Showing posts with label 2020. Show all posts
Showing posts with label 2020. Show all posts

1 Jan 2020




Kwa zaidi ya miaka 10 sasa nimekuwa na utaratibu wa kufanya ubashiri kuhusu yanayotarajiwa kutokea katika mwaka mpya, zoezi ninalolifanya siku ya kwanza ya mwaka mpya husika.

Mwaka huu 2020 unatarajiwa kuwa mgumu sana kwa Tanzania. Na bila kuumauma maneno, ugumu wa mwaka huo utachangiwa na "utawala wa mkono wa chuma" - unaozidi kuota mizizi -wa Rais John Magufuli. 

Moja ya matukio yatakayotawala vichwa vya habari mwaka huu ni pamoja na watu kadhaa maarufu kutoka kada mbalimbali "kupotea." Wahanga wakubwa wanatarajiwa kuwa wanaharakati wanaodiriki kukemea maovu mbalimbaliyanayofanywa na utawala wa Rais Magufuli.

"Kupotea" huko kutaendelea kufanya tishio la "Watu Wasiojulikana" liendelee kuwasumbua Watanzania kama ilivyokuwa mwaka jana 2019.

Kinachotarajiwa kufanya hali kutokuwa nzuri ni pamoja na hofu isiyo na msingi aliyonayo Rais Magufuli kuhusu uwezekano wa yeye kuchaguliwa kuwa mgombea urais kwa tiketi ya CCM na uwezekano wa yeye kushinda nafasi hiyo. 

Hofu hiyo inachangiwa na kile Waingereza wanasema "the guilty are always afraid." Sio siri kwamba Rais Magufuli amejitahidi sana kuwavunja moyo watu wengi tu ambao sio tu walikuwa na matarajio makubwa kwake bali baadhi yao  - ikiwa ni pamoja na mie -walishiriki kumnadi kwa nguvu zote katika kampeni za uchaguzi mkuu wa mwaka 2015.

Kubwa zaidi lililowavunja moyo watu hao ni "valid excuse" ya Rais Magufuli kuwa Watanzania waelekeze nguvu zao kwenye kuchapa kazi ilivyogeuka kuwa excuse ya kuwanyima raia haki zao za msingi. Kukandamiza haki ya kikatiba ya vyama vya upinzani kufanya shughuli zao za kisiasa, kukandamiza uhuru wa vyombo vya habari, kuwabambikiziawatumbalimbali kesi zisizo na kichwa wala miguu, kuendeleza siasa za chuki, ubaguzi na ukanda wa mchana kweupe, matusi ya hadharani dhidi ya watendaji mbalimbali wa serikali, na mlolongo wa vitu visivyopendeza. 

Kwa vile Rais Magufuli anafahamu kuwa "amewageuka" wengi wa waliomnadi na kumuunga mkono, anajikuta akiwa kwenye kundi la "the guilty are always afraid." Gulity for what? Well, hadi muda huu serikali yake inabaki suspect number one katika "kupotea" kwakda maarufu wa Chadema Ben Saanane ambaye alikuwa critic mkubwa wa Rais Magufuli; suspect number one katika jaribio la kumuua Tundu Lissu; suspect number one katika "kupotea" kwa mwanahabari Azory Gwanda; suspect number one katika yanayodaiwa kuwa "mauaji ya mamia" huko Mkuranga, Kibiti na Rufiji (MKIRU), suspect number one katika kifo cha afisa wa hazina kitengo cha EU, Marehemu Leopold Lwajabe ambaye kabla ya kuuawa alitekwa, akateswa na kubakwa. Unyama usiomithilika.

Serikali ya Rais Magufuli ni suspect number one katika kinachodaiwa kuwa ufisadi wa kihistoria wa fedha za umma, jambo lililopelekea kuondolewa kwa CAG Prof Assad ili ufisadi huo uendelee kufichwa.

In short tema, Rais Magufuli anaishi na hofu ya kitakachomtokea pindi akiwa sio rais, iwe kwa kushindwa uchaguzi, kung'olewa madarakani au kumaliza muhula wake. Kilicho wazi ni kwamba kwa aliyokwishatenda katika miaka hii minne kuelekea mitano, sio rahisi kwake japo kufikiria kuhusu kuwa nje ya nafasi ya urais. 

Na kwa vile mbinu yake kuu ya utawala - UBABE - inaelekea kuwa na ufanisi, kwa maana ya kwamba hakuna jitihada zozote zilizofanyika kupambana na mengi yasiyopendeza yanayofanywa na utawala wake, mwaka huu unatarajiwa kushuhudia ubabe maradufu. Kwa upande mmoja ubabe huo utakuwa mwendelezo tu wa yanayojiri muda huu lakini kwa upande mwingine utakuwa ni mkakati wa kuhakikisha anarudi Ikulu baada ya uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwezi Oktoba.

Talking of uchaguzi mkuu, inatarajiwa kuwa uchaguzi huo mkuu utatawaliwa na hila na vituko na hujuma na mbinu chafu maradufu ya ilivyokuwa kwenye mzaha wa kisiasa uliopewa jina la "uchaguzi wa serikali za mitaa," ambapo pasi haya, chama tawala CCM kilijitangaza mshindi kwa asilimia 99.

Wakati endapo kila kitu kitabaki "constant" (yaani endapo hakutokuwa na mabadiliko), Rais Magufuli na CCM yake watajitangaza washindi wa kishindo kwenye uchaguzi huo mkuu ambapo kura zake na za CCM zitakuwa zaidi ya asilimia 90.

Kadhalika, endapo kila kitu ktabaki "constant," vyama vya upinzani vitaambulia kati ya viti 10 hadi 20 tu (yawezekana vikawa hata pungufu ya 10) vya ubunge kwenye uchaguzi huo mkuu.

Kadhalika, kadri uchaguzi huo mkuu utakavyozidi kujongea ndivyo Rais Magufuli na CCM yake watakavyozidi kuongeza jitihada za kuwanunua wabunge na madiwani wa vyama vya upinzani ili wajiondoe kwenye vyama vyao na kutangaza kujiunga na CCM. Mkakati huo ni sehemu ya jithada za kukomboa majimbo yaliyo chini ya wabunge wa upinzani.

Sambamba na hilo ni kukua kwa "uhasama" kati ya Chadema na ACT-Wazalendo, kitu kitakachochochewa na jitihada endelevu za CCM kuhujumu vyama vyaupinzani sambamba na jitihada za mapandikizi waliomo kwenye vyama hivyo vya upinzani wakiwana jukumu moja tu- kuvikwamisha.

Ukandamizwaji dhidi ya wanasiasa utawakumba pia baadhi ya wana-CCM hususan wanaohisiwa kuwa karibu na Bernard Membe, mwanasiasa anayemnyima usingizi Rais Magufuli kwa kudhani kuwa anataka kuchuana nae kwenye kinyang'anyiro cha kuwania urais kwa tiketi ya CCM.

Kuna uwezekano mkubwa kwa wana-CCM kadhaa wenye majina makubwa kufukuzwa uanachama. Licha ya hatua hiyo, wana-CCM hao watafunguliwa kesi za uhujumu uchumi.

Kwa upande mwingine, mwaka huu utashuhudia angalau mabadiliko mawili ya baraza la mawaziri. Sambamba na hilo, endapo Rais Magufuli atafanikiwa kuwa mgombea pekee wa CCM, inatarajiwa atashinikiza kuteuliwa kwa mgombea mwenza mwingine badala ya Mama Samia. 

Kuna uwezekano wa kujitokeza matishio ya mashambulizi ya kigaidi yatakayohusiana na hali tete iliyopo kwenye mpaka wa Tanzania na Msumbiji. 

Kuhusu Idara ya Usalama wa Taifa, nabashiri kutokea kwa mabadiliko makubwa yanayoweza kupelekea Mkurugenzi Mkuu wa sasa, Diwani Rajabu kuondolewa kwenye wadhifa ho na nafasi yake kuchukuliwa na aliyewahi kuwa Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Idara hiyo, Robert Makungu ambaye awali alitumbuliwa na kuwa RAS huko Tabora. 

Kiuchumi, vyuma vitaendelea kukaza. Na hali inatarajiwa kuwa ngumu zaidi mwaka huu kwa sababu CCM itaongeza jitihada za kukusanya fedha kwa ajili ya uchaguzi mkuu. Neno "jitihada" hapa linamaanisha mbinu chafu na za kifisadi kama ilivyokuwa kwenye skandali ya EPA/Kagoda.

Uchumi pia unatarajiwa kuwa mgumu kwa sababu kuna uwezekano wa baadhi ya nchi wahisani kusitisha misaada yao kufuatia ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu nchini Tanzania. 

Jambo jingine linalotarajiwa kuathiri uchumi na matumizi holela yanayofanywa na serikali ya Rais Magufuli bila kuzingatia idhini yabunge au/na kanuni za bajeti. 

Moja ya matukio ya nje ya Tanzania yanayoweza kuigusa Tanzania ni uhasama endelevu kati ya Rais Museveni na Kagame. Unfortunately, Tanzania ni eneo muhimu kimkakati kwa nchi zote mbili hasa kwa vile ndipo kunapotokea "vita ya kijasusi" kati ya Uganda na Rwanda. Kwamba nchi hizo mbili zinaweza kuingia vitani sio jambo lisilowezekana japo sio rahisi sana.

Kabla ya kuhitimisha makala hii, naomba kusisitiza kuwa ubashiri huu sio exact science bali ni matokeo ya mie mtumishi wako kumudu kusoma mwenendo wa mambo (trends) huko Tanzania. Japo ni rahisi kuhisi kwamba MATAGA na Praise Teram watatafsiri ubashiri huu kuwa ni "kazi ya kibaraka wa mabeberu kuiombea mabaya Tanzania," ukweli ni kwamba ubashiri huu umefanyika objectively.

Mwisho, haitokuwa jambo la kushangaza endapo mgombea urais wa CCM katika uchaguzi mkuu ujao hatokuwa Rais Magufuli. Si kwamba jina lake litakatwa lakini "laweza kutokea la kutokea."

Nimalizie kwa kuwatakia nyote heri ya mwaka mpya 2020.



Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.