Showing posts with label Ezekiel Wenje. Show all posts
Showing posts with label Ezekiel Wenje. Show all posts

5 Feb 2012

Viongozi wa Chadema jana tarehe 4 Februari 2012 wamekutana na kufanya Mazungumzo na Watanzania wanaoishi Washington DC . Katika msafara huo ambao umeongozwa na Mwenyekiti wa Chadema Mheshimiwa Freeman Mbowe na Mbunge wa Nyamagana na Waziri kivuli wa Mambo ya nje Mheshimiwa Ezekiel Wenje, wameongelea mambo mbalimbali ikiwemo suala la Mipango ya Maendeleo ya Chama na Mikakati ya kujiandaa na chaguzi zijazo hususani uchaguzi mkuu wa mwaka 2015.

Hali kadhalika wakazi hao wa Washington DC wametumia fursa hiyo kumuuliza maswali mbalimbali hususani suala la upatikanaji wa Katiba mpya. Akichangia katika mjadala huo Prof N. Boazi amewakumbusha viongozi hao umuhimu wa kuwa na katiba mpya ambayo itampunguzia madaraka Rais tofauti na sasa inayompa Rais  madaraka  makubwa na kunyima fursa kwa wengine.


Pia wakazi wa Washington DC walimuuliza Mheshimiwa Freeman Mbowe kuhusu suala la mgomo wa madaktari unaoendelea. Akijibu suala hili Mheshimiwa mbowe amesema kuwa alipata nafasi ya kuwasiliana na Viongozi wa mgomo huo lakini walimjibu kwamba hawataki kulifanya suala hilo la Mgomo kuonekana la kisiasa kwa kuwahusisha Chadema.



Mheshimiwa Freeman Mbowe akiwahudubia Watanzania wanaoishi  Washington DC jana jumamosi Feb, 4 2011 Nchini Marekani




 Wakazi wa Washington DC wakimsikiliza Mheshimiwa Freeman Mbowe kwa makini katika mkutano huo.




Mbunge wa Nyamagana na Waziri kivuli wa Mambo ya nje Mheshimiwa Ezekiel Wenje akiongea katika mkutano huo.


Baada ya Mheshimiwa Freeman Mbowe na  Ezekiel Wenje kuongea,  Watanzania waliohudhuria walipata nafasi ya kuliza masuali, na  moja ya maswali aliyoulizwa Mhe Freeman Mbowe ni ile dhana kuwa CHADEMA ni "chama cha waChagga na matajiri". Hapa chini anafafanua dhana zote hizo na ile aliyosema iliwahi kusambaa kuwa ni "chama cha waKristo"


CHANZO: Swahilivilla. Shukrani pia kwa Mzee wa Changamoto Mubelwa Bandio kwa kunitumia kiungo (link)

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.