, Kariakoo (Simu 0754-269-042)
ZAI BOOKSHOP, Kariakoo (Simu0754-292-532)
ELITE BOOKSTORE, Mbezi Beach Tangi Bovu karibu na Goba Road (Simu 0754-767-336)

MOSHI: APE BOOK, Rindi Lane, Opoosite I&M Bank (Simu 0754767336)

ARUSHA: KASE BOOKSTORE, ELCT Building, Joel Maeda Street

TANGA: HAFAT BOOKSHOP, Barabara ya Saba (Simu HASSAN SHEDAFA 0767-216-403)

MWANZA:
GUNDA BOOKSHOP Karibu na NHC Regional Office Bantu Street/Kemondo (Simu 0753-969-421)
VICTORIA BOOKSHOP, along Bantu Street, Kemondo (Simu 0755-375-034)

MUSOMA: NYAMBUSI BOOKSHOP, Opposite NMB Bank Main Branch (0767-578-565)

IRINGA: LUTENGANO INVESTMENT (Bakwata House), Miomboni St mkabala na Akiba House (Simu 0763-751-978)

KIGOMA: NDAMEZYE ENTERPRISES, Mkabala na NBC Bank (0713534116)

MBEYA VOLILE BOOKSHOP, Mount Loleza, mkabala na TRA (Simu SANGA 0754412075)

MOROGORO: Wasiliana na Marcelino kwa simu 0767612566 ; 0621081500; 0655612566. 






0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.