17 Mar 2020


Imeniwia vigumu sana kuandika makala hii fupi lakini nalazimika kuiandika hivyo hivyo maana kukaa kimya is not an option. Kuna busara moja maarufu inayosema kinachohitajika kwa uovu kushamiri ni kwa watu wema kukaa kimya.


Hebu tutupie jicho mlolongo wa matukio jana kuhusu ishu ya Coronavirus.



Mnamo majira ya saa 4 asubuhi, "msema chochote" wa serikali anabwabwaja kuwazodoa wananchi wenye haki ya kuwa na hofu kuhusu Coronavirus.


Majira ya saa 7 mchana, Magufuli akawahadaa Watanzania kuwa Coronavirus haijaingia Tanzania

Na akaendelea kutawala anga za habari kwa "maigizo" yake yaliyomhusisha pia rafiki yake Kamwele.

baadaye kidogo Waziri Ummy akatangaza kuwa Corona virus imeingia rasmi Tanzania

Lakini ili uelewe vema sarakasi hizi ni muhimu utambue kuwa jana pia ilikuwa siku ambapo Mwenyekiti wa Chadema Taifa, Freeman Mbowe alikuwa anaongea na Watanzania kupitia mkutano wake na waandishi wa habari.

Na huhitaji kuwa jasusi mstaafu kama mie kubaini kuwa sarakasi hizo za jana zililenga "kuharibu"  mkutano huo wa Mbowe.


Endapo walifanikiwa azma yao hiyo au la, wanajua wao.



Lakini si lengo la makala hii kuongelea "hujuma hiyo dhidi ya Mbowe," bali kutanabaisha kuwa Magufuli na serikali yake hawasemi ukweli kuhusu Coronavirus. 



Hata hivyo badala ya mie "raia wa kawaida" kuthibitisha kuwa kuna urongo unafanyika kuhusu suala hilo, nawapa changamoto viongozi wakuu wa upinzani, Mheshimiwa Mbowe na Mheshimiwa Zitto Kabwe kuchunguza suala hili na kisha kuwaambia Watanzania ukweli.



Rekodi ya Magufuli katika kudili na majanga ni mbovu mno. Kila mmoja wetu anakumbuka matusi yake kwa wahanga wa tetemeko la rdhi huko Kanda ya Ziwa (nyumbani kwake huko) kuwa si yeye aliyeleta tetemeko hilo.


Na akawadhihaki zaidi
Lakini kingine cha muhimu ni kwamba kama nilivyotahadharisha katika makala hii, Magufuli ni mtu anayetaka habari nzuri tu hata kama ni za hadaa. Na hili la Coronavirus sio tu ni habari mbaya lakini pia linaweza kuonyesha mapungufu makubwa ya utawala wake ambao umekuwa ukificha mapungufu hayo kwa kutumia ubabe dhidi ya uhuru wa kujieleza, kuvibana vyama vya upinzani na kuvifunga mdomo vyombo vya habari.

Nimalizie makala hii kwa kuwakumbusha Waheshimiwa Mbowe na Zitto kufuatilia hadaa waliyofanyiwa Watanzania kuhusu Coronavirus na ikiwezekana wao ndio wachukue uongozi wa umma katika kukabiliana na janga hili hatari. 



0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.