Showing posts with label NARC. Show all posts
Showing posts with label NARC. Show all posts

30 Dec 2007

Hatimaye Mwai Kibaki ametangazwa mshindi katika uchaguzi mkuu nchini Kenya.Ni rahisi kuhisi Raila Odinga ameporwa ushindi kutokana na namna matokeo ya uchaguzi huo yalivyochukua muda mrefu kuliko ilivyopaswa.Wakati matokeo haya yanaweza kuwaacha watu wengi,hususan wafuasi wa Raila,wakiwa hawaamini kinachoendelea,binafsi naona ni mwendelezo wa "kanuni isiyo rasmi" ya siasa za Afrika ambapo mara nyingi CHAMA TAWALA HAKISHINDWI UCHAGUZI ISIPOKUWA PALE KINAPOLEWA MADARAKA NA KUJIONDOA CHENYEWE KWA UZEMBE.KANU haikushindwa uchaguzi na NARC (enzi hizo) kwa vile wapinzani walikuwa na nguvu sana au wananchi walikuwa wameichoka sana,bali ilijifunga "own goal" kwa kusimamisha mgombea butu.Vyama pinzani vinaweza kufanya kila jitihada kukiondoa chama tawala madarakani lakini tatizo linabaki kuwa katika chaguzi nyingi za Afrika,vyama pinzani ni sawa na mshtakiwa aliyeko mahakamani ambapo hakimu,mwendesha mashtaka na baraza la wazee wanatoka upande wa mshtaki (ni dhahiri hapo hakutakuwa na haki kwa mshtakiwa).Na katika soka,mkiwa mnashindana na timu ambayo refa,kamisaa na washika vibendera ni manazi wa wapinzani wenu,basi hapo ni kipigo tu hata mtumie mbinu za Brazil.

Kwanini vyama tawala vya Afrika vipo tayari kufanya lolote linalowezekana kuhakikisha vinabaki madarakani?Well,jibu jepesi ni kwamba viongozi wengi wa vyama hivyo ni mafisadi wanaojua bayana kwamba wakiondoka madarakani wanaweza kujikuta wanaishia jela kwa maovu yao.Japo kwa ujumla siasa ni mchezo mchafu,kwa Afrika siasa ni zaidi ya mchezo mchafu,na pengine sio mchezo at all bali mazingaombwe.

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.