19 Jan 2008

Miongoni mwa matukio ya mwaka jana yaliyoathiri huduma hapa Uingereza ni pamoja na mgomo wa wafanyakazi wa Royal Mail (kufupisha maelezo,tuliite "shirika la posta la hapa").Pamoja na madai mengine yaliyopelekea mgomo huo,ni upinzani wa wafanyakazi hao dhidi ya mpango wa Royal Mail kuongeza teknolojia ambazo zingepelekea kupunguza wafanyakazi.Teknolojia ina faida na hasara zake,na moja ya "hasara" kubwa ni kupunguza utegemezi wa binadamu katika sehemu ya kazi.Ni dhahiri kwamba kiwanda "kikiajiri" robots basi kuna watu watakosa cha kufanya mahala hapo.

Bila shaka unakumbuka mada ya Mapinduzi ya Viwanda (Industrial Revolution) ambapo maendeleo katika sayansi na teknolojia yalipelekea baadhi ya vibarua kujikuta wanatimuliwa kazi.Katika kupambana na hali hiyo,ziliibuka harakati zilizojulikana kama Luddism.Kwa kifupi kabisa,harakati hizo zilihusisha hujuma dhidi ya mitambo iliyoonekana kama adui dhidi ya ajira.

Nimesoma habari flani ya kuchekesha katika tovuti ya Allhiphop.com kwamba rapa Mike Jones "ameboresha" video moja ya wimbo wake Drop&Gimme 50 kwa kutumia wanenguaji vikatuni (animated cartoon vixens).Nafahamu bayana kwamba vikatuni haviwezi kuchukua kabisa (completely) nafasi ya video vixens,lakini kwa kumbukumbu ya Luddism na mgomo wa Royal Mail,nikajikuta najiuliza:je hao warembo wanaonadhifisha video mbalimbali wangechukua hatua gani iwapo (kwa kufikirika) wanamuziki wengi wangeamua kutumia teknolojia ya vikatuni badala ya warembo hao?Au ndio akina Buffie the Body,Ki-Toy Johnson,KD Aubert,na wengineo wangeishia kuwa virtual tu (kama kwenye computer games) kama sio kusahaulika kabisa?Just thinking aloud.

Video nayozungumzia ni hii


Miongoni mwa video za nyimbo zilizotamba japo wahusika walikuwa vikatuni ni pamoja na Piggy Bank ya 5o Cent (Caution: explicit lyrics)


Na hii Be Faithfull ya Fatman Scoop

0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.