Imeniwia vigumu sana kuandika makala hii fupi lakini nalazimika kuiandika hivyo hivyo maana kukaa kimya is not an option. Kuna busara moja maarufu inayosema kinachohitajika kwa uovu kushamiri ni kwa watu wema kukaa kimya.
Hebu tutupie jicho mlolongo wa matukio jana kuhusu ishu ya Coronavirus.
Mnamo majira ya saa 4 asubuhi, "msema chochote" wa serikali anabwabwaja kuwazodoa wananchi wenye haki ya kuwa na hofu kuhusu Coronavirus.
VIDEO: “Ukiona Mtu kachukuliwa na Ambulance Airport sio kwamba ana corona, hatupimi corona Airport bali ni kupima joto kwanza, juzi ilitokea Kilimanjaro Mtu joto lilizidi Watu mitandaoni Watu corona corona” -Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbasi https://t.co/nOCECMicRd pic.twitter.com/onRuoA4UoU— millardayo (@millardayo) March 16, 2020
Majira ya saa 7 mchana, Magufuli akawahadaa Watanzania kuwa Coronavirus haijaingia Tanzania
Big liar! pic.twitter.com/K8oXIyixUY— Evarist Chahali (@Chahali) March 16, 2020
Na akaendelea kutawala anga za habari kwa "maigizo" yake yaliyomhusisha pia rafiki yake Kamwele.
JPM: Hakuna kitu cha uzembe Wizara ya Ujenzi mmefanya kama hiki Daraja la Kiyegeya,Waziri ulipaswa kumsimamisha Meneja wa TANROADS, eti mnampeleka Makao Makuu!KAMWELWE: Rais nimekosea, nilitakiwa nitamke siku ileile kuwa nimemfukuza kazi, naomba msamaha,Rais nimekosea nisamehe. pic.twitter.com/EsWuLworJ4— millardayo (@millardayo) March 16, 2020
baadaye kidogo Waziri Ummy akatangaza kuwa Corona virus imeingia rasmi Tanzania
“Habari njema ni kwamba mgonjwa ni Mtanzania ila ametoka nje, ugonjwa haujaanzia Tanzania,tunawafuatilia wote waliokutana nae tangu jana alipofika uwanja wa ndege KIA tutawaweka ktk nyumba za uangalizi kwa siku 14 ili kuhakikisha tunaidhibiti corona"-UMMYhttps://t.co/mYRvs8BI1g pic.twitter.com/bkcjYeGVKC— millardayo (@millardayo) March 16, 2020
Lakini ili uelewe vema sarakasi hizi ni muhimu utambue kuwa jana pia ilikuwa siku ambapo Mwenyekiti wa Chadema Taifa, Freeman Mbowe alikuwa anaongea na Watanzania kupitia mkutano wake na waandishi wa habari.
— millardayo (@millardayo) March 16, 2020LIVE: Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe anaongea na Waandishi kwa mara ya kwanza toka atoke gerezani >>> https://t.co/TIFdaAk5mh pic.twitter.com/kiA5OkMFCN
Na huhitaji kuwa jasusi mstaafu kama mie kubaini kuwa sarakasi hizo za jana zililenga "kuharibu" mkutano huo wa Mbowe.
Endapo walifanikiwa azma yao hiyo au la, wanajua wao.
Lakini si lengo la makala hii kuongelea "hujuma hiyo dhidi ya Mbowe," bali kutanabaisha kuwa Magufuli na serikali yake hawasemi ukweli kuhusu Coronavirus.
Hata hivyo badala ya mie "raia wa kawaida" kuthibitisha kuwa kuna urongo unafanyika kuhusu suala hilo, nawapa changamoto viongozi wakuu wa upinzani, Mheshimiwa Mbowe na Mheshimiwa Zitto Kabwe kuchunguza suala hili na kisha kuwaambia Watanzania ukweli.
Rekodi ya Magufuli katika kudili na majanga ni mbovu mno. Kila mmoja wetu anakumbuka matusi yake kwa wahanga wa tetemeko la rdhi huko Kanda ya Ziwa (nyumbani kwake huko) kuwa si yeye aliyeleta tetemeko hilo.
Magufuli: Tetemeko halijaletwa na Serikali, watu wafanye kazi- Wataokusanya misaada kitapeli, wakamatwe
— Jamii Forums (@JamiiForums) September 17, 2016
Na akawadhihaki zaidi
Magufuli: Tetemeko halijaletwa na Serikali, watu wafanye kazi- Wataokusanya misaada kitapeli, wakamatwe
— Jamii Forums (@JamiiForums) September 17, 2016
Lakini kingine cha muhimu ni kwamba kama nilivyotahadharisha katika makala hii, Magufuli ni mtu anayetaka habari nzuri tu hata kama ni za hadaa. Na hili la Coronavirus sio tu ni habari mbaya lakini pia linaweza kuonyesha mapungufu makubwa ya utawala wake ambao umekuwa ukificha mapungufu hayo kwa kutumia ubabe dhidi ya uhuru wa kujieleza, kuvibana vyama vya upinzani na kuvifunga mdomo vyombo vya habari.
Nimalizie makala hii kwa kuwakumbusha Waheshimiwa Mbowe na Zitto kufuatilia hadaa waliyofanyiwa Watanzania kuhusu Coronavirus na ikiwezekana wao ndio wachukue uongozi wa umma katika kukabiliana na janga hili hatari.
0 comments:
Post a Comment